Uzima tele

Uzima tele With God all things are possible
(Yote yanawezekana kwa Mungu) walete wote walioonewa na kuteswa na Ibilisi nao watawekwa huru Kwa Jina La Yesu Aliye Hai!

Tupo Kikalakala Mzinga Kongowe, Bwana Yesu anatenda yale ambayo yeye tu anaeza kutenda karibu sana!

04/05/2026

jifunze kitu

Karibu ukutane na Nguvu ya Neno
11/04/2026

Karibu ukutane na Nguvu ya Neno

Karibu uabudu nasi Jumapili hii
29/03/2026

Karibu uabudu nasi Jumapili hii

29/03/2026

Shalom, Nakukaribisha kwenye Ibada kuu ya Kuukuza Utu wa Ndani, Karibu

MWONGOZO WA MAOMBI YETU YA LEO TAREHE 12/1/2026Kumbuka kwenye Youtube Yetu tutakuwa tunatuma masomo na maombi ya Live us...
12/01/2026

MWONGOZO WA MAOMBI YETU YA LEO

TAREHE 12/1/2026

Kumbuka kwenye Youtube Yetu tutakuwa tunatuma masomo na maombi ya Live usikose jitahidi subscribe , like, comment na kushare bofya hapa:
https://youtu.be/AzyrnWvQbFM?si=kdHQl5WrzlfJl2Yk

Endelea

🗣️Siku ya Shukrani, Matamko na Sadaka ya Kuhitimisha maombi yetu ya siku 21! Kwa K*tuma sadaka ambayo tumepanga kununua zawadi kwa ajili ya Yatima na kuwasilisha siku ya Jumamosi hii, Tuma kwenye namba hizi
0615748464, 0713757417 majina ni Gwerino Andrew Ngulo, KARIBU TUKAWAONE YATIMA!
ISAYA 58:5-8

🔥 Matamko 26 yenye moto na upako wa Kinabii kwa ajili ya Mwaka Mpya 2026,

🔥Tunatamka Kwa jina la Yesu!🔥

👉Tenga Muda wa kutosha wa Kumshukuru Mungu kwa kukuwezesha kuwa na maombi haya siku 21
✓Onyesha shukrani, Pongezi kwa Roho Mtakatifu kusimama na wewe na kuwa upande wako wakati wote wa maombi👏
🗣️Imba sifa na Tenzi, nyimbo za sifa za kutosha, abudu vya kutosha.
👉Dhihirisha Imani yako kuwa kila ombi uliloomba limejibiwa.
âś…Onyesha matarajio ya kupokea kila Jibu la ombi uliloomba.

1.Natamka na kutangaza kuwa mwaka huu utakuwa mwaka wangu wa kumiliki mali, kitu, ndoa, biashara, kazi na kutawala kimwili na Kiroho pamoja na kuongezeka sana Mwanzo 47:27

2.Natamka na kutabiri kuwa mwaka huu mpya utakuwa mwaka wa utanifadhili, kibari, upendeleo na Ustawi usio kawaida! (Zaburi 102:13)

3.Natamka na kutabiri ulinzi wa Mungu juu ya maisha yangu, familia yangu na hatima yangu mwaka huu! (Zaburi 121:7–8)

4.Natamka na kutangaza kwamba hakuna silaha itakayofanyika dhidi yangu itakayofanikiwa mwaka huu! (Isaya 54:17)

5.Natamka na kutabiri mbingu zilizo wazi juu ya maisha yangu katika mwaka huu mpya! Kwa Jina la nguvu la Yesu. (Kumbukumbu 28:12)

6.Natamka na kutangaza afya njema na nguvu za kiungu juu yangu mwaka huu mzima! (Waraka wa Yohana 3:2)

7.Natamka na K*tangaza Bwana ataongoza hatua zangu katika haki mwaka huu! (Zaburi 37:23)

8.Natamka na kutabiri mafanikio ya ajabu na uvunjaji wa vizuizi kwenye kila eneo la maisha yangu mwqka huu! (Mika 2:13)

9.Natamka na kutangaza hekima ya kiungu kwenye maamuzi na mikakati yangu yote ya mwaka huu! (Yakobo 1:5)

10.Natamka na kutangaza kibali cha kiungu kitanizunguka k**a ngao 2026! (Zaburi 5:12)

11.Natamka kutabiri ongezeko la kifedha, kineema, upako na utoshelevu wa kimungu mwaka huu! (Wafilipi 4:19)

