Baba paroko80

Baba paroko80 Bwana ndiye MCHUNGAJI wangu kamwe sintopungukiwa na kitu katika malisho ya majani YEYE uniongoza

NYWELE ZAKO ZIKUFUNDISHE, SAUTI YA MUNGU.Kwanini Mungu akuumbe hivyo ulivyo?usipoweza kuelewa utendaji kazi wa mwili wak...
01/10/2024

NYWELE ZAKO ZIKUFUNDISHE, SAUTI YA MUNGU.

Kwanini Mungu akuumbe hivyo ulivyo?

usipoweza kuelewa utendaji kazi wa mwili wako jinsi viungo vinavyoshirikiana huwezi kuelewa jinsi kanisa la Kristo linavyopaswa kufanya kazi likutanikapo, kwasababu sisi tunaitwa viungo mbalimbali ndani ya mwili wa Kristo.

Umeona?
Bwana akasema kiungo kimoja kikiumia, vyote vimeumia.

Hivyo tumeumbwa, kimalengo sio kimwonekano bora au kiuzuri,.
Ni sawa na mtu aulizwe kati ya jiko, na maua kipi kina umuhimu zaidi kuwepo ndani mwako.
Ni wazi kuwa atasema jiko,kwasababu litamsaidia kupika.
Hakulichagua kwasababu lina mwonekano bora, lakini kwasababu lina matumizi muhimu zaidi ya vingine.

Vivyo hivyo na wewe ujitazamapo mwili wako, usijitazame kiuzuri kuliko viumbe vingine, au wanadamu wenzako, bali fikiria tu katika picha ya matumizi ya kila kiungo ulichopewa, kinakufundisha nini kuhusu muumba wako au kinatimiza kusudi gani kwa Mungu wako.
Hilo ndio lengo hasaa la wewe kubuniwa hivyo ulivyo.

Leo tutaanza na NYWELE,

_Utazamapo nywele zako Bwana anataka ujue yafuatayo;_

1️⃣ *Mambo yako yote, yapo katika hesabu za Mungu.*

Mathayo 10:30-31
30 lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.
31 Msiogope basi; bora ninyi kuliko mashomoro wengi

Ni kawaida kudhani kuwa Mungu hathamini, au hajui kila kitu, au anasahau sahau. Lakini sivyo, ukimfuata Mungu, vitu vyako vyote vinavyotoka na kuingia vipo kimahesabu, hakuna kitu kinachotokea kwa ghafla tu, bila yeye kujua au kuruhusu, Hivyo mashaka yakija, kumbuka nywele zako zilivyo nyingi lakini zimehesabiwa, vivyo hivyo mambo yako yote yamehesabiwa.

2️⃣ *Huwezi epukana na maadui.*

Zaburi 69:4
4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli.
Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua

Jinsi nywele zako zilivyo nyingi, maadui nao vivyo hivyo.
Na maadui zetu sio wanadamu bali ni mapepo ambayo mara nyingine huweza pia yavaa wanadamu, kutudhuru. Hivyo usiwe mtu wa kunung’unika au kulamimika, ujue kila mwanadamu yupo vitani.
K**a Bwana wetu Yesu Kristo hakuwa na dhambi hata mmoja lakini alikuwa na jopo la maadui kwanini wewe usiwe nao.
Hivyo kuwashinda ni kuwa mwombaji daima, na kutembea katika njia za Bwana sikuzote.
Ukikumbuka kuwa maadui ni jambo la kawaida, k**a tu nywele zako zilipo hapo kichwani.

3️⃣ *Si kila kitu unaweza kufanya. hivyo kuwa na kiasi.*

Mathayo 5:36
36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.

Wakati mwingine, tunajiaminisha na kujihakikishia mambo na kuweka na viapo juu yake kana kwamba mambo yote yapo ndani ya uwezo wetu.
Kauli k**a, “leo nife,k**a sitakupa hiyo fedha” au “Mungu anipige hapa hapa k**a ninalokuambia ni uongo” Kauli k**a hizi, za kuongezea hakikisho lingine juu, hazitokani na Mungu, maneno yetu tumeambiwa yawe ndio ndio, au sio sio, zaidi ya hapo yanatokana na Yule mwovu.
Kwahiyo popote unapojiona unakaribia kuzidi mipaka kumbuka hizo nywele zilizo juu yako hujawahi kuzifanya ziwe hivyo ulivyo, Bwana ndiye azibadilishaye, hivyo jiwekee mipaka.

