03/01/2020
FITINA
1.Wapenzi katika Kristo Yesu tumesikia habari ya neno hili katika maeneo yetu,pengeni hatukulipa uzito mkubwa kwa kutojua zaidi athali zake ndani maisha yetu,ndaƱi ya huduma na nafasi nyingine kwa ujumla wake,Kati ya mambo yanayo litesa kanisa sasa ni fitina.
2.Asilimia kubwa ya neno hili inatokana na wivu mbaya wenye uchungu.Kazi kubwa ya fitina ni kuleta mafarakano(faraka),kutokuelewana kati ya mtu kwa mtu,mtu na watu wengine.
3.Lengo uwa ni kuwafanya watu wasiwe na umoja WAFILIPI 2:5-8.
4.Jamani wawili wawezaje pita njia moja ikiwa hawakupatana?
5.Tukisema Mungu ni mmoja halafu hatupatani huo ni unafki wazi basi ni lazima yatokee,majivuno,mashindano kila mmoja akitaka mwenzake aone kuwa yeye ni zaidi
6.1WAKOR 11:17-18. 17Lakini ktk kuagiza haya ,siwasifu,ya kwamba mmekusanyika,si kwa faida bali kwa hasara
18.Kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu nami nusu nasadiki.
7.Mnajua kwann kuna faraka kanisani?
Hapa naomba niseme ukweli kwamba hili kundi la walokole lilijipenyeza ndani ya kanisa ili kutufarakanisha wakristo na ndiyo maana unaweza kuona kanisa limeandikwa Pentecost lakini ndani ni walokole,t.a.g lakini ndani walokole
8.WAFILIPI 1:15 Wengine wanahubiri habari za kristo kwa sababu ya husda na fitina;na wengine kwa nia njema.
By; Mwl Edward john