Neno Ministry

Neno Ministry Ukrasa huu ni kwa ajili ya kujifunza na kuelimishana juu ya imani ya kikristo

‎‎HESHIMU WATU – Tafakari ya leo ‎‎Ndugu zangu wapendwa, leo napenda tuchukue muda tufikirie maneno hili: KUWAHESHIMU WA...
30/01/2026


‎HESHIMU WATU – Tafakari ya leo

‎Ndugu zangu wapendwa, leo napenda tuchukue muda tufikirie maneno hili: KUWAHESHIMU WATU, nasema kuwaheshimu wafu na zinasema mtu.Hapa maanisha wakiwemo hata wale walio dhaifu.

‎Kwa nini?

‎Kwanza, lazima tujue kuwa kila kiumbe aliye duniani, iwe binadamu au mnyama, pengine hata mimea Mungu amemuumba kwa ajili ya kusudi lake na moja wapo ya kimakusudi hayo ili mwanadamu aishi duniani kwa furaha. Fkiria kuhusu dunia bila uwepo wa mimea itakuwaje?.

‎ Kwa hiyo Hata viumbe au watu wale ambao kwa mtazamo wa dunia hawawezi kuonekana kuwa na thamani mfano vichaa, Mungu amewaweka kwa kusudi maalum.

‎Amewaweka ili wafanyiwe msaada kwako wakati wa uhitaji wakiwa, wakati wewe mwenyewe huwezi kutatua changamoto yako, hivyo hatupaswi tukisha kwa upendo na kuheshimu uimbaji wa Mungu.

‎Mfano: Mungu aliwatumia nzige na simba kuwadhibu wale waliokiuka maagizo yake. (2Wafalme17:25-26)

‎Mfano mwingine: Rahabu, kahaba, alitumika kuokoa Waisraeli, na pia akahifadhi familia yake. (Yoshua 2:1-21), japo ukweli alikuwa kahaba, na pengine family yake haakumdhamini kwa tabia yake ya ukahaba lakini ndiye ayealiwaokoa

‎Hivyo basi, si jambo jema kuwabeza wengine kwa sababu ya hali yao ya sasa. Kwa macho ya dunia wanaweza kuonekana dhaifu, watu wenye dhambi au wasio na thamani, lakini jua kuwa Mungu anaweza kuwatumia katika baraka au msaada ambao haukutarajiwa.

‎Ngoja niseme hili. N kweli Mungu anachukia dhambi, dhambi hututenga mbali na Mungu, dhambi inaharibu mpango wa Mungu katika maisha yetu. Lakini nataka ufahamu kuwa Mungu akiamua kumsogelea mwenye dhambi, dhambi basi itakimbia yenyewe wala haiwezi kamwe kumchafua Yesu.

‎Ngoja niseme kwa mifano.

‎Tunasoma habari za
‎Mama aliyeugua ugonjwa wa kutoka damu kwa muda mrefu alipomsogelea Yesu, alihisi huruma na kuponywa bila kumdharau na tunaona kwa dhambi za yule mama hakumdhuru Yesu. (Marko 5:25-34)

‎Unaona hapa. Kwa muijibu k**ani au sheria za Musa mtu akitokwa na damu alikuwa anatengwa na wengine kwa sababu yu najisi na chochote atakachogusa kitakuwa najisi. Lakini unaona huyu mama alipomgusa Yesu, Yesu hakuwa najisi

‎Binti aliyepasua kibweta cha mafuta kumgusa Yesu, ingawa alikuwa mwenye dhambi, ile dhambi yake haikumdhuru Yesu bali iliondoka kwa yule mama maana Yesu alisema umesamehewa dhambi zako.(Mathayo 26:6-13)

‎Hivi ndicho inavyokuwa pale Mungu huamua kutupa zawadi ya wokovu, hatusomgelei sisi kwanza ingali tuna dhambi zetu, si kwamba tunaanza sisi kinaongelewa Mungu la hasha bali Mungu ndiye kuanzisha mchakato wa wokovu ndani yetu.

‎Ni vema tuelewe kuwa hata sisi kabla ya kumjua Mungu tulikuwa tumechafuka na dhambi, neema ya kristo kupitia Damu yake imetusafisha. K**a vile tulivyo pata neema hiyo jua kubwa hata hao Mungu aweza kuwapa neema hiyo.


‎Mara nyingi Mungu huwaleta watu katika maisha yetu kwa sababu maalum

‎Kila mtoto, kila mtumishi, kila mtu aliye karibu nawe ana sababu maalumu kwako, anaweza kuwa chombo cha baraka.

‎Mfano: Yosefu, aliyekuwa houseboy, ndani ya nyumba ya Potufa alileta amani na baraka ndani ya nyumba ya Potifa. (Mwanzo 39:2-6)

‎Potifa alipotazama baraka hizi zote ajua hakika zimekuja kwa sababu ya huyu kijana Josefu, akaamua kumheshimu kwa kumfanya awe mkuu wa nyumba yake.

‎Ninani aliyetarajia kuwa Josefu atakuja kuwa msaada kwa taifa lote la Misiri?.vipi wale mak**anda kule gerezani walio mtumikisha Josefu walijisikiaje Joseph alipoinuliwa juu ya taifa zima.