4️⃣ *Zithamini nguvu zako za rohoni.*

Nywele zako hufunua nguvu zako za rohoni. Wanadhiri wote wa Mungu hawakuruhusiwa kukatwa nywele, Samsoni alipewa nguvu, kwa agano la kutokatwa nywele, kufunua kuwa watakatifu wote nywele zao za rohoni ndio nguvu zao.
Lakini unapoacha mpango wa Mungu adui anazikata, k**a ilivyokuwa kwa Samsoni.
Lakini baadaye alipojua amefanya makosa ziliota tena lakini katika gharama za ‘kutoona’ tena.

Waamuzi 16:22
22 Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake.

Tunza nguvu zako, usiruhusu kiwembe chochote cha mwovu kikupitie.
Kwasababu hata zikirejea tena, hutakuwa k**a hapo mwanzo.

5️⃣ *Uwe na nyakati za maombolezo.*

Yeremia 7: 29
29 Zikate nywele zako, Ee Yerusalemu, uzitupe, Ukafanye maombolezo juu ya vilele vya milima; Kwa maana Bwana amekikataa na kukitupa Kizazi cha ghadhabu yake.

Zamani, kukatwa nywele zote kuisha kabisa ilikuwa ni ishara ya kuingia kwenye maombolezo, kwasababu utukufu wako umeuvua.

Maombolezo, kwa agano jipya sio kulia k**a msiba, hapana bali kuingia kwenye maombi ya ndani kabisa, ya kuutafuta uso wa Mungu, ambayo huambatana na mifungo. Na leo, ni kila mara tunakwenda saluni kukata nywele zetu.
Tujue Bwana anatutaka k**a vile tukatavyo nywele zetu mara kwa mara ndivyo tukumbuke maombi ya kujimimina sana mbele zake.

6️⃣ *Jisitiri*

1 Wakorintho 11:15
15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi.

Nywele ni vazi lililobuniwa na Mungu la kujisitiri hususani kwa mwanamke.

Uzitazamapo nywele zako, tambua, ni ujumbe wa kujisitiri mwili wako. Vaa vizuri.

Ubarikiwe saana
From Baba Paroko

NGUVU YA IMANI .Namtukuza Mungu kwa neema yake anayozidi kuiachilia juu yangu mimi na wewe hata kupata nafasi ya kukutan...
19/09/2024

NGUVU YA IMANI .

Namtukuza Mungu kwa neema yake anayozidi kuiachilia juu yangu mimi na wewe hata kupata nafasi ya kukutana tena na kujifunza neno la Mungu .

*IMANI NI NINI?*

*Neno la Mungu linaitaja Imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayi yaani ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Kwa lugha nyepesi Imani ni kuona vitu visivyoonekana kwa macho ya kawaida ya Damu na nyama.*

Waebrania 11:1
[1]Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

*Neno linaendelea kusema kuwa msingi wa kila anayemwabudu Mungu ni Imani juu ya huyo Mungu na Mungu anasema mwenye haki wake ataishi kwa kuona yasiyoonekana na sio kuishi kwa yale anayoyaona.*

Warumi 1:17
[17]Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; k**a ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.

*YAFUATAYO NI MAMBO AMBAYO IMANI INAWEZA KUFANYA/MAMBO UNAYOWEZA KUYAFANYA UKIWA NA IMANI*

Ukiwa na kiwango kikubwa cha imani kwake Yesu Kristo yaani kumwamini na kuyaishi maagizo yake kwa nguvu zako zote, akili yako yote na bidii yako yafuatayo ni mambo ambayo utaweza kuyapata kwa Imani yako kwake. (WAEBRANIA 11:32-40)

*1. USHINDI DHIDI YA VIKWAZO VYA WEWE KUSONGA MBELE*

Imani imebeba nguvu ya kushinda dhidi ya vikwazo ambavyo adui huvituma kwako ili upate kuangamia. Imani huinua ukuu wa Mungu katikati ya vikwazo na majaribu yanayoinuka na kushusa chini ukubwa wa jaribu.

