Holy Spirit Connect

Holy Spirit Connect Kujifunza Neno
Kukua Kiroho
Uhusiano na Roho Mtakatifu
Maombi

"Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako."Mwanzo 17:6Huku tukiwa t...
03/06/2026

"Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako."
Mwanzo 17:6

Huku tukiwa tunaendelea na maombi ya uzao wa tumbo, tumia mstari huu kukiri juu ya uzao wa tumbo lako.

Kiri mstari huu kwa imani, huku ukiamini kabisa kwa moyo wako wote kwamba mstari huu ni wako.

Jiambie mwenyewe huku ukiwa umeshika tumbo lako

"Mimi nimebarikiwa na Mungu. Mimi nina uzao mwingi sana, na wafalme watatoka katika uzao wa tumbo langu katika jina la Yesu Kristo."

Kiri mstari huu na maneno haya mara kwa mara, na hakika utarudi na shuhuda. Haleluya!!!!

Leo usikose maombi ya uzao wa tumbo live katika YouTube channel yetu ya Holy Spirit Connect kuanzia saa nne kamili usiku, karibu tuombe pamoja.

Mpendwa, Mungu anatenda, Mungu anabariki, Mungu anafungua matumbo ya watu. Haleluya!!!! Don't miss it!

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

SIKU YA TATU YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO 1. Omba Mungu anyooshe mkono wake aguse uzao wa tumbo lako. Tambua kwamba mkono ...
02/06/2026

SIKU YA TATU YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO

1. Omba Mungu anyooshe mkono wake aguse uzao wa tumbo lako.

Tambua kwamba mkono wa Bwana ni mkono wenye nguvu. Ni mkono unao tenda makuu. Mkono wa Bwana ukikugusa hutabaki k**a ulivyokuwa.

Mkono huu uligusa vipofu wakaona, uligusa viziwi wakasikia, uligusa waliokuwa hawawezi kupokea watoto wakapokea, uligusa wakoma wakatakasika.

"Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika."
Mathayo 8:3

Leo amini kwamba mkono huu ukikugusa hutobaki k**a ulivyokuwa. Mwambie Yesu leo akuguse kwa mkono wake katika uzao wa tumbo lako.

MAOMBI:
"Ee Bwana Yesu, asante kwa upendo wako kwangu. Ninajua Wewe ni Mungu mwenye nguvu. Nyosha mkono wako Bwana Yesu uguse uzao wa tumbo langu katika jina la Yesu Kristo. Amina."

2. Omba Bwana Yesu atende jambo jipya katika uzao wa tumbo lako.

"Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani."
Isaya 43:19

MAOMBI:
"Ee Bwana Yesu, ninakupenda sana. Ninaomba utende jambo jipya katika uzao wa tumbo langu katika jina la Yesu Kristo. Amina."

3. Utakemea na kuvunja kila mashambulizi ya ndoto ambayo yameathiri uzao wa tumbo lako kwa namna moja ama nyingine.

"Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli."
Yohana 8:36

- Labda unaota ndoto za kuingiliwa kimwili.
- Labda unaota ndoto unashambuliwa na wanyama wakali k**a nyoka, simba n.k
- Labda unalishwa vyakula kwenye ndoto na ukiamka tumbo linakuuma sana.

Kila aina ya mashambulizi ya ndoto ambayo yamekuathiri uzao wako kwa namna moja ama nyingine.

4. Utamshukuru Mungu kwa maombi haya ya siku tatu.

Utamshukuru Mungu kwa kujibu maombi yako. Utamshukuru Mungu kwa kukapa nguvu ya kufunga na kuomba.

Utamshukuru Mungu kwa kukupa kicheko.

Tutakuwa live saa nne kamili usiku katika YouTube channel yetu ya Holy Spirit Connect.

Kwa hiyo usikose, ni usiku wa baraka wa kumuona Bwana akitenda katika maisha yetu.

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

Usisahau kusubscribe YouTube Channel yetu ya Holy Spirit Connect ili kupata mafundisho na maombi. Link ipo kwenye bio yetu hapo juu.

02/06/2026

SIKU YA PILI YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO 02/06/2026 by Innocent Morris

Contacts: +255652796450 (WhatsApp)

Instagram Page: holyspiritconnect page: Holy Spirit Connect

Contact: +255652796450 (WhatsApp)

Instagram Link:

/

holyspiritconnect

Facebook Link:

/

holyspiritconnect

YouTube Link:

/ holyspiritconnect

Holy Spirit Connect

SIKU YA PILI YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO 1. Utafuta kila maneno mabaya uliyotamkiwa au uliyojitamkia. Kuna maneno mengi t...
01/06/2026

SIKU YA PILI YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO

1. Utafuta kila maneno mabaya uliyotamkiwa au uliyojitamkia.

Kuna maneno mengi tu ambayo umewahi kutamkiwa au kujitamkia na unaona kabisa yamekuathiri kwa namna moja ama nyingine.

