Valley of Life Church

Valley of Life Church Raising an Army of Soul-winning Believers

03/08/2026
SOMO: FAHAMU NAMNA MUNGU ANAVYOTAJIRISHA WATU WAKEI. UTANGULIZITunamuabudu na kumtumikia Mungu tajiri. Vyote ambavyo una...
11/07/2026

SOMO: FAHAMU NAMNA MUNGU ANAVYOTAJIRISHA WATU WAKE

I. UTANGULIZI
Tunamuabudu na kumtumikia Mungu tajiri. Vyote ambavyo unaviona na usivyoviona ambavyo ni utajiri ni mali yake
- Hagai 2:8, Zaburi 24:1

Kupitia wokovu tunaunganishwa na utajiri wa Mungu na kufanyika wana - warithi pamoja na Kristo Yesu
- Warumi 8:16-17,
- 2 Wakorintho 8:9

Fahamu kwamba, MUNGU AMEKUKUSUDIA WEWE UWE TAJIRI, ikiwa bado umekumbatia umaskini, basi wewe ndiye umeamua hivyo.

II. NAMNA GANI MUNGU HUTAJIRISHA WATU WAKE?
Mungu ana njia zake ambazo huzitumia kuwaungamanisha watu wake na utajiri wake hapa duniani.
- Isaya 55:8-11.

Unachotakiwa sio kupingana na njia hizo, au kujiwekea mikakati ya kibinadamu, bali:
1. Tafuta kujua njia za Mungu (Zaburi 25:4-5)
2. Jinyenyekeze ukubali Mungu akuongoze (Zaburi 25:9)
3. kuwa mwaminifu kuzifuata njia za Mungu (Isaya 1:19-20, Yoshua 1:8)

Hizi hapa ni njia ambazo Mungu anatumia kutajirisha na kustawisha watu wake:

1.Anakupa maono ya utajiri mkuu
- maono hukufaya kujiona tajiri k**a Mungu anavyokuona
- maono hukupa msukumo wa kuanzisha jambo la kiuchumi

Mwanzo 12:2
- "nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki (kukutajirisha) na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;"

2.Anakubariki ili uwe tajiri
- Baraka yoyote unayopata ni mbegu ya kukutajirisha
- baraka inaweza kuwa elimu, ujuzi, nguvu, kazi, biashara, watu, n.k

Mithali 10:22
- "Baraka ya BWANA hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo."

3.Anakupa nguvu ya kupata utajiri (uweza wa kutengeneza utajiri)
- utajiri haupatikani kwa matamanio, unapatikana kwa nguvu za kiroho (3 Yohana 1:2)
- nguvu inaweza kuwa maono, ujuzi, ubunifu, elimu, n.k-

Kumbukumbu la Torati 8:18
- "Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana *ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri;* ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, k**a hivi leo"

4.Anakufundisha na kukuongoza katika njia za kupata utajiri (namna ya kufanya ili uwe tajiri)
- utajiri unazo njia zake. Kwa lugha rahisi utajiri una kanuni zake. *Mungu hukufundisha kuzijua kanuni zake za utajiri* (Yoshua 1:8).
- Mfano wa kanuni hizo ni: utumishi, utoaji, kazi, bidii, n.k

Isaya 48:17
- "BWANA, mkombozi wako,... asema hivi; Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.

5.Ameachilia neema maalumu ya kukutajirisha.
- neema ni uwezesho wa kiungu ndani Yako unaokupa uweza wa kufanya mambo kwa namna ya kiungu.

