NENO la MUNGU

NENO la MUNGU Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from NENO la MUNGU, Church of God, janethkabota77@gmail. com, Dar es Salaam.

BWANA YESU ASIFIWE NAPENDA TUELEWE MAANA AU TAFSIRI YA MANENO YA BIBLIA TUKIANZA NA NENO•  Nzige.Jamii mbalimbali za pan...
12/04/2019

BWANA YESU ASIFIWE NAPENDA TUELEWE MAANA AU TAFSIRI YA MANENO YA BIBLIA TUKIANZA NA NENO• Nzige.
Jamii mbalimbali za panzi wanaohama katika makundi makubwa. Katika Sheria ya Musa, walionwa kuwa safi na wangeweza kuliwa. Makundi makubwa ya nzige yanayotafuna kila kitu kokote yanakopita na kusababisha uharibifu mkubwa, yalionwa kuwa pigo.—K*t 10:14; Mt 3:4.
O
• Omeri.
Kipimo cha vitu vikavu kilichokuwa sawa na lita 2.2, au sehemu moja ya kumi ya efa. (K*t 16:16, 18)—Angalia Nyongeza B14.
P
• Pakanga.
Vijiti vya mimea mbalimbali vyenye ladha chungu sana na harufu kali inayovutia. Pakanga hutumiwa kwa njia ya mfano katika Biblia kufafanua matokeo machungu ya uasherati, utumwa, ukosefu wa haki, na uasi imani. Katika Ufunuo 8:11, “pakanga” humaanisha kitu kichungu chenye sumu, kinachoitwa pia absinthe.—Kum 29:18; Met 5:4; Yer 9:15; Am 5:7.
• Paradiso.
Bustani maridadi, au shamba lililo k**a bustani. Paradiso ya kwanza ilikuwa Edeni, ambayo Yehova aliwatayarishia wanadamu wawili wa kwanza. Yesu alipokuwa akizungumza na mmoja wa wahalifu waliotundikwa kando yake kwenye mti wa mateso, alidokeza kwamba dunia itakuwa paradiso. Katika andiko la 2 Wakorintho 12:4, ni wazi kwamba neno hilo linarejelea paradiso ya wakati ujao, na katika Ufunuo 2:7, linarejelea paradiso ya kimbingu.—Wim 4:13; Lu 23:43.
• Pasaka.
Sherehe ya kila mwaka iliyofanywa siku ya 14 ya mwezi wa Abibu (baadaye mwezi huo uliitwa Nisani) ili kuadhimisha ukombozi wa Waisraeli kutoka Misri. Iliadhimishwa kwa kumchinja na kumchoma mwanakondoo (au mbuzi), na kumla kwa mboga chungu na mikate isiyo na chachu.—K*t 12:27; Yoh 6:4; 1Ko 5:7.
• Patakatifu Zaidi.
Chumba cha ndani zaidi katika hema la ibada na hekaluni, ambamo sanduku la agano liliwekwa; panaitwa pia Patakatifu pa Patakatifu. Mbali na Musa, ni kuhani mkuu peke yake aliyeruhusiwa kuingia Patakatifu Zaidi, naye angeweza kuingia humo siku moja tu katika Siku ya kila mwaka ya Kufunika Dhambi.—K*t 26:33; Law 16:2, 17; 1Fa 6:16; Ebr 9:3.
• Patakatifu.
Chumba cha kwanza kikubwa zaidi katika hema la ibada au katika hekalu, nacho ni tofauti na chumba cha ndani zaidi, yaani, Patakatifu Zaidi. Katika hema la ibada, Patakatifu palikuwa na kinara cha taa cha dhahabu, madhabahu ya uvumba ya dhahabu, meza ya mikate ya wonyesho, na vyombo vitakatifu; katika hekalu, mahali hapo palikuwa na madhabahu ya dhahabu, vinara kumi vya taa vya dhahabu, na meza kumi za mikate ya wonyesho. (K*t 26:33; Ebr 9:2)—Angalia Nyongeza B5 na B8.