-> Labda ulitamkiwa kwamba hutazaa.

-> Labda ulitamkiwa kwamba hutadumu kwenye ndoa.

-> Labda ulitamkiwa kwamba hutaolewa au hutaoa.

-> Labda ulitamkiwa watoto wako watakuwa wakuhangaika hangaika tu.

Leo yafute maneno hayo kwa damu ya Yesu Kristo.

MSTARI:
"Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa."
Isaya 7:7

2. Utavunja vizuizi vya kila aina katika kila eneo la uzao wa tumbo lako.

Tambua kwamba Mungu amekupa mamlaka ya kung'oa, na kubomoa, na kuharibu na kuangamiza; ili kujenga na kupanda.

"Angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa, na kuharibu, na kuangamiza; ili kujenga na kupanda."
Yeremia 1:10

-> Kila kizuizi kilicho kaa kwenye uzao wako ambacho kinazuia usipate ujauzito kivunjike katika jina la Yesu.

-> Kila kizuizi kinachoharibu mimba kiondoke katika jina la Yesu Kristo.

-> Kila kinacho haribu mfumo wako wa uzazi kiondoke kwa jina la Yesu Kristo.

Kila pando lililopandwa katika mfumo wako wa uzazi au katika uzao wako ling'oke katika jina la Yesu Kristo.

MSTARI:
"Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa."
Mathayo 15:13

Tutakuwa live saa nne kamili usiku katika YouTube channel yetu ya Holy Spirit Connect.

Kwa hiyo usikose, ni usiku wa baraka wa kumuona Bwana akitenda katika maisha yetu.

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

Usisahau kusubscribe YouTube Channel yetu ya Holy Spirit Connect ili kupata mafundisho na maombi. Link ipo kwenye bio yetu hapo juu.

Pia follow Instagram page yetu ya shuhuda inaitwa

01/06/2026

SIKU YA KWANZA YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO 01/06/2026 by Innocent Morris

Contacts: +255652796450 (WhatsApp)

Instagram Page: holyspiritconnect
page: Holy Spirit Connect

Contact: +255652796450 (WhatsApp)

Instagram Link:
/ holyspiritconnect

Facebook Link:
/ holyspiritconnect

YouTube Link:
/ holyspiritconnect
, , , , , , , ,

01/06/2026

MAOMBI YA MWEZI WA SITA (6) - Innocent Morris

SIKU YA KWANZA YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO Katika maombi ya leo  tutaombea maeneo mbalimbali na makundi mbalimbali ya wat...
31/05/2026

SIKU YA KWANZA YA MAOMBI YA UZAO WA TUMBO

Katika maombi ya leo  tutaombea maeneo mbalimbali na makundi mbalimbali ya watu.

1. TOBA
Tutaanza na toba kwa maana sisi ni wanadamu tunakosea. Unaweza kukuta kuna eneo ulikosea na likaathiri uzao wa tumbo lako kwa namna moja ama nyingine. Kwa hiyo tunahitaji kushughulika na maeneo haya kwa damu ya Yesu.

Utaomba
"Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu."
Zaburi 51:1

2. KICHEKO
Omba Mungu akupe kicheko, furaha na shangwe.

"Unifanye kusikia furaha na shangwe, Mifupa uliyoiponda ifurahi."
Zaburi 51:8

MAOMBI:
"Ee Bwana Yesu, unifanyie kicheko na kila atakaye sikia acheke pamoja nami katika jina la Yesu Kristo. Amina."

MSTARI:
"Sara akasema, Mungu amenifanyia kicheko; kila asikiaye atacheka pamoja nami."
Mwanzo 21:6

3. Omba Bwana akuangalie kwa jicho lake la upendo.

MSTARI:
"Naye Bwana akamwangalia Hana, naye akachukua mimba, akazaa watoto, wa kiume watatu na wa k**e wawili. Naye huyo mtoto Samweli akakua mbele za Bwana."
1 Samweli 2:21

MAOMBI:
"Ee Bwana Yesu Kristo, ninaomba uniangalie kwa jicho lako la upendo ukanipe kicheko katika maisha yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina."