12.Natamka na kutangaza urejesho wa kila kitu ambacho adui aliniibia miaka iliyopita mwaka huu! (Yoeli 2:25–26)

13.Natamka na kutangaza moto mpya juu ya madhabahu ya maombi yangu mwaka huu! (Warumi 12:11–12)

14.Natamka na kutabiri kasi ya kiungu na maendeleo ya haraka katika kila eneo maisha yangu 2026! Kwa Jina la Yesu. (1 Wafalme 18:46)

15.Natamka na kutabiri watu wakuu kusaidia hatima yangu na kunipa miunganisho ya kimungu mwaka huu mzima! (Isaya 60:10)

16.Natamka ushindi katika kila vita vilivyopangwa dhidi ya hatima yangu! Kwa Jina la Ushindi la Yesu (1 Wakorintho 15:57)

17.Natamka na kutangaza kuwa macho yangu yataona na masikio yangu yatasikia habari njema mwaka huu mzima! Kwa Jina la Mamlaka la Yesu(Yeremia 29:11)

18.Natamka na kutangaza kuwa 2026 sitakufa bali nitaishi na kuuhubiri(kuutangaza) utendaji wa Bwana! (Zaburi 118:17)

19.Natamka amani ya Mungu itatawala moyoni mwangu na nyumbani mwangu! (Wakolosai 3:15)

20.Natamka na kutangaza milango mipya, nafasi mpya na viwango vipya mwaka huu! Kwa Jina la Uweza la Yesu (Ufunuo 3:8)

21.Natamka na kutangaza msaada wa malaika na usaidizi wa kiungu mwaka mzima! (Zaburi 91:11)

22.Natamka na kutangaza ulinzi wa kiungu katika safari na mitembeo yangu yote mwaka huu! (Zaburi 121:8)

23.Natamka na kutangaza kuwa 2026 hatua zangu hazitabadilika wala miguu yangu haitajikwaa! (Methali 3:23)

24.Natamka na kutanga ukuaji wa kiroho, ukomavu na ukaribu na Mungu usio wa kawaida mwaka huu! (Yakobo 4:8)

25.Natamka kuwa nyumba(kazi/biashara taja na kingine) yangu imebarikiwa na kufunikwa kwa damu ya Yesu! (K*toka 12:13)

26.Natamka na kutangaza kuwa mwaka huu hautanimeza mimi, familia yangu wala hatima yangu! (Zaburi 91:16)

27.Natamka na kutangaza kuwa huu ndio mwaka wangu wa ushuhuda, utukufu na udhihirisho wa Mungu! (Warumi 8:19)

11/01/2026

Karibu sana Kwenye ibada ya Leo

MWONGOZO WETU WA MAOMBI YA LEO SIKU YA 21Bofya hapa kwa kutupata youtube, tutakuwa na maombi na maombezi na mafundisho, ...
11/01/2026

MWONGOZO WETU WA MAOMBI YA LEO

SIKU YA 21
Bofya hapa kwa kutupata youtube, tutakuwa na maombi na maombezi na mafundisho, tembelea subscribe, like, comment share!

https://youtu.be/AzyrnWvQbFM?si=f6u4DsQOVWyfygrQ

11/1/2026

*AWALI YA YOTE*
👉Nikupongeze sana kwa kushiriki maombi haya ya siku 21 ambayo hujulikana k**a Maombi ya Danieli, Daniel 10:13
MUNGU akutumie malaika akutangulie mwaka 2026 *andika Malaika nitangulie 2026!*
👉Hongera sana wewe uliyeomba pamoja nasi iwe kwa kufunga au kuomba pasi na kufunga kwa sababu zozote halali,
🔥Tarajia mambo makubwa na yasiyo ya kawaida 2026!
👉Kama ambavyo umeomba ulikuwa unapanda mbegu njema 2026 hivyo tarajia mavuno ya kutosha.
Mungu si Mtu hata aseme uongo ikiwa amesema "Ombeni nanyi Mtapewa Math.7:7" Tarajia kupewa/kujibiwa.
âś…ikiwa amesema apandacho mtu ndicho atakachovuna;-
🗣️“Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”
— Wagalatia 6:7
Jiandae kuvuna mwaka mzima 2026.

ZINGATIA;-
🙏🏼Tutakuwa na kuwaona watoto yatima na kutoa sadaka zetu kwa ajili ya mfungo wetu sawa na
Soma ISAYA 58:3-11
“Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?”
— Isaya 58:7--

🙏🏼🙏🏼USIKOSE KESHO SIKU YA
(1)SHUKRANI,
(2)MATAMKO NA
(3)SADAKA(YATIMA)
(4)WAKFU.

