21/03/2026
MWAMININI MUNGU - Hii ni siraha kubwa sana kwenye maisha yetu ya kila siku, hatua ya kwanza ya uponyaji wako, wa kuvuka kwenye vikwazo, kuona Mungu akikuvusha na kukupigania kwenye kila jambo na hali yoyote ni kumwamini yani kujenga imani ndani yako kwamba hakuna jambo lisilowezekana kwa huyu Mungu tunaemubudu katika Kristo Yesu.
_
Mahali popote ulipo anza kumuamini Mungu kwanza kabla ya mtu yoyote, amini kwamba Mungu anaweza kukuvusha hapo, anaweza kukuponya na magonjwa yote, na anaweza kukunyenyua tena mahali ulipoanguka.
_
Kwa namna gani utamwamini Mungu ni kwa kusoma Neno lake, kwa kusikiliza watumishi wa Mungu na shuhuda mbalimbali wanazozitoa watu ambao ameisha wavusha katika majaribu yao.
_
Sijui unapitia nini, ila nachoweza kusema mwamini Mungu, amini hilo tatizo lako linaenda kuisha maadamu umeomba na umemwamini Mungu aliye hai katika Kristo Yesu.