• Pazia.
Kitambaa kilichofumwa kwa njia maridadi na kutariziwa kwa michoro ya makerubi ambacho kilitenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi katika hema la ibada na pia hekaluni. (K*t 26:31; 2Nya 3:14; Mt 27:51; Ebr 9:3)—Angalia Nyongeza B5.
• Pembe za madhabahu.
Sehemu zilizochomoza k**a pembe kwenye kona nne za madhabahu fulani. (Law 8:15; 1Fa 2:28)—Angalia Nyongeza B5 na B8.
• Pembe.
Neno hili linarejelea pembe za wanyama, ambazo zilitumiwa k**a vyombo vya kunywea, vyombo vya mafuta, vyombo vya wino na vipodozi, na ala za muziki au za kutoa ishara fulani. (1Sa 16:1, 13; 1Fa 1:39; Eze 9:2) “Pembe” hutumiwa mara nyingi kwa njia ya mfano kumaanisha nguvu na ushindi.—Kum 33:17; Mik 4:13; Zek 1:19.
• Pentekoste.
Sherehe ya pili kati ya sherehe tatu kuu ambazo wanaume wote Wayahudi walipaswa kusherehekea kule Yerusalemu. Neno Pentekoste, linalomaanisha “(Siku) ya Hamsini,” ndilo neno linalotumiwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo kurejelea Sherehe ya Mavuno au Sherehe ya Majuma inayotajwa katika Maandiko ya Kiebrania. Sherehe hiyo ilifanywa siku ya 50 kuanzia Nisani 16.—K*t 23:16; 34:22; Mdo 2:1.
• Pete ya muhuri.
Aina ya muhuri uliovaliwa kwenye kidole au kutiwa kwenye kamba, na huenda ulivaliwa shingoni. Pete hiyo ilikuwa ishara ya mamlaka ya mtawala au ofisa. (Mwa 41:42)—Tazama MUHURI.
• Pigo.
Katika Maandiko ya Kiebrania, kwa kawaida neno hili linamaanisha tauni, ugonjwa, au adhabu ya msiba kutoka kwa Yehova. Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo linamaanisha kupiga kwa kiboko au mjeledi wenye vifundo au ncha kali.—Hes 16:49;Yoh 19:1.
• Pima.
Kipimo cha urefu kinachotumiwa kupima kina cha maji, ni sawa na mita 1.8 (futi 6). (Mdo 27:28)—Angalia Nyongeza B14.
• Pimu.
Kipimo cha uzito na pia bei ambayo Wafilisti walitoza ili kunoa vifaa mbalimbali vya chuma. Mawe kadhaa ya kupimia uzito yaliyopatikana katika machimbo ya vitu vya kale katika nchi ya Israel yana konsonanti za kale za Kiebrania za neno “pimu”; kwa wastani yana uzito wa gramu 7.8, ambao ni karibu theluthi mbili za shekeli.—1Sa 13:20, 21.
• Porneia.—
Tazama UASHERATI.
• Purimu.
