Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church

Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church GlobalFamilyGatherings

25/08/2026

Ni muhimu kupata Ufunuo unaposoma Neno la Mungu

**amchanga


25/08/2026

Matumizi ya Neno Mwana kwenye Biblia

**amchanga


24/08/2026

Huduma bila maombi ni kazi bure

**amchanga



24/08/2026

Matumizi ya maneno (Kristo,Masihi & Mpakwa mafuta) kwenye Biblia

**amchanga

Ukitaka kuwa confused,  tafuta utambulisho wako namna hii.. utakuja kuchoka balaa. Leo uangalie nyota.. mara mimi ni Gem...
23/08/2026

Ukitaka kuwa confused, tafuta utambulisho wako namna hii.. utakuja kuchoka balaa. Leo uangalie nyota.. mara mimi ni Gemini ♊️ unaanza kuangalia nyota weeee.. unagundua GEMINI HAWANA HASIRA.. kesho ni group O... unasoma tabia zako, unaanza kuzifuata.. UNAGUNDUA GROUP O WANA CHUKI NI BALAA. Wakati haujakaa sawa.. kesho unaambiwa wewe ni GEN Z na GEN Z NI WAKOROFI unaanza kupotezea upole wako. Unaanza fujo. Mara uambiwe wewe ni sanguine unaanza kujitafuta kwenye USANGUINE.. watu wenye makelele. haujakaa vizuri unaambia ni INTROVERT.. unataka kukaa kimya.. kesho unaambia ni MCHAGA... Wachaga wako 123.. hujakaa vizuri unaambiwa Wewe ni Mtanzania na WATANZANIA NI WAPOLE. Hujakaa vizuri unaambiwa wewe ni mwanaume.. usikubali mambo kizembe PAMBANA.. Mwisho wa siku unakuwa na CONFUSED IDENTITY.. Unaanza kuwa na mgogoro wa UTAMBULISHO. Huwezi kupata utambulisho wa mwanadamu kwa kumtazama mwanadamu. Mwanadamu hakujiumba kwa sura na mfano wake mwenyewe.... aliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Mwanadamu anapaswa kujitambua katika Mungu. Musa alipouliza "MIMI NI NANI?" alijibiwa "NITAKUWA PAMOJA NAWE" — unajipata tu pale unapojua uko na Mungu. Ndiyo maana "aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye" Mungu naye amejitambulisha kwetu katika Kristo kwa hiyo.. Utambulisho wa MWAMINI ni Kristo (Mungu). K**a Kristo hana kitu fulani hicho huna pia. K**a Kristo ameshinda na wewe umeshinda pia. Baba akikutazama anamwona mwanae k**a Kristo. Hivyo haoni aibu kusema "Huyu ni mwanangu mpendwa ninayependezwa naye". Kristo ni mwenye haki? Na mwamini pia. Kristo ni Mtakatifu? Na MWAMINI pia. Kristo hana waa lolote? Na MWAMINI pia. Tumetwaa asili yake mazima. Yaani alivyo ndivyo tulivyo. Mungu ni Baba yetu. Sisi ni watoto wapendwao! Waefeso 5:1 kwa habari ya mwenendo, Mungu anataka ujifunze kwake. Uenende k**a Yeye katika ulimwengu huu.. usiige kwingine. Unatakiwa kusema Kristo anakaa ndani yangu… ukuaji wangu ni ili niweze kumdhihirisha Yeye katika kila eneo. Habari njema ni kwamba Yeye hutenda kazi hiyo ndani yangu. Ushirikiano wangu ni kutomzuia Yeye kuwa wazi ndani yangu kwa kufahamu mimi ni nani ndani yake. Mwisho wa siku.. NIJIONE NDANI YAKE k**a Yeye ANAVYOJIONA NDANI YANGU. Namjifunza Yeye ili nimfananie Yeye katika mwenendo wangu maana hakika ASILI YAKE NINAYO. Haleluya!
Kumjua Yesu ni kujijua wewe mwenyewe. Tulipoamini alitufanya washirika wa Roho wake… hivyo Utambulisho wake (identify), Nafasi yake (position), Mamlaka yake (authority) pamoja na Asili yake (character) vyote vipo ndani yetu. Unavyomfahamu sana Mwana wa Mungu ndivyo unavyozidi kumdhihirisha ulimwenguni. Unajifunza habari za nani?
Usipotambua vile Mungu anakuita; ulimwengu utakuita majina mengi mpaka uchanganyikie.. sanguine, nyota ya mizani, gen z, alpha male, mtanzania, mmasai, mtu mweusi, last born, introvert, na mengine mengi.. na kila utambulisho utakaoukubali utakulazimisha uwe na tarajia la tabia fulani fulani. Ukitambulishwa na wanasaikolojia, wanajamii, watu wa nyota, wapiga ramli... mwisho wa siku utaishi katika mgogoro wa utambulisho (identity crisis).. Mungu anasema WEWE NI NANI?
— Global Family Gatherings
"God's Standards"

FUATILIA KUHUSU UTAMBULISHO WAKO..