LEO TUTAJIKITA KUUTAKA MSAADA WA MUNGU USIO WA KAWAIDA

Day 21

âś…Anza maombi kwa Shukrani, kisha toba na rehema

1.Kila mlango uliolala/uliofungwa 2026 ufunguke kwa moto wa Mungu, kwa jina la Yesu! (“Fungueni malango…” — Isa 26:2)

2.Ee Bwana, vunja vizuizi vyote vinavyozuia ndoto zangu kutimia, kwa jina la Yesu! (“Nitamvunja mavuno yake…” — Hos 2:12)

3.Natangaza mpenyo wa fursa, mali, ajira, kazi, upako, ndoa (n.k) 2026 kwa jina la Yesu! (“Atavunja milango ya shaba…” — Isa 45:2)

4.Ee Mungu, niingize katika maeneo ambayo nimezuiwa kwa miaka mingi, kwa jina la Yesu! (“Atakufungua hazina za gizani…” — Isa 45:3)

âś… UPENDELEO WA GHAFLA & MIUJIZA YA PAPO KWA PAPO (SUDDEN FAVOR & INSTANT MIRACLES)

5.Ee Mungu wa ghafla, mwaka huu nifanyie miujiza ya haraka na ya papo kwa papo na inaovunja sheria za kawaida, kwa jina la Yesu! (“Namelisema ghafla yakatokea.” — Isa 48:3)

6.Ee Bwana, geuza machozi yangu kuwa ushindi wa papo kwa papo, kwa jina la Yesu! (“Usiku kuna kilio, asubuhi furaha.” — Zab 30:5)

7.Ee Mungu, 2026 niinulie watu watakaonisaidia kwa haraka na bila masharti, kwa jina la Yesu! (“Haraka Nikolasiri.” — Mdo 12:7)

8.2026 Miujiza ambayo haijawahi kutokea nyumbani(kazini/ofisini/mtaani/shuleni/n.k) kwetu itokee ghafla kwangu, kwa jina la Yesu! (“Yeye hufanya mambo mapya.” — Isa 43:19)

9.Ee Bwana, weka kasi ya kimungu kwenye maisha yangu, kwenye kila nifanyacho ili nisichelewe tena, kwa jina la Yesu! (“Atakimbiza mambo…” — Amosi 9:13)

10.Natangaza mipango au harakai au hekaheka zote za Adui za kuchelewesha miujiza yangu ziungue moto, kwa jina la Yesu! (“Kwa kuwa si kuchelewa…” — Hab 2:3)

11.Ee Bwana, weka neema ya majibu ya haraka na ushindi wa haraka juu yangu mwaka huu, kwa jina la Yesu! (“... yahimize hayo.” — Isa 60:22)

âś… KUTOFAUTISHWA KIMUNGU (DIVINE DISTINCTION)

12.Ee Mungu, mwaka huu nistawishe na nitofautishe kwa hekima ya mbingu, kwa jina la Yesu! (“Danieli alionekana bora…” — Dan 6:3)

13.2026 Kila roho ya kutokuonekana, kufichwa, kusahauliwa na kupuuzwa ivunjike kwa moto, kwa jina la Yesu! (“Arise, shine…” — Isa 60:1)

14.Ee Baba, nitofautishe na watu wa kizazi hiki kwa upako wa kipekee na usio wa kawaida! (“Nitamchagua…” — K*t 33:16)

15.Natangaza kuwa mwaka huu sitakuwa k**a wengi walivyo, nitakuwa k**a Mungu anavyotaka, kwa jina la Yesu! (“Mmeketishwa na Kristo.” — Efe 2:6)

16.Ee Bwana, nibebe kwa nguvu zako na kunifanya kuwa ushuhuda wa utukufu wako 2026, kwa jina la Yesu! (“Nanyi mtakuwa ushahidi.” — Mdo 1:8)

17.Ee Mungu, niondolee sura ya kawaida, nivalishe sura ya utukufu, kwa jina la Yesu! (“Utukufu wa Bwana umekuzukia.” — Isa 60:1)

18.Natangaza tofauti ya kimbingu juu yangu katika kazi, biashara, huduma na taifa, kwa jina la Yesu! (“Ndipo mtakapopambanua…” — Mal 3:18)

