Tanzania Prayer Warriors

Tanzania Prayer Warriors This is an institution of CHRISTIANS founded by man of GOD Renatus B.Mwesiga in 2013.It joins togeth

TANZANIA PRAYER WARRIORS brings together all the CHRISTIANS regardless of differences in denominations.It was found in 2013 by the man of GOD Renatus B.mwesiga at Kazima Secondary School. It has been having a successful history in its activities because through its activities family matters have been settled,people with ulcers have been cured,infamies have been broken,satan's chains have been brok

en and other spiritual miracles. In secondary schools,it joins groups of Ukwata,CASSFETA,UHIMA,ASSA,TYCS and other Christian groups. It works under the base of the HOLLY BIBLE and it has the constitution to guide members.

19/05/2026

🔥 SOMO: MUNGU HUTUMIA SHINIKIZO KUZALISHA UTUKUFU 🔥
“Pressure is not punishment, ni maandalizi ya ushindi”
📖 “Mambo yote hufanya kazi pamoja kwa wema kwa wale wampendao Mungu.” – Warumi 8:28
Watu wengi hudhani kwamba matatizo ni ishara Mungu amewaacha… lakini ukweli ni huu:
👉 Shinikizo (pressure) si mwisho wako
👉 Ni darasa la kukuandaa kwa hatua ya juu
👉 Ni sehemu ya mchakato wa utukufu wako
Musa alipitia jangwani kabla ya kuongoza Israeli
Yusufu alipitia gereza kabla ya kuwa mkuu Misri
Daudi alipitia pango kabla ya kiti cha ufalme
🔥 Hii inamaanisha nini? Mungu hakuchukui njia ya kukupitisha bila kukutengeneza kwanza
💡 UKWELI WA KIROHO:
Kila shinikizo lina kusudi:
✔ Kukuvunja tabia za zamani
✔ Kukujenga ndani (character)
✔ Kukufundisha kumtegemea Mungu
✔ Kukusogeza kwenye level mpya
⚠️ USIDANGANYIKE:
K**a maisha yako yanaonekana kubana sana… huenda sio kupotea, bali ni “kuumbwa upya”
📌 Mungu akitaka kukuinua, kwanza anakukanda 📌 Akitaka kukuongoza, kwanza anakutenganisha 📌 Akitaka kukuweka juu, kwanza anakupitisha chini
🔥 UJUMBE WA LEO:
Usiombe shinikizo liondoke kabla halijamaliza kazi yake ndani yako.
Badala yake omba hivi: 🙏 “Bwana, nifanye niweze kuelewa unachonitengenezea kupitia hii hali”
✨ Kumbuka:
Kinachokukandamiza leo, ndicho kitakachokukuinua kesho.


Angalia hyo picha,jambo gani umelipuuza,lifanyie kazi
12/05/2026

Angalia hyo picha,jambo gani umelipuuza,lifanyie kazi

SOMO: MAADUI WA HATIMAMaana ya HatimaHatima ni kusudi, mpango, na mwisho ambao Mungu ameuweka juu ya maisha ya mtu.Ni sa...
12/05/2026

SOMO: MAADUI WA HATIMA
Maana ya Hatima
Hatima ni kusudi, mpango, na mwisho ambao Mungu ameuweka juu ya maisha ya mtu.
Ni sababu ya kuzaliwa kwako duniani.

Kila mtu ana:
●Wito
●Kusudi
●Kipawa
●Sehemu yake katika mpango wa Mungu

Mfano: Bible inaonyesha:
Yeremia 1:5
“Kabla sijakuumba tumboni nalikujua…”
Hii inaonyesha kuwa kabla hujazaliwa, Mungu tayari alikuwa na mpango juu yako.

MAADUI WAKUBWA WA HATIMA
1. UJINGA (Kutokujitambua)
Watu wengi hawaharibiwi na shetani kwanza… Wanaharibiwa na kutokujua wao ni nani.
Hosea 4:6
“Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.”
Ukishindwa kujitambua:
●Utaishi chini ya kiwango chako
●Utauza thamani yako kirahisi
●Utapoteza muda mwingi
●Utachagua mazingira mabaya

Dalili za mtu asiyojitambua:
●Kuiga maisha ya wengine
●Kukosa mwelekeo
●Kukata tamaa haraka
●Kuishi kwa maoni ya watu
Suluhisho:
●Soma Neno la Mungu
●Jifunze uwezo wako
●Omba Mungu akuonyeshe kusudi lako
●Kaa karibu na watu wenye

2. DHAMBI
Dhambi ni adui mkubwa wa hatima kwa sababu humtenganisha mtu na Mungu.
Mfano:
Samson alikuwa na nguvu kubwa lakini tamaa ilimwangusha.