‎Mfano mwingine: binti wa nyumba ya mkuu wa majeshi, alileta uponyaji wa ukoma. (2 Wafalme 5:1-14)

‎Binti huyu mtumwa katika nyumba ya majeshi huyu alileta furaha ya kudumu kwa majeshi huyu mashuhuri

‎Kwa hivyo, usiwanyanyase wale walio chini yako au dhaifu kwako, labda ni binti wa kazi au ni mfanyakazi wako n.k, waombee, wapende na uwalee kwa upando Wanaweza kuwa msaada wa Mungu, hata k**a leo hawaonekani sasa kubwa na thamani.

‎Ukweli wa upendo

‎Heshimu watu,hata wale walio dhaifu. Hii inatufundisha kuwa kila mtu anstahili upendo na heshima, kwa sababu hatuwezi kujua mpango wa Mungu katika maisha yao.

‎Angalia, Yesu alikuwa wanafunzi wake wa karibu sana, sasa angalia alipo kufa wanafunzi wake wote wakakimbia, huoni wakijadili namna ya kumzika Bwana wao kaburini hawapo kabisa. Lakini Mungu alimwinua mtu asiyejulikana, wala hakuwa na ukaribu au urafiki na Yesu, Yosefu ndiye uweka mwili wa Yesu kaburini kwa gharama zake mwenyewe. (Mathayo 27:57-60).

‎Usiwe na kiburi kwa sababu umezungukwa na watu muhimu, huwezi jua je ni yapi atakaye kutwa misaada kwako.Heshimu watu.

‎Kumbuka tabia mhimu ya Mungu tunaye mwabudu ni kubwa yeye ni pendo na anata wote wamwabuduo wawe na tabia ileile aliyo nayo.

‎"K**a mtu anasema: ‘Ninaupendo kwa Mungu,’ lakini hana upendo kwa ndugu yake, ndiye mdanganyifu." (1 Yohana 4:20)

‎Hitimisho

‎Heshimu kila mtu unayemkutana naye, iwe maskini, mdhambi, mzee au mtoto.

‎Upendo na heshima kwa wengine huonyesha uwepo wa Mungu katika maisha yetu.

‎Usiwe na dharau kwa wale ambao bado hawajapata wokovu; Mungu anaweza kuwatumia baraka zisizotarajiwa katika siku zijazo.

‎Tafakari leo: je, unawaona wote walio karibu nawe kwa macho ya upendo na heshima, au unaona tu kile wanacho au hawana?

Neno Ministry -Tz
Mwl.Samuel A.Mwakatajila
© January 2026



🌱 TENDO LIGUSALO HISI ZA MTU 🌱Kulikuwa na watu wawili ambao japo walikuwa juu ya uso wa nchi lakini walishi dunia mbili ...
16/01/2026

🌱 TENDO LIGUSALO HISI ZA MTU 🌱
Kulikuwa na watu wawili ambao japo walikuwa juu ya uso wa nchi lakini walishi dunia mbili tofauti kabisa.

Mmoja aliitwa Mwalinyasyo – tajiri, mwenye mali nyingi, lakini moyo wake haukuwa na nafasi ya kumsikiliza Mungu. K**a ilivyoandikwa katika Mithali 18:11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni k**a ukuta mrefu katika mawazo yake. Mwingine aliitwa Kisoti – kijana maskini sana, asiye na kitu cha kujivunia isipokuwa upendo wake kwa Mungu na kwa watu.

Kisoti alikuwa mgeni wa kudumu katika kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu. Hakwenda huko kwa sababu ya kamera, wala kwa sifa. Alienda kwa sababu ya moyo. Aliwaombea watoto, aliimba nao nyimbo za kumsifu Mungu, na aliwafundisha kuwa thamani yao haipungui kwa sababu ya hali yao.
“Bwana yu karibu na waliovunjika moyo.” (Zaburi 34:18)

Siku moja, akiwa katikati ya watoto hao, wazo zito likamgonga moyo wake:
“Laiti watoto hawa wangekuwa na baiskeli za walemavu, wangetabasamu zaidi, wangetembea kwa uhuru zaidi.”
Lakini mara moja akakumbuka ukweli mchungu — umasikini wake. Alikuwa na nia, lakini hakuwa na uwezo.
Usiku ule hakutaka akitafakari na kuomba Mungu ameonyeshwa njia.Akitafakari kwa muda mrefu, na mwisho akapata wazo kumwendea rafiki yake tajiri,

Alipofika kwa Mwalinyasyo.
Kwa unyenyekevu akasema:
“Rafiki yangu, moyo wangu unatamani jambo moja tu… je, waweza kunisaidia?”
Mwalinyasyo akajibu kwa mzaha:
“Usiniambie tena habari za Mungu, nilishakuambia sitaki kusikia.”
Kisoti akatabasamu kwa utulivu:
“Sio habari za Mungu leo. Naomba msaada wa viti na baiskeli za walemavu 100.”
Tajiri akacheka kwa sauti:
“Basi sawa, nitakusaidia. Lakini acha hayo mambo ya Mungu, nianzishe biashara kwanza.”
Kisoti hakubishana. Alishukuru.
Kwa sababu upendo haubishani, upendo hutenda na kuvumilia.
“Upendo huvumilia yote.” (1 Wakorintho 13:7)

Tajiri Mwalinyasyo akafanya haraka kuagiza Mzigo, mzigo ukafika bandarini DSM, Mwalunyasyo akambidhi Kisoti. Kisoti alimshutumu Mwalunyasyo na kusema naomba pia unisindikeze kwa watoto hawa, wewe ndiye atakaye kabidhi zawadi hizi kwa watoto hawa.
Siku ya kukabidhi zawadi ikafika.
Mwalinyasyo, kwa mara ya kwanza, akaingia katika kituo cha watoto walemavu.
Walipoingia tu. Watoto walipomuona Kisoti walimkubalia na kumkumbatia wengine wakimbuzi kisoti mikono yake huku wakiimba nyimbo za kumsifu Mungu kwa furaha kuu.