âś… UPAKO WA KIBALI + MIPENYO + MIUJIZA

19.Ee Mungu,Mwaka huu mimina juu yangu mafuta ya kibali, mpenyo na miujiza kwa wakati mmoja! (“Kibali cha Bwana kiwe juu yetu.” — Zab 90:17)

20.Natangaza huu ni msimu wa uwezo na wa kufungua milango na kushinda bila mapambano, kwa jina la Yesu! (“Si kwa nguvu wala si kwa uwezo…” — Zak 4:6)

21.Ee Bwana, weka mkono wako juu ya miradi yangu ili ishuhudie miujiza ya kiungu, kwa jina la Yesu! (“Bwana alikuwa pamoja naye…” — Mwa 39:23)

22.Natangaza mpenyo wa wingu la utajiri, wingu la mafanikio na wingu la neema 2026, kwa jina la Yesu! (“Utajiri wa mataifa utakufuata.” — Isa 60:5)

23.Ee Mungu, kutana nami katika viwanja vya fursa, fedha, afya na makusudi yako, kwa jina la Yesu! (“Atakutangaza…” — Zab 20:4)

24.Ee Baba, wafanye watu wanitambue, wanikumbuke, ili wanisaidie na waniinue 2026, kwa jina la Yesu! (“Wakurugenzi wakamnufaisha.” — Neh 2:8)

25.Natangaza ushindi unaokuja kwa njia zisizo za kawaida, bila kutumia nguvu ya mwili, kwa jina la Yesu! (“Si wao kwa upanga wao…” — Zab 44:3)

26.Ee Bwana Yesu nipe kushinda kila vita kwenye malango yangu na malango ya adui zangu bila kutumia nguvu kwa jina kuu la yesu.(Wakamshinda Kwa Damu na kwa Neno la ishuhuda...ufu 12:11)

✳️Pata muda wa Kumshukuru Mungu kwa Kujibu maombi ya siku 21 ✳️

MUNGU AKUBARIKI SANA NA AJIBU MAOMBI YAKO MWAKA 2026

UWE MSHINDI.

SHALOM!

MWONGOZO WA MAOMBI YA LEO JAN.6/1/2026Day 16subscribe, like share, comment hapahttps://youtube.com/shorts/jQosg59CMn0?si...
06/01/2026

MWONGOZO WA MAOMBI YA LEO

JAN.6/1/2026
Day 16

subscribe, like share, comment hapa
https://youtube.com/shorts/jQosg59CMn0?si=q0ccvt2z5bfMfOsw

Mada: kushinda vizuizi 2026.

Utangulizi
vizuizi au vipingaminizi ni sehemu ya njia za kuufikia ukuu fulani katika maisha, uko upinzani wa
[1]kibinafsi huu ni upinzani unaotokea kwa sababu mbalimbali ikiwemo uzembe, uvivu kukosa sifa/vigezo n.k
[2]kishetani hii ni pale shetani na mawakala wake hupinga kila kitu kwa sababu ya wivu na wakati mwingine bila hata sababu yoyote. 1Wakorintho 16:9 ...wengi wanipingao.
[3] wa Kimungu pale ambapo Mungu mwenyewe humpinga mwenye kiburi na kuumpa neema (urahisi) mnyenyekevu
1Petro5:5"...hupinga ...na huwapa neema.."

Nakuombea 2026 Ushinde vizuizi/upinzani na vikwazo na changamoto zote. Andika *Napokea ushindi 2026!*

Maombi haya
âś…tunaomba kwa imani
âś…
tunaomba kwa sauti
âś…tunaomba tukitembeatembea.
âś…Utakatifu ndio maisha yetu wakati huu wa maombi
âś…Omba tena na tena na kwa muda maalumu
tena usiku na mchana.
âś…Mwisho wa maombi tuna sadaka ya kuambatana na tutafanya kitu kwa ajili ya Yatima.
Endelea
🔥Pata muda wa kusifu na kuabudu kw zana au kwa maneno.

