Cornerstone Bible Baptist Church

Cornerstone Bible Baptist Church Church services

We pray that the good Lord gives you victory every step of the way. As you turn a year older, keep in mind that we will ...
08/10/2020

We pray that the good Lord gives you victory every step of the way. As you turn a year older, keep in mind that we will continue following the light you have shown and made us beleive in. We love you Pastor, Happiest Birthday Pastor!

Tunasherehekea na kufurahia maisha yako Baba. Tunakuombea maisha marefu ukiendelea kulitimiza kusudi uliloitiwa hap duniani.

Team ya Vijana,
Cornerstone Bible Baptist Church.
+1 highly favored.

Life begins at 40.
Zaburi 90:12.

Heri ya siku yako ya kuzaliwa Mch Peter Kitang'wa            +1 Lead Pastor,Cornerstone Bible Baptist Church.Kigamboni, ...
06/10/2020

Heri ya siku yako ya kuzaliwa Mch Peter Kitang'wa

+1

Lead Pastor,
Cornerstone Bible Baptist Church.
Kigamboni, kisiwani.

WEMA KATIKATI YA UBAYA>> Katika Ulimwengu wa leo tunaoishi, ni kawaida watu kupishana au kukosana kwasababu mbalimbali.>...
23/09/2020

WEMA KATIKATI YA UBAYA
>> Katika Ulimwengu wa leo tunaoishi, ni kawaida watu kupishana au kukosana kwasababu mbalimbali.
>> Na mara nyingi watu wakifanyiwa ubaya au wakifanyiana ubaya na wao huwa wanataka kulipa kisasi yaani kulipa ubaya kwa ubaya.
>> Sisi k**a watu wa Mungu hatutakiwi kulipa baya kwa baya au kulipiza kisasi kwa watu waliootufanyia ubaya. Tunakiwa “tusishindwe na ubaya, bali tuushinde ubaya kwa WEMA.” Warumi 12:21
>> Tunatakiwa kuiga mfano wa Yesu.
>> Yesu aliushinda ubaya wa ulimwengu kwa wema wa kujitoa kwa ajili ya wengine bila kujali wangapi walimkubali na wangapi hawakumkubali.
>> Si kazi yetu kulipa kisasi, kisasi ni juu ya Bwana. Warumi 12:19

>> Mungu atusaidie tuushinde kila UBAYA kwa kutenda WEMA kwa kila mtu.

USHINDE UBAYA KWA KUTENDA WEMA

Mtumishi William Michael
Cornerstone Bible Baptist Church
Kigamboni, Kisiwani,
Karibu.

Zekaria 2:8 “Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; m...
19/09/2020

Zekaria 2:8
“Kwa maana BWANA wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake.”

Mimi ni mboni ya jicho lake; wewe ni mboni ya jicho lake. USIJIDHARAU.


UBAYA KATIKATI YA WEMA~ Kuna wakati katika maisha wema wetu unachochea ubaya kati ya watu wanaotuzunguka.~ Lengo kuu la ...
15/09/2020

UBAYA KATIKATI YA WEMA
~ Kuna wakati katika maisha wema wetu unachochea ubaya kati ya watu wanaotuzunguka.
~ Lengo kuu la kufanya wema ni kuwa mwema kwa watu na kuishi vizuri na watu wote wanaotuzunguka.
~ Lakini, mitazamo na mapokeo ya watu wakati unawatendea wema yanaweza kuwa hasi, na mtokeo yake ni UBAYA KATIKATI YA WEMA.
~ Hata Yesu mwenyewe, watu wale wale aliowahurumia wakati wana njaa akawapa mikate, aliwaponya magonjwa wakati ni wagonjwa na kufanya miujiza mingi katikati yao; NDIO HAO HAO WALIOPAZA SAUTI ZAO NA KUPIGA KELELE KUWA ASULUBIWE. (Yohana 6:10-12 & MATHAYO 27:22-23)
~ Pamoja na hayo yote, neno la Mungu linatutaka kuwapenda watu wote pamoja na hao wanaotuudhi (Mathayo 5:44)
~ Tumetaadharishwa kuwa makini na wanadamu tunaowafanyia wema ( Mathayo 10:17) lakini tusiache kutenda wema (Wagalatia 6:9).

