30/05/2026
NGUVU YA MAOMBI KATIKA UZAO WA TUMBO
Maombi yana nguvu sana ya kufungua milango ya baraka katika uzao wa tumbo k**a tukiomba katika Roho.
Katika Biblia wapo wengi walioomba au kuliliwa mbele za Mungu kuhusu uzao wa tumbo, na Mungu akafungua milango ya baraka ya watoto.
Mfano:
i) Hana
Huyu Hana alikuwa tasa kwa muda mrefu, akaomba kwa uchungu mbele za Mungu, huku akimlilia Mungu sana 😭😭😭 na kuweka nadhiri mbele za Bwana. Alimimina moyo wake kwa Bwana kwa imani.
"Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni mwake, akamwomba Bwana akalia sana."
1 Samweli 1:10
Ndipo Mungu akampa mtoto aitwaye Samweli. Haleluya!
"Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba kwa Bwana."
1 Samweli 1:20
Hakika Mungu anasikia maombi k**a tukiomba kwa kumaanisha, k**a tukiomba kwa imani, k**a tukiomba kwa Roho.
K**a Mungu alisikia maombi ya Hana na akatenda, atatenda na kwako pia.
Mfano mwingine ni Raheli. Raheli alimlilia Mungu kuhusu watoto, na Mungu akafungua tumbo lake akamzaa Yusufu.
"Mungu akamkumbuka Raheli; MUNGU AKAMSIKIA, akamfungua tumbo."
Mwanzo 30:22
Raheli hakuchoka kuomba, aliendelea kuomba na kuomba, Biblia inasema Mungu akamkumbuka Raheli, Mungu akamsikia, akamfungua tumbo. Haleluya.
Mfano mwingine ni Rebeka, Biblia inasema Isaka alimwombea mkewe kwa sababu alikuwa tasa, na Mungu akajibu maombi yake.
"Isaka AKAMWOMBA Bwana KWA AJILI YA MKE WAKE, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba."
Mwanzo 25:21
Isaka alibeba hitaji hili kuomba kwa ajili ya mke wake, aliomba kwa mzigo na Mungu akatenda.
Kuna nguvu katika maombi tunapoomba kwa imani na kwa moyo wa kweli. Mungu husikia na hutenda. Amini kwamba Mungu anasikia na hutenda, naye atakutendea na wewe. Haleluya.
Ubarikiwe sana.
Innocent Morris
+255652796450 (WhatsApp)
Usikose maombi ya kufunga na kuomba kwa ajili ya uzao wa tumbo kuanzia tarehe 1 mpaka 3 mwezi wa sita na kila siku ya mfungo tutakuwa live tukiomba pamoja katika YouTube Channel yetu ya Holy Spirit Connect kuanzia saa nne kamili usiku.