2 Wakorintho 8:9
- "Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake".

6. Anakupa fursa ya kumtumikia ili kuungamanika na utajiri wake
- Kutoka 23:25-26.

Kila fursa ya kumtumikia Mungu ni fursa ya kuungamanika na utajiri wa kiungu,
- utumishi unabariki, baraka hutajirisha
- utajiri hugusa na kufunua moyo wa Mungu, moyo wa Mungu una Siri za mafanikio na utajiri
- n.k

III. MAMBO YA KUZINGATIA
Hivyo, fahamu kwamba:
- utajiri sio dhambi, dhambi ni kutumia njia za kishetani kujitafutia mali na utajiri.
- utajiri sio dhambi, dhambi ni kuufanya utajiri kuwa Mungu wako

UTAJIRI AU UMASKINI: UCHAGUZI NI WAKO
Licha ya kwamba Mungu amekuwekea vyote vinavyohitajika ili uwe tajiri, lakini kuwa tajiri ni hiari na uchaguzi wako mwenyewe.

Mungu anataka na anakushauri uchague kuwa tajiri: wewe na uzao wako
- Kumbukumbu la Torati 30:19.

Ukichagua kupata utajiri wa Kiungu, sharti:
- ukubali njia na maelekezo ya Mungu,
- utii na kutatendea KAZI k**a alivyoelekeza (Yoshua 1:8, Kumbukumbu la Torati 28:1-14)

IV. OMBI MAALUMU
- Baba, naomba neema maalumu ya kuniwezesha kuchukua hatua, kulipa gharama zinazohitajika kuufikia Utajiri ambao umeweka mbele yangu katika jina la Yesu Kristo (Mwanzo 4:1-7).

UBARIKIWE SANA. NAKUONA UKIPAA JUU KATIKA JINA LA YESU KRISTO.

Valley of Life Church

ELEWA DHANA YA KUFUNGA NA KUOMBAValley of Life Church 1.Maana ya KufungaKufunga ni tendo la kujizuia kula na/au kunywa k...
07/07/2026

ELEWA DHANA YA KUFUNGA NA KUOMBA
Valley of Life Church

1.Maana ya Kufunga
Kufunga ni tendo la kujizuia kula na/au kunywa kwa muda fulani kwa ajili ya kutafuta uso wa Mungu kwa maombi na ibada. Kufunga ni tendo la kiroho linalosaidia mtu kumkaribia Mungu kwa kujinyima mambo ya mwili na kujikita katika mambo ya kiroho. Katika Biblia, kufunga kunaambatana na maombi, toba, unyenyekevu, na kutafuta mwongozo wa Mungu.

2. Kwa nini Tunafunga?
Kufunga kuna sababu mbalimbali za kiroho, ikiwa ni pamoja na:

i. Kutafuta Uso wa Mungu (Yeremia 29:13) – Kufunga huongeza ukaribu na Mungu kwa kuomba na kumtafuta kwa bidii.

ii. Kutubu na Kuomba Msamaha wa Dhambi (Yona 3:5-10) – Wananchi wa Ninawi walifunga na Mungu akawaonea huruma.

iii. Kupata Ukombozi na Ushindi wa Kiroho (Isaya 58:6) – Kufunga huvunja nira za utumwa wa kiroho na kuleta uhuru.

iv. Kupata Maelekezo na Hekima ya Mungu (Ezra 8:21-23) – Ezra na watu wake walifunga ili kupata mwongozo wa Mungu.

v. Kuomba Uponyaji (2 Samweli 12:16) – Daudi alifunga na kuomba Mungu amponye mtoto wake.

vi. Kuimarisha Maombi (Mathayo 17:21) – Yesu alisema kuwa kuna mapepo yanayotoka kwa kufunga na kuomba.

vii. Kuomba Ulinzi wa Mungu (2 Mambo ya Nyakati 20:3-4) – Mfalme Yehoshafati alitangaza kufunga kwa taifa ili kuomba ulinzi wa Mungu.

vii. Kujitakasa na Kujiandaa kwa Huduma (Mathayo 4:1-2) – Yesu alifunga siku 40 kabla ya kuanza huduma yake.