Mwalunyasyo alisimama pale… akashangaa.
Watoto walikuwa wanacheka, wanaimba nyimbo za kumsifu Mungu, wakimkumbatia Kisoti kana kwamba ni ndugu yao wa damu. Hakukuwa na unafiki, hakukuwa na maigizo — palikuwa na furaha ya kweli.
Kisoti akawatuliza watoto na kusema:
“Leo, kila mmoja wenu atapokea zawadi ya baiskeli.”
Furaha ikalipuka tena. Nderemo, vifijo, machozi ya shukranivilitawala eneo lote la kituo.
Kisha Kisoti akaongeza kwa sauti ya upole lakini yenye uzito:
“Sio mimi nimenunua hizi zawadi. Mimi sina uwezo. Ashukuriwe Mungu, aliyempa mtumishi wake huyu mali, si kwa kujisitiri, bali kwa kuleta furaha kwa wengine.”
“Kwa maana kila mmoja amepewa kwa faida ya wote.” (1 Wakorintho 12:7)
Leo mtu huyu ametusaidia sisi pale mkono wetu hauwezi kuguswa , nasi kesho utamsaidia yeye pale mkono wake hauwezi kuguswa kwa njia hoi furaha yetu sote htumilika kwa maana Mungu aliumba ili tupate kuhitajikana. Amini nawaambieni hakuna hata mmoja wetu anaye kutosheleza kwa kila kitu.
Watoto walilia — si kwa huzuni, bali kwa kuguswa moyo na maneno ya Kisoti.

Mtoto mmoja akasimama na kusema:
“Nilidhani matajiri wanajali pesa zao tu. Leo nimeona upendo. Mtazamo wangu umebadilikakuhsu matajiri.”
Mwalinyasyo hakujua k**a anaota au yuko macho.
Alipoitwa kugawa zawadi, machozi yakamtoka. Akasema:
“Hakika Mungu anawapenda ninyi. Tunasikia wito wa kusaidia, lakini mioyo yetu huwa migumu. Sisi tuliojariwa uwezo lakini hata hatujui kwa nini tumeshakuwa uwezo, kwa sababu hoi tumejikita tunatumia kile tumejaliwa kwa vitu visivyo na maana.”
Watoto wakaimba kwa sauti:
“Mungu awasamehe nyote maana Mungu wetu humsamehe uovu.”
Walipokuwa wakiondoka, mtoto mmoja alimshika mguu Mwalinyasyo na kusema:
“Naomba uniambie jina lako. Nikifika mbinguni, nitakutafuta. Nataka uwe rafiki yangu milele.”
Njiani, Mwalinyasyo akamwambia Kisoti kwa sauti ya kunyenyekea:
“Nibatize. Nataka kuijua furaha hii. Nataka moyo wangu ubadilike.”
Tangu siku hiyo, Mwalinyasyo akawa mfadhili wa kituo kile.
Sio kwa kulazimishwa.
Bali kwa injili iliyohubiriwa kwa vitendo.
“Kwa maana nilikuwa na njaa, mkanipa chakula.” (Mathayo 25:35)

📌 FUNZO LA MAISHA
Ziko njia nyingi za kuhubiri injili.
Wakati mwingine mikono husema zaidi kuliko midomo.
Usimzuie mtu kutoa, hata k**a haamini k**a wewe.
Mwelekeze mahali sahihi pa kutoa— Mungu atafanya yaliyobaki.Nami nataka kukuambia kuna madhabahu iliyo hai katika kutoa sadaka zinazo visa maisha ya mtu binafsi hawa wahitaji wa kweli, Yesu ametufundisha hili kuptia
Mfano wa Msamaria Mwema (Luka 10:33–37)
❤️ Injili inayogusa maisha ndiyo injili inayoacha alama.

Na Mwl. Samuel A.Mwakatajila.

Neno Ministry
© January 16 2026

SALAMU ZA MWAKA MPYA 2026Kutoka kwa:Mwl. Mr & Mrs. Samuel A. MwakatajilaKwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakat...
01/01/2026

SALAMU ZA MWAKA MPYA 2026

Kutoka kwa:
Mwl. Mr & Mrs. Samuel A. Mwakatajila

Kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
Tunawasalimu wapendwa wote katika upendo wa Kristo Yesu.
Heri ya Mwaka Mpya! Tunamshukuru Mungu kwa ulinzi wake katika mwaka uliopita na kwa neema ya kutuvusha kuingia katika mwaka mpya wa matumaini, urejesho na mwanzo mpya.

“Hata hivyo fadhili za Bwana hazikomi, rehema zake hazina mwisho; ni mpya kila asubuhi.”
— Maombolezo 3:22–23

Mpendwa wetu tunapukaribisha mwaka 2026 tunapenda kukuhirikisha haya machache ambayo Roho wa Bwana amesema nasi katika safari ya kuelekea mwaka 2026. ametushirikisha juu ya HiTORIA

Ni jambo la kweli na la msingi kwamba hakuna mwanadamu asiye na historia. Hatuiombi historia ije, bali tunajikuta tumeibeba. Historia ni sehemu ya maisha, iwe ni ya furaha au ya huzuni, ushindi au maumivu.

Pengine unajiuliza: Historia ni nini?
Kwa ufafanuzi rahisi, historia ni mkusanyiko wa matukio ya maisha yaliyopita—maamuzi, makosa, majeraha, baraka, na mazingira yaliyotujenga au kutuumiza.