Series audio ipo https://globalfamilygatherings.co.tz/album/mimi-ni-nani/

Series video swahili MIMI NI NANI?: https://www.youtube.com/playlist?list=PLebXJnc1glwRu3_RKwExbMSth9_qf4pzc

Series video English WHO AM I?: https://www.youtube.com/playlist?list=PLebXJnc1glwQ2tR9iWeKwxrmpmKv2wig4

KUULINDA UTAMBULISHO WAKO https://globalfamilygatherings.co.tz/album/kulinda-utambulisho-wako/

MOTO WA NDANI KWA NDANI Kiongozi mkuu Musa hakupambana na maadui wa nje pekee (k**a Farao), bali alipitia changamoto ngu...
22/08/2026

MOTO WA NDANI KWA NDANI

Kiongozi mkuu Musa hakupambana na maadui wa nje pekee (k**a Farao), bali alipitia changamoto ngumu sana kutoka kwa watu wake wa karibu na taifa lake mwenyewe.
Hapa kuna migawanyiko mikuu miwili ya upinzani wa ndani (kutoka kwa Kora na ndugu zake) iliyotikisa uongozi wake:
✊ 1. Kundi la Kora, Dathani, na Abiramu (Uasi wa Madaraka na Uongozi)
Wapinzani: Kora (Mlawi) pamoja na viongozi wengine 250 wa mkutano.
Chanzo cha Upinzani: Walipinga mamlaka ya kipekee ya Musa na Haruni. Walimwambia Musa moja kwa moja: "Mbona mnajikuza juu ya kusanyiko la Bwana? Kusanyiko lote ni watakatifu, na Bwana yumo kati yao!"
(Hesabu 16)
Siblings rivalry? Hapa ndipo mambo yalipoharibika zaidi: 👇
👥 2. Miriamu na Haruni (Uasi wa Ndani ya Familia)
Wapinzani: Dada na kaka wa damu wa Musa mwenyewe (Miriamu na Haruni).
Chanzo cha Upinzani: Walitumia kisingizio cha mke wa Musa (kwa kuoa mwanamke Mkushi), lakini kiini halisi kilikuwa ni wivu wa kiroho na madaraka. Walihoji: "Je, Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia?"
(Hesabu 12)

Wakati mwingine upinzani mkubwa na wenye maumivu makali zaidi hautoki kwa adui wa nje, bali kutoka kwa watu wa karibu unaowapigania na kuwahudumia!

Unajifunza nini hapa?
1. Usiwaige hawa ndugu.
2. Uwe k**a Musa, mtazame Mungu k**a mtetezi na msaada wako.
3. Kujilinda na haya yote. Jiombee na uwaombee viongozi wako.

~Apostle Shemeji Melayeki
— Global Family Gatherings
"God's Standards"

22/08/2026

DO YOU UNDERSTAND?

YESU ALIKUTANA  NA MAKUNDI ya KIDINI na KIJAMII...Wakati wa huduma yake duniani, jamii ya Uyahudi haikuwa na msimamo mmo...
22/08/2026

YESU ALIKUTANA NA MAKUNDI ya KIDINI na KIJAMII...

Wakati wa huduma yake duniani, jamii ya Uyahudi haikuwa na msimamo mmoja wa kidini. Kulikuwa na migawanyiko ya kipekee ya kiimani, kisiasa, na kijamii. Hapa kuna makundi makuu aliyokutana nayo:
🔥 1. Mafarisayo
Kundi lenye ushawishi mkubwa kwa wananchi wa kawaida. Walikuwa wakishika Torati na "mapokeo ya wazee" kwa ukali sana. Waliamini ufufuo, lakini Yesu alikosana nao mara kwa mara kutokana na tabia yao ya unafiki na kujionyesha kuwa watakatifu huku wakipuuza upendo na haki ya kweli.
🏛️ 2. Masadukayo
Hili lilikuwa tabaka la juu la utajiri na ukuhani (makuhani wakuu walitoka hapa). Walisimamia Hekalu. Tofauti na Mafarisayo, hawakuamini ufufuo wa wafu, malaika, wala maisha baada ya kifo. Walishirikiana kwa karibu na Warumi kulinda mamlaka yao.
🏜️ 3. Waeseni (Waesene)
Kundi lililochoshwa na ufisadi wa viongozi wa Hekalu Yerusalemu, wakaamua kujitenga na kwenda kuishi maisha ya utawa kule jangwani (k**a eneo la Qumran). Walikuwa wacha Mungu waliokuwa wakingojea ufalme wa Mungu. (Hawatajwi moja kwa moja kwa jina hili kwenye Biblia, lakini walikuwepo!)
⚔️ 4. Wazeloti (Wanaharakati/Wanamapinduzi)
Kundi lililochanganya dini na siasa kwa msimamo mkali. Waliamini kuwa Israeli inapaswa kuwa huru na walitetea matumizi ya nguvu za kijeshi kuwaondoa Warumi. Kumbuka: Mwanafunzi wa Yesu Simoni Zeloti alitoka hapa!
📌 Makundi mengine ya ziada yaliyotajwa:
* Waandishi ✍️ : Wataalamu na walimu wa Sheria ya Musa.
* Herodiani : Wafuasi wa kifalme waliounga mkono utawala wa Herode na Warumi.
* Wasamaria: Hawa ni wale waliotengwa na Wayahudi wa kawaida na kuwa na kitovu chao cha ibada Mlima mmoja huko Samaria.