3. Namna ya Kufunga kwa Ufanisi
Ili kufunga kwa ufanisi, mtu anapaswa kufuata hatua zifuatazo:

i. Kuwa na Kusudi Laini la Kiroho – Usifunge bila lengo, jua unataka Mungu afanye nini kupitia mfungo huo.

ii. Tubu na Jitakase – Usifunge ukiwa na dhambi, bali tubu kwanza ili mfungo wako uwe na matokeo (Isaya 59:1-2).

iii. Omba na Kusoma Neno la Mungu – Hakikisha unatumia muda mwingi kuomba na kusoma Biblia (Yoshua 1:8).

iv. Epuka Mazingira Yanayokufanya Ulegee – Jiepushe na mambo yatakayokusababishia kushindwa kufanikisha mfungo wako.

v. Kuwa na Mpango wa Kiroho – Panga muda wa maombi, ibada, na kutafakari Neno la Mungu.

vi. Endelea Kuwa na Imani – Amini kuwa Mungu anasikia na atajibu maombi yako.

vii. Vunja Mfungo kwa Hekima – Usianze kula chakula kingi kwa ghafla baada ya mfungo, anza taratibu.

4. Adui wa Mfungo
Kuna mambo yanayoweza kudhoofisha au kuharibu mfungo, k**a vile:

i. Kufunga Bila Kusudi la Kiroho – Kufunga tu kwa desturi bila kusudi la kweli.

ii. Dhambi na Kutotubu – Mungu hashughulikii maombi ya wenye dhambi wasiotubu (Isaya 59:2).

iii. Kuwaza Sana Chakula – Kuwaza chakula badala ya kuzingatia maombi na Neno la Mungu.

iv. Kujihusisha na Mambo ya Dunia – Kupoteza muda kwa mambo yasiyo ya kiroho wakati wa mfungo.

v. Kukata Tamaa Mapema – Kufikiri Mungu hajibu haraka na kuacha mfungo kabla ya muda wake.

vi. Majivuno na Kujionyesha – Kufunga kwa ajili ya kuonekana na watu badala ya kumridhisha Mungu (Mathayo 6:16-18).

5. Aina za Mfungo

i. Mfungo wa Kawaida – Kujizuia kula chakula lakini kunywa maji (Mathayo 4:2).

ii. Mfungo Kamili – Kujizuia kula na kunywa kabisa kwa muda fulani (Esta 4:16, Mambo ya Walawi 23:27).

iii. Mfungo usio kamili (Mfungo wa Danieli) – Kula vyakula rahisi na kujizuia vyakula vilivyotengenezwa (Danieli 10:2-3).

iv. Mfungo wa Saa Fulani – Kufunga kwa muda maalum wa siku k**a kuanzia saa 6 asubuhi hadi jioni.

v. Mfungo wa Maisha – Kujizuia na baadhi ya vyakula au mambo fulani kwa maisha yote kwa ajili ya Mungu (Waamuzi 13:4-5).

6. Mifano ya Kufunga katika Biblia

i. Musa – Alifunga siku 40 na alipokea Amri Kumi (Kutoka 34:28).

ii. Daudi – Alifunga kwa ajili ya toba na maombi (2 Samweli 12:16).

iii. Esta – Alitangaza mfungo wa siku 3 kwa taifa la Israeli (Esta 4:16).

iv. Danieli – Alifunga na akaepuka chakula chenye ladha nzuri kwa siku 21 (Danieli 10:2-3).

v. Yesu Kristo – Alifunga siku 40 jangwani kabla ya kuanza huduma yake (Mathayo 4:1-2).

vi. Kanisa la Kwanza – Walifunga na kuomba kabla ya kufanya maamuzi makubwa (Matendo 13:2-3).

Hitimisho

Kufunga ni zana muhimu ya kiroho kwa Mkristo yeyote anayetaka kupata ushindi wa kiroho, mwongozo wa Mungu, uponyaji, na upako wa kipekee. Kufunga kwa bidii na kwa njia sahihi huleta mabadiliko makubwa ya kiroho na ushindi katika maisha ya waumini.