UKIRI:
i) Kizazi changu kimebarikiwa.
Maana yake watoto wako na wajukuu wako, vitukuu vyako wote wamebarikiwa.

MSTARI:
"Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake. Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa."
Zaburi 112:1-2b

Wenye watoto utaombea watoto wako, afya zao, masomo yao n.k

Katika maombi ya live ya saa 4 kamili usiku katika YouTube channel yetu ya Holy Spirit Connect leo tutaombea maeneo mengi sana na tutatumia muda mwingi tu kuomba hapa nimeandika kidogo ili kila mtu apate muongozo wa kutumia katika maombi haya.

Kwa hiyo usikose, ni usiku wa baraka wa kumuona Bwana akitenda katika maisha yetu.

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

Usisahau kusubscribe YouTube Channel yetu ya Holy Spirit Connect ili kupata mafundisho na maombi. Link ipo kwenye bio yetu hapo juu.

Pia follow Instagram page yetu ya shuhuda inaitwa

SIMAMIA AHADI ZA MUNGU JUU YA UZAO WA TUMBO LAKOMungu ni Mungu wa ahadi, na ahadi zake ni za kweli na za kuaminika. Kuna...
31/05/2026

SIMAMIA AHADI ZA MUNGU JUU YA UZAO WA TUMBO LAKO

Mungu ni Mungu wa ahadi, na ahadi zake ni za kweli na za kuaminika. Kuna ahadi nyingi sana ambazo Mungu ameahidi juu ya uzao wa tumbo. Hivyo, tunapaswa kusimama juu ya ahadi hizo kwa imani na kuzikiri kwa vinywa vyetu.

Mungu anasema "Nami nitawaelekezea uso wangu, na kuwapa uzazi mwingi, na kuwaongeza."
Mambo ya Walawi 26:9

Mungu ameahidi kutupa uzazi mwingi, na ameahidi kutuongeza sana. Kwa hiyo na wewe unaweza kusimamia ahadi hii, na kukiri juu ya uzao wa tumbo lako kwa sauti na kwa imani. Huku ukiamini kabisa kwa moyo wako wote kwamba Mungu amekupa uzazi mwingi na kukuongeza.

Wakati mwingine hali za maisha zinaweza kuonekana kinyume na kile Mungu alichoahidi. Hata hivyo, imani ya kweli hushikilia ahadi za Mungu hata pale ambapo matokeo hayaonekani kwa macho. Hivyo ndivyo alivyofanya Ibrahimu. Aliamini ahadi ya Mungu kuhusu uzao wake licha ya hali yake ya kimwili kuonekana kutowezesha jambo hilo kutokea.

Biblia inasema

"Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao."
Kutoka 1:7

Na wewe jitamkie kwamba "Mimi nina uzazi mwingi sana, nami nitaongezeka sana, na kuzidi sana."

Usikate tamaa kwa sababu ya hali ya sasa. Endelea kuamini, kuomba, na kusimama juu ya ahadi za Mungu. Yeye aliyeahidi ni mwaminifu, na kwa wakati wake atalitenda neno lake.

MAOMBI:
"Ee Bwana Yesu, nakushukuru kwa ahadi zako za uzima na baraka. Ninaamini kwamba Wewe ni mwaminifu kutimiza kila neno ulilonena. Nisaidie kusimama katika imani na kutokata tamaa. Naomba uzao wenye baraka na ongezeko kulingana na mapenzi yako. Katika jina la Yesu, Amina."

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

MSTARI WANGU WA WIKI"Nami nitawaelekezea uso wangu, na kuwapa uzazi mwingi, na kuwaongeza; nami nitalithibitisha agano l...
31/05/2026

MSTARI WANGU WA WIKI

"Nami nitawaelekezea uso wangu, na kuwapa uzazi mwingi, na kuwaongeza; nami nitalithibitisha agano langu pamoja nanyi."
Mambo ya Walawi 26:9

Leo ni siku ya jumapili ambayo ipo maalum kwa ajili ya ile programu yetu ya kushika mstari moja katika wiki. Unachotakiwa kufanya leo ni kuandaa mstari wako alafu utauandika kwenye kikaratasi ambacho utatembea nacho kila sehemu ukiushika huo mstari na kuuweka kichwani na moyoni.

Pia utakuwa ukiukiri huo mstari wako kwa sauti utakapo amka asubuhi nausiku utakapo taka kulala, unaweza kuukiri pia wakati wowote utakao taka. Kukiri neno la Mungu kutaleta matokeo makubwa sana katika maisha yako.

