RAGT - Sikari

RAGT - Sikari Karibuni wote kwa huduma za kiroho ,Mungu wetu kupitia Yesu Kristo atakuhudumia ,pia ushauri Wa kiroho na maombezi vinapatikana.

22/08/2024

Habari za muda huu, unaweza kutune radio ya Upendo fm 107.7 - Usikie kuhusu Agano lililo Bora kuanzia saa 3.20 Asubuhi hii

Jenga tabia ya usomaji wa vitabu, ili upate maarifa yatakayokusaidia katika Maeneo mbalimbali.
15/08/2024

Jenga tabia ya usomaji wa vitabu, ili upate maarifa yatakayokusaidia katika Maeneo mbalimbali.

Uzinduzi wa Kitabu" Agano lililo Bora" Tarehe 25/08/2024.Mawasiliano 0622485519.Usipange kukosa....
13/08/2024

Uzinduzi wa Kitabu" Agano lililo Bora" Tarehe 25/08/2024.
Mawasiliano 0622485519.
Usipange kukosa....

Kwa wale wa Dodoma kitabu kinapatikana Capita bookstores- Karibu na Nyerere square. Pata nakala yako.
02/08/2024

Kwa wale wa Dodoma kitabu kinapatikana Capita bookstores- Karibu na Nyerere square. Pata nakala yako.

Ishinde vita ya madhabahu (milango) za siri. Zinazopitisha vikwazo na uharibifu, kwenye uchumi, huduma, ndoa nakadhalika...
30/05/2024

Ishinde vita ya madhabahu (milango) za siri. Zinazopitisha vikwazo na uharibifu, kwenye uchumi, huduma, ndoa nakadhalika.
AGANO LILILO BORA.
Weka oda yako kupitia namba 0766253411
Popote ulipo kitakufikia

01/03/2024

SOMO : KUMTAFUTA MUMGU

Kanuni Na 02. KUZALIWA KATIKA ROHO
Kuzaliwa ni kitendo cha kiumbe kuanza maisha mapya ( New beginning). Kwa sababu Mungu ni roho ili niweze kumtafuta na kumpata ni lazima ukubali kuzaliwa mara ya pili kwa jinsi ya rohoni.

Yesu aliwahi kumwambia Mfarisayo mmoja alifahamika kwa Jina la Nikodemo kuwa " Hakuna anayeweza kuingia katika ufalme wa Mungu k**a hajazaliwa kwa maji na kwa Roho"
Kuzaliwa katika Roho ni kitendo cha kumkiri na Kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako.

Yohana 1 (¹² Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
¹³ waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.

Kwa hiyo Mungu humfanya mwana kwa jinsi ya Roho yule aliyempokea Yesu Kristo, ukishazaliwa kwa Roho mambo ya rohoni, utayaelewa kwa maana hutambulika kwa jinsi ya rohoni (1Wakorinto 2:14-15).
Kumuona na kumuelewa Mungu hakutegemei ukubwa wa elimu uliyonayo, umasikini wala utajiri ila kunahitaji kuzaliwa mara ya pili.

Omba nami Sala hii
Bwana Yesu ninakupokea, uwe Bwana na mwokozi wa maisha yangu, nisamehe dhambi zangu, nisaidie niishi maisha matakatifu ya kukupendeza wewe, mwisho nifike kwako Amina.

27/02/2024

“Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;”
— Isaya 55:6 (Biblia Takatifu)

SOMO: KUMTAFUTA MUNGU

Kumtafuta Mungu ni kitendo cha kuelekeza macho yako kwa Mungu, kumtegemea na kumtanguliza Mungu katika kila jambo.
Maandiko yanasema tumtafute Mungu kwa sababu anapatikana.
Kwanini tumtafute Mungu wakati anapatikana ? Kinachotafutwa ni kile ambacho hakionekani sikuzote, Je Mungu haonekani ?.

Sababu kwanini - Tumtafute Mungu.
A. Mungu ni Roho ( Yohana 4:24), roho ipo kila mahali ila haionekani kwa macho ya nyama, ili uweze kuiona roho na kuielewa inakulazimu kuwa rohoni ( 1Kor 2:14-15). Na ili uweze kuwa rohoni inakulazimu kufuata kanuni za Roho na kukubali kuongozwa na Roho.

Kanuni za kuingia katika ulimwengu wa roho -
Kwanza naomba tufahamu kuwa ulimwengu wa roho ni nini?
Ulimwengu wa roho -Ni ufalme au miliki inayotawaliwa na kusimamiwa na ufalme na majeshi yake kwa jinsi ya rohoni, ambayo huwezi kuona kwa namna ya mwilini.