“Kumbuka siku za zamani, zitafakari miaka ya vizazi vingi.”
— Kumbukumbu la Torati 32:7

Cha kushangaza zaidi, hata jina la mtu linaweza kubeba historia, na mara nyingi historia huwa na tabia ya kujirudia kutoka kizazi hadi kizazi (Kutoka 20:5). Huzuni huwa nzito zaidi pale historia ya mtu au familia imejaa maumivu, kwa sababu maumivu huanza kuonekana k**a sehemu ya kawaida ya maisha.

Kwa maneno mengine, historia inaweza kuwa kikwazo kikubwa katika maisha ya kila siku—kiroho na kimwili. Hebu tulitazame jambo hili kwa mwanga wa Biblia.

HISTORIA KATIKA NURU YA BIBLIA

1. Historia ya familia: Kisa cha Yakobo

Tunaposoma habari za Yakobo, tunaona wazi namna historia ya familia ilivyokuwa kikwazo katika safari yake ya kupata mke aliyempenda (Mwanzo 29:25–26). Badala ya Raheli, alipewa Lea, kwa sababu ya desturi na historia ya familia:

“Haitendeki hivyo kwetu, kumpa mdogo kabla ya mkubwa.”
— Mwanzo 29:26

Hapa tunaona wazi kuwa historia ya familia ilimkwamisha Yakobo, hata katika jambo la msingi k**a ndoa.

👉 Hili si simulizi la kale tu. Hata leo:

Kuna familia zenye historia ya uchawi au migogoro

Kuna makabila yenye historia zinazowatisha wengine

Kuna mabinti na vijana waliokosa kuoa au kuolewa si kwa sababu hawakupendwa, bali kwa sababu ya historia ya familia

2. Historia inayohama kupitia jina

Biblia inatupa taswira ya kushangaza kuhusu majina. Jina linaweza kubeba kumbukumbu na tabia.

Kwa mfano jina Yuda:

Yuda mwana wa Yakobo alihusishwa na tamaa ya mali (Mwanzo 37:26–27)

Yuda Iskariote alimsaliti Yesu kwa fedha (Mathayo 26:14–15)

Hii haimaanishi kila aitwaye Yuda ni msaliti, bali inatufundisha kwamba historia inaweza kujificha hata katika majina, na bila Mungu kuingilia kati, historia inaweza kujirudia.

“Jina jema lapasa kuchaguliwa kuliko mali nyingi.”
— Mithali 22:1

3. Historia ya eneo: Kisa cha Nazareth

Nazareth ni mji aliokulia na kuzaliwa Yesu Kristo. Hata hivyo, jamii ilishangaa:

“Je, jambo jema laweza kutoka Bethlehemu?”
— Yohana 1:46

Hii inaonyesha kuwa mji huu ulikuwa na historia isiyotegemewa. Lakini Mungu akachagua eneo hilo hilo kuleta Mwokozi wa ulimwengu.

👉 Hili linatufundisha kuwa:

Eneo linaweza kuwa na historia mbaya, na k**a unafuatilia kwa ukaribu masomo yahusuyo ardhi na vitu vilivyo bebwa na a arithi ya mji huo utaelewa kuwa uko uhusiano kati ya mji na wakaazi wa mji huo.

Hata katika maisha haya hatushangai kuona kiongozi wa nchi ametoka eneo fulani, lakini kuna maeneo likitajwa tunajua hakuna kitu huko.

Lakini Mungu anaweza kubadilisha taswira ya eneo hilo

4. Historia ya mtu binafsi: Gideoni na Sauli

Gideoni

Gideoni alijiona mdogo kwa sababu ya historia ya familia yake:

“Kabila langu ni maskini zaidi… nami ndimi mdogo kuliko wote.”
— Waamuzi 6:15

Lakini Mungu alimwita:

“Bwana yu pamoja nawe, wewe shujaa hodari.”
— Waamuzi 6:12

K**a Mungu asingeingilia kati, Gideoni angepoteza fursa ya maisha yake.

Sauli (Paulo)

Baada ya kuokoka, kanisa lilimkimbia Sauli kwa sababu ya historia yake ya mateso:

“Wote wakamwogopa, wasiamini ya kwamba ni mwanafunzi.”
— Matendo 9:26

Ni mpaka Mungu aliingilia kati kupitia kwa mtumishi wake Barnaba ndipo huduma ya Paulo ilipata nafasi (Matendo 9:27).

👉 Hapa tunaona ukweli mmoja:
Historia inaweza kuwa kikwazo hata baada ya toba, k**a Mungu hakuingilia kati itakusumbua.

HISTORIA NA MAISHA YA SASA

Mpendwa, mifano ni mingi, lakini somo ni moja:
👉 Moja ya maadui wakubwa wa mafanikio ya kiroho na kimwili ni matukio ya historia ya maisha yako.

Mara nyingi, unapokaribia kuinuliwa, adui huitumia historian yako kukukwamisha

Biblia inamwita shetani:

“Msh*taki wa ndugu zetu.”
— Ufunuo 12:10

👉 Shetani hamsh*taki mtu asiye na hatima.
👉 Historia yako ndiyo ushahidi anaoutumia kukuzuia usiinuliwe.

Mfano wa Biblia – Kuhani Yoshua:

“Kuhani Yoshua alikuwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili amsh*taki.”
— Zekaria 3:1

Yoshua alikuwa:

Tayari kwa nafasi mpya

Tayari kwa huduma mpya
Lakini historia yake (mavazi machafu) ilitumika kumzuia.