Imani ndio iliyompatia Musa na taifa la Israeli kuondoka mikononi mwa Farao na kuanza safari ndefu ya kuelekea Kaanani kwa njia ngumu ya jangwani na hiyo hiyo ndio iliyowapa nguvu ya kupita kwenye maji pasina hofu.(Waebrania 11:33)

*Usitishwe na ukubwa wa jaribu lililopo na kuona litakumeza ila wewe mwamini zaidi Yesu Kristo mwenye nguvu na uwezo wa kukuvusha kwenye kwazo lililopo mbeleni naye atakushindia.*

*2. KUPOKOEA AHADI ZA MUNGU*

*Neno la Mungu limebeba ahadi nyingi, lakini ahadi hizi hazipo kwa yule anayezisoma tu au kuzisikia ila Ahadi hizi zipo kwao wale waaminio yaani walio na Imani.*

Neno la Mungu halitendi kazi kwa kila mtu anayepita ila hutenda kazi kwa yule ambaye ambaye hulisikia na kuliamini na kuona kuwa katikati ya Neno hilo ipo kweli na inaweza kutokea. (Waebrania 11:33)

*NENO LINASEMA " Aliutwaa udhaifu wetu na kuyachukua magonjwa yetu" lakini Neno hili linatenda kazi kwa yule mwenye Imani pekee kuwa Yesu aliyabeba Magonjwa na udhaifu wake.*

Walikuwepo wagonjwa wengi ndani ya Israeli yote na Yuda lakini waliopata kupona ni wale waliokuwa na Imani juu ya Uwezo wa Yesu Kristo. Waliopona sio wale waliomuita au kumshika mikono na hata kuishi naye ila waliopona ni wale waliomwamini kuwa anaweza kuwaponya.

Ahadi za Mungu hazipo kwa kila mtu tu ,hazipo kwa wasomaji wa Neno ,au wasikiaji wa Neno au wanaosali sana au kuomba ila zipo kwa wale wenye imani na uwezo wa NENO LAKE.

*Usiogope kupoteza ahadi za wanadamu ambazo walikuahidi, usiogope kupoteza kwa kumwamini Yesu Kristo ila kubali kuzipoteza ahadi za wanadamu kwa ajili yake Yesu Kristo kwani ndani ya wanadamu hakuna Mungu lakini ndani ya Mungu zipo ahadi*

*3. KUWAZUIA MAADUI WASIKUDHURU.*

Imani imebeba Nguvu ya kufunga mianya ya maadui kupitisha silaha za kukuangamiza yaani Imani ni ngao dhidi ya silaha na mabaya yote ambayo shetani anayatuma kwako yaani kila yakitumwa kwako kukuangusha chini hayawezi kwani yanakutana na Imani.

Imani ndio ambayo iliwafunga midomo simba ambao mfalme Nebukadreza aliwaandaa ili wamuangamize Danieli yaani simba wenye njaa ambao walitamani chakula hawakuweza kuinua mdomo kwa Danieli kwani Imani yake ilikuwa ngao kwake dhidi ya Simba wakali. (Waebrania 11:33)

*Hata wewe usitishwe na vitisho na maneno ya maadui wanayoyatuma kwako upate kuanguka ila simama na Yesu Kristo ambaye ndani yake anayonguvu ya kukukinga na silaha zote za maadui , Usiangalie ukubwa wa silaha zao ila mwangalie Yesu ambayo ndiye ngao yako*

*4. KUPUNGUZA UZITO NA UKALI MAUMIVU WAKATI WA MATESO*

Imani imebeba nguvu na ushindi mkubwa dhidi ya mateso yaani uchungu na maumivu ya nyakati ngumu huondolewa kwa uwezo uliopo ndani ya Imani yaani huwezi kushinda nyakati nguvu kwa kulisikia au kusoma tu Neno la Mungu ila unaweza kuzishinda kwa kuliamini na kuliishi Neno la Mungu k**a kweli inayoishi.