Kanuni Na 01. IMANI.
Imani ni kuwa na uhakika ( ushahidi) wa jambo flani unaotokana na taarifa, na ni bayana na mambo yasiyoonekana kwa macho ya nyama ( Waebrania 11:1).
Imani haikutaki wewe mpaka ukione kitu kwa macho ndo uamini kipo hapana! Imani inakutaka utegemee taarifa tu kuona ambayo hujayathibitisha kwa macho ya nyama.
Neno linasema mtafuteni Mumgu maadam anapatikana, unachotakiwa wewe ni kuamini tu, halafu nenda ukamtafute ukiwa na imani yupo utamkuta, na kile utamwomba atakupa kwa sababu yupo ( Waebrania 11:6).
Nikupe mfano huu Mvuvi anakwenda baharini kutega vyavu katika eneo flani kwa imani tu atapata samaki, wakati mwingine hajaona kuwa hilo eneo lina samaki, lakini anatega na mwisho wa siku anapata samaki.
Dereva bajaji, bodaboda na wengine wengi, wanaamka mapema kabisa wanasema ngoja leo nikachukue abiria wangu kadhaa ntapata kiasi flani, hao abiria hajawaona, wala hajaagana nao, anatoka kwa imani anakutana na abiria kweli, na pesa anapata.

Kwa hiyo Imani haitegemei kuona kitu kwa macho ila taarifa tu inatosha kuthibitisha kitu kipo...
Mtafute Mungu kwa maana anapatikana.....
Somo litaendelea.....
Barikiwa uwe na siku njema...

Hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea 1Wakorintho 10:13
24/02/2024

Hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea 1Wakorintho 10:13

24/02/2024

“Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.”
— Mhubiri 12:1 (Biblia Takatifu)

Kipindi cha ujana ni kipindi muhimu sana katika maisha ya binadamu ni kipindi ambacho Mungu amempa Kijana nguvu za aina mbili;
1.Nguvu za Kimwili ( both mental and physical strength)- Katika kipindi hiki kijana anaweza kwenda popote, kufanya lolote kwa kuwa nguvu za kimwili na kiakili zinaruhusu, ni kipindi ambacho k**a kijana hutatumia nguvu zako vizuri katika kufanya kazi yako na ya Mungu hakika utakuja kujutia kipindi nguvu zako zitakapoisha ( uzeeni).
Tumia wakati huu vizuri, k**a ni kazi fanya kazi ,acha uvivu, na ndio wakati pia hata wa kutafuta watoto ili uweze kuwatunza wakati bado una nguvu, mtafute Mungu wakati huu maadam una nguvu na unaweza kufanya hivyo.

2.Nguvu za Kiroho ( Spiritual strength)-
Lazima ufahamu kuwa mwanadamu ni kiumbe cha roho katika mwili, kinachoweza kutoa uhai ni roho sio mwili (Yohana 6:63 ). Nguvu za kiroho zinategemea sana nguvu za kimwili katika kufanya kazi, hivyo shetani ( roho) pia anategemea sana kuwatumia watu katika kipindi hiki cha ujana, na ndio maana watu wengi katika umri huu wa ujana wanasukumwa sana, kufanya uovu, wanapokuwa wazee hawawezi tena kwa sababu hawana nguvu tena za kimwili.
Kwa hiyo rafiki yangu hiki ndicho kipindi tunachoweza kuziona nguvu za Mungu za ajabu zikitenda kazi ndani yetu k**a tutakubali Mungu atutumie.

Mchungaji wangu ( Glory) aliwahi kusema hivi " Unapojua haya ndio majira yako basi ng'ang'ana, pambana usikubali watu, mazingira yakupunguzie mwendo"
Barikiwa na ujumbe huu....

UKIMYA WA MUNGUUkimya ni hali ya kutokuongea,kusema au kupiga kelele.Ni ile hali ya kutokupata mafunuo,ndoto,au kusikia ...
01/07/2020

UKIMYA WA MUNGU

Ukimya ni hali ya kutokuongea,kusema au kupiga kelele.
Ni ile hali ya kutokupata mafunuo,ndoto,au kusikia sauti yoyote kutoka kwa Mungu.

Kipindi hiki cha ukimya ,huwa kina wafadhaisha wengi haswa waombaji na watu wanaopitia kwenye magum,hudhani k**a Mungu hasikii ,au hajibu na kuona kuwa Mungu amewaacha kabisa.

