28/07/2024
Askofu Dr.Peter Francis Lukindo muasisi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa kanisa la Christian Life Church. Napenda kuujulisha uma kuwa Mchungaji Dominique Kashala Dibwe alijiondoa Kanisani kwetu tangu tar 31/1/24 kwa kuhitaji kuwa na Kanisa lake mwenyewe.Tulishauriwa na ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Temeke turudishe kibali chake cha makazi nasi tulifanya hivyo kwa barua rasmi iliyopokelewa na Uhamiaji Makao makuu na kugongwa muhuri wa kupokelewa mnamo tar 3/4/24. Tulirudisha kibali chake cha makazi tangu tarehe hiyo. Nachukua nafasi hii kuipongeza Ofisi ya Msajili wa kiraia kwa kusimamia katiba na kanuni za Makanisa na kuchukua hatua stahiki kwa kulifungia Kanisa la Mchungaji huyo aliyejulikana pia km Kiboko cha Wachawi. Naambatanisha barua yake ya kujitoa kwake rasmi kwetu pia naambatanisha barua ya kukabidhi kibali chake cha makazi Uhamiaji ambayo nakala ilikwenda pia kwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.Christian Life Church tunaheshimu na kusimamia misingi ya Imani ya Kanisa la Kipentekoste.