Al-Furqaan TV

Al-Furqaan TV Al- Furqaan is a well-established faith-based Islamic organisation registered since 2008.

ISRAEL NA HEZBOLLAH ZAFYATULIANA MAKOMBORA MPAKANIJeshi la Israel limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya anga kwenye...
01/02/2024

ISRAEL NA HEZBOLLAH ZAFYATULIANA MAKOMBORA MPAKANI

Jeshi la Israel limetangaza kuwa limefanya mashambulizi ya anga kwenye miundombinu na majengo ya kijeshi ya Hezbollah kusini mwa Lebanon.

Siku ya Alhamisi asubuhi, Hezbollah ya Lebanon ilirusha makombora mawili kutoka kwa vifaru vyake kuelekea eneo la jeshi la Israel katika Mlima Hermon kaskazini mwa Israel, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Israel.

Hakuna habari iliyoripotiwa kuhusu majeraha yoyote.

Jana usiku, Hezbollah ilitangaza kuuawa kwa mmoja wa wanachama wake, na kufanya idadi ya vifo kufikia 177 tangu Oktoba 8.

UKRAINE YAISHAMBULIA NA KUIZAMISHA MELI YA URUSI KWA MAKOMBORAVikosi vya Ukraine vinasema kuwa vimeharibu mashua ya kuru...
01/02/2024

UKRAINE YAISHAMBULIA NA KUIZAMISHA MELI YA URUSI KWA MAKOMBORA

Vikosi vya Ukraine vinasema kuwa vimeharibu mashua ya kurusha makombora ya Urusi katika operesheni maalum katika eneo la Crimea linalokaliwa na Urusi.

Ivanovets - meli ndogo ya kivita - ilishambuliwa "moja kwa moja " na kuzama, ilisema idara ya ujasusi ya jeshi .

Ukraine imetoa picha za video ambazo zinalenga kuonyesha wakati wa shambulizi ikifuatiwa na mlipuko mkubwa.

Hakujakuwa na tamko lolote kuhusu tukio hilo kutoka kwa mamlaka ya Urusi.

Hata hivyo, mwanablogu wa kijeshi wa Urusi "Voenkor Kotenok" aliandika kwenye mtandao wa Telegram kwamba boti hiyo ilikuwa imezama baada ya kushambuliwa mara tatu na ndege zisizo na rubani.

Vipengele kadhaa vinavyoonekana kwenye meli kwenye video ya Ukraine vinalingana na Tarantul, au Project 12411, boti za makombora zinazoendeshwa na wanamaji wa Urusi na Ivanovets ni mali yake.

Hii ni pamoja na mpangilio wa mlingoti na vitambuzi juu ya muundo wake.

Idara kuu ya Ujasusi ya Ukraine ilisema mashua hiyo iliharibiwa na wanajeshi wa kitengo chake maalum cha "Group 13" katika Ziwa Donuzlav, ghuba ya maji ya chumvi upande wa magharibi wa peninsula ya Crimea ambayo ina kambi ya jeshi la wanamaji.

Ilisema meli hiyo ilikuwa na thamani kati ya $60-70m (£47m-55m).

WATU 215 WAMEPOTEZA MAISHA GAZA KATIKA SAA 24 ZILIZOPITAWizara ya afya katika Ukanda wa Gaza imesema kwamba takriban wat...
30/01/2024

WATU 215 WAMEPOTEZA MAISHA GAZA KATIKA SAA 24 ZILIZOPITA

Wizara ya afya katika Ukanda wa Gaza imesema kwamba takriban watu 26,637 wameuwawa katika eneo hilo la Palestina katika vita kati ya kundi la wanamgambo la Hamas na Israel.

Taarifa ya wizara hiyo imesema idadi hiyo inajumuisha vifo vya watu 215 vilivyotokea ndani ya kipindi cha saa 24 zilizopita, huku watu 65,387 wakiwa wamejeruhiwa tangu vilipozuka vita hivyo Oktoba 7.

Wakati huo huo, waziri wa usalama wa Israel kutoka kambi ya wenye misimamo mikali, Itamar Ben Gvir amewatolea mwito walowezi wa Kiyahudi kurejea Gaza.

Matamshi ya waziri huyo yaliyotolewa jana mbele ya mkusanyiko mkubwa, yameibuwa kauli za hasira kutoka kwa Wapalestina wanaosema yanaongeza makali ya mwito unaolenga kuwalazimisha Wapalestina waihame ardhi yao.