Watu wenye mitazamo tofauti hawawezi kukosekana katika jamii... lakini pamoja na hayo Yesu Kristo aliweza kuwavua wengi huko kwa sababu zifuatazo..
1. Yesu alifundisha kwa ujasiri kitu alichokuwa anakielewa vema.
2. Hakujiona sehemu ya kundi lolote bali yeyote anayekaa katika kweli.
3. Alifundisha kwa ishara na ajabu.
4. Aliishi maisha ya mfano. Hawakuona kosa lolote kwake zaidi ya tuhuma na visingizio. Upendo ukiwa ndio mtindo wa huduma yake.

Mambo haya yote yanawezakana kwetu hata leo.. na nitakuambia ya kuwa kuna makundi mengi leo zaidi kuliko miaka 2000 iliyopita na taarifa ni nyingi tena zinaenda kasi ya ajabu.

Siku nyingine nitawatajia makundi yaliyopo leo!

Lakini mimi na wewe tunafanya nini?

👉 Tunahibiri Injili ya Yesu Kristo k**a wanafunzi wake walivyofanya... usemi sahihi na ujasiri huku tukilidhibitisha neno hilo katika karama na tunda la Roho.

📚 Mathayo 28:18-20, Marko 16:15-20, Luka 24:47-48, Yohana 20:21-23, Matendo 1:8

Apostle Shemeji Melayeki
— Global Family Gatherings
"God's Standards"

Miaka michache ambayo nimefanya uchungaji, nitakuambia:4.  Vipawa vinaweza kukuponza kwenye kuchagua viongozi. Mtu ambay...
20/08/2026

Miaka michache ambayo nimefanya uchungaji, nitakuambia:

4. Vipawa vinaweza kukuponza kwenye kuchagua viongozi. Mtu ambaye yuko "gifted" lakini hatii mamlaka, anajiamulia mambo, yaani yuko independent, anakiamini kichwa chake tu... usifanye haraka kumpa uongozi. Mara nyingi mtu anayepatikana muda wote akihitajika, anapenda kufuata utaratibu na maelekezo, ni mtii — hata k**a hana vipawa vinavyong'aa na kuvutia ni muhimu zaidi kwenye uongozi. Mtu mwenye "uwezo kidogo" lakini utii mwingi akisaidiwa huo kiongozi bora. Mtu mwenye uwezo mkubwa lakini hasikilizi mtu wala kutii mamlaka ni bomu linalosubiri kulipuka.

📍MTU AMBAYE HAWEZI KUTII MAMLAKA, ASIPEWE MAMLAKA MAANA ATATUMIA VIBAYA MAMLAKA.. Waebrania 13:17, 1 Wathesalonike 5:12-13, 1 Timotheo 5:17, 1 Petro 5:5

A gifted rebel is a liability. A loyal and available person is worth growing into leadership than a gifted and unavailable rebellious person.

Tuwafanyeje? Endelea kuwaombea na kuwafundisha kwenye nafasi zao za uanafunzi siyo kwenye uongozi. Utapunguza unnecessary heartbreak 💔

K**a hujawahi kuwa mchungaji angalau huwezi kuelewa hii. Pita tu..

"God's Standards"

Mungu hategemei wewe kutoendelea. Mchungaji wako anakuona uko mahali kesho. Anategemea kuona mwenendo wako ukibadilika. ...
19/08/2026

Mungu hategemei wewe kutoendelea. Mchungaji wako anakuona uko mahali kesho. Anategemea kuona mwenendo wako ukibadilika. Anategemea kuona maamuzi na machaguo yako kwenye maisha yanakua kufanania asili yako na mpango wa Mungu juu ya maisha yako. Anategemea kuona miitikio yako juu ya hali zote kwenye maisha ukiwa bora zaidi. Ukijiona hivyo pia, utaomba zaidi, utajifunza zaidi.
— Global Family Gatherings
"God's Standards"

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church:

Shortcuts

Share