30/01/2026
HESHIMU WATU – Tafakari ya leo
Ndugu zangu wapendwa, leo napenda tuchukue muda tufikirie maneno hili: KUWAHESHIMU WATU, nasema kuwaheshimu wafu na zinasema mtu.Hapa maanisha wakiwemo hata wale walio dhaifu.
Kwa nini?
Kwanza, lazima tujue kuwa kila kiumbe aliye duniani, iwe binadamu au mnyama, pengine hata mimea Mungu amemuumba kwa ajili ya kusudi lake na moja wapo ya kimakusudi hayo ili mwanadamu aishi duniani kwa furaha. Fkiria kuhusu dunia bila uwepo wa mimea itakuwaje?.
Kwa hiyo Hata viumbe au watu wale ambao kwa mtazamo wa dunia hawawezi kuonekana kuwa na thamani mfano vichaa, Mungu amewaweka kwa kusudi maalum.
Amewaweka ili wafanyiwe msaada kwako wakati wa uhitaji wakiwa, wakati wewe mwenyewe huwezi kutatua changamoto yako, hivyo hatupaswi tukisha kwa upendo na kuheshimu uimbaji wa Mungu.
Mfano: Mungu aliwatumia nzige na simba kuwadhibu wale waliokiuka maagizo yake. (2Wafalme17:25-26)
Mfano mwingine: Rahabu, kahaba, alitumika kuokoa Waisraeli, na pia akahifadhi familia yake. (Yoshua 2:1-21), japo ukweli alikuwa kahaba, na pengine family yake haakumdhamini kwa tabia yake ya ukahaba lakini ndiye ayealiwaokoa
Hivyo basi, si jambo jema kuwabeza wengine kwa sababu ya hali yao ya sasa. Kwa macho ya dunia wanaweza kuonekana dhaifu, watu wenye dhambi au wasio na thamani, lakini jua kuwa Mungu anaweza kuwatumia katika baraka au msaada ambao haukutarajiwa.
Ngoja niseme hili. N kweli Mungu anachukia dhambi, dhambi hututenga mbali na Mungu, dhambi inaharibu mpango wa Mungu katika maisha yetu. Lakini nataka ufahamu kuwa Mungu akiamua kumsogelea mwenye dhambi, dhambi basi itakimbia yenyewe wala haiwezi kamwe kumchafua Yesu.
Ngoja niseme kwa mifano.
Tunasoma habari za
Mama aliyeugua ugonjwa wa kutoka damu kwa muda mrefu alipomsogelea Yesu, alihisi huruma na kuponywa bila kumdharau na tunaona kwa dhambi za yule mama hakumdhuru Yesu. (Marko 5:25-34)
Unaona hapa. Kwa muijibu k**ani au sheria za Musa mtu akitokwa na damu alikuwa anatengwa na wengine kwa sababu yu najisi na chochote atakachogusa kitakuwa najisi. Lakini unaona huyu mama alipomgusa Yesu, Yesu hakuwa najisi
Binti aliyepasua kibweta cha mafuta kumgusa Yesu, ingawa alikuwa mwenye dhambi, ile dhambi yake haikumdhuru Yesu bali iliondoka kwa yule mama maana Yesu alisema umesamehewa dhambi zako.(Mathayo 26:6-13)
Hivi ndicho inavyokuwa pale Mungu huamua kutupa zawadi ya wokovu, hatusomgelei sisi kwanza ingali tuna dhambi zetu, si kwamba tunaanza sisi kinaongelewa Mungu la hasha bali Mungu ndiye kuanzisha mchakato wa wokovu ndani yetu.
Ni vema tuelewe kuwa hata sisi kabla ya kumjua Mungu tulikuwa tumechafuka na dhambi, neema ya kristo kupitia Damu yake imetusafisha. K**a vile tulivyo pata neema hiyo jua kubwa hata hao Mungu aweza kuwapa neema hiyo.
Mara nyingi Mungu huwaleta watu katika maisha yetu kwa sababu maalum
Kila mtoto, kila mtumishi, kila mtu aliye karibu nawe ana sababu maalumu kwako, anaweza kuwa chombo cha baraka.
Mfano: Yosefu, aliyekuwa houseboy, ndani ya nyumba ya Potufa alileta amani na baraka ndani ya nyumba ya Potifa. (Mwanzo 39:2-6)
Potifa alipotazama baraka hizi zote ajua hakika zimekuja kwa sababu ya huyu kijana Josefu, akaamua kumheshimu kwa kumfanya awe mkuu wa nyumba yake.
Ninani aliyetarajia kuwa Josefu atakuja kuwa msaada kwa taifa lote la Misiri?.vipi wale mak**anda kule gerezani walio mtumikisha Josefu walijisikiaje Joseph alipoinuliwa juu ya taifa zima.
Mfano mwingine: binti wa nyumba ya mkuu wa majeshi, alileta uponyaji wa ukoma. (2 Wafalme 5:1-14)
Binti huyu mtumwa katika nyumba ya majeshi huyu alileta furaha ya kudumu kwa majeshi huyu mashuhuri
Kwa hivyo, usiwanyanyase wale walio chini yako au dhaifu kwako, labda ni binti wa kazi au ni mfanyakazi wako n.k, waombee, wapende na uwalee kwa upando Wanaweza kuwa msaada wa Mungu, hata k**a leo hawaonekani sasa kubwa na thamani.
Ukweli wa upendo
Heshimu watu,hata wale walio dhaifu. Hii inatufundisha kuwa kila mtu anstahili upendo na heshima, kwa sababu hatuwezi kujua mpango wa Mungu katika maisha yao.
Angalia, Yesu alikuwa wanafunzi wake wa karibu sana, sasa angalia alipo kufa wanafunzi wake wote wakakimbia, huoni wakijadili namna ya kumzika Bwana wao kaburini hawapo kabisa. Lakini Mungu alimwinua mtu asiyejulikana, wala hakuwa na ukaribu au urafiki na Yesu, Yosefu ndiye uweka mwili wa Yesu kaburini kwa gharama zake mwenyewe. (Mathayo 27:57-60).
Usiwe na kiburi kwa sababu umezungukwa na watu muhimu, huwezi jua je ni yapi atakaye kutwa misaada kwako.Heshimu watu.
Kumbuka tabia mhimu ya Mungu tunaye mwabudu ni kubwa yeye ni pendo na anata wote wamwabuduo wawe na tabia ileile aliyo nayo.
"K**a mtu anasema: ‘Ninaupendo kwa Mungu,’ lakini hana upendo kwa ndugu yake, ndiye mdanganyifu." (1 Yohana 4:20)
Hitimisho
Heshimu kila mtu unayemkutana naye, iwe maskini, mdhambi, mzee au mtoto.
Upendo na heshima kwa wengine huonyesha uwepo wa Mungu katika maisha yetu.
Usiwe na dharau kwa wale ambao bado hawajapata wokovu; Mungu anaweza kuwatumia baraka zisizotarajiwa katika siku zijazo.
Tafakari leo: je, unawaona wote walio karibu nawe kwa macho ya upendo na heshima, au unaona tu kile wanacho au hawana?
Neno Ministry -Tz
Mwl.Samuel A.Mwakatajila
© January 2026