Mungu hakubishana na Shetani kwa hoja juu ya HiTORIA hiyo, bali alimletea:

“Ondoleeni mavazi machafu.”
— Zekaria 3:4

👉 Hii inatufundisha kuwa:

Historia lazima iondolewe kabla ya kuinuliwa na si jambo mepesi kujitetea mwenyewe juu ya kikwazo vya histori maana ni ushahidi halali wa matendo yako, unamwitaji Yesu akusaidie

Mungu mwenyewe ndiye anayeondoa historia, si juhudi za mtu.

Wakati Mungu anakuinua, si shetani pekee anayekumbuka historia yako, bali hata wanadamu.

Mfano – Yesu Kristo:

“Je, huyu si mwana wa seremala? Tunamjua baba yake na mama yake.”
— Mathayo 13:55–57

Walimkataa Yesu si kwa sababu hakuwa na mafuta, bali kwa sababu:
👉 Walijua historia yake ya kimwili

Hata Biblia inasema:

“Hawakupata kuamwai.”
— Mathayo 13:58

👉 Kuna watu leo:

Hawawezi kukukubali k**a mchungaji kwa sababu wanajua jana yako

Hawawezi kukuona k**a kiongozi kwa sababu wanakumbuka makosa yako

Hawawezi kukuamini kwa sababu wanajua ulipotoka.

Ni historian ya nabii ndio humfanya nabii alitambulika e katika mji wake mwenyewe

Watu wengi leo hawajazuiliwa na watu, bali wamefungwa na sauti ya historia ndani yao.
Unajiona mdogo, dhaifu, hustahili—si kwa sababu ni kweli, bali kwa sababu historia imekufundisha hivyo.

“K**a mtu ajifikiriavyo moyoni mwake, ndivyo alivyo.”
— Mithali 23:7
HABARI NJEMA: MUNGU ANAWEZA KUBADILI HISTORIA YAKO.

Hatufahamu historia yako:

Ya ujana, Ya ndoa ,ya a jina lako, ya familia au eneo lako

Lakini tunamfahamu jambo moja kubwa kuwa Mungu hubadili histori za watu wake:

Isaya 43:19
“Angalia, nafanya jambo jipya; sasa linachipuka, je, hamlitambui? Nitaweka njia katika nyika, na mito jangwani.”

Alibadilisha:

Historia ya Gideoni aliye kutoka kabila masikini akawa mtu mkuu

Historia ya Bethlehemu, mji ulio dharauliwa ukawa ndio mkiwaalikozaliwa nasihi.

Historia ya Yabesi aliyelia kwa Mungu

“Ee Bwana, unibariki kweli, uipanue mipaka yangu.”
— 1 Mambo ya Nyakati 4:9–10

Mwaka huu mpya ni mwaka wa tumaini.
Ni mwaka wa kufutwa kwa historia mbaya.
Ni mwaka wa kuumbwa kwa jambo jipya.

“Angalia, nafanya jambo jipya.”
— Isaya 43:19
Mungu hana kuja kusahau, unapaswa jambo moja tu kumligna Mungu wako k**a alivyofanya Yabesi

Jambo moja muhimu saanà ni uwà mwagalifu sana vile unaishi leo kwa sababu leo ndio inajenga histori yako ya kesho

Tunataka kuomba pamoja nawe sasa k**a uko tayari, tuombe:

Ee Baba wa mbinguni,
Kwa jina la Yesu Kristo, tunakushukuru kwa maisha ya kila msomaji wa ujumbe huu.
Katika mwaka huu mpya, tunakuomba uingilie kati.

Bwana:

Futa historia ya maumivu

Vunja minyororo ya yaliyopita

Badilisha kumbukumbu za machozi kuwa ushuhuda

Uandike historia mpya ya baraka, neema na ushindi

“Nitawarejeshea miaka iliyoliwa na nzige.”
— Yoeli 2:25

Tunatangaza kwamba:
Historia mbaya haitatawala tena.
Neema yako itatawala.

Tunaomba haya kwa imani,
Kwa jina la Baba, la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

Amina.

Na Mwl.Mr&Mrs Samuel A Mwakatajila
Neno Ministry
Januari 1 2026

25/10/2025

Mathayo 7:12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.

04/09/2025

Uzinzi ni dalili ya kushindwa kucontrol mwili wako. Ni udhaifu sio sifa.
Kikojozi == Mzinzi

03/09/2025

Kristo ni yeye yule jana , leo hata milele

29/06/2025

PALIPO YESU YOTE... YANAWEZEKANA:

🕊️ "Kwa wanadamu haiwezekani; bali kwa Mungu, yote yawezekana." – Mathayo 19:26

Naomba niseme nawe kwa sauti ya utulivu alfajili ya leo.

Wakati mwingine, tunaangalia maisha yetu na kuona magofu.
Tunaona ndoto zilizokufa, maumivu yasiyoelezeka, hali zisizobadilika.
Lakini leo, Roho wa Mungu anatufunulia siri hii kuu:
Palipo Yesu... yote yanawezekana.

✍️ . PALIPO YESU, HAKUNA TENA KIKOMO

Ndugu yangu napenda ujue hili ya.kuwa, "unakuwa mali Yesu yupo na kumkaribisha ndani ya moyo wako, haukaribishi tu historia ya dini, unakaribisha nguvu ya kugeuza historia ya maisha yako."

