Tayo Msewe

Tayo Msewe Tanzania Anglican Youth Organization (Tayo Msewe) ni umoja wa vijana wa kanisa la Anglikana Mt. Stephano-MSEWE DSM

Kauli Mbiu yetu: VIJANA NGUZO YA KANISA

UTANGULIZI KUHUSU TAYO MSEWE
Tanzania Anglican Youth Organisation-Msewe yaani Umoja wa Vijana wa Anglikana Tanzania ipo ndani ya kanisa la Mtakatifu Stephano-Msewe chini ya usimamizi wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam. Huu ni umoja unaowaunganisha vijana wa Kianglikana Msewe na Tanzania kwa ujumla. MSINGI WA TAYO MSEWE:
Kuimarisha upendo, utumishi katika kanisa na mshik**ano wa vijana

ndani ya kanisa la Anglikana Msewe pamoja na madhehebu mengine kiujumla. MADHUMUNI:
• Kusimamia huduma zote za vijana katika nyanja zote ikiwemo uinjilisti kwa njia ya uimbaji, michezo mbalimbali nk.
• Kuwalea vijana kiroho zaidi na katika mwenendo mzima wa Kikristo.
• Kukuza moyo wa ushirikiano baina ya vijana, waumini na watu wote katika kuleta umoja ndani ya kanisa.
• Kuhakikisha shughuli zote za kikanisa zinazohusu vijana zinasimamiwa ipasavyo na kutekelezwa na umoja huu.
• Kutumia vikao zaidi kuweza kupata mawazo ya vijana ili kuleta na kuharakisha maendeleo ya umoja na kanisa kiujumla.
• Kushirikiana na asasi mbalimbali kwa lengo la kuwaelimisha vijana juu ya mambo mbalimbali ya kijamii.
• Kuwaunganisha vijana walio ndani na nje ya kanisa na kuzidisha ushirikiano na makanisa/madhehebu mbalimbali.
• Kumjua, kumpenda na kumtumikia Yesu Kristo k**a Bwana na Mwokozi wetu. MALENGO YA TAYO MSEWE:
• Kuleta na kudumisha mshik**ano.
• Kujiimarisha kiuchumi na kukusanya wanachama wapya katika umoja.
• Kueneza neno la Mungu kwa kufanya uinjilisti.
• Kuandaa warsha/semina kwa vijana ili wapate muda wa kujifunza neno la Mungu.
• Kusimamia maisha ya vijana kiroho, kiafya, kielimu na ndoa.
• Kutoa msaada kwa wahitaji. MOTTO:
Motto wa umoja huu ni “Vijana Nguzo ya Kanisa”. Mwisho tunawakaribisha kwa maoni, ushauri nk. tuweze kupiga hatua ili tutoke hapa tulipo na hatimae twende mbele zaidi.

13/10/2016

Bwana Yesu apewe sifa,
Kutokana na kushindwa kukamilika kwa mipango, napenda kuchukua fursa hii kuwataarifu kwamba safari yetu ya SERENGETI NATIONAL PARK iliyokuwa ianze leo imesogezwa mbele hadi hadi hapo baadae.

Baada ya siku chache zijazo nitawajulisha tarehe na siku nyingine rasmi ya safari hivyo naomba wale wote waliokuwa wameshatoa MICHANGO wawe na subira kwani kwa mapenzi ya Mungu, safari/ Serengeti tour lazima itakuwepo.

Bila shaka taarifa hii itawasikitisha lakini haya yote ni mapenzi ya Mungu kwani k**a mnakumbuka hata safari yetu ya SAADAN PARK nayo iliahirishwa mara kadhaa lkn hatimae baadae kila kitu kilienda sawa na kila mmoja wetu aliyeshiriki kwenye tour ile ali-enjoy zaidi ya maelezo.

Hivyo kwa niaba ya uongozi wa TAYO MSEWE, naomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza baada ya kuahirishwa kwa SERENGETI AMAZING TOUR.

Gabriel Malile,
Mwenyekiti.

01/07/2016

***SERENGETI AMAZING TOUR WITH TAYO MSEWE***

TAREHE: 13-17 Oct' 2016
MCHANGO: TSH. 150,000 @
Kwa maelezo zaidi Piga: 0716 059 678

Tumia nafasi hii adimu kutalii mbuga kubwa na maarufu zaidi duniani.!!

18/06/2016
07/06/2016

TAYO DAY 2016
Vijana wa Mt. Stephano-Msewe tunatarajia kuadhimisha SIKUKUU yetu kwa mwaka huu (TAYO DAY 2016) itakayofanyika J'PILI ya tarehe 26 mwezi huu. Sherehe hii itatanguliwa na ibada (ambayo itaongozwa na vijana wenyewe) itaanza saa 2:00 Asubuhi.

Kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu, tunatarajia kuandaa sherehe kubwa na ya kuvutia pamoja na uwepo wa BURUDANI na kwaya mbalimbali maarufu k**a Uinjililisti K.K.K.T-Kijitonyama, Kanani-Ubungo Anglican nk.

Mgeni rasmi kwenye Sherehe hii ambayo itaongozwa na MC/Msanii maarufu zaidi hapa nchini, atakakuwa Diwani Kata ya Kimara Mh. PASCAL MANOTA.

Hivyo ili kufanikisha huduma zote hizo, tunaomba sana MCHANGO (kiasi chochote) na uwepo wako siku hiyo kwani shuhuli hii inakuhusu.
Unaombwa kutuma mchango wako kwa Katibu/Mhazini wa K**ati ya maandalizi dada ROSEMARY HIZA kupitia 0718 05 83 93.