Madhara ya dhambi:
●Kupoteza neema
●Kupoteza nguvu za kiroho
●Kupoteza heshima
●Kuchelewa kufika kwenye kusudi
Warumi 6:23
“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti.”
Suluhisho:
●Toba ya kweli
●Kuishi maisha matakatifu
●Kukimbia mazingira ya majaribu

3. UVIVU
Hatima huhitaji kazi, nidhamu, na uvumilivu.
Mithali 6:10-11
“Usingizi mchache… umaskini wako utakuja…”
Watu wengi wana ndoto kubwa lakini hawana bidii.
Uvivu huleta:
●Kuchelewa maisha
●Kutegemea wengine
●Kukosa maendeleo
●Vipawa kufa
Suluhisho:
●Kuwa na ratiba
●Kuacha kuahirisha mambo
●Kuwa mtu wa kujifunza kila siku

4. HOFU
Hofu ni gereza la hatima.
Watu wengi wanajua wanatakiwa kufanya nini… lakini wanaogopa:
●Kushindwa
●Kukosolewa
●Kuanza
●Kuonekana tofauti
2 Timotheo 1:7
“Mungu hakutupa roho ya woga…”
Mfano:
Musa aliogopa kuongea, lakini Mungu alimwinua.
Suluhisho:
●Kuamini Mungu
●Kuchukua hatua hata ukiwa na hofu
●Kujizunguka na watu wa imani

5. MARAFIKI WABAYA NA MAZINGIRA MABAYA
Mazingira yanaweza kujenga au kuharibu hatima.
1 Wakorintho 15:33
“Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.”
Watu wengine walipoteza maono yao kwa sababu ya:
●Makundi mabaya
●Ushauri mbovu
●Mahusiano ya sumu
Dalili:
●Unazidi kurudi nyuma
●Maombi yamepoa
●Maadili yanashuka
●Ndoto zako zinakufa
Suluhisho:
●Chagua watu wanaokujenga
●Kaa karibu na watu wenye maono
●Epuka mazingira yanayozima imani

6. KUJILINGANISHA NA WENGINE
Ukijilinganisha sana:
●Utapoteza amani
●Utadharau hatua zako
●Utalazimisha maisha yasiyo yako
Mungu hakuiti kuwa “nakala” ya mwingine.
Wagalatia 6:4
“Kila mtu aipime kazi yake mwenyewe.”
Suluhisho:
●Thamini safari yako
●Furahia hatua ndogo
●Tambua kila mtu ana muda wake

7. KUACHA MAOMBI
Maombi ni ulinzi wa hatima.
Bila maombi:
●Maamuzi huharibika
●Nguvu hupungua
●Maono huzimika
Luka 22:31-32
Yesu Kristo alimwambia Petro:
“Shetani ametaka kuwapepeta…”
Lakini maombi yalimhifadhi.
Suluhisho:
●Jenga altar ya maombi
●Omba kwa consistency
●Funga na kuomba

ISHARA KWAMBA HATIMA YAKO INAPIGANIWA
●Unapitia vita visivyoeleweka
●Unaanza kitu lakini hakidumu
●Unahisi kuchoka kiroho
●Unapoteza focus mara kwa mara
●Kuna vipingamizi kila unapokaribia breakthrough

JINSI YA KULINDA HATIMA YAKO
1. Kuwa karibu na Mungu
Hakuna anayelinda hatima kuliko Muumba wa hatima.
2. Linda akili yako
Kila vita huanza kwenye mawazo.
3. Chagua watu sahihi
Watu wanaweza kuwa daraja au shimo.
4. Kuwa na nidhamu
Hatima kubwa huhitaji tabia kubwa.
5. Omba na kufunga
Nguvu za kiroho hushinda vita vya hatima.

HITIMISHO
Hatima kubwa huvuta vita vikubwa.
Usishangae unapopitia:
_upinzani,
_kucheleweshwa,
_maumivu,
_majaribu.
Mara nyingi ni ishara kuwa kuna kitu kikubwa ndani yako.
Kumbuka:
“Usikubali adui akuibie kile ambacho Mungu alikiweka ndani yako kabla hujazaliwa.”

