04/06/2026
Zakaria alikuwa ameishi na maombi ya muda mrefu ambayo yalionekana ni k**a hayatajibiwa tena. Lakini siku moja, Mungu alituma habari njema kupitia malaika wake: “Mke wako Elizabeth atazaa mwana.” Kilichoonekana hakiwezekani kutokea kikawa ushuhuda!
Je, kuna jambo ambalo umekuwa ukiliombea kwa muda mrefu? Je, kuna ndoto ambayo umeanza kuiona k**a haiwezekani tena kutimia? Mungu yule wa Zakaria hajabadilika hata leo. K**a alivyomkumbuka Zakaria katika wakati wake, ndivyo anavyoweza kuleta habari njema katika maisha yako leo.
MUNGU ametupa Mkesha wa Habari Njema usiku wa Tarehe 12 mwezi June, Usiku huu utakuwa ni usiku wa kupokea habari njema kutoka kwa Mungu. Usipange kabisa kukosa, Huenda huu ukawa usiku ambao Mungu atageuza maisha kuwa ushuhuda.