15/12/2016
SHALOM NDUGU MSOMAJI WANGU
Leo tunaendelea na somo letu la IMANI ambalo tulilianza wiki iliyopita, hata hivyo naomba radhi kwa kwa kuchelewesha mwendelezo wake
KAZI YA IMANI AMA JINSI YA KUTENDA KAZI KWA IMANI
1 Imani ni suluhisho la peponi ambalo hutoa uhai, nguvu na vitendo kwa msukumo wa fikra
2 2 Imani pia ndiyo mwanzo wa malimbikizo yote mafanikio ya mtu na kila kitu anachokitaka ama alicho nacho maana kila kitu huanza kwa imani alafu kinakuwa katika uhalisia
3 Lakini pia imani ndio msingi wa miujiza na maajabu yote ambayo hayawezi kuchanganuliwa kwa kanuni za kisayansi
(mathayo 8;5-13)
4 Pia imani ni kiasili ama kemikali ambayo ikichanganywa na maombi humpa mtu mawasiliano ya moja kwa moja na nguvu kuu ya asili (MUNGU) (1 WAFALME18 ; 1-46)
5 Vile vile imani ni kiungo kinachobadilisha mtetemo wa kawaida wa fikra za mtu, unaotengenezwa na akili ya kawaida ya mtu kwaenda katika hali ya kiroho iliyokuwa na ukubwa sawasawa na imani yake aliyonayo,.
6 Imani ndiye wakala pekee ambaye kupitia kwake nguvu kuu zisizo za kawaida na zisizokuwa na mwisho (MUNGU) zinaweza kuvunwa na kutumiwa.
IMANI INAHITAJI VITU VIFUATAVYO KULETA MATUNDA
1 Kwa shauku uliyo nayo akilini mwako, hii hukufanya kuona kua imani uliyonayo kuwa inaishi na ipo siku kila kitu kitakua sawa
2 Uvumilivu ulionao katika hali unayo kutana nayo, Hapa wengi huwa tunaiacha imani tuliyonayo kwa kuona tumechelewa na kufuata ama kutafuta upande wa pili ambao ni lahisi kwetu na mwisho wake kupoteza kila kitu
Ukikutana na hali ngumu usikimbie imani uliyo nayo baali pigania imani yko hakika utaona matunda yeke
3 Lakini pia kuwa mbunifu kwa ili kuijega imani yako kwa kutafuta maarifa mapya kwa kuipanua zaidi na zaidi soma vitabu vitakatifu vinavyojenga imani
AMINA MPENDWA KWA LEO TUFIKIE HAPA KESHO TUTAENDLEA NA SOMO LETU BADO LINAENDELEA