13/11/2025
MAJI YAMEGAWANYIKA KWENYE MAKUNDI MKUBWA MAWILI KIBIBLIA.
Kundi la kwanza i/
Ni MAJI TU K**A MAJI YA KAWAIDA AMBAYO KIROHO HUFAHAMIKA K**A MAJI YALIYO CHINI YA MBINGU.
Ambayo watu huyatumia kwa shughuli mbalimbali k**a vile kufua, kujenga kuoshea vyombo.
Au hata kumwangilia bustani k**a alivyofanya Adam pale kwenye bustani ya Edeni.
Na wazo hili unalipata kwenye kitabu hiki cha Mwanzo 1:9 inayosema,
" Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja ili pakavu paonekane; ikawa hivyo " ( Mwanzo 1:9 ).
Haya maji ni maji tu ya kawaida k**a yalivyo maji mengine yote tunayoyatumia kwenye shughuli zetu za kila siku.
K**a vile kwenye kilimo, kwenye kuzalisha umeme n.k. Maana ni maji yaliyo chini ya mbingu.
Au maji yanayofikika au yanayofikiwa na binadamu kwa ajiri ya kuyatumia kwa shughuli zao.
Na kundi la pili ii/ la maji ni MAJI MENGI K**A HAYA YA UFUNUO 17:1 ALIYOYAKALIA K**A SI KUYAKETIA HUYU KAHABA WA UFUNUO 17:1 na UFUNUO 17:15.
Maji haya si maji k**a maji ya kawaida ila humaanisha jamaa au makutano au mataifa ya watu au watu na lugha zao.
Na wazo hili unalipata kwenye kitabu hiki cha Ufunuo 17:15 inayosema.
" Kisha akaniambia, yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha " ( Ufunuo 17:15 ).
Hivyo ni muhimu kujua kuwa si kila mahali Mungu au mwandishi wa kitabu hiki kitakatifu.
Kiitwacho Biblia anapozungumzia maji basi atakuwa anazungumzia maji tu k**a maji ya kawaida.
ila kuna wakati atazungumzia maji mengi au maji k**a jamaa au makutano au mataifa ya watu au watu na lugha zao.
Ndio maana ili kumsaidia mtu huyu wa kitabu hiki cha Ufunuo ambaye ndiye Yohana.
Akamwambia " maji yale uliyoyaona " ni jamaa na makutano na mataifa na lugha si kwa bahati mbaya.
Ila kwa makusudi ili ajue maji yana tafsri mbili (2) katika ulimwengu wa roho. k**a tulivyoona huko juu.
Asije akaenda na tafsiri moja tu na akakosa kupata ujumbe au kile ambacho mungu amekusudia akipate.
Hivyo hata wewe unayesoma ujumbe huu ni muhimu kufahamu kuwa maji yana tafsri kubwa mbili.
Ya kwanza ni maji tu k**a maji ya kawaida au Maji yaliyo chini ya mbingu
Na ya pili ni maji k**a jamaa au makutano au mataifa ya watu au watu na lugha zao k**a tulivyoona kwenye kitabu cha Ufunuo 17:1,15.
Na hii itakusaidia kuelewa vizuri kile ambacho Mungu au mwandishi atakuwa au amekusudia ukielewe kwenye uandishi wake.
BARIKIWA na usiache kufuatilia mafundisho haya muhimu kwa ajiri ya ustawi wako wa kiroho.