K**ati ya maandalizi na uongozi wa TAYO kiujumla tunatanguliza SHUKRANI nyingi za dhati kwa USHIRIKIANO wako mkubwa ktk kufanikisha shererhe hii na Mwenyezi Mungu AKUBARIKI sana.!!!

07/06/2016

TAYO DAY 2016
Vijana wa Kanisa la Anglican Mt. Stephano-Msewe tunatarajia kuadhimisha SIKUKUU yetu kwa mwaka huu (TAYO DAY 2016) itakayofanyika J'PILI ya tarehe 26 mwezi huu. Sherehe hii itatanguliwa na ibada (ambayo itaongozwa na vijana wenyewe) itaanza saa 2:00 Asubuhi.

Kwa mapenzi yake Mwenyezi Mungu, tunatarajia kuandaa sherehe kubwa na ya kuvutia pamoja na uwepo wa BURUDANI na kwaya mbalimbali maarufu k**a Uinjililisti K.K.K.T-Kijitonyama, Kanani-Ubungo Anglican nk.

Mgeni rasmi kwenye Sherehe hii ambayo itaongozwa na msanii maarufu zaidi hapa nchini, atakakuwa Diwani Kata ya Kimara Mh. PASCAL MANOTA.

Hivyo ili kufanikisha huduma zote hizo, tunaomba sana MCHANGO (kiasi chochote) na uwepo wako siku hiyo kwani shuhuli hii inakuhusu.

Unaombwa kutuma mchango wako kwa Katibu/Mhazini wa K**ati ya maandalizi dada ROSEMARY HIZA kupitia 0718 05 83 93.

K**ati ya maandalizi na uongozi wa TAYO kiujumla tunatanguliza SHUKRANI nyingi za dhati kwa USHIRIKIANO wako mkubwa ktk kufanikisha shererhe hii na Mwenyezi Mungu AKUBARIKI sana.!!!

19/05/2016

Uongozi wa TAYO MSEWE umeandaa BEACH TOUR kwa vijana wote wa Msewe & marafiki BEACH-KIGAMBONI siku ya J'PILI tarehe 22/05/2016 kwa mchango wa Sh. 16,000 tu (per head). Mchango unajumuisha usafiri, kiingilio na chakula.

Nafasi bado zipo hivyo unaweza kutuma mchango wako kwa CHISEKO MLEKANO kupitia 0715 986910

Safari (kupitia daraja jipya la Kigamboni) itaanzia kanisani MSEWE mida ya saa 4:30 asubuhi mara baada ya ibada ya PILI.
Wote MNAKARIBISHWA.!!

TAYO Msewe wakikabidhi baadhi ya zawadi za PASAKA kwa watoto YATIMA walipokwenda kuwatembelea kwenye kituo cha VALENTINE...
31/03/2016

TAYO Msewe wakikabidhi baadhi ya zawadi za PASAKA kwa watoto YATIMA walipokwenda kuwatembelea kwenye kituo cha VALENTINE kilichopo BUZA wilayani TEMEKE 20 March 2016.

Vijana wa Mt. Stephano Msewe tarehe 20/03/2016 tuliwatembelea watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha VALENTINE kilic...
24/03/2016

Vijana wa Mt. Stephano Msewe tarehe 20/03/2016 tuliwatembelea watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha VALENTINE kilichopo Buza wilaya ya Temeke

walifurahi mno maana licha ya zawadi tulizowapelekea tulicheza nao michezo mbali mbali.

07/03/2016

KUTEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA:

Vijana wa Mt. Stephano Msewe tunatarajia kwenda kuwatembelea watoto yatima ambao wanalelewa kwenye kituo kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam kilichopo Buza wilayani Temeke siku ya J’Pili tarehe 20/03/2016 mara baada ya Ibada ya Pili.

Hivyo kwa yeyote mwenye kitu chochote k**a nguo, viatu, mchele, sabuni, sukari, unga wa sembe/ngano, juice, pesa taslimu nk. anakaribishwa kuleta kwenye ofisi ya mchungaji wa kanisa la Anglikana Msewe Baba Sydney Chinyuka muda wowote kuanzia sasa ili siku hiyo tuwapelekee watoto wale k**a zawadi ya PASAKA hatimae na wao wakaona wanathaminiwa k**a wenzao wanaoishi na wazazi wao.

Mwenyezi Mungu atakubariki kwa chochote utakachotoa kwa ajili ya watoto wale.
Asante sana.!!

24/01/2016

IBADA YA VIJANA:
Tutakuwa na Ibada maalum ya vijana itakayokuwa inafanyika kila Jumapili ya mwisho wa mwezi kuanzia J'PILI ya tarehe 31/01/2016.

K**a kawaida Ibada zitakuwa mbili lakini Ibada ya PILI ambayo kwa kawaida inaanza saa 2:00 asubuhi ndio itakuwa maalum kwa vijana.
Taratibu mbalimbali za ibada k**a kusoma masomo, mahubiri, kuongoza washiriki, kuhesabu sadaka nk. zitafanywa na vijana wenyewe.

Pia ili kuongeza upekee wa ibada hii, uongozi wa TAYO utakuwa unazialika KWAYA mbalimbali ili zije kuhudumu kwenye ibada yetu kwa kushirikiana na kwaya yetu ya SHAHIDI.

Hivyo mnaombwa MSIKOSE kuhudhuria ibada hii na nyingine zote.
Asanteni sana na Mwenyezi Mungu awabariki.

*****VIJANA NGUZO YA KANISA*****

15/01/2016

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tayo Msewe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share