12/04/2024
FAIDA ZA KIFO CHA YESU MSALABANI
Msalaba ni nini?
Msalaba ni adhabu ya kifo ya kutundikwa juu ya mti mpaka kufa na kila aliyeangikwa juu ya mti alilaniwa.
Kumbu 21:22-23 “ikiwa mtu ametenda dhambi impasayo kufa,akauawa,akauawa,nawe ukamtundika juu ya mti;mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti lazima utamzika siku iyo hiyo;kwani aliyetundikwa amelaniwa na Mungu asije akatia unajisi katika nchi yako akupayo BWANA Mungu wako,iwe urithi wako.
Agano Jipya
Msalaba ni nguvu ya MUNGU IOKOAYO.
1wakoritho 1:18 “Kwa sababu neno msalaba kwao wanaopotea ni Upuzi,bali kwetu sisi tunaokolewa ni nguvu ya Mungu.
Kwa hiyo thamani ya wokovu wetu imetokana na msalaba nje ya msalaba kusekuwa na wakovu
ZABURI 14:2,3,7 “Toka Mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu ,Aone k**a yuko mtu mwenye akili,Amtafutaye Mungu Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,Hakuna atendaye mema,La! Hata mmoja.Laiti wokovu wa Israeli utoke katika sayuni!BWANA atawarudisha wafungwa wa watu wake;Yakobo atashangilia, atafurahi.
Mathayo 27:45,46,50,51-53. “Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.Na k**a saa tisa,Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akasema,Eloi,Eloi,lama sabakthani?Yaani Mungu wangu ,mbona unaniacha?Naye Yesu akisha kupaza sauti tena kwa nguvu,akaitoa roho yake.Na tazama ,pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini,nchi ikatetemeka,miamba ikapasuka,makaburi yakafunuka;ikainuka miili mingi Ya watakatifu waliolala,nao wakiisha kutoka makaburini mwao,baada ya kufufuka kwake,wakaingia mji mtakatifu,wakawatokea wengi.
TUANGALIE FAIDA ZA KIFO CHA YESU MSALABANI
1:Msalaba ulilipa adhabu ya dhambi ya Mauti na Kutupatanisha na Mungu.
Mwanzo 3:9,24 ” Bwana Mungu akamwita Adamu,akamwambia uko wapi?Basi akamfukuza huyo mtu,akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni na upanga wa moto uliogeuka hukona huko kulinda njia ya mti wa uzima.
Kumbuka kila mmoja alipwasa kulipwa mauti k**a mshahara wa dhambi zetu.
Warumi 6:23 “kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti;bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Warumi 5:10 “kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake;zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.
Warumi 5:17 “Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja,zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema,na kile kipawa cha haki,watatawala katika uzima kwa yule mmoja,Yesu Kristo.
Zaburi 130:3-4 “BWANA k**a ungehesabu maovu,Ee Bwana,nani angesimama?Lakini kwako kuna msamaha ili wewe uogopwe.
Je bado kwenye maisha yako ni mauti ipi inayokusumbua wakati Yesu amerejesha uzima.
Somo litaendelea................................
Mwl. Samwel Wambura
Prayer &Deliverance Ministry Page
KMT- Tambani Msongora.
March,29,2024.