Wanyenyekevu wa Mama Maria

Wanyenyekevu wa Mama Maria Karibuni katika tafakari na sala kwa heshima ya Mama yetu Bikira Maria, Mama Maria ni Mama wa Matumaini, Mama Maria ni Mama wa Shauri Jema..

05/06/2026

Ee.. Bwana nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Barikikazibya mikono yangu

04/06/2026

Karibuni tusali Alhamisi ya Kuabudu Ekaristi Takatifu

02/06/2026

MASOMO YA MISA, JUMANNE YA JUMA LA TISA, KIPINDI CHA KAWAIDA, MWAKA II, JUNI 2, 2026
RANGI YA KILITURJIA: KIJANI KIBICHI 💚

SOMO LA KWANZA
2 PETRO 3:11b—15a, 17—18

Tunatarajia mbingu mpya na nchi mpya.

Somo katika barua ya pili ya Mtakatifu Petro

Ndugu wapendwa: Je haiwapasi ninyi kuishi kitakatifu zaidi na kumcha Mungu, kungoja na kuukimbilia ujio wa siku ya Mungu, ambapo mbingu zitateketea moto na kutoweka, na viumbe vitayeyushwa kwa mwako wa moto? Kisha tunatazamia - k**a alivyoahidi - mbingu mpya na nchi mpya zenye uadilifu. Mkisubiri hayo, ndugu wapendwa, mjibidishe kuishi bila mawaa ili mkutwe katika amani. Bila shaka, subira ya Bwana wetu inawapatia salama. Lakini, ninyi, ndugu wapendwa, mmeonywa juu ya mambo hayo. Kwa hiyo jihadharini, msije mkachukuIiwa na maoni ya uongo ya wahalifu, kupotewa na uthabiti wenu na kuanguka. Zidini katika neema na ufahamu wa Bwana wetu na mwokozi Yesu Kristo. Utukufu kwake, sasa na hata milele. Amina.

NENO LA BWANA... TUMSHUKURU MUNGU

ZABURI YA KUITIKIZANA
ZABURI 90:2, 3—4, 10, 14 na 16 (K 1)

K. Wewe Bwana, umekuwa kimbilio letu, toka kizazi hata kizazi.

Kabla ya kuzaliwa milima,
na hujaumba dunia au ulimwengu,
toka milele hata milele, wewe upo, ee Mungu. K.

Unamrudisha mtu mavumbini.
ukisema, "Rudini, enyi wanadamu."
Maana miaka elfu machoni pako
ni k**a siku ya jana, iliyokuja na ikapita,
au k**a lindo la usiku. K.

Jumla ya miaka yetu ni sabini.
au tukiwa na afya njema, themanini.
Na mingi ya miaka hiyo ni taabu na shida
Nayo yapita mbio, nasi twatoweka mara. K.

Alfajiri, utushibishe kwa huruma yako:
nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote.
Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako,
na utukufu wa nguvu yako kwa watoto wao. K.

SHANGILIO LA INJILI
TAZAMA WAEFESO 1:17—18

K. Aleluya. W. Aleluya.
K. Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, ayaangaze macho ya mioyo yetu, ili tupate kujua tumaini la mwito wetu jinsi lilivyo.
W. Aleluya.

SOMO LA INJILI
MARKO 12:13—17

Mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.

† Somo la Injili takatifu ilivyoandikwa na Marko

Wakati ule: Waliwatuma baadhi ya Mafarisayo na watu wa Herode kwa Yesu kusudi wamnase katika kuongea. Nao walimjia, wakamwambia, "Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mwadilifu, tena hufanyi ubaguzi, wala cheo cha mtu si kitu kwako, bali unafundisha njia ya Mungu kwa ukweli tu. Je, ni halali kumlipa Kaisari kodi au sivyo? Tumlipe au tusimlipe?" Naye alitambua unafiki wao, akawaambia, "Mbona mnanijaribu? Nileteeni sarafu niitazame." Wakaileta, naye akawaambia, "Sanamu hii na hati hii ni ya nani?"" Wakamjibu, "Ni ya Kaisari." Yesu akawajibu, "Mpeni Kaisarí yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu." Wakamstaajabia sana.

INJILI YA BWANA... SIFA KWAKO EE KRISTO

Leo Siku ya Jumanne June 02, tunawaheshimu Watakatifu Marcellinus na Petro, Mashahidi - Mtuombee
02/06/2026

Leo Siku ya Jumanne June 02, tunawaheshimu Watakatifu Marcellinus na Petro, Mashahidi - Mtuombee

Jumapili ya Pentecost
24/05/2026

Jumapili ya Pentecost

Sherehe ya Pentekoste: Kazi ya Roho Mtakatifu katika maisha na utume wa KanisaSherehe ya Pentekoste: Kazi ya Roho Mtakat...
24/05/2026

Sherehe ya Pentekoste: Kazi ya Roho Mtakatifu katika maisha na utume wa KanisaSherehe ya Pentekoste: Kazi ya Roho Mtakatifu katika maisha na utume wa Kanisa
Kanisa
Sherehe ya Pentekoste 2026: Roho Mtakatifu Katika Maisha na Utume wa Kanisa
Siku ya Pentekoste, mwisho wa juma saba za Pasaka, Pasaka ya Kristo inatimilika kwa kumimina Roho Mtakatifu, ambaye amedhihirishwa, ametolewa na kushirikishwa k**a nafsi ya Mungu: kutoka utimilifu wake Kristo, Bwana anamimina Roho kwa wingi. Hii ni siku ambayo Utatu Mtakatifu ulifunuliwa katika ukamilifu wake. Kwa ujio wake ambao hauna mwisho, Roho Mtakatifu anauingiza ulimwengu katika nyakati za mwisho, nyakati za Kanisa, ufalme uliorithiwa tayari...

21/05/2026

Karibuni Alhamisi ya Kuabudu Ekaristi Takatifu, tuombee Familia zetu,Jumuiya zetu, kazi zetu na Tuombee wagonjwa wapone

Tafakari Dominika ya 7 ya Mwaka A wa Kanisa: Upendo na Maisha ya Utakatifu Tukitaka kuupata ufalme wa Mungu sharti tuwe ...
16/05/2026

Tafakari Dominika ya 7 ya Mwaka A wa Kanisa: Upendo na Maisha ya Utakatifu

Tukitaka kuupata ufalme wa Mungu sharti tuwe watakatifu. Viashiria vya kuwa watakatifu ni kuishika na kuiishi vyema amri kuu ya mapendo: Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote (Kumb 6:5) na Mpende jirani yako k**a unavyojipenda mwenyewe (Wal 19:18). Amri hii inatutaka tuwe na moyo wa unyenyekevu ili tuweze kuishi.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255654684864

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wanyenyekevu wa Mama Maria posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Wanyenyekevu wa Mama Maria:

Share