*Imani ndio iliyompa nguvu Ayubu ya kuvumilia mateso na magonjwa ambayo Ibilisi aliyainua juu yake akiamini kuwa Mungu atampatia makubwa zaidi ya yale aliyoyapoteza.*

Imani ilimpa nguvu ya kuvumilia maumivu ya kufiwa, kupoteza mali na vitu vyote vya mwilini na kuona yupo Mwingine ambaye anaweza kuyarejeshe yote pasina shaka.

*Hata wewe nyakati zako ngumu unazozipitia zisikudhoofishe ila mwamini Mungu ambaye atakuondolea maumivu na kukupa tumaini jipya kwenye teso lako yaani usiangalie ukubwa wa moto ila mtazame Mungu mwenye nguvu ya kuuzima moto*

*5. HUWAINUA WALIOANGUKA NA WALE WALIODHAIFU*

Imani imebeba nguvu na uwezo wa kutia moyo na kuwainua tena wale waliokata tamaa yaani wakati ambapo mwili huona haiwezekani Imani huinuka na kuupa mwili nguvu ya kusonga mbele na kuona inawezekana tena.

*Wakati madaktari wametoa taarifa kwako ya kuangamia na kuwa hauna maisha tena Imani huinuka na kukupa ujasiri kuwa "sitakufa nami nitaishi na kuyasimulia matendo makuu ya Bwana"*

Imani yako juu ya Mungu ndio itakayoamua k**a unaweza kuendelea kulala chini au unaweza kuinuka juu.

*IMANI NI KILE UNACHOKIONA PASINA UHALISIA, IMANI NI KILE UNACHOKIWAZA NA KUKINENA KINYWANI MWAKO

From Baba Paroko

WATENDA KAZI SHAMBANI MWA BWANA.Mathayo 9:3838 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.Ma...
05/09/2024

WATENDA KAZI SHAMBANI MWA BWANA.

Mathayo 9:38

38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

Maombi ni jambo kuu na la msingi sana.

Hapa biblia inasema TUOMBE
(Bwana apeleke watenda kazi).

Kumbe Maombi ya kuomba uamsho wa watenda kazi ni muhumu!.
Kwasababu hiyo basi ni lazima tujiwekee utaratibu wa mara kwa mara kuomba Bwana aongezee watenda kazi.

Na yafuatayo ni baadhi ya maeneno yanayohitaji watenda kazi zaidi.

1.KANISANI.

Hii ni sehemu ya kwanza inayohitaji watenda kazi.
Waalimu wa madarasa ya jumapili wanahitajika zaidi ndani ya kanisa,
halikadhalika waalimu wa watoto,
pia watendakazi katika kuongoza sifa
na maombi na wengine wengi.

Hivyo ni muhimu kutenga muda wa kutosha kumwomba BWANA anyanyue watenda kazi yeye anajua yupi anatafaa mahali fulani sisi kazi yetu ni kuzidi kumsihi Bwana awanyanyue wengi.

2. MASHULENI.

Shule kuanzia zile za awali (chekechea) mpaka zile za juu (vyuoni) panahitajika sana watenda kazi, watakaofanya kazi ya mavuno..

Hivyo ni muhimu watu wa Mungu kuomba ili Bwana anyanyue jeshi la watenda kazi (wahubiri) kwenye mashule.

Kwani mbali na mambo mazuri yanayopatikana mashuleni lakini.
huko huko pia ndio kitovu cha watoto kujifunza tabia chafu na kupokea maroho ya mapepo.

Na wakati mwingine ni ngumu mtu wa nje kuwafikia na kuwahubiria,
hivyo mimi na wewe tukisimama kumwomba Bwana anyanyue watenda kazi katikati yao,
basi Bwana atatusikia na kunyanyua vijana miongoni mwao huko huko waliko ambao watawatengeneza wenzao au atawanyanyulia walimu miongoni mwa walimu wanaowafundisha na watawafundisha na kuwakuza kiroho.

3. MAHOSPITALINI.

Hii ni sehemu ya tatu inayohitaji watenda kazi. Vituo vingi vya afya vinategemea kupokea watumishi kutoka nje kwaajili ya maombi kwa wagonjwa…

Wakati mwingine jambo hili linakuwa ni gumu sana,
kutokana ni vizuizi vya kiserikali na uchache wa watenda kazi…
na hivyo wagonjwa wengi wanakufa katika dhambi na wengine kuonewa vikali na ibilisi na mapepo yake yachocheayo magonjwa.