🔥Anza kuomba kwa Jina la Yesu...🔥

1. Ninavunja kila laana na uovu unaotiririka katika ukoo wangu, kwa jina la Yesu.
“Kristo alitukomboa katika laana ya sheria.” (Wagalatia 3:13)

2. Ninaharibu kila zuio la kiroho la ustawi kutoka upande wa mama na baba yangu, hadi vizazi 10 nyuma, kwa jina la Yesu.
“Rehema zake ni kwa vizazi elfu kwa wamchao.” (K*toka 20:6)

3. Kila agano la giza lililounganishwa na mahali nilipozaliwa, livunjike sasa, kwa jina la Yesu.
“Nitaivunja minyororo yao.” (Zaburi 107:14)

4. Kila nguvu ya Ikabodi juu ya hatima yangu, kufa mara, kwa jina la Yesu.
“Utukufu wangu sitampa mwingine.” (Isaya 42:8)

5. Kila tatizo/(Changamoto) linalotesa, au kuharibu utukufu wangu, kufa,kufa ,kufa kwa jina la Yesu.
“Hakuna silaha itakayofanikiwa.” (Isaya 54:17)

6. Utukufu wa maisha yangu ulioibiwa tangu tumboni, napokuwa, naposoma, nakurejesha kwa moto, kwa jina la Yesu.
“Nitawarudishia miaka iliyoliwa.” (Yoeli 2:25)

7. Wadanganyifu na wezi wa utukufu wangu 2026, niachieni sasa na mfe kwa jina la Yesu.
“Mwizi amekuja kuiba, kuua na kuharibu.” (Yohana 10:10)

8. Ninyi vichochezi vya nira, ubaya, matatizo sikieni neno la Bwana: mfe, kwa jina kuu la Yesu.
“Upako utavunja nira.” (Isaya 10:27)

9. 2026 Siku zangu hazitakuwa za taabu, bali zitaitwa siku za kustareheshwa na Bwana, kwa jina la Yesu.
“Siku zote nilizokusudia ni za amani.” (Yeremia 29:11)

10. Kila jambo jema lililokufa maishani mwangu kwa ujinga, uzembe/uvivu kuwa hai sasa, kwa jina la Yesu.
“Nitafufua mifupa mikavu.” (Ezekieli 37:5)

11. Macho yangu, fungukeni ili kuona kile Mungu anachofanya 2026, kwa jina la Yesu.
“Ninakuomba macho ya mioyo yenu yafunguliwe.” (Waefeso 1:18)

12. “Niko Ambaye Niko,” simama upande wangu 2026 ili udhihirishe nguvu zako na unipeleke kiwango kingine, kwa jina la Yesu.
“Mimi ni Bwana, hakuna mwingine.” (K*toka 3:14)

13. Ee Bwana, ninaunganisha hatima yangu na soketi ya upako ya Roho Mtakatifu ili nipokee kuinuliwa 2026, kwa jina la Yesu.
“Yeye anyanyuashe chini na juu.” (Zaburi 75:7)

14. Ee Bwana, ninaunganisha maisha yangu na soketi ya Roho Mtakatifu ili nipokee kasi ya kimungu 2026, kwa jina la Yesu.
“Nitakimbia bila kuchoka.” (Isaya 40:31)

15. Napanda farasi wa vita na kuingia nchi(mahali) ya mafanikio yangu, kwa jina la Yesu.
“Bwana afundisha mikono yangu kupigana.” (Zaburi 144:1)

16. Nyundo ya Mungu, vunja kila mguu mwovu unaotembea kinyume na kuinuliwa kwangu mwaka huu, kwa jina la Yesu.
“Silaha za vita vyetu zina nguvu kwa Mungu.” (2 Wakorintho 10:4)

17. Seremala wa mbinguni, wafunge hadi kifo wezi wote wa kiroho waliopangiwa kunizuia 2026, kwa jina la Yesu.
“Bwana atapigana kwa ajili yenu.” (K*toka 14:14)

18. Roho wote waovu angani wanaopinga kuinuliwa kwangu, tawanyikeni na muwe ukiwa, kwa jina la Yesu.
“Tunapigana na falme za giza.” (Waefeso 6:12)

19. Roho wote waovu katika ardhi/milima/misitu wanaozuia maendeleo yangu, tawanyikeni, kwa jina la Yesu.
“Upepo ukatii neno lake.” (Zaburi 148:8)

20. Roho wote waovu/ majini/mapepo wanaozuia hatua za kuinuliwa kwangu 2026, tawanyikeni, kwa jina la Yesu.
“Bwana atawapita maadui wako.” (K*toka 15:19)

muda wa kumshukuru Mungu kwa kujibu maombi.

Uwe mshindi 2026!

(2026 mwaka wa upako wa Gosheni)

Address

Dar Es Salaam
TEMEKE

Telephone

+255713757417

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uzima tele posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Uzima tele:

Share