13/10/2016
Bwana Yesu apewe sifa,
Kutokana na kushindwa kukamilika kwa mipango, napenda kuchukua fursa hii kuwataarifu kwamba safari yetu ya SERENGETI NATIONAL PARK iliyokuwa ianze leo imesogezwa mbele hadi hadi hapo baadae.
Baada ya siku chache zijazo nitawajulisha tarehe na siku nyingine rasmi ya safari hivyo naomba wale wote waliokuwa wameshatoa MICHANGO wawe na subira kwani kwa mapenzi ya Mungu, safari/ Serengeti tour lazima itakuwepo.
Bila shaka taarifa hii itawasikitisha lakini haya yote ni mapenzi ya Mungu kwani k**a mnakumbuka hata safari yetu ya SAADAN PARK nayo iliahirishwa mara kadhaa lkn hatimae baadae kila kitu kilienda sawa na kila mmoja wetu aliyeshiriki kwenye tour ile ali-enjoy zaidi ya maelezo.
Hivyo kwa niaba ya uongozi wa TAYO MSEWE, naomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza baada ya kuahirishwa kwa SERENGETI AMAZING TOUR.
Gabriel Malile,
Mwenyekiti.