Usiwasahau watoto wako wa andikie mstari wao na uwe unakiri nao kila jioni mnapo kuwa pamoja. Hii itajenga kitu kikubwa sana katika familia yako. Hata k**a hawawezi kusoma basi jitahidi kuwasomea. Pia k**a una mume/mke au mpenzi mnaweza kuwa na mstari mmoja na mkawa mnapata muda ambao mtakuwa mkiukiri huu mstari kwa pamoja na kuurudia rudia. Itajenga kitu cha msingi sana katika uhusiano wenu. Uhusiano wenu unajengwa na msingi wa neno la Mungu. Jenga moyo wako na familia yako katika msingi wa neno la Kristo. Moyo wako na familia yako itakuwa imara siku zote.

K**a utaupenda mstari ambao mimi nitautumia huo hapo juu unaweza kuutumia pia. Lakini k**a utakuwa na mstari wako umeandaa itakuwa ni jambo njema sana ukishare na sisi hapa ili k**a mtu akiupenda mstari wako aweze kuutumia katika wiki hii.

"Maana ni vizuri kuyahifadhi ndani yako, hali yakithibitika pamoja midomoni mwako."
Mithali 22:18

Mpendwa, ukimpenda Mungu utalishika neno lake na Mungu atakupenda. Na Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu watakuja kufanya makazi ndani yako.

"Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake."
Yohana 14:23

Hii programu ni kwa ajili ya kujaza neno la Mungu ndani ya mioyo yetu na katika akili zetu na kulitendea kazi neno lake.

Unaweza kushare na watu wengine programu hii.

Ubarikiwe sana

Innocent Morris
+255652796450 (Whatsapp)

Page yetu ya shuhuda

NGUVU YA MAOMBI KATIKA UZAO WA TUMBOMaombi yana nguvu sana ya kufungua milango ya baraka katika uzao wa tumbo k**a tukio...
30/05/2026

NGUVU YA MAOMBI KATIKA UZAO WA TUMBO

Maombi yana nguvu sana ya kufungua milango ya baraka katika uzao wa tumbo k**a tukiomba katika Roho.

Katika Biblia wapo wengi walioomba au kuliliwa mbele za Mungu kuhusu uzao wa tumbo, na Mungu akafungua milango ya baraka ya watoto.

Mfano:

i) Hana
Huyu Hana alikuwa tasa kwa muda mrefu, akaomba kwa uchungu mbele za Mungu, huku akimlilia Mungu sana 😭😭😭 na kuweka nadhiri mbele za Bwana. Alimimina moyo wake kwa Bwana kwa imani.

"Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba Bwana akalia sana."
1 Samweli 1:10

Ndipo Mungu akampa mtoto aitwaye Samweli. Haleluya!

"Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana."
1 Samweli 1:20

Hakika Mungu anasikia maombi k**a tukiomba kwa kumaanisha, k**a tukiomba kwa imani, k**a tukiomba kwa Roho.

K**a Mungu alisikia maombi ya Hana na akatenda, atatenda na kwako pia.

Mfano mwingine ni Raheli. Raheli alimlilia Mungu kuhusu watoto, na Mungu akafungua tumbo lake akamzaa Yusufu.

"Mungu akamkumbuka Raheli; MUNGU AKAMSIKIA, akamfungua tumbo."
Mwanzo 30:22

Raheli hakuchoka kuomba, aliendelea kuomba na kuomba, Biblia inasema Mungu akamkumbuka Raheli, Mungu akamsikia, akamfungua tumbo. Haleluya.

Mfano mwingine ni Rebeka, Biblia inasema Isaka alimwombea mkewe kwa sababu alikuwa tasa, na Mungu akajibu maombi yake.

"Isaka AKAMWOMBA Bwana KWA AJILI YA MKE WAKE, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba."
Mwanzo 25:21

Isaka alibeba hitaji hili kuomba kwa ajili ya mke wake, aliomba kwa mzigo na Mungu akatenda.

Kuna nguvu katika maombi tunapoomba kwa imani na kwa moyo wa kweli. Mungu husikia na hutenda. Amini kwamba Mungu anasikia na hutenda, naye atakutendea na wewe. Haleluya.

Ubarikiwe sana.

Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)

Usikose maombi ya kufunga na kuomba kwa ajili ya uzao wa tumbo kuanzia tarehe 1 mpaka 3 mwezi wa sita na kila siku ya mfungo tutakuwa live tukiomba pamoja katika YouTube Channel yetu ya Holy Spirit Connect kuanzia saa nne kamili usiku.

Address

P. O. Box 65409
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Holy Spirit Connect posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share