Sherehe ya kila mwaka iliyofanywa siku ya 14 na ya 15 katika mwezi wa Adari. Inaadhimishwa ili kukumbuka jinsi Wayahudi walivyokombolewa ili wasiangamizwe katika siku za Malkia Esta. Neno pu·rimʹ ambalo si la Kiebrania linamaanisha “kura.” Sherehe ya Purimu, au Sherehe ya Kura, iliitwa hivyo kwa sababu ya tendo la Hamani la kupiga Puri (Kura) ili kuamua siku ambayo angetekeleza njama yake ya kuwaangamiza Wayahudi.—Est 3:7; 9:26.
R
• Rahabu.
Jina linalotumiwa kwa njia ya mfano katika kitabu cha Ayubu, Zaburi, na Isaya (si mwanamke Rahabu anayetajwa katika kitabu cha Yoshua). Katika kitabu cha Ayubu, muktadha unafunua kwamba huyu Rahabu ni mnyama mkubwa sana wa baharini; katika maandiko mengine mnyama huyu mkubwa sana wa baharini anatumiwa kufananisha Misri.—Ayu 9:13; Zb 87:4; Isa 30:7; 51:9, 10.
• Rehani.
Kitu kinachomilikiwa na mkopaji ambacho anampa mkopeshaji ili kumhakikishia kwamba atalipa mkopo. Kitu hicho kiliitwa pia dhamana ya mkopo. Sheria ya Musa ilikuwa na maagizo yaliyohusu rehani ambayo yaliwalinda maskini na raia wa taifa hilo ambao hawakuwa na mtetezi.—K*t 22:26; Eze 18:7.
• Roho takatifu.
Kani ya utendaji isiyoonekana inayotumiwa na Mungu kutimiza mapenzi yake. Ni takatifu kwa sababu inatoka kwa Yehova, ambaye ni safi na mwadilifu kwa kiwango cha juu zaidi, na kwa sababu ndiyo njia anayotumia Mungu kutimiza mambo matakatifu.—Lu 1:35; Mdo 1:8.
• Roho waovu.
Viumbe waovu wa roho wasioonekana wenye nguvu zinazozidi za wanadamu. Kwa kuwa wanaitwa “wana wa Mungu wa kweli” katika Mwanzo 6:2 na “malaika” katika Yuda 6, hawakuumbwa wakiwa waovu; badala yake, walikuwa malaika waliojifanya wenyewe kuwa maadui wa Mungu kwa kutomtii katika siku za Noa na kujiunga na Shetani katika kumwasi Yehova.—Kum 32:17; Lu 8:30; Mdo 16:16; Yak 2:19.
• Roho.
Neno la Kiebrania ruʹach na neno la Kigiriki pneuʹma, ambayo kwa kawaida hutafsiriwa kuwa “roho” yana maana kadhaa. Yote mawili yanarejelea kitu ambacho macho ya wanadamu hayawezi kuona na huthibitisha kuwapo kwa nguvu inayotenda. Maneno hayo ya Kiebrania na Kigiriki hutumiwa kurejelea (1) upepo, (2) nguvu ya uhai inayotenda ndani ya viumbe walio duniani, (3) nguvu za msukumo zinazotoka katika moyo wa mfano na kumfanya mtu aseme na kutenda mambo kwa njia fulani, (4) maneno yaliyoongozwa na roho yanayotoka katika chanzo kisichoonekana, (5) Mungu na viumbe wa roho, na (6) nguvu za utendaji za Mungu, au roho takatifu.—K*t 35:21; Zb 104:29; Mt 12:43; Lu 11:13.
S
• Sabato.
Neno hili linatokana na neno la Kiebrania linalomaanisha “kupumzika; kukoma.” Ni siku ya saba katika juma la Kiyahudi (ilianza Ijumaa baada ya jua kutua mpaka Jumamosi baada ya jua kutua). Siku nyingine za sherehe katika mwaka ziliitwa pia siku za