Lakini tukisimama kuomba kwamba Bwana anyanyue watenda kazi basi,
Bwana atasikia kwasababu ndiye aloyetuambia tuombe.

Na matokeo ya kuomba ni madaktari wengi kuokoka na manesi na wahudumu wa vituo hivyo vya afya na hivyo wagonjwa wengi wataombewa na kufunguliwa na kumpokea BWANA YESU, pasipo kusubiri watumishi kutoka nje.

4. SERIKALINI.

Hii ni sehemu ya nne inayohitaji watenda kazi wengi…
kwani huko serikalini ikiwemo katika mabunge, wizara na mahak**a,
adui anadhulumu wengi na kuwapoteza wengi, na hiyo ni kutokana na upungufu wa watenda kazi.

Lakini tukisimama kuomba,
Bwana YESU atasikia na kunyanyua watenda kazi ndani ya serikali..
Watanyanyuka watu mfano wa akina Danieli na Yusufu ambao watahubiri na kufundisha na kukemea kazi za ibilisi katika mahak**a,
bunge na katika asasi zote za serikali.

5. MITAANI.

Hili ni eneo la tano linalohitaji watenda kazi wengi…
Kwani katika mitaa ndiko watu wanakofanyia kazi,
wanakokusanyika katika vigenge vya mizaha,
au wanakofanyia mabaya.

Hivyo kunahitajika injili sana,
ili watu waokolewe…
na wakati mwingine inakuwa ni ngumu kufika kila mtaa kuhibiri,
au watumishi wa Mungu kuzunguka kila mahali kuhubiri na kuombea watu.

Lakini k**a tukisimama kumwomba BWANA anyanyue watenda huko basi kazi

(katikati ya hao hao wahuni, au hao hao wanaofanya kazi haramu, au wanaoketi katika vijiwe vya mizaha)

basi kazi ya injil itakuwa nyepesi sana na yenye matunda mengi.

Tutashangaa kuona wale waliokuwa walevi namba moja ndio wahubiri namba moja,
wale waliokuwa makahaba namba moja ndio wainjilisti namba moja n.k

6.MITANDAONI

Hii ni sehemu ya sita na muhimu sana inayohitaji watenda kazi.

Kwani katika mitandao ndiko watu wanakojifunzia mambo yote maovu,
ndani ya mitandao watu wanajifunza
mauaji,
kiburi,
uasherati,
uchawi,
utapeli,
wizi,
na mambo yote mabaya ambayo biblia inayataja k**a malango ya kuzimu.

Na wanaotumia mitandao hiyo kuhubiri habari njema ni wachache ukikinganisha na wale wanaoitumia kusambaza maovu.

Lakini tukisimama na kumwomba Bwana awageuze watu na kuwafanya watenda kazi shambani mwake,
tutaona mageuzi makubwa.

Kwani wale waliokuwa wanahamasisha wizi, uasherati,
utapeli na uhuni ndio watakaokuwa vipaumbele kuitumia mitandao hiyo hiyo kumhubiri YESU na kusaidia wengi,..

Wale waliokuwa watangazaji watageuzwa na kutangaza habari njema,
wale waliokuwa waigizaji wa tamthilia za mapenzi ya kishetani sasa wanatengeneza mafundisha ya kuwajenga watu kiroho n.k

Lakini ikiwa tutaomba kwa bidii sana.

Hayo ni meneo sita yanayohitaji watenda kazi, yapo na maeneo mengine mengi lakini haya sita ndio yenye vipaumbele zaidi.

Hivyo k**a mtu uliyeokoka usiishie tu kuombea familia yako,
au kazi zako au ndugu zako au kanisa lako..

Piga hatua zaidi kuombea ongezeko la watenda kazi katika shamba la Mungu,
kwani maombi hayo ni ya muhimu na yenye thawabu nyingi.

Mathayo 9:38 “Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.