📖 "Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu haiwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana." – Mathayo 19:26

Hakuna ugonjwa mgumu mno mbele zake.
Hakuna ndoa iliyochafuka sana isiyoweza kurekebishwa na mikono yake.
Hakuna mtoto aliye potea sana asiyepaswa kurudi.

Yesu si hadithi – Yeye ni msaada uliopo wakati wa mateso.

✍️. "PALIPO YESU HATA MAGONJWA HUTIBKA ".

Wengine wakikuona umevunjika, wanakutazama kwa huruma.
Yesu akikuona, anainua mkono wa kukuponya.

📖 "Kwa maana alisema, Nikiyagusa tu mavazi yake, nitaponywa... Mara chanzo cha damu yake kikakauka." – Marko 5:28-29

Yule mwanamke hakuhitaji majina makubwa, wala shangwe za watu.
Alihitaji tu Yesu.
Na alipoamua kumpa moyo wake – akaponywa.

🕯️ Wewe pia... mguse Yesu kwa imani. Hakuna anayegusa, halafu abaki vile alivyo.

✍️. jua hili " PALIPO YESU HATA VLIVYO KUFA HUPTA UHAI ".

Matha alijua kuwa Yesu angekuwepo ndugu yake asinge kufa. kumbe kifo kilitokea tu kwa sabau Yesu hakuwepo. Hii ni siri ya ajabu kujua kwamba Vitu vingi vimekufa maishani mwetu sababu Yesu hayupo.

Je nawe unaona vitu vimekufa?. si wewe peke yako lakini niayo habari njema kwako kuwa mwite Yesu vitapata uhahi.

esu akamwambia matha nipo hapa leo ndugu yako atakuwa hai tena. ndiyo Yesu abapo tokea mahali yote yalio kufa yana weza kuwa hai tena, anacho subiri ufungue mlango wa imani, ndio maana alimtaka Matha aamini ndugu yake ataishi.

Wengine walilia juu ya kaburi la Lazaro.
Yesu alilia – kisha akaita uzima kutoka kaburini!

📖 "Akasema kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje!" – Yohana 11:43

Roho Mtakatifu asema:
👉🏾 Ndoto zako hazijakufa, zimesinzia.
👉🏾 Ndani yako kuna wito uliozikwa — Yesu yuko tayari kuuita tena.
👉🏾 Hali yako haijafungwa na dunia, bali inangoja sauti ya Mwokozi.

Usiseme tena 'imechelewa'... pale Yesu alipo, saa haichelewi.

✍️ Mpendwa amini neno hili "PALIPO YESU, LAANA HUGEUKA NEEMA"

Ndio, Wanafunzi walikuwa wamekata tamaa baharini. Upepo ulikuwa mkali, mashua ikazidiwa. Lakini Yesu alipoinuka...

📖 "Akaiambia bahari: Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu." – Marko 4:39

Ule upepo unaokupiga sasa – si mwisho wako.
Yule anayesema kwa bahari, anaweza kusema pia kwa moyo wako:

"Tulia, mwanangu. Mambo hayajakwisha. Mimi ni Bwana wa dhoruba."

Ni kweli:

Unateseka? Umekata tamaa? Umepitia mengi ambayo huwezi hata kueleza? lakin Yesu anasena

➡️ "Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha." (Mathayo 11:28)

Palipo Yesu, hakuna mzigo mzito sana.
Hakuna giza refu sana.
Hakuna doa la dhambi lisilofutika.

Yesu hayuko mbali. Yuko karibu sana kuliko macho yako.
Anagonga mlango wa imani ndani yako , si kwa hasira, bali kwa upole.
je unaufungu leo?

15/06/2025

Shalom kanisa.
Tunamshukuru Mungu kutupa neema tena ya kuwepo hapa, hatukuwa hewani kwa muda mrefu account yetu ilipata shida. Asanteni kwa uvumilivu wenu na maombi yenu. Mungu awabariki nyote

17/09/2024

NAKULILIA TANZAaNIA

Bwana Yesu Asifiwe!.

Natamani kusema na tanzania siku ya ya leo. Lakini kabla ya kusema yale Robo wa Mungu ananihimiza kusema nawe Tanzania naomba tusome sote maandiko haya:

Nehemia 1:2-4
2 Hanani, mmoja wa ndugu zangu, akanijia, yeye na watu wengine waliotoka Yuda; nami nikawauliza habari za Wayahudi waliopona, hao watu wa uhamisho waliosalia; na habari za Yerusalemu.

3 Wakaniambia, Watu wa uhamisho, waliosalia huko katika wilaya ile, wamo katika hali ya dhiki nyingi na mashutumu; tena ukuta wa Yerusalemu umebomolewa, na malango yake yameteketezwa kwa moto.

4 Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni;
Na tena tusome pia kutoka katika kitabu cha

Danieli 9:2-3
2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.

Haleluya!.
Mpendwa tanzania katika maandiko haya tumeyasomo hapo juu tuona jambo ambapo linafanana likitokea kwa wahusika wawili tofauti.

Nehemiah alipata ufunfuo alipo sikia juu ya mji wake wa kuzaliwa ( Jerusalem) juu ya mambo mabaya yaliyo tokea, hii ikawa sababu ya Nehemiah kumtafuta Mungu.

kadhalika Daniel naye alipata ufunuo kwa kuvisoma vitabu akapata kujua majira yapasayo taifa la Israel kutoka katika utumwa na kurudi katika aridhi yake.

