23/08/2026
Ukitaka kuwa confused, tafuta utambulisho wako namna hii.. utakuja kuchoka balaa. Leo uangalie nyota.. mara mimi ni Gemini ♊️ unaanza kuangalia nyota weeee.. unagundua GEMINI HAWANA HASIRA.. kesho ni group O... unasoma tabia zako, unaanza kuzifuata.. UNAGUNDUA GROUP O WANA CHUKI NI BALAA. Wakati haujakaa sawa.. kesho unaambiwa wewe ni GEN Z na GEN Z NI WAKOROFI unaanza kupotezea upole wako. Unaanza fujo. Mara uambiwe wewe ni sanguine unaanza kujitafuta kwenye USANGUINE.. watu wenye makelele. haujakaa vizuri unaambia ni INTROVERT.. unataka kukaa kimya.. kesho unaambia ni MCHAGA... Wachaga wako 123.. hujakaa vizuri unaambiwa Wewe ni Mtanzania na WATANZANIA NI WAPOLE. Hujakaa vizuri unaambiwa wewe ni mwanaume.. usikubali mambo kizembe PAMBANA.. Mwisho wa siku unakuwa na CONFUSED IDENTITY.. Unaanza kuwa na mgogoro wa UTAMBULISHO. Huwezi kupata utambulisho wa mwanadamu kwa kumtazama mwanadamu. Mwanadamu hakujiumba kwa sura na mfano wake mwenyewe.... aliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Mwanadamu anapaswa kujitambua katika Mungu. Musa alipouliza "MIMI NI NANI?" alijibiwa "NITAKUWA PAMOJA NAWE" — unajipata tu pale unapojua uko na Mungu. Ndiyo maana "aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye" Mungu naye amejitambulisha kwetu katika Kristo kwa hiyo.. Utambulisho wa MWAMINI ni Kristo (Mungu). K**a Kristo hana kitu fulani hicho huna pia. K**a Kristo ameshinda na wewe umeshinda pia. Baba akikutazama anamwona mwanae k**a Kristo. Hivyo haoni aibu kusema "Huyu ni mwanangu mpendwa ninayependezwa naye". Kristo ni mwenye haki? Na mwamini pia. Kristo ni Mtakatifu? Na MWAMINI pia. Kristo hana waa lolote? Na MWAMINI pia. Tumetwaa asili yake mazima. Yaani alivyo ndivyo tulivyo. Mungu ni Baba yetu. Sisi ni watoto wapendwao! Waefeso 5:1 kwa habari ya mwenendo, Mungu anataka ujifunze kwake. Uenende k**a Yeye katika ulimwengu huu.. usiige kwingine. Unatakiwa kusema Kristo anakaa ndani yangu… ukuaji wangu ni ili niweze kumdhihirisha Yeye katika kila eneo. Habari njema ni kwamba Yeye hutenda kazi hiyo ndani yangu. Ushirikiano wangu ni kutomzuia Yeye kuwa wazi ndani yangu kwa kufahamu mimi ni nani ndani yake. Mwisho wa siku.. NIJIONE NDANI YAKE k**a Yeye ANAVYOJIONA NDANI YANGU. Namjifunza Yeye ili nimfananie Yeye katika mwenendo wangu maana hakika ASILI YAKE NINAYO. Haleluya!
Kumjua Yesu ni kujijua wewe mwenyewe. Tulipoamini alitufanya washirika wa Roho wake… hivyo Utambulisho wake (identify), Nafasi yake (position), Mamlaka yake (authority) pamoja na Asili yake (character) vyote vipo ndani yetu. Unavyomfahamu sana Mwana wa Mungu ndivyo unavyozidi kumdhihirisha ulimwenguni. Unajifunza habari za nani?
Usipotambua vile Mungu anakuita; ulimwengu utakuita majina mengi mpaka uchanganyikie.. sanguine, nyota ya mizani, gen z, alpha male, mtanzania, mmasai, mtu mweusi, last born, introvert, na mengine mengi.. na kila utambulisho utakaoukubali utakulazimisha uwe na tarajia la tabia fulani fulani. Ukitambulishwa na wanasaikolojia, wanajamii, watu wa nyota, wapiga ramli... mwisho wa siku utaishi katika mgogoro wa utambulisho (identity crisis).. Mungu anasema WEWE NI NANI?
— Global Family Gatherings
"God's Standards"
FUATILIA KUHUSU UTAMBULISHO WAKO..
Series audio ipo https://globalfamilygatherings.co.tz/album/mimi-ni-nani/
Series video swahili MIMI NI NANI?: https://www.youtube.com/playlist?list=PLebXJnc1glwRu3_RKwExbMSth9_qf4pzc
Series video English WHO AM I?: https://www.youtube.com/playlist?list=PLebXJnc1glwQ2tR9iWeKwxrmpmKv2wig4
KUULINDA UTAMBULISHO WAKO https://globalfamilygatherings.co.tz/album/kulinda-utambulisho-wako/