SALA YA BWANA UtanguliziWanafunzi wa Yesu walimuomba awafundishe kusali k**a vile ambavyo Yohana aliwafundisha wanafunzi...
15/04/2024

SALA YA BWANA

Utangulizi

Wanafunzi wa Yesu walimuomba awafundishe kusali k**a vile ambavyo Yohana aliwafundisha wanafunzi wake kusali.
Naye Bwana akawafundisha sala ambaya inatambulika zaidi k**a Sala ya Bwana
(kwa sababu Bwana mweyewe ndiye aliyeifundisha)
aliwaambia msalipo semeni hivi;

"Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani k**a mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, k**a tunavyowasamehe na sisi waliotukosea, usitutie katika vishawishi, Lakini utuopoe na yule muovu"

Nyongeza katika sala ya Bwana, Baadaye katika sala ya Bwana maneno yafuatayo yaliongezwa

"Kwa kuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele Amina."

Ukuu wa sala ya Sala ya Bwana

Sala hii imepokea heshima na hadhi kubwa kwenye kanisa tangu wakati huo mpaka leo.

"Zipitieni sala zote zilizo katika maandiko na siamini k**a mtakuta humo kitu chochote ambacho hakimo katika sala ya Bwana"

"Sala ya Bwana ndiyo iliyo kamili kuliko sala zote.
Ndani yake hatuombi tu kile tunachoweza kutamani kwa haki, bali pia kadri ya mpango ambao unafaa kukitamani, hivi ni kwamba sala hii haitufundishi tu kuomba bali pia inaunda shauku zetu zote"

Sala hii zaidi ya yote inatupa mwongozo wa namna ya kuomba kwa Mungu wetu.
Ukiitazama inaonesha mfano wa sala iliyobora, yenye kuinua sifa na utukufu wa Bwana, kuomba msamaha na pia kupeleka maombi.

Maana ya maneno "Baba yetu Uliye Mbinguni"

Haya ndiyo maneno ya mwanzo katika Sala ya Bwana, maneno haya manne kwa pamoja yana maana kubwa sana;

Tunaaanza kuonesha ukuu wa Mungu, tunasema yupo juu ya vitu vyote, hii ni sifa ya Mungu. Japokua tunajua kuwa Mungu yupo kila mahali, tunaposema Baba yetu Uliye Mbinguni, tunasema Baba Yetu uliye juu ya vitu vyote.

Tunakubali na kukiri kwamba tunaye Baba Mmoja aliye Mbinguni, tunakiri ukuu na uweza wake.
Tunaikiri amri ya kwaza ya Mungu kwamba yeye ndiye Mungu wetu.

Vivyo hivyo tunakubali kuwa sisi tu familia kubwa moja.
Ndio maana hatusemi Baba yangu, hivyo tunakiri ushirika wa familia moja ya kikristo. Tunakubali kwamba sisi tumeumbwa na naye nasi tu wamoja

Lakini tunapomtaja Mungu k**a Baba tunamleta karibu zaidi, tunaongea naye k**a mwanafamilia mwenzetu pia tunaongea naye k**a mwenye nguvu na uweza wa kutusaidia, k**a vile tunavyoomba kwa baba zetu wa duniani nao wakatupatia, Baba yetu huyu wa Mbinguni atatupatia zaidi ya baba wa duniani.

Maneno haya yanafanya mambo makuu matatu kwa wakati mmoja;
1, Tunamuabudu,
2,Tunambariki
3, Tunampenda
ndio maana tunamuita Baba Yetu wa Mbinguni.

Maombi Saba (7)
yanayopatikana katika Sala ya Bwana.

Maombi haya Saba yamegawanyika katika makundi mawili makuu. Kwanza ni maombi matatu ya kimungu zaidi haya hutuvutia zaidi kwa Mungu, na sehemu ya pili ni maombi manne ya kibinadamu tunaposali kwa kuomba msaada wa Baba Yetu.

MAOMBI YA KIMUNGU;

1,Jina lako litukuzwe

tunalitakatifuza jina tukufu la Mungu. Ieleweke kuwa Mungu pekee ndiye mwenye uwezo wa Kutukuza na kutakatifuza. Tunaposema maneno haya tunaliinua jina lake juu.
Tunaingia katika mpango wa Mungu na kulitukuza jina lake

2 Ufalme wako Ufike

Tunaukiri Ufalme wa Mungu wetu wa Mbinguni, vivyo hivyo tunaomba Mungu ashushe na atushirikishe ufalme na neema zipatikanazo katika ufalme wa mbinguni. Tunaziita baraka za ufalme wa Mungu katika maisha yetu ya kila siku.