SOMO: UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YA MPANGILIOValley of Life Church 1. UtanguliziTunamuabudu na kumtumikia Mungu wa mpangil...
21/06/2026

SOMO: UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YA MPANGILIO
Valley of Life Church

1. Utangulizi
Tunamuabudu na kumtumikia Mungu wa mpangilio, anaamini na kutenda mambo yake kwa mpangilio (Mwanzo 1:1-31)

Kuishi kwa mpangilio ni msingi wa:
- mafanikio,
- amani,
- ukuaji, na
- kutimiza kusudi la Mungu katika maisha.

Mungu ni Mungu wa utaratibu, na anapenda watoto wake waishi kwa nidhamu na hekima.

1 Wakorintho 14:40
- “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.”

II. MAENEO YA KUJIPANGILIA

1. Pangilia Maisha Yako ya Kiroho
Maisha ya kiroho yasipokuwa na mpangilio huwa dhaifu na yasiyo na mwelekeo. Mkristo anatakiwa kuwa na ratiba na nidhamu ya kiroho.

(a) Uhudhuriaji wa Ibada
- Ikiwa kwenye ratiba Yako hupangi Mungu wa kumuabudu Mungu, maisha yako yatakosa mpangilio.
- Kuwa mwaminifu katika kushiriki ibada, mafundisho, na ushirika wa waamini. Kutokukusanyika huondoa nguvu za kiroho.

Waebrania 10:25
- “Wala tusiache kukusanyika pamoja…”

(b) Usomaji wa Neno la Mungu
- Panga muda wa kusoma na kutafakari Neno kila siku. Neno la Mungu huleta mwongozo, imani, na ukuaji wa kiroho.

Yoshua 1:8
- “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako…”

(c) Maisha ya Maombi
Mwombaji ni mtu mwenye nguvu kiroho. Panga muda wa maombi binafsi, maombi ya familia, na maombi ya kufunga.

1 Wathesalonike 5:17
- “Ombeni bila kukoma.”

(d) Maisha ya Utakatifu
Pangilia mwenendo wako, mazungumzo yako, mavazi yako, na maamuzi yako ili yawe ya kumpendeza Mungu.

1 Petro 1:15-16
- “Iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.”

2. Pangilia Maisha Yako ya Kijamii

Watu wanaokuzunguka wana mchango mkubwa katika maisha yako. Mahusiano yasiyo sahihi yanaweza kuharibu kusudi lako.

(a) Chagua Marafiki Vizuri

Jiulize:
- Nani ni rafiki yangu?
- Ana mchango gani katika maisha yangu?
- Ananijenga au ananibomoa?

Mithali 13:20
- “Aendaye na wenye hekima atakuwa mwenye hekima.”

(b) Pangilia Mazungumzo Yako

Sio kila mtu anatakiwa kujua siri zako, mipango yako, au udhaifu wako.

Mithali 17:27
- "Mwenye maarifa hujizuia katika maneno yake.”

(c) Chagua Wanaokushauri.
Ushauri mbaya huharibu maisha mazuri. Tafuta watu wenye hekima, hofu ya Mungu, na ushuhuda mzuri.

Mithali 11:14
- “Penye mashauri mengi pana usalama.”

3. Pangilia Maisha Yako ya Uchumi
Fedha zisipokuwa na mpangilio huleta madeni, migogoro, na maisha ya shida hata kwa mwenye kipato kizuri.

(a) Pangilia Utoaji
Jifunze kutoa zaka, sadaka, na kusaidia kazi ya Mungu kwa uaminifu.

Malaki 3:10
- “Leteni zaka kamili ghalani…”

(b) Pangilia Matumizi ya Fedha
Usitumie fedha bila mpango. Tofautisha kati ya mahitaji na tamaa.

Luka 14:28
- “Ndiye yupi katika ninyi akitaka kujenga mnara asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama?”

