27/06/2018
MFIKIE MTOTO UUFIKIE ULIMWENGU
by Bulengela AncoB
Mkutano wa Idara ya Huduma za Watoto ulioandaliwa kwa ushirikiano wa Majimbo makuu yote mawili, umehitimishwa tarehe 26 June 2018, ambapo wajumbe zaidi ya 170 wamepatiwa mafunzo ya Malezi ya Watoto, Kuendesha masomo ya Kiungo Cha Neema, ufundishaji ulio hai, kukuza imani, kuwahusisha Watoto katika kujifunza, ni baadhi tu ya Masomo. Tutarajie maboresho na ufanisi toka kwa waalimu hawa.
Baadhi ya sentensi makini;
"Watoto wenye umri wa Miaka 12 wanapoonyesha wamekuwa wakristo na kutaka kubatizwa wasizuiwe, wabatizwe endelea kuwafundisha, ukiwazuia wakagairi itakuwa ngumu kuwarejesha tena" Mr. Yusto E. Mwano- (NTUC)
"Tuwalinde Watoto wetu wasisikilize, kutazama na kujaribisha kila kitu kisicho katika wakati sahihi na Wala kwenda sehemu za starehe"; WAVULANA sikia "usichongechonge penseli yako itaisha kabla ya mtihani"; WASICHANA sikia usifungue soda yako asubuhi gesi itaisha kabla ya sherehe, maana sherehe ni jioni" Pr. Eli Mchome
"Na tukomeshe unyanyasaji kwa Watoto wetu katika Mambo ya kiroho, tuwapatie viti wasikae chini, tusiwape wadogo zao kuwabeba/kuwalea darasani, wapewe mazingira Bora na zana za kujifunzia; Darasa liwe angalau watoto watatu. Tuwalinde" Mrs Hodia Mtani - mkurugenzi Jimbo dogo la kusini mwa Tanzania (SHC)
"Na tuwekeze kwa Watoto sasa maana wakati fulani hatutakuwepo; wao ndio watalitegemeza Kanisa la Mungu" Pr. Mariam Samo - Mkurugenzi Jimbo kuu la kaskazini mwa Tanzania NTUC
"Wengine wameonekana kukimbizana na Watoto wao ili kuwaadhibu; Usimkimbize mtoto K**a kuku, ili kumwadhibu, umitaka kumk**ata kuku dondosha mahindi msululu Hadi kwenye Banda k**ata Chinja. Sikia msubiri mtoto atakuja kwenye Banda/nyumbani ndipo shughulika naye", Ndege ni wako manati ya nini?" Mrs. Devota Shimbe - Mkurugenzi Jimbo dogo Mashariki na Kati (ECT)
Kuwafundisha kwa jinsi iliyohai kutawafanya Watoto kuelewa haraka na kuuhisi upendo wa Mungu kwao. Mrs Neema Erasto M. Mkurugenzi Jimbo dogo la Kusini Mashariki mwa Tanzania (SEC).
Ni Busara kutambua utofauti si wa umri tu Bali tukitambua tofauti ya Kizazi na Kizazi, itasaidia kuleta mlingano wa urithishaji wa elimu, ujuzi na ufahamu. Mrs. Ruth Eyembe - Mkurugenzi Jimbo kuu la Kusini mwa Tanzania (STUM)
Pongezi Vongozi wa Majimbo Makuu ni Miriam Shamo (NTUC) na Mrs. Dr. Ruth Eyembe (STUM)