07/06/2024
TAMANI KUTUMIWA KWA VIWANGO
Luka 2:25-26
25 Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
Bwana Yesu asifiwe mtu wa Mungu
Natamani urudie kusoma hiyo mistari hapo juu uuone upekee, heshima na neema aliyopewa mtumishi wa Mungu Simeoni, mpaka kutolewa mfano, na kuwa sehemu ya kutufundisha katika kizazi na vizazi sio kawaida kunakitu kikubwa alichokua amefanya kipindi chote cha maisha yake
Maandiko yanatuambia Simeon alikua mtu mwenye haki, mcha Mungu, hakua mcha-Mungu wakubabaisha bali alidhamilia kwa dhati kuwa mchaji, aliacha vyote na kumfuata Mungu, aliachana na dunia alifuata kutenda ya Mungu kiasi cha kushuhudiwa na Roho mtakatifu kuwa hata kufa kabla hajamuona mwokozi wa ulimwengu Kristo Yesu
Simeoni anatufundisha tujitoe asilimia 100 kwa Mungu, jua liwake na mvua inyeshe tusimuache Bwana, ikimaanisha tupitapo katika hali zote za raha na maumivu tusimuache Mungu tumtegemee yeye tumuamini yeye tufanye yaliyo yake tu
Mtunga zaburi ya 37:5 anatuambia ‘Umkabidhi Bwana njia yako, Pia umtumaini, naye atafanya.’, na anasema pia ‘Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.’, maana yake anataka tuzame kwake, tuzame ndani ya Roho mtakatifu ambae yeye ni kiongozi wetu, na yeye ndio nguvu yetu
Nikwambie Roho mtakatifu alimshuhudia Simeoni kuwa maono ya kumuona Kristo Yesu yatatimia, na ilimpasa Simeoni afanye bidii yakutunza yale maono, mtu wa Mungu haikua rahisi k**a unavyodhani, bali alijikana nakufuata maelekezo ya Roho mtakatifu, alikua ni msomi wa maandiko tunapata wapi kujua hayo, maandiko yanatuambia alikua mchaji, na mtu wa haki alijifunza kuishi katika haki na jinsi yakua mcha Mungu halisi
Injili ya Yohana mtakatifu mlango 4:23 unasema ‘Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu k**a hao wamwabudu’ Ili uwe mcha Mungu halisi, mwabudu halisi inatakiwa uwe mtu wakujifunza sana Neno la Mungu na kutenda, kuyaishi yale unayo jifunza, unapofanya kila siku ndipo unapokuja kuwa jabali la rohon katika uchaji na kupitia hayo utatamani kuwatendea watu mema, kutenda katika haki kwenye jamii unayoishi
Kwenye jamii yako, familia yako, na nchi yako tafuta kuwa watofauti, tafuta kuwa mtu wa Baraka kwa Wengine, tafuta watu wajifunze ucha Mungu wako na mazuri unayo yafanya ili hata utakapo ondoka kwenye ulimwengu huu yawepo mengi mema yanayoishi na kuwabariki watu badala yako na hapo tutasema huyu mtu amelala mauti lakini kazi zake zinaishi
Ili uweze kuacha alama isiyofutika kwenye ulimwengu huu lazima ujikane, lazima ujitoe jumla kwa Bwana, maandiko yanatuambia katika Warumi 12:1-2 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
Tunaonyeshwa mambo kadhaa kwenye hayo maandiko kuitoe miili yetu dhabihu kwa Bwana, kuishi kitakatifu, utakatifu unaozungumziwa hapo ni kujitenga na dhambi na mambo yasiyo faa mbele za Mungu, katika hayo ndipo kuna sehemu hautaweza kwenda ili kutunza uchaji ulio ndani yako, kuna mavazi hauta vaa kuendana na fasion ili kutunza uchaji wa rohoni, kwaujumla mtume Paulo anatuambia tusifuatishe namna ya dunia hii bali tugeuzwe kwa upya nia zetu katika Kristo,
Nia yamwili ni kutenda yasiyo faa mbele za Mungu lakini tunapaswa kuomba Nia zetu zigeuzwe zimtii Kristo na zitende yaki-Mungu{Ombea sana Nia yako} kwakua nia ndio inapelekea kuamua uishije na umfuate Mungu au laa
Mtu wa Mungu simeoni alimtafuta Mungu sana, nandie aliewekwa kuomba ili Bwana Yesu azaliwe, aliomba kuondoa vikwazo vitakavyozuia Kristo asizaliwe alikua yeye na Nabii mke Anna Binti Fanueli
Nikusihi na wewe mtu wa Mungu tamani kwa dhati kutumiwa na Mungu, na katika tamaa hizo tafuta kwabidii kuishi maisha matakatifu yanayo mpendeza Mungu, hata k**a akili na mwili havitaki lazimisha kumpenda Mungu na kufanya ya Ki-Mungu na kadiri unavyofanya ndivyo mabadiliko yanavyotokea katika maisha yako ambapo uchaji na haki vinadhihilika ndani yako
Ninakuombea badiliko kubwa na kuwa mtu wa viwango vyakuubadilisha ulimwengu katika jina la Yesu.
K**a umebarikiwa na ujumbe huu share kwa rafiki zako facebook na Whatsup. Pia like page yetu ya "Nyumba ya Sala kwa Mataifa Yote" kwa masomo mengi zaidi.
Ukipenda kutumiwa masomo ya Neno la Mungu tuma majina yako mawili kwenye whatsup nambari ya +255 657 048393, Kwa ushauri na maombi piga namba zilizopo hapo chini.
Merito Tagalile
+255 657 048393
Nyumba Ya Sala Kwa Mataifa Yote