24/12/2025
Mwamini yeyote yule anapaswa awe chini ya uangalizi katika kanisa la mahali kwa sababu kanisani ni mahali pekee ambapo malighafi(mwamini) inachakatwa kuwa bidhaa adhimu ifaayo kuingia sokoni( mwamini aliyefunzwa vizuri huduma). KANISA LA MAHALI ni mpango wa milele wa Mungu katika ukombozi. Kanisa la mahali ni karakana au kiwanda kinachotengeneza bidhaa inayoitwa mwamini anayetenda kazi ya huduma yaani awe mtendakazi katika nyumba ya Mungu asilimia mia moja. Lakini pia kanisa la Mahali ni Shule kwa sababu inawaweka waamini darasani kwa ajili ya mafunzo ya huduma. Ukuaji wa kiroho unaanzia katika kanisa la mahali.Ni sehemu ambayo itashepu mtindo wa maisha yako ili ufuate mpango wa Mungu hata katikati ya dunia hii mbovu.
Tukiangalia wanafunzi na mitume katika kanisa la kwanza huduma zao zilizaliwa katika kusanyiko la watakatifu.
Tumwangalie stefano kwenye matendo ya mitume sura ya 6 na 7 ambaye alikuwa shemasi katika kanisa la mahali alifunzwa neno la Mungu vizuri akaishia kumhubiria sauli na wengine wengi sana kabla ya kifo chake.
Matendo 6:3
[3]
Basi ndugu, *chagueni watu saba miongoni mwenu,* walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;
Paulo na Barnaba kabla ya kutumwa na kanisa kwenda kuhuburi Asia walipokea mafunzo katika kanisa la mahali lililokuwa Antiokia.
Matendo 13:1
[1]
Na huko *Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba,* na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na *Sauli* .
Timotheo kabla ya kuchukuliwa na paulo alikuwepo katika kanisa la mahali lililopo Listra na alishuhudiwa vema na watakatiku katika kanisa kwa sababu ya mwenendo wake mzuri
Matendo 16:1-3
[1]
Basi akafika Derbe na Listra, na *hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo,* mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani.
[2]
*Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio.*
[3]
*Paulo akamtaka huyo afuatane naye,* akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani.
Mtindo kamili wa uanafunzi tunaona unaanzia katika kanisa la mahali.Ni katika kanisa la mahali tunafunzwa jinsi ya kutenda kazi ya huduma kwa ubora.Ni katika kanisa la mahali tunajifunza namna ya kuenenda kwa upendo na kuwatumikia watakatifu wengine. Ni katika kanisa la mahali tunapokea marekebisho,maonyo na maelekezo maalumu ya namna bora ya kutenda kazi ya huduma. Ni katika kanisa la mahali utaratibu maalumu wa jinsi ya kutimiza mpango wa Mungu juu ya maisha yetu unawekwa kwa uwazi.
Kuwa chini ya uangalizi wa kanisa la mahali inakusaidia kuwa na uwajibikaji wa machaguzi yako kila siku. Tii mamlaka iliyopo hapo.Fuata maelekezo ya mahali hapo.Watumikie watakatifu wengine mahali hapo. Katika nia yako vaa vazi la utumishi na kuwatanguliza wengine. Jifunge unyenyekevu wakati wote hata katikati ya sifa na pongezi kutoka kwa wanadamu unabaki na mtazamo kwamba wengine ni bora kuliko nafsi yako.
Kanisa la mahali ni nguzo ya lazima na muhimu kwa kila mwamini kujizoeza UPENDO KWA VITENDO,UNYENYEKEVU KWA VITENDO NA KUHESABU MAISHA YAKO KILA SIKU KWA VITENDO. Mambo haya ni rahisi zaidi kujizoeza ukiwa katikati ya watakatifu wengine katika kanisa la mahali. Mpango wa Mungu taangia mwanzo imekuwa ni kanisa na si mtu mmoja mmoja. Ndio maana kuna maelekezo ya kutoacha kukusanyika k**a ilivyodesturi ya wengine. Tunadumu katika hili siku zote.
Biblia inarecord kwamba wale watu 3000 waliookoka siku ya pentekoste walikuwa wakidumu katika ushirika na watakatifu wengine
Matendo2:42
[42]
*Wakawa wakidumu* katika fundisho la mitume, na *katika ushirika* , na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Jipate katika kusanyiko la watakatifu katika kanisa la mahali. Tumika hapo. Fikia mahitaji ya kanisa na watakatifu wengine hapo. Tii na heshimu uongozi wa mahali hapo. Pokea maelekezo kutokea hapo.
Baada ya hapo subiria matokeo yanayoshikika na utendaji wa neema ya Mungu katika maisha yako.
Umewezeshwa!
—Believers Community Church
"Making your life count "