Tukikumbuka umbali Wa Agano LA kale mpaka agano jipya (malaki hadi mathayo).
Ni miaka *400* ambayo Mungu alikaa kimya..
Katika kipindi hiki hakukuwa na unabii wala mtume yeyote..ni kipindi cha ukimya.

Ila tunajifunza kitu katika ukimya huo..kuwa alikuwa akifanya maandalizi juu ya ujio Wa Yesu ulimwenguni.Hapa aliandaa watu,mahali na njia ya Yesu kupita ili iwe rahisi kueneza injili kwa watu wote.

Yamkini unaweza kuona kimya kwenye mambo yako,kazi,ndoa ,biashara ,na mipango yako,usifadhaike mpendwa Mungu anaandaa surprise kwa ajili yako.

Mambo ya msingi kuelewa pale unapohisi Mungu amekaa kimya kwako.

▪️ *Amini uwepo Wa Mungu* (Trust God's Presence in your life)

Ukimya Wa Mungu hauna maana eti kuwa Yeye hayupo, kukaa kimya hakuna maana ya mhusika hayupo...

Mathayo1:23, Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.

Kuja kwa Yesu duniani,kulibeba maana hiyo kubwa sana,yakuwa Mungu yupo pamoja nasi, *hatuachi ,wala hatatuacha* mda wote yupo Pamoja nasi.
"So don't be depressed but feel the presence of God in any situation that you're, because Our Lord Jesus will not forsake us even in a single breath."
Trust him with all your heart.

▪️ *Mungu anaandaa mpango mzuri kwa ajili ya maisha yako*
Wakati Wa huzuni ,ni wakati ambao unahisi upo peke yako,ila nataka nikwambie kuwa ndo wakati Mungu anaandaa kicheko kwa ajili yako..
Mungu siku zote ,Yeye ni bora ,hatua (process) zake zinaweza kuwa ngumu au zenye maumivu ,lakimi hatima yake ikawa nzuri zaidi.
Yer 29:11, Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.*

Pengine Israel walipokuwa utumwani Babeli walilia ,wakizani wapo pekee yao,na kujua kuwa habari yao ndio mwisho utumwani.
Maana waliona k**a Mungu amewanyamazia...hata k**a kulikuwa na manabii Wa uongo wakitoa nabii zisizotimia.

Lakini Mungu kupitia nabii wake,anaawaambia yakuwa siku zenu za mwisho zitakuwa njema..maana yake, *Mungu alikuwa akiiandaa hatima ya kila mmoja wao*
Mungu anaandaa hatima yako.
"Trust God's process ,He is preparing your destiny for good."

▪️ *Kaa tayari kupokea*
"Get ready to receive"

Usitoke katika uwepo Wa Mungu kwa sababu ya kelele za watu,eti Mungu wako amenyamaza.
Kaa tayari kupokea uliyoyaomba.
"God is going to break that silent soon and with a big surprise to you"

Huu ndo mda Wa kumsikiliza Mungu kwa makini sana na ndo mda Wa kuendelea kuomba sana..
*Soma neno lake ,jifunze,tafakari neno lake*

*Yer 33:3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.*
Endeleea kuita,endelea kuomba atakujibu kwa majira yake.

Mungu akubariki. Uwe na mwanzo mwema Wa mwezi Julai 2020.

Imeandaliwa na Mtumishi Ditrick Milinga
Kutoka Sikari-Kitunda,DSM.

"Mlango haumfuati MTU ili apite ila MTU huufuata mlango"Kuna mambo hayata kusubiria uyapate maishani isipokuwa umeamua k...
24/09/2019

"Mlango haumfuati MTU ili apite ila MTU huufuata mlango"

Kuna mambo hayata kusubiria uyapate maishani isipokuwa umeamua kuyatafuta ,acha kukaa chini na kunung'unika inuka ukapambane....inuka ukatafute fursa...

Kumbuka fursa zinatafutwa na watu..sio fursa zinazotafuta watu...

Ezra 10:4...Inuka shughuli hiyo inakuhusu wewe....

Mungu akubariki uwe na siku njema.

By EV.Ditrick Milinga

Karibuni sana kwenye ibada zetu,ushauri wa neno LA Mungu na mambo mengine ya kijamii.
21/09/2019

Karibuni sana kwenye ibada zetu,ushauri wa neno LA Mungu na mambo mengine ya kijamii.

Address

Kitunda Machimbo
Dar Es Salaam
70563

Telephone

+255622485519

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when RAGT - Sikari posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to RAGT - Sikari:

Share