(c) Weka Mipango ya Kifedha
Kuwa na:
- Bajeti
- akiba
- Malengo ya maendeleo
- Nidhamu ya matumizi

Mithali 21:20
- “Katika nyumba ya mwenye hekima mna hazina ya thamani…”

(d) Epuka Ubadhirifu na Madeni Yasiyo ya Lazima
Maisha ya kuiga wengine huleta matatizo ya kifedha. Ishi kulingana na uwezo wako.

Warumi 13:8
- “Msiwiwe na deni lo lote…”

4. Pangilia Muda Wako

Muda ni maisha. Watu wengi hupoteza miaka yao kwa kukosa mpangilio wa muda.
- Panga ratiba yako
- Tambua vipaumbele
- Epuka uvivu

Tumia muda kwa mambo yenye faida

Waefeso 5:15-16
- “Mkiukomboa wakati…”

III. Hitimisho
Kuishi kwa mpangilio ni ishara ya hekima, ukomavu, na uwajibikaji. Pangilia:
- Maisha yako ya kiroho
- Mahusiano yako
- Fedha zako
- Muda wako
- Malengo yako

Mpangilio huleta amani, maendeleo, heshima, na baraka za Mungu.

Maombi
“Bwana, nifundishe kuishi kwa nidhamu, hekima, na mpangilio katika kila eneo la maisha yangu ili nitimize kusudi lako. Amina.”

UBARIKIWE

HAPPY FATHER'S DAY TO THE MAN OF GOD, OUR SPIRITUAL FATHER, MENTOR AND LEAER APOSTLE DR. Robert Boniface Israel
21/06/2026

HAPPY FATHER'S DAY TO THE MAN OF GOD, OUR SPIRITUAL FATHER, MENTOR AND LEAER APOSTLE DR. Robert Boniface Israel

SOMO: KUUMBWA UPYA.... SEHEMU YA PILI: MAMBO YA KALE YAMEPITA, Valley of Life Church Andiko Kuu: 2 Wakorintho 5:17- "Hat...
07/06/2026

SOMO: KUUMBWA UPYA.... SEHEMU YA PILI: MAMBO YA KALE YAMEPITA, Valley of Life Church

Andiko Kuu: 2 Wakorintho 5:17
- "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya."

I. UTANGULIZI
Moja ya ushahidi mkubwa wa kuumbwa upya ni kuachana na maisha ya kale. Mtume Paulo anasema wazi kwamba mtu akiwa ndani ya Kristo, mambo ya kale yamepita.

Hii ina maana kwamba Mungu hajatuita kubeba maisha ya zamani pamoja na maisha mapya kwa pamoja, bali kuishi maisha mapya katika uhalisia wa kile alichotufanya kuwa ndani ya Kristo.

Watu wengi wameokoka, lakini bado wanaendelea kuongozwa na kumbukumbu za jana, yaani:
- majeraha ya zamani,
- dhambi za zamani,
- hofu za zamani, na
- mtazamo wa zamani.

Mungu anataka tuache yaliyopita ili tuweze kuingia kikamilifu katika maisha mapya aliyotuandalia.

Isaya 43:18-19
- [18] Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani

- [19] Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.

II. MAMBO YA KALE YANAYOPASWA KIPITA

1.Maisha ya Dhambi

Warumi 6:14
- "Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi..."

Muumini mpya hapaswi kuendelea kuishi chini ya utawala wa dhambi. Neema ya Mungu hutuwezesha kushinda dhambi na kuishi maisha ya utakatifu.
- 1 Yohana 5:4-5

2.Hofu na Mashaka

2 Timotheo 1:7
- "Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya ujasiri...."

Mambo ya kale yanajumuisha hofu, kukata tamaa, na mashaka. Ndani ya Kristo tumepokea ujasiri, nguvu, na imani.
- Warumi 8:1-2

3.Utambulisho wa Zamani

Wagalatia 3:26
- "Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu."