Kauli ya waziri huyo wa usalama wa Israel inapishana na msimamo wa serikali uliotolewa na waziri mkuu Benjamin Netanyahu uliosisitiza kwamba Israel haina dhamira ya kuikalia Gaza.

WAZIRI MKUU WA ZAMANI PAKISTAN AHUKUMIWA MIAKA 10 JELAMahakama maalum Pakistan, yamkuta na hatia Waziri Mkuu wa zamani I...
30/01/2024

WAZIRI MKUU WA ZAMANI PAKISTAN AHUKUMIWA MIAKA 10 JELA

Mahakama maalum Pakistan, yamkuta na hatia Waziri Mkuu wa zamani Imran Khan ya kuvujisha siri nyeti za serikali kwa umma na kumuhukumu kifungo cha miaka 10 jela. Chama chake kimesema kitakata rufaa.

Hukumu hiyo imetolewa leo Jumanne na mahakama maalum mjini Islamabad ikiwa zimebaki siku 10 nchi hiyo iingie kwenye uchaguzi mkuu.

Hukumu ya kifungo cha miaka 10 dhidi ya waziri mkuu wa zamani Imran Khan imewaghadhabisha wanasiasa kwenye chama chake cha Pakistan Tehreek e-Insaf,kinachosema ni hukumu kali kabisa kuwahi kutolewa hadi sasa dhidi ya mwanasiasa huyo wakati nchi ikijiandaa kuingia kwenye uchaguzi mkuu.

Mahakama maalum iliyokuwa ikisikiliza kesi hiyo imemkuta Imran Khan na hatia ya kuvujisha kwa umma siri za serikali zilizokuwa kwenye ujumbe uliotumwa kwa serikali ya Islamabad na balozi wa Pakistan mjini Washington.

Kesi hiyo pia imemuhusisha waziri wa zamani wa mambo ya nje Shah Mehmood Qureshi aliyehukumiwa kifungo cha miaka 10

Wakili wa Imran Khan, Naeem Panjutha amesema hawakubaliani na uamuzi huo wa mahakama ambao kwa mtazamo wao sio halali na kwamba chama cha PTI, yaani Pakistan Tarek-e-Insaf cha mwanasiasa huyo kitachukua hatua kuupinga uamuzi wa Mahakama.

Chanzo DW

30/01/2024
Education for better life
09/12/2022

Education for better life

*Bismillah Rahmanir Rahiim.*    *TAARIFA KWA WOTE.*  ```Shule ya  Awali na Msingi AL-FURQAAN iliyopo Mtaa wa Minga Manis...
09/12/2022

*Bismillah Rahmanir Rahiim.*

*TAARIFA KWA WOTE.*

```Shule ya Awali na Msingi AL-FURQAAN iliyopo Mtaa wa Minga Manispaa ya Singida inawatangazia kuwa kuna nafasi kwa wanafunzi wanaotaka kuanza darasa la Awali na darasa la kwanza na pia nafasi za kuhamia kwa darasa la 2 mpaka darasa la 6.
``` ```Kwa wale wanaotaka kuhamia kwa madarasa tajwa hapo juu``` *USAILI* ( *interview)* utafanyika siku ya Jumatatu tarehe *12.12.2022* Saa mbili asubuhi hapa shuleni *AL-FURQQAN.*
Ndugu wazazi wenye watoto shuleni AL-FURQQAN K**a Kuna ndugu,jamaa na marafiki wanaotaka kuwasomesha wanao shuleni *AL-FURQQAN* tunawaomba muwape taarifa kuwa *USAILI* ( *interview)* utafanyika tarehe 12.12.2022 hivyo wawalete watoto wao kwa ajili ya Usaili(Interview).
```MLETE MWANAO SHULENI APATE ELIMU BORA NA MALEZI BORA .

KARIBUNI SANA AL-FURQAAN``` .

28/03/2022

Assalaam Alaykm... Yaa Allah nakuomba mjaalie mja wako huyu utulivu katka nafsi yake, tabasam katika uso wake, siha katika mwili wake, tawfiq katika maisha yake na nuru katika kaburi lake baada ya umauti wake... Aamin 🤲🏼

Address

Dar Es Salaam
KINONDONI

Telephone

+255716830856

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Al-Furqaan TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Al-Furqaan TV:

Share