29/07/2026
ROHO MTAKATIFU ATAKUWA PAMOJA NAWE KATIKA SHIDA KUKUSAIDIA
Yesu ameahidi anasema "Sitawaacha ninyi yatima."
(Yohana 14:18), bali "Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele." (Yohana 14:16).
Roho Mtakatifu ni Msaidizi wetu, yupo pamoja na wewe katika kila hali. Kwenye raha yupo pamoja na wewe, kwenye shida yupo pamoja na wewe.
Mungu anasema "Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza."
Isaya 43:2
Hata ukiwa katika moto, Yeye atakuwa pamoja nawe hata kuacha. Hata k**a unajihisi uko peke yako, tambua kwamba Roho Mtakatifu yupo pamoja nawe.
Shadraka, Meshaki na Abednego walitupwa katika tanuru la moto, lakini Bwana hakuwaacha. Bwana alikuwa pamoja nao (Danieli 3:19). Haijalishi adui atakutupa katika tanuru gani la moto, Roho Mtakatifu hatakuacha; atakuwa pamoja nawe kwa maana Yeye ni Msaidizi wetu.
Roho Mtakatifu atakusaidia hadi ufike pale ambapo Mungu anataka ufike. Wakati wa shida atakupa furaha, atakupa amani na atakupa utulivu.
Tunahitaji tuwe karibu sana na Roho Mtakatifu ili aweze kutusaidia katika kila eneo la maisha yetu. Tunaposhindwa tumwambie Yeye, kwamba Roho Mtakatifu hapa siwezi kwa nguvu zangu, nisaidie, naye atakusaidia.
K**a kuna eneo unajiona ni dhaifu, mwambie Roho Mtakatifu, kwamba Roho Mtakatifu katika eneo hili, mimi ni dhaifu, naye atakusaidia. Atakupa nguvu ya kushinda udhaifu huo.
Ni ngumu sana kuishi maisha ya ukristo pasipo Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu ndiye atakayetuwezesha kuishi maisha ya utakatifu na uaminifu. Roho Mtakatifu ndiye atupaye nguvu za kushinda kila changamoto ambazo mkristo anakutana nazo.
Tunatakiwa tujiachilia kwa Roho Mtakatifu. Tunatakiwa tuwe karibu naye kuliko kitu kingine chochote duniani. Roho Mtakatifu akawe furaha yetu, Roho Mtakatifu akawe tumaini letu, Roho Mtakatifu akawe kila kitu kwetu.
MAOMBI:
"Ee Roho Mtakatifu, ninakupenda sana. Wewe ndio kimbilio langu na msaada wangu. Unishike mkono pale ninaposhindwa, unitie nguvu pale nilipo dhaifu. Unipe amani pale ninapokosa amani, unipe utulivu pale ninapokosa utulivu katika jina la Yesu Kristo. Amina"
Ubarikiwe sana.
Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)