23/03/2019

Bwana Yesu KRISTO Asifiwe wapendwa katika KRISTO.

Ujumbe:ITUNZE FAMILIA YAKO
===================
🔷Ndugu zangu NENO La KRISTO Linatuambia hivi
👇

Tusome 1TIMOTHEO 5:8

✔Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Ndugu zangu katika KRISTO

👉Kuwajali Watu Wa Nyumbani Mwako Ni Pamoja na Kuwajali, Kuwatimizia Mahitaji Yao.
Kuwalisha Kuwavika, Kuwasomesha, Kuwatunza Na Mambo Mengine k**a Hayo.

✔Hayo 👆Ni kwa ajili ya Kila Mmoja Anayeikiri IMANI ya Kikristo, Haijalishi Ni Mchungaji, Mtume, Nabii, Mwinjilisti, Askofu, Mwalimu, Shemasi,Mwambaji,Na Yeyote Yule Ni Jukumu lako wewe Kuwajali watu wa Nyumbani mwako.

▶Kuwa Mchungaji wa Kanisa Haiondoi Ubaba wako ndani ya Familia yako wewe; Inakupasa usimame Katika Zamu Yako k**a Baba wa Familia Kuwatunza Na Kuwajali Wana Familia yako.
Wewe K**a Baba au Mama wa Familia hivi Usipoitunza Familia yako, Usipowajali Watu wa Nyumbani mwako unategemea Nani Mwingine aje akutunzie watoto wako?.

👉Unashindwa Kuwatafutia watoto wako Chakula, Mavazi, Elimu Bora,wamechakaa Utafikiri Baba au Mama yao Haupo Tena Ulimwenguni.
Unaposhindwa Kuitunza Nyumba yako Yaani Familia yako Utawezaje Kulitunza KANISA LA KRISTO?
▶Watoto wenu wanaonekana k**a Mayatima Wakati Wazazi wao Bado mko Hai, Aibu gani hiyo Wapendwa?.

NENO linatuambia kwamba

Tusome 1TIMOTHEO 3:4-5

4 Mwenye Kuisimamia nyumba yake vema, Ajuaye kutiisha watoto katika Ustahivu;

5 (Yaani, Mtu asiyejua Kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

➡Wa Nyumbani Mwako Yaani Ile Familia ya Kimwili ambayo Mungu amekuwezesha Kuipata Yakupasa Kuitunza Na Kuisimamia Vema.
Inatia aibu Sana Unaitwa Mchungaji, Askofu, Nabii, Mtume.... Watoto wanaitwa wavuta Bangi...
Hujui K*tiisha watoto wako, Hivi kweli Utaweza Kuwatiisha Kondoo wa Malisho ya Mungu?.

👉Ifundishe Familia yako Katika Misingi bora na imara, Waleee Watoto wako Katika Njia Iwapsayo, Ambayo Hawataisahau kamwe hata wakiwa Wazee .
Wewe Baba Mtumishi wa Mungu Mtunze Mkewako, Watunze Watoto wako, Watunze Wazazi wako.... hao Ndio Wa Nyumbani Mwako.
Familia yako iwe Mfano wa Kuigwa na Wengine jamani.
Isiwe Unaitwa Mtumishi wa Mungu Lakini Familia yako Inatia Aibu.

👉Ni Jambo gumu sana Kukiona Kibanzi Katika Jicho la Mwenzako, wakati katika Jicho lako mwenyewe kuna Boriti.
Ni vigumu sana nakuambia.

👉Sio Kila Kitu Mtumishi Kanisa Unalolichunga Na Kulilisha, Kukutimizia Matakwa ya Familia yako yote, Mengine yakupasa Ujisimamie Wewe K**a Baba au Kiongozi wa Familia yako.
Watumishi wa Mungu Tukumbuke Kuzitunza Familia zetu, ziwe Mfano bora na wa Kuigwa.
Kanisa halitakusaidia mambo Yote ya Familia yako.

👉Usipowajali, Usipowatunza, Usipoisimamia Nyumba yako Vema, Wewe ni MBAYA Kuliko Hata Yule Ambaye Hajaamini NENO LA KRISTO.
Kumbuka wewe ni Baba au Mama wa Watoto, Mama au Baba Wa Familia, Unataka Nani Mwingine Aje akutunzie watoto wako?
Unataka nani aje akutunzie mkewako au Mumewako?.