Hatupaswi kujitambulisha kwa utambulisho WA kale wa maisha na uliyokuwa nayo kabla ya wokovu:
- hali kushindwa kwetu,
- historia yetu, au
- mazingira yetu.
Sasa sisi ni watoto wa Mungu na tunao utambulisho mpya katika Kristo:
- sisi ni washindi na zaidi ya kushinda
- sisi tuko ndani ya Kristo
- sisi tumesamewa dhambi hivyo ni wenye haki wa Mungu
- n.k

4.Chuki, Uchungu na Kutokusamehe

Waefeso 4:31-32

Muamini aliyeumbwa upya anapaswa kuachilia uchungu, hasira, na kinyongo, na kujifunza kusamehe k**a Kristo alivyotusamehe.

5.Njia za kufikiri za kale

Warumi 12:2

Mabadiliko ya kweli huanza katika akili. Mungu anatutaka tufanywe wapya katika fikra zetu ili tuweze kutambua mapenzi yake mema na makamilifu. Tuondokane na fikira na mtazamo wa kale, tuwe na mtazamo na fikira mpya.

KWA NINI LAZIMA TUACHE MAMBO YA KALE

1. Mambo ya kale yanazuia ukuaji wa kiroho.
2. Yanatuzuia kuona na kuingia kwenye kusudi la Mungu.
3. Yanatufunga katika maisha ya kushindwa, hivyo tunashindwa kupiga hatua
4. Yanazuia matunda ya maisha mapya kuonekana.
5. Yanatuzuia kuingia katika viwango vipya vya neema na ushindi.

IV. JINSI YA KUACHANA NA MAMBO YA KALE
- Kubaki ndani ya Kristo kila siku.
- Kujazwa na Neno la Mungu.
- Kuongozwa na Roho Mtakatifu.
- Kutubu na kuacha dhambi.
- Kuwa na ushirika mzuri wa waamini.

V. HITIMISHO
Kuumbwa upya kunahitaji kuachana na yale yaliyopita. Mungu ametufanya viumbe vipya ili tuishi maisha mapya. Hatupaswi kurudi katika yale ambayo Kristo ametukomboa kutoka kwake.

Kadiri tunavyoendelea kutembea na Mungu, ndivyo maisha ya kale yanavyozidi kupoteza nguvu ndani yetu, na maisha mapya ya Kristo yanavyozidi kuonekana ndani yetu.

Tamko
"Mambo ya kale yamepita katika maisha yangu. Nimeachana na dhambi, hofu, uchungu, na fikra za zamani. Ninatembea katika uhuru, ushindi, na maisha mapya niliyopewa na Kristo. Kwa neema ya Mungu, nitaishi k**a kiumbe kipya kila siku. Katika jina la Yesu, Amina."

UBARIKIWE

Valley of Life Church , MwanzaKazi inaendelea: Wokovu na Kuinua Jeshi la Waamini.
07/06/2026

Valley of Life Church , Mwanza
Kazi inaendelea: Wokovu na Kuinua Jeshi la Waamini.

JUNI 2026 – MWEZI WA KUUMBWA UPYASEHEMU YA KWANZA: MAANA YA KUUMBWA UPYAAndiko Kuu: 2 Wakorintho 5:17- "Hata imekuwa, mt...
06/06/2026

JUNI 2026 – MWEZI WA KUUMBWA UPYA

SEHEMU YA KWANZA: MAANA YA KUUMBWA UPYA

Andiko Kuu: 2 Wakorintho 5:17
- "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya."

I. Utangulizi
Moja ya miujiza mikubwa ambayo Mungu hufanya katika maisha ya mwanadamu ni *muujiza wa kumuumba upya kupitia Yesu Kristo*, yaani wokovu.

Wokovu si kusamehewa dhambi tu, ni zaidi ya hivyo. Wokovu ni kupewa maisha mapya na asili mpya ya Mungu.

Unapompokea Yesu Kristo k**a Bwana na Mwokozi yako, Mungu hufanya kazi ya uumbaji mpya ndani yako. *Unabadilishwa kutoka kuwa mtu wa zamani aliye chini ya utawala wa dhambi na kuingia kuwa mtu mpya - katika maisha mapya ya:
- haki,
- amani, na
- ushirika na Mungu.