Mpendwa Tanzania ndugu zetu hawa milango yao ya fahamu ( macho na masikio) viliwasaidia kupata ufunuo kwa ajili ya taifa lao nao wakachukua hatua ya kiimani, unaona Mungu akiwasaidia.

Eh mpendwa Tanzania, je masikio yako na macho yako yamekusidiaje juu ya habari ulizo sikia na mambo uliyo yaona juu yako?. Je unachukua hatua gani.

Ndio, umesikia juu ya mauaji na utekaji watu wako unaoendelea katika aridhi yako Je unachukua hatua gani.

Kuna ripoti zingine zina sema watu 83 tangu mwaka huu uanze hawajulikani walipo, ikiwa ripoti hizo ni za kweli nami nitasema wazi kabisa kuwa Tanzania umezingirwa unahitaji msaada wa Mungu.

Tanzania si hayo ya utekaji tu, pia kuna tarifa kuwa kule Dodoma kuna mgaga wa kienyeji nyumbani kwake imfukuliwa miili ya watu 9 amabao walizikwa kwa kukalishwa sawa na Imani ya mganga huyo. mawili wa 10 ulipatikana polini aliko utupa. Haya yanafanyika juu yako Tanzania wato 10 sio jambo la kulifumbia macho.

Tanzania nikuambie ukweli kabisa kuwa dhamani ya utu wako imepotea kabisa umeithamini pesa kuliko utu. Zamani gari likipata akali watu wa eneo ambapo ajali imetokea walimiminika kutoa msaada kwa majeruhi.

Ajabu ni kwamba sasa hivi ajali ikitokea watu wanamiminika kwenda kuwasachi marehemu na majeruhi wa akali hiyo mifukoni mwano, wanapora mali zao, hata pale majeruhi angejitahidi kuonyesha yupo hai au ikilinda mali yake hupigwa na kummalizia afe kabisa, mmh hii ni laana kubwa. Badilika mpendwa wangu tanzania.

Nimesoma mitandaoni juu ya kifo cha Dreva wa basi nasafiri ni mabasi ya Mtei k**a sijakosea. Mwandishi anasimilia kuwa dereva huyu alipigwa na mtu mpaka umati ukampata huku abiria wake zaidi ya hamsini wakishuhudia na wengine wakichukua video bila kuwaamua pole Tanzania.

Hakika mambo yanayotokea kwako Tanzania hata ukiyasikia masikio yanawasha. Utafanya nini mpendwa?.

Unamwitaji Mungu akusaidia urudie utu wako wa kwanza umthamini binadamu mwenzako ndio utakaa salama.

Inawezekana ni kweli hauoni umhimu wa haya niyasemayo kwa kuwa msiba upo kwa jirani lakini siku ukifikà kwako utalia kwa uchungu sana na hutapata msaada.

Inaumiza mno mpendwa wako wako amekuaga asubuhi halafu harusi tena nyumbani nawe hujui nini kimempata, siku zinzidi kwenda aaah ni maumivu makali.

Unamwitaji Mungu akusaidia juu ya watu hawa wanao fanya matukio haya, naamini ni watanzania wenzako au ni watu toka nje.

Tanzania mtafute Mungu naye ataonekana kwako, wewe mwenyewe unaelewa kuwa hata serikali yako imesema haiwajui watu hao sasa utaponea wapi Tanzania k**a hauta mwita Mungu katika hili akusaidie.

Tanzania inawezekana nikweli serikali yako haiwajui watu hawa lakini ambo la kufurahisha ni kuwa Mungu anawajua na anao uwezo wa kuwakatilia mbali nawe hutawaona tena.

Ndio mwamini Mungu si unakumbuka hivi majuzi tu ulipo patwa na janga la Corona ulimlilia Mungu k**a taifa naye aliponya na ugonjwa ule hatari je k**a aliweza kukuokoa na ugonjwa usioonekana atashindwaje kukuponya na kikundi cha watekaji hawa, atashindwaje kukuponya na waganga k**a hawa wenye kuua watu.

Mwamini Mungu Tanzania.

Eeh kanisa nawe uko wapi njoo tumlilie Mungu wetu maana yeye ni mwema sana kwetu. Enyi maasikofu, mitumie, maanabii nayi wachungaji njooni tumlilie Mungu wetu.

Hebu katika Ibaada zetu sasa tuwe walau na dakikika kidogo tumlilie Mungu kusudi atuponye na watu hawa waovu wenye kujipatia utajiri kupitia damu za watu zisizo na hatua.

Tanzania chukua hatua sasa

Kwa wale watapenda kuungana nasi katika kuomba rehema na msaada wa Mungu juu ya jambo hili karibuni sana, tunakutana kupitia group la whatsapp ambapo maombi huwekwa na kila member hushiriki maombi hayo kwa muda apatapo nafasi ndani ya siku husika.

Huge nasi kupitia link hii
https://chat.whatsapp.com/HHQ1sACqiZ7CI7JQMXWLvo

Maombi yatanza jumapili, karibuni sana.

kumbuka Tunaunganishwa kwa Imani na tunaamini kila moja wetu hushiriki maombi haya. Shahid wetu wa kwanza kwamba tunaomba ni robo mtakatifu na shahid wa pili ni robo zetu zinazoshudia ndani yetu kwamba tumeomba au la.

Asante Tanzania kwa kunisikiliza naamini umenielewa.

Ni mimi mtazania mwenzako na kuhani wa Mungu aliye hai.
Mwl.Samuel A.
Neno ministry-tz
© September 2024

Shalom watendakazi wa Mubgu.Leo natamani tutete kidogo sisi kwa sisi. Hebu tusome kwanza mistari juu.Luka 8:39 "Rudi nyu...
27/08/2024

Shalom watendakazi wa Mubgu.