3 Utakalo lifanyike Duniani K**a Mbinguni

Tunayakubali mapenzi ya Mungu, jinsi inavyompendeza yeye tunakubali iwe hivyo, lakini pia tunaomba wokovu wa dunia nzima na ukombozi wetu. Pia tunaomba kwa ajili ya ukombozi wa ulimwengu mzima.

MAOMBI YA KIBINAADAMU

4 Utupe leo kizuri yetu ya kila siku

Tunaomba wote kwa pamoja k**a ndugu malisho ya kiroho na kimwili. Tunamuomba Mungu atulishe na aishibishe miili yetu pia roho zetu. Mkate hutusaidia kukua na tunapoomba kukua kiroho tunaomba pia kukua kimwili.

5 Utusamehe makosa yetu, k**a tunavyo wasamehe na sisis waliotukosea

tunakubali kuwa sisi ni wakosefu nasi tunaomba huruma ya Mungu kutusamehe. Zaidi ya hayo tunakubali kuwa sisi tunawasamehe wengine, vivyo hivyo tunaweka ahadi ya kuwasamehe wengine. Hii ni muhimu sana, na ukisali maneno haya usisali kwa mazoea sali ukimaanisha kuwa nawe unawasamehe wengine.

6 Usistutitie majaribuni

tunamuomba Mungu atuepushe na kushika njia inayotupelekea kutenda dhambi, tunamsihi atupe Roho Mtakatifu wa kung`amua kuwa tunaelekea katika dhambi na kutusaidia kuepuka vishawishi hivyo.

7 Lakini utuokoe na yule muovu

Yesu alikwisha mshinda Shetani na akamnyanganya funguo za kuzimu. Tunaposali hapa tunaomba nguvu ya kumshinda ibilisi pamoja na nguvu zote za giza. Tunaomba nguvu za kimungu za kupambana na yule muovu.

HITIMISHO

Tuitukuze na kuipenda sala hii ya Bwana, tunapoisali tuisali kwa taratibu na tupate nafasi ya kutafakari maneno tunayoyatamka maana yana maana kubwa sana. Tusiisali sala ya Bwana k**a ngonjera bali tutafakari kila neno linalotoka katika kinywa chetu. Hii itatusaidia kusali kwa ukamilifu.

From Baba Paroko💪🏼

```CHIMBA NA KUREJESHA TENA VISIMA VILIVYOFUKIWA NA KUGOMBANIWA NA ADUIMwanzo 26:-18 Isaka akarudi akavichimbua vile vis...
12/04/2023

```CHIMBA NA KUREJESHA TENA VISIMA VILIVYOFUKIWA NA KUGOMBANIWA NA ADUI

Mwanzo 26:-18
Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

Mwanzo 26:-20(a)
Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu.

👉wafugaji wa gerari walivigombania visima ambavyo watumwa wa isaka walikuwa wamevifukua baada ya kuwa vilifukiwa na wafilisti.

👉Kunatabia ambazo tukiziruhusu zinafukia visima vyetu vya kiroho. Wengi leo wamekauka kiroho baada ya visima vyao kufukiwa na tabia za kigeni.

👉Kuna wafugaji wa gerari wamegombania visima vya watu wengi, visima vya maombi, ibada na neno ndani ya mioyo ya watu wengi vimefukiwa na mambo ya kidunia.

👉Wengine wafugaji wagerari ni social medias, mtu mmoja yupo whatsapp, yupo facebook, instagram, twitter, kila kona yupo na sikwafaida, akiomba kidogo anakumbuka hajaweka status whatsapp , haja comments Fb, haja tuma picha instagram au haja twit.

👉Muda 'fresh' au mzuri wa kuomba, kusoma neno akili zikiwa zimechangamka umechukuliwa na medias na mambo yasiyojenga.

👉Wengine wafugaji wa gerari ni kazi zao, tamthilia, move, kampani, nk, wameshachukua kiu ya kumtafuta MUNGU.