Kuumbwa upya ni kazi ya neema ya Mungu, si matokeo ya jitihada za kibinadamu.
- Waefeso 2:8.

Hakuna elimu, mali, dini, au matendo mema yanayoweza kumfanya mtu awe kiumbe kipya; ni Kristo pekee anayebadilisha maisha ya mwanadamu kutoka ndani kwenda nje.
- Waefeso 2:9-10

II. KUUMBWA UPYA NI NINI?

Waefeso 2:10
- "Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo."

1.Ni kupokea maisha mapya kutoka kwa Mungu kupitia Kristo Yesu
- Yohana 3:3
- Mtu huzaliwa mara ya pili kiroho.

2. Ni kupata asili mpya ya Kiungu
- 2 Petro 1:4
- Muumini anashiriki tabia ya Kimungu.

3. Ni kuondokana na maisha ya kale ya utumwa wa dhambi na uovu
- Warumi 6:6
- Utumwa wa dhambi unavunjwa. K**a hujazaliwa upya kwa uhalisia unakuwa chini ya ushawishi na kutumikishwa na dhambi (Waefeso 2:1-10)

4.Ni kupewa utambulisho mpya ndani ya Yesu Kristo
- Wagalatia 2:20
- Sasa tunaishi ndani ya Kristo na Kristo anaishi ndani yetu. Huu ni muujiza mkubwa sana.

5. Kutoka kwenye kumtumikia shetani na kusudi lake, na kuingia katika kumtumikia Mungu
- Waefeso 2:10
- unaumbwa upya katika kusudi la Mungu, unarejeshwa upya katika mpango na kusudi la Mungu - utumishi.

III. DALILI ZA MTU ALIYEUMBWA UPYA

Mathayo 7:15-20
- "Mtawatambua kwa matunda Yao,...."

Mtu aliyeumbwa upya hutambulika. Baadhi ya viashiria ni:
- Ana hamu na shauku ya Mungu na Neno lake.
- Anachukia na kujitenga dhambi na njia za uovu
- Anaonyesha matunda ya Roho: upendo, uaminifu, utu wema, n.k
- Ana upendo kwa Mungu na watu.
- Ana kiu ya kukua kiroho.
- ana kiu ya kumtumikia Mungu

IV. FAIDA YA KUUMBWA UPYA
- Kusamehewa dhambi zote (1 Yohana 1:9)
- Kufanyika mwana wa Mungu (Yohana 1:12)
- Kupokea uzima wa milele (Yohana 3:16-17)
- Kuwa na amani na Mungu - unapatanishwa na Mungu (2 Wakorintho 5:20)
- Kuwa na urithi katika Ufalme wa Mungu (Wagalatia 4:7)
- kuingia kwenye mpango na kusudi la Mungu (Waefeso 2:10)

V. HITIMISHO
Msingi wa maisha ya Kikristo ni kuumbwa upya. Kabla ya kutafuta mafanikio, huduma, karama, au baraka, mtu lazima awe kiumbe kipya ndani ya Kristo.

Mungu habadilishi tu tabia za mwanadamu; humuumba upya kabisa ili aishi maisha yanayompendeza Yeye.

Tamko la Ukiri
- "Nimeumbwa upya katika Kristo Yesu. Mimi si mtu wa zamani tena.
- Dhambi, hofu, na vifungo vya kale havina mamlaka juu yangu.
- Nina maisha mapya, utambulisho mpya, na kusudi jipya katika Kristo.
Katika jina la Yesu, Amina."

UBARIKIWE

Address

Kigamboni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 19:00
Tuesday 08:00 - 19:00
Wednesday 08:00 - 19:00
Thursday 08:00 - 19:00
Friday 08:00 - 19:30
Saturday 08:00 - 19:00
Sunday 08:00 - 19:00

Telephone

+255789955305

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Valley of Life Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Valley of Life Church:

Shortcuts

Share