Leo natamani tutete kidogo sisi kwa sisi. Hebu tusome kwanza mistari juu.

Luka 8:39
"Rudi nyumbani kwako, ukahubiri yalivyo makuu Mungu aliyokutendea. Akaenda zake, akihubiri katika mji wote, yalivyo makuu mambo aliyotendewa na Yesu.

Haleluya!.
Katika andiko hili tunaona huyu ndugu akijitoa kumfuata Yesu katika huduma yake ili naye awe sehemu ya wale walio ongozana na Yesu na pengine apare kumtumikia.

Jibu la Yesu ni la kush*tusha anamwabia rudi nyumbani kwenu ukahubiri huko matendo makuu ambayo Mungu amekutendea.

Inawezekana hata sisi kwa nyakati tofauti tunakutana na jibu hili na pengine ikawa ngumu kwetu kuelewa. Kuna wakati tunajikuta Tupo mahali ambapo hapana hata godoro, maji yana rangi ya maziwa na pengine hakuna huduma mhimu. Wapendwa yatupasa tunashukuru Mungu pia kwa kutupa hata eneo la mama hiyo tumtumikie kwani hai pia wanaoishi eneo hilo ni Kazi ya Mkono yake Mungu na wanahitaji wokovu waningie zizini mwake

Fahamu kuwa kuna watumishi wanaomba Mungu awatume wakahubiri lakini yeye anawambia hapa a subiri au rudi kahubiri nyumbani kwako.

Wanaomba kwenda kuhubiri si kwa sababu wanataka sifa au mali hapana, kwa watumishi waliopewa Kazi na Mungu mnafahamu sana kuwa ni jambo liumizalo sana kwa mtumishi kukosa pa kutumika na wakati huo ndani yako kuna vitu Mungu anakupa. Kwa kweli ni k**a moto uwakao ndani yako.Nabii Yeremia alielezea hilo akisema

Yeremia 20:9
"Nami nikisema, Sitamtaja, wala sitasema tena kwa jina lake; basi, ndipo moyoni mwangu kumekuwamo k**a moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia."

Ndio ni ngumu kustahimili hali hiyo, ndio utalazimika kuomba Mungu lakini kwa hekima yake anasema subiri mwangu nikufundishe.
Ukiwa una agizo la Mungu huwezi kutulia kwa jweli.
Yeremia 47:7
Utawezaje kutulia, Ikiwa Bwana amekupa agizo? .....

Kwa hiyo wale tuliopata neema ya kuhudumu iwe kwa kuhubiri, kufundisha kuomba au kuimba n.k fanya kazi ya Mungu k**a vile hutakuwepo kesho ukijua kuwa kuna watu wanaitamani hiyo nafasi.

Si kwamba wanataka mahali penye faida wakahudumu hapo hapana na si kwamba nia yao sio njema hapana ila Mungu mwenyewe ameona vema wawe kielelezo katika familia zao na pengine bado anawaanda.

Hivyo sisi tulio jariwa kuzunguka kila mahali yatupasa tuseme asante Mungu kutupa neemahiyo ya kufika hapo palipo na maji ya rangi ya maziwa.

Huyu ndugu hakulalamika bali alirudi na kuhubiri habari njema kwa watu wa nyumbani make, sijui huko kqa watu wa nyumbani kwako kulikuwa na hali gani kimaisha, lakini yeye hakujali akarudi kuhubiri, hakujali kqa watu wanajua kuwa ni alikuja kichaa bali yeye akaza moyo wake kuhubiri injili.

Watumishi wakati umefika sasa hasa tuliopo hapa jijini au maeneo ya mjini tukumbuke kule tuliko zaliwa tukawahubirie ndugu zetu nao wapate neema hiyo tulionayo ndani yetu.

Mtume paulo pamoja na kuwa mhubiri wa kimataifa lakini bado arudi na kuwahubiria watu wa nyumbani mwake au eneo alikukulia

Matendo ya Mitume 21:13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.

Je kitu gani kinakutiisha kwenda kuhuri injili kwa watu wako?. Je unaogopa kufa, unaogopa nini. Hautakufa Yesu anaye kulinda mahali pengine ndiye huyo atakulinda na huko kwenu. K**a hatutarudi kwenda kuwahubiria ndugu zetu basi giza halitaondoka maeneo hayo na wataenelea kuwa watumwa wa mila zisizo faa. Twende leo tupeleke nuru ya kristo.

Najua kuwa makazi yetu ni maeneo ya mjini na sijasema tuhamie vijijini ba nashauri kuwa kqa sadaka zetu tupeleke injili kule, tuboreshe maeneo yao ya ibaada, tununue na spika ,mjenerata n.k. tupeleke huko. Tuundeni vikundi vya ijili, tutoe sadaka zetu turudi kuhubiri injili vijijini mwetu tusipo hubria sisi nani akahubiri huko. K**a hatuwezi kwenda wenyewe basi tutumie watu waende wakahubiri huko utakuwa njema pia. Biblia imeuliza swali hili

Warumi 10:15
" Tena wahubirije, wasipopelekwa? K**a ilivyoandikwa, Ni mizuri k**a nini miguu yao wahubirio habari ya mema!"

Mpendwa twende tukahubiri nyumbani.
Mungu akubariki.
Mwl. Samuel A.Mwakatajila
Neno Ministry
© September 2024

Address

Mabibo Garage, , P. O. Box 7583
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share