👉Ndio maana watu wengi wanaotetea movie, bongo flavor na tamthilia kiroho chao lazima kina shida eneo flani.

👉Lakini pia kiutumishi kunaviwango huwezi fika hadi baadhi ya mambo yaondoke mfano matamthilia na movie, na k**a utafika hivyo viwango basi vitakuongoza kuacha hayo mambo.

👉Biblia inasema wafugaji wa gerari walivigombania visima, lakini kila walipogombania watumwa wa Isaka walichimba kingine.

👉Kuna watu maisha yao yamegombaniwa na adui kwa shughuli nyingi za dunia au mambo Ya kimwili yamewazidia na wamenyamaza kimiya!

👉Usinyamaze chimba tena kisima chako cha maombi, kisima chako cha bubujiko la ROHO MTAKATIFU, cha kunena kwa lugha. Ondoa hao wafugaji wakigeni katika maisha yako.

👉Wengine wamekauka kiroho, kiroho chao kinalia 'battery low', kumbe kisima kimeshafukiwa, chaji tena kiroho chako. Fukua kisima chako.

Ubarikiwe sana na BWANA YESU Kristo.```

From baba paroko💪🏼

Glory to God
28/04/2022

Glory to God

28/04/2022
22/11/2021

*MAMBO MHIMU YA KUOMBA PINDI UNAPOKUWA NYAKATI NGUMU AMBAZO HAUJUI UTAFANYA NINI*

Kibiblia kipo kipindi kigumu ambacho mtu anaweza akapitia na asijue afanye nini na k**a mtu huyu asipopata msaada wa haraka katika nyakati k**a hizi anaweza akafanya maamuzi mabaya ambayo asingeyafanya au anaweza kujikuta anayumba kabisa kiimani.

▶️BIBLIA INAKIRI YAKWAMBA KILICHOTARAJIWA KIKIKAWIA KUJA MOYO WA MTU HUUGUA

*👉Mithali 13:12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.*

👆🏻Narudia tena kipindi k**a hiki cha kuugua mtu asipopata msaada wa haraka anaweza akafanya mambo mabaya yanayoweza yakaigharimu imani yake.

*✔Mtu anaweza akapita nyakati ngumu kwenye ndoa, kwenye uchumba, kwenye biashara, kazini, kwenye utafutaji, au kuchelewa kufanikiwa kwa ndoto zake n.k*

✔Sasa leo nitakupa point kadhaa za vitu unavyotakiwa kuombea ili upate majibu ya Mungu yatakayokuwezesha usiyumbe kiimani kwenye nyakati k**a hizi ngumu ambazo haujui utafanya nini.

*1.Omba Mungu akupe wazo sahihi la kukusaidia kutoka kwenye hayo mapito*

Ukiona unapita kwenye nyakati ngumu ambazo haujui utafanya nini jifunze kumwomba Mungu kwa imani ili akupe wazo mpya la kitu cha kufanya ili uyashinde au uyastahimili hayo mapito.

Biblia inasema hivi

*👉Yakobo1:5 Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.*

👆🏻Maandiko haya yanasema hivi MTU AKIPUNGUKIWA NA HEKIMA NA AOMBE DUA KWA MUNGU, kwa maana nyingine mwandishi anamaanisha yakwamba 👉mtu akikosa ufahamu wa nini afanye au akifika mwisho wa kuamua anapaswa kuomba ufahamu au maarifa kwa Mungu ili yamsaidie katika nyakati ngumu anazopitia kwa kipindi hicho..

*✔Kwahiyo ili uvuke kwenye kipindi cha mpito salama unapaswa kuomba wazo kutoka kwa Mungu litakalokufanya uishi bila wasiwasi katika kipindi hicho kigumu ulichomo*

✔Mungu anaweza kukupa wazo hilo kwa njia ya fikra, ndoto au mtu kwahiyo jifunze kuomba...

✍Changamoto nikuwa wa

02/11/2021

God is good

29/10/2021

Mungu atukuzwe

15/07/2020

Electrical

Address

Po Box 450
Dar Es Salaam

Telephone

+255774252514

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Baba paroko80 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share