▶Mpendwa Mtumishi wa Mungu Itunze, Uisimamie, Na Uijali Familia yako Vema, la sivyo Utakuja kuitwa Umeikana Imani

21/03/2019

KUMFAHAMU ROHO MTAKATIFU
saba za Mungu
Soma: Isa 11: 1-2
Roho hizi zimo ndani ya Roho Mtakatifu, Roho saba ni ukamilifu wa Roho Mtakatifu na zipo ndani ya kila aliyempokea Roho Mtakatifu. Tumekwisha jifunza kwa habari ya Roho ya Bwana na Roho ya maarifa na leo tunaendelea kujifunza juu ya Roho ya Ufahamu...
(C) Roho ya Ufahamu
Baada ya kupata maarifa ni lazima uyatendee kazi lakini huwezi kuyafanyia kazi k**a umekosa Roho ya Hekima, na kabla ya kufika katika utendaji unahitaji Roho ya Ufahamu maana ndiyo inayounganisha maarifa na Hekima.
Wapendwa wengi tunajua maandiko lakini tatizo letu ni kukosa Roho ya Ufahamu. Maangamizi kwa wakristo wengi yanatokana na kukosa ufahamu. Neno la Mungu ni Mungu mwenyewe na ni uhai, na Mungu hafanyi lolote mpaka Neno lake liende kwanza... Hivyo kabla ya kufanyia kazi Neno lake ni lazima uelewe kwanza. Ndio maana baada ya mtume Paulo kugundua kwamba wakolosai walikuwa wakitembea katika upendo wa kiroho yaani Upendo wa Mungu aliwaombea yafuatayo;
"Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;" KOL. 1:9
Mtume Paulo aliwaombea mambo makuu matatu, maarifa ya mapenzi ya Mungu, Hekima yote na ufahamu wa kiroho. Hizi ni Roho za muhimu sana kwa wakristo kuzielewa na kuhakikisha zinafanya kazi. Mpango wa Mungu ni kwamba sisi tukue katika ufahamu wa rohoni. Kila mtu ana mapenzi /matakwa yake binafsi lakini ukitaka kutembea na Mungu ni lazima ukubali kufanya anachotaka. Ukikosa Roho ya Ufahamu unaweza ukafanya mambo ukadhani ni mapenzi ya Mungu kumbe sio, unahitaji maarifa ya mapenzi ya Mungu katika Hekima yote na ufahamu wa rohoni.
Tazama jinsi ambavyo kukosa Roho ya Ufahamu hupelekea matatizo makubwa:
"Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe. Basi Wayahudi wakamnung’unikia, kwa sababu alisema, Mimi ni chakula kilichoshuka kutoka mbinguni."YN. 6:35‭, ‬41
Yesu aliongea maneno ya Rohoni lakini waliosikiliza kwa kukosa Roho ya Ufahamu walikwazika na kuanza kugombana.
" Basi watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia, walisema, Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia? Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima. "YN. 6:60‭, ‬63
Hata wanafunzi wake walikwazika kwa sababu ya kupokea maneno ya kiroho kwa jinsi ya kimwili. Kwa sababu ya maneno haya wengi wa wanafunzi wake walirudi nyuma.
“Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu. Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena." YN. 6:65‭-‬66
Ukitaka kuona watu wanakukimbia basi hubiri kweli, sikuzote kweli inauma ni mtu mwenye Roho ya Ufahamu tu ndiye anaweza kuelewa kweli inapohubiriwa. Chanzo cha migogoro mingi katika familia na mahusiano mengi ni kukosekana kwa maelewano.
"Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu; Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu."MIT. 10:13
Hekima hufanya kazi kwa mtu mwenye ufahamu, sikuzote asiye na ufahamu hufundishwa na kiboko cha ulimwengu. Kuna watu wanapitia shida nyingi sana kutokana na kukosa ufahamu, epuka matatizo kwa kutembea na Roho ya ufahamu

Address

Janethkabota77@gmail. Com
Dar Es Salaam

Telephone

+255687287273

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NENO la MUNGU posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category