Upo ubaya katikati ya wema, lakini usishilikiane na ubaya na wala usichoke kutenda mema. (Luka 6:35)

sitoshirikiana na ubaya na sitaacha kutenda mema #

Mtumishi William Michael
Cornerstone Bible Baptist Church,
Kigamboni, Kisiwani.
Karibuni sana.
Mungu akubariki sana.

UMOJA UNAVYOWEZA KUIMARISHA FAMILIAZaburi 133:1 “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja....
01/09/2020

UMOJA UNAVYOWEZA KUIMARISHA FAMILIA
Zaburi 133:1
“Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.”
>> Biblia inasema ni vema na inapendeza ndugu wanapokaa pamoja lakini sio tu kukaa pamoja, bali wanapokaa pamoja na kwa umoja.
>> Ipo nguvu kubwa sana katika Umoja; waswahili wanasema Umoja ni Nguvu, utengano ni udhaifu.
>> Familia yenye nguvu ni familia inayokaa pamoja na kwa umoja. Familia yenye nguvu ndiyo inayoleta kanisa lenye nguvu (Ibada njema inaanzia nyumbani).
>> Kanisa k**a kanisa linaweza kufanikiwa katika vitu vingi k**a likiwa na umoja.
>> Kanisa ni mwili wa Kristo, na sisi sote tu viungo katika mwili wa Kristo.
>> Waefeso 4, inaelezea juu ya Umoja katika mwili wa Kristo.

Tuweni na Umoja k**a Wao walivyo wamoja
Yohana 17:22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja k**a sisi tulivyo na umoja.

Mtumishi Obedi Christopher,,
Cornerstone Bible Baptist Church,
Kigamboni, Kisiwani,
Karibuni.

UTUKUFU MPAKA AIBU (HOSEA 4:7)~ Maisha ya mwanadamu akiwa duniani yamejawa na mahitaji mengi sana.~ Mahitaji mengi ya mw...
25/08/2020

UTUKUFU MPAKA AIBU (HOSEA 4:7)

~ Maisha ya mwanadamu akiwa duniani yamejawa na mahitaji mengi sana.
~ Mahitaji mengi ya mwanadamu ni kwa ajili ya kuridhisha matamaniyo ya moyo.
~ Moyo ukisharidhika unatabia ya kujisahau/kujidanganya. Yeremia 17:9
~ Mahitaji ya mwanadamu hupelekwa mbele za Mungu k**a maombi.
~ Wapo watu wanamuomba Mungu cheo, nafasi, pesa, kampuni, ndoa, nyumba, heshima n.k.
~ Kuna wakati Mungu hatupi tumuombayo, sawa sawa na maombi yetu, kwa sababu tunaomba vibaya. Yakobo 4:3
~ Kuna wakati Mungu anatupa, yale tunayoyaomba sawa sawa na maombi yetu, kwa ajili ya UTUKUFU wake. Waefeso 3:20
~ Lakini baada ya kupata tunayoyahitaji, baada ya kupata majibu ya maombi yetu, badala ya kumpa Mungu utukufu tunajisahau na kujitwalia wenyewe utukufu. Tunakuwa wajuaji, viburi, kisilani n.k Luka 12:16-19
~ Lakini hicho kinachokufanya ujitwalie utukufu, Mungu anao uwezo wa kukibadilisha na kuwa aibu mara moja. Luka 12:20 & Hosea 4:7

>>> Tumefanya au tulifanya au tunafanya neema ya Mungu ni kubwa kuliko makosa yetu.
>>> Mungu anatutaka tumrudie na kutubu na atatubariki tena kwa utukufu wake. Matendo 3:19

MWISHO WA UTUKUFU WA MWANADAMU NI AIBU

Mtumishi William Michael,
Cornerstone Bible Baptist Church,
Kigamboni, Kisiwani,
Karibuni.

