03/05/2024
Mwaka huu wa 2024 tunaadhimisha miaka 90 ya uwepo wa Kanisa Kuu la Mt. Albano, Dar es Salaam.
Kuelekea Maadhimisho haya, Kanisa Kuu la Mt. Albano kwa kushirikiana na Bw. David Ocheng (mzee mwenye umri wa miaka 72, mstaafu wa fani ya maabara ya matibabu mwenye ulemavu wa miguu ambaye hutembea kwa msaada wa magongo) pamoja na Bw. Noel Gumbo (mlemavu wa macho), tumeandaa Tukio la Matembezi na Kukimbia kwa ajili ya Kuchangisha Fedha ili kusaidia miradi ya kijamii.
Tukio hili linalenga kukusanya fedha kwa ajili ya juhudi za kuifikia na kuitendea mema jamii kupitia Mkono wa Msamaria na mradi wa uwekezaji.
Hivyo, tunakukaribisha katika Uzinduzi Rasmi wa Matembezi haya ambayo utafanyika Jumapili hii tarehe 5 Mei, 2024 katika Misa zote tatu hapa Kanisa Kuu la Mt. Albano Dar es Salaam.
Tafadhali usipange kukosa.