Southern Tanzania Union Mission

Southern Tanzania Union Mission Southern Tanzania Union Mission ni Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania la Waadventista wa Sabato. Makao yake makuu ni Mbweni, Dar es Salaam.

02/06/2026

Mwanaume ni mbeba maono wa familia. Anapomweka Mungu mbele na kuiongoza familia katika njia sahihi, hujenga msingi imara wa upendo, umoja na mafanikio. Familia nyingi huenda kule ambako maono ya kiongozi wake yanaelekeza; hivyo kila mwanaume anapaswa kuishi kwa kusudi na kuwajibika kwa wale waliowekwa chini ya uangalizi wake.

01/06/2026

Kwaya ya Galilaya kutokea Dar es salaam wakitoa huduma ya Uimbaji pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Njombe na waumini wengine ambao wamekuwa wakibarikiwa na huduma nzuri ya kwaya hii….

01/06/2026

Kwaya ya watumishi kutoka Unioni Misheni ya Kusini mwa Tanzania wakitoa huduma ya uimbaji katika hitimisho la Mkutano wa Njombe Net Event

Tunamshukuru sana Mch. Jonas Singo kwa mafundisho yenye kugusa moyo kupitia Kipindi cha Turejee Madhabahuni. Tumekumbush...
01/06/2026

Tunamshukuru sana Mch. Jonas Singo kwa mafundisho yenye kugusa moyo kupitia Kipindi cha Turejee Madhabahuni. Tumekumbushwa umuhimu wa kurejesha uhusiano wetu na Mungu, kujenga maisha ya maombi, kujifunza Neno la Mungu na kufanya ibada ya familia kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku.

Katika dunia yenye shughuli nyingi na changamoto mbalimbali, wito wa kurejea madhabahuni ni wito wa kurejea kwenye chanzo cha nguvu, amani na ushindi wa kweli. Tusiwe wasikilizaji wa neno pekee, bali tuwe watendaji kwa kuyafanyia kazi mafundisho tuliyopokea.

Tunamshukuru sana Mch. Thomas Bihene kwa mafundisho yenye kujenga kuhusu mahusiano na ndoa. Kupitia mafundisho haya, tum...
01/06/2026

Tunamshukuru sana Mch. Thomas Bihene kwa mafundisho yenye kujenga kuhusu mahusiano na ndoa. Kupitia mafundisho haya, tumekumbushwa umuhimu wa kumweka Mungu katikati ya mahusiano yetu, kuishi kwa usafi wa moyo kabla ya ndoa, na kujenga ndoa juu ya msingi wa upendo, heshima na uaminifu.

Mahusiano mazuri hayajengwi kwa hisia pekee, bali kwa maamuzi sahihi, mawasiliano bora na kumtii Mungu. Vivyo hivyo, ndoa yenye mafanikio huhitaji kujitoa, uvumilivu na kujifunza kukua pamoja kila siku. Tuchukue yale yote tuliyojifunza na kuyatumia katika maisha yetu ili kujenga familia imara zitakazomtukuza Mungu.

Tunamshukuru sana Dr. Magomere kwa mafundisho yenye thamani kuhusu afya na lishe bora. Maarifa tuliyopokea si kwa ajili ...
01/06/2026

Tunamshukuru sana Dr. Magomere kwa mafundisho yenye thamani kuhusu afya na lishe bora. Maarifa tuliyopokea si kwa ajili ya kusikika tu, bali ya kutusaidia kufanya maamuzi bora yanayolinda afya zetu na familia zetu.

Tukumbuke kuwa afya njema hujengwa na uchaguzi wa kila siku. Tuwe na nidhamu ya kuzingatia kanuni tulizofundishwa kuhusu lishe bora, mazoezi, mapumziko ya kutosha na mtindo wa maisha unaokuza afya. Elimu bila matendo haileti mabadiliko; hivyo tuyafanyie kazi yale yote tuliyojifunza ili tuwe na maisha yenye afya na yenye furaha.

Watu wengi wanamiliki Biblia, lakini si wote wanaoruhusu Neno la Mungu libadilishe maisha yao. Biblia haikuandikwa kwa a...
31/05/2026

Watu wengi wanamiliki Biblia, lakini si wote wanaoruhusu Neno la Mungu libadilishe maisha yao. Biblia haikuandikwa kwa ajili ya kuwekwa kwenye kabati au kubebwa tu, bali ni ili isomwe, itafakariwe na kuiishi kila siku.

Neno la Mungu linapopata nafasi moyoni, hubadilisha fikra, tabia na mwelekeo wa maisha. Fungua Biblia yako, na umpe Mungu nafasi ya kukubadilisha.

NJOMBE – Mkutano wa uinjilisti wa Njombe Net Event 2026 wenye kaulimbiu ya “Tumaini Lenye Baraka” umehitimishwa kwa mafa...
31/05/2026

NJOMBE – Mkutano wa uinjilisti wa Njombe Net Event 2026 wenye kaulimbiu ya “Tumaini Lenye Baraka” umehitimishwa kwa mafanikio makubwa mkoani Njombe, ukisimamiwa na Chama cha ATAPE kwa kushirikiana na Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania.

Katika hitimisho la mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mheshimiwa Antony Mtaka, alikabidhiwa Tuzo na Cheti cha Utambuzi kwa kuthamini mchango wake mkubwa katika kuunga mkono shughuli za kanisa na ushirikiano wake wa karibu na Chama cha ATAPE katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijamii na kiroho.

Viongozi wa ATAPE walieleza kuwa Mheshimiwa Mtaka ameendelea kuwa mshirika muhimu wa kanisa tangu kuanzishwa kwa mikutano hiyo, jambo ambalo limechangia mafanikio ya shughuli mbalimbali zinazolenga kuleta maendeleo na ustawi wa jamii.

Mkutano huo uliwakutanisha washiriki, viongozi wa dini, wadau na wawezeshaji mbalimbali kwa lengo la kuhubiri injili, kuimarisha maadili na kuhamasisha matumaini kwa wananchi kupitia mafundisho ya kiroho na huduma za kijamii.

ATAPE wametoa shukrani za dhati kwa washiriki wote, wadau, viongozi, wawezeshaji na kila aliyeshiriki kwa namna moja au nyingine kufanikisha mkutano wa Njombe Net Event 2026, wakieleza kuwa mkutano huo umeendelea kuwa chombo muhimu cha kuleta tumaini, mabadiliko chanya na baraka kwa watu wengi katika jamii.

Watu wanaweza kukukatisha tamaa, kukuhukumu au hata kukuacha katika nyakati ngumu za maisha. Lakini Yesu habadiliki. Upe...
30/05/2026

Watu wanaweza kukukatisha tamaa, kukuhukumu au hata kukuacha katika nyakati ngumu za maisha. Lakini Yesu habadiliki. Upendo wake haupimwi kwa mafanikio yetu wala hauondolewi na mapungufu yetu. Hata tunapoanguka, bado anatuita kwa neema na kutupa tumaini la kuanza upya. Ndani ya Kristo daima kuna tumaini lenye baraka.

UKAWE NA SABATO NJEMA YENYE MIBARAKA TELEUsisahau Kesho kuungana pamoja nasi katika Mianzo ya Njombe Net Event 2026 utab...
08/05/2026

UKAWE NA SABATO NJEMA YENYE MIBARAKA TELE

Usisahau Kesho kuungana pamoja nasi katika Mianzo ya Njombe Net Event 2026 utabarikiwa zaidi🙏

Address

Mbweni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0756075004

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Southern Tanzania Union Mission posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share