HAKUNA UTUKUFU BILA AIBU~ Hakuna kuinuliwa bila kupita kwenye aibu au changamoto mbalimbali (Dhahabu hupita kwenye moto)...
24/08/2020

HAKUNA UTUKUFU BILA AIBU
~ Hakuna kuinuliwa bila kupita kwenye aibu au changamoto mbalimbali (Dhahabu hupita kwenye moto).
~ Na hii ndo maana kuna mithali nyingi wahenga waliziweka kuonyesha hilo k**a vile “Mchumia juani hulia kivulini”.
~ Hata Biblia nayo imejaribu kuelezea jambo hilo kwenye mithali ya Mfalme Suleiman
“Mithali 13:11 Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.”
~ Hata Yesu kabla kupewa utukufu wote na mamlaka yote alipita/alipitishwa kwenye maisha ya aibu kwanza.

MAISHA YA YESU MPAKA UTUKUFU
1. Alizaliwa mahali pa aibu, mahali pa chafu ( kwenye z**i la kulia ng’ombe) Luka 2:1-7
2. Yesu hakuwa na mahali pa kulala(nyumba) katika kipindi chote cha huduma yake au utumishi wake hapa duniani. Luka 9:57-58
3. Ndugu zake walimdhihaki, walimdharau wakati wa kipindi cha huduma/ utumishi wake. Mathayo 13:55-57
4. Yesu aliteswa, alijeruhiwa na alichubuliwa. Marko 15:16-20

>>Mwisho wa yote, Yesu anatukuzwa na kupewa mamlaka juu ya Yote. Yohana 17

> Heshima ya mwanadamu yoyote ni kumiliki kitu,> Hatuwezi kuishi au kuchukua maisha ya mbinguni kuyaleta au kuyaishi dun...
04/08/2020

> Heshima ya mwanadamu yoyote ni kumiliki kitu,

> Hatuwezi kuishi au kuchukua maisha ya mbinguni kuyaleta au kuyaishi duniani wakati tumeuvaa mwili,

> Mafanikio yoyote hapa duniani hayaji ghafla, mafanikio yoyote yanaanza na maandalizi.
Mithali 10:4

> Kufanya kazi kwa uvivu/ulegevu ni maandalizi ya kuwa maskini.

> Hivi tulivyo leo ni maandalizi yaliyofanywa Jana.

Hatuwezi kumiliki chochote tusipojiandaa.

Mch Peter Kitang'wa
Cornerstone Bible Baptist Church,
Kigamboni kisiwani.



KUTAWALA NA KUMILIKI (1)Zaburi 24:1Vitu vyote vijazavyo nchi ni mali ya Bwana, na sisi tu watoto wa Mungu kwahiyo ni mal...
22/07/2020

KUTAWALA NA KUMILIKI (1)

Zaburi 24:1
Vitu vyote vijazavyo nchi ni mali ya Bwana, na sisi tu watoto wa Mungu kwahiyo ni mali zetu pia ila hatujui jinsi ya kuvitawala na kumiliki.

Luka 15:25-32
Habari ya mwanampotevu.
Mwana mkubwa hakujua k**a vitu vyote alivyonavyo baba yake ni mali zake pia, hivyo alishindwa kuvitawala na kuvimiliki.

Pastor PK,
Karibu Cornerstone Bible Baptist Church.




#2020

Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe...
14/07/2020

Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?
Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote?

MUNGU YUPO UPANDE WETU, HAKUNA AWEZAYE KUWA JUU YETU.
MUNGU ANATUKIRIMIA NA MAMBO YOTE, MUNGU YUPO NASI.

Karibu Cornerstone Bible Baptist Church,
Kigamboni, Kisiwani Makaburini.

Address

Kisiwani, Kigamboni
Dar Es Salaam
36061

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Cornerstone Bible Baptist Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share