RENATUS BUBERWA MWESIGA
BABA WA IMANI_Shujaa wa Kweli.

10/05/2026

NJIA YA KUANZA KUIONA KESHO YAKO.
“Kesho yako huanza kuonekana pale unapokataa kuishi kwa hisia za leo.”

Njia ya kuanza kuiona kesho yako:
1. Kuwa na maono
Mtu asiye na maono huishi kwa bahati. Jiulize: “Nataka maisha yangu yaweje miaka ijayo?”

2.Badili mawazo yako
Kabla maisha hayajabadilika, akili lazima ibadilike.
Watu wengi wamefungwa si kwa sababu hawana uwezo… bali wanaamini hawawezi.

3.Anza na kidogo ulicho nacho
Usisubiri mazingira perfect.
Daudi alianza na kombeo, lakini ndani yake kulikuwa na mfalme.

4.Jifunze kuomba na kuchukua hatua
Maombi bila hatua huzaa matumaini yasiyo na matokeo.

5.Kesho nzuri hujengwa leo.
Ondoka kwa watu wanaoua ndoto zako
Kuna watu ukikaa nao, unaanza kuona haiwezekani.
Lakini kuna watu wakiongea nawe, unaanza kuona mbali.

6.Muone Mungu ndani ya safari yako
Wakati mwingine huoni njia, lakini Mungu anaiona mwisho wa safari yako.
📖 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia…”
— Bible Yeremia 29:11

🔥 Ujumbe wa nguvu:
“Usihukumu maisha yako kwa hali ya leo.
Mbegu haifanani na kesho ya mti wake.”

Jumapili njema

Shujaa wa kweli.

Usikate tamaa,endelea kuomba,Unakaribia ushindi.
09/05/2026

Usikate tamaa,endelea kuomba,
Unakaribia ushindi.

11/10/2018

*UNAONA NINI NAFSINI MWAKO?*

Mithali 23:7a
_Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo_.

✍Je katika ufaham wako uaona nini? Je fikra zako umeseti vipi, na zinafikiri juu ya hatima yako. Unajiona huwezi lolote au chochote hapa duniani?

✍Katika masomo yako unaona nini? Je unaona kufaulu, kufanikiwa katika kiwango chako au unaona kuferi, ku discontinue, kupata supp ?

✍Katika mipango yako unaona nini? Je! Unaona mipango kusonga mbele na kutimia au unaona kufa na kupotea kwa maono yako?

✍Katika huduma yako unaona nini?. Je! Unaona kusonga mbele au unaona kushindwa, kukata tamaa, kuvunjika moyo, kuacha kutumika?

✍Katika mahitaji yako unaona nini? Je! unaona kufanikiwa kuyatimiza au kutofanikiwa?

✍Katika ndoa/ uchumba wako unaona nini? Je! unaona ndoa au uchumba kuvunjika?.

📌Sikia nikwambie ndugu yangu mpendwa, badili mtazamo wako tafadhali,

📌Mambo yote, mafanikio au kutofanikiwa huanza katika fikra, acha kufikiri kushindwa sasa. Anza kukiri ushindi katika mambo yako!

📌Katika ufaham mambo yote tunayoyaona ndiko yalianzia. Kila jambo huanza katika ulimwengu usioonekana ( ufaham)

*MUNGU mwenyewe kabla ya kuumba vyote tubavyoviona, kwanza aliviona katika ufaham wake ndipo akaanza kuvidhihirisha ili vionekane katika macho yetu.*

🔥Tumia ufahamu wako vizuri kwa ajili ya maendeleo yako, kanisa na taifa kwa ujumla.

UBARIKIWE SAANA

31/08/2018

WAHI KUTUBU ILI MAPIGO YALIYO ACHILIWA KWAKO YASIKUPATE TENA

1Samwel 7:9-10
9 Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa nzima; Samweli akamlilia Bwana kwa ajili ya Israeli; Bwana akamwitikia.
10 Hata Samweli alipokuwa akiitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakakaribia ili kupigana na Israeli; walakini Bwana akapiga ngurumo, mshindo mkubwa sana, juu ya Wafilisti siku ile, akawafadhaisha; nao wakaangamizwa mbele ya Israeli.

Bwana Yesu asifiwe mwana wa Mungu.

Hakuna kitu kibaya k**a dhambi, dhambi inaondoa uhalali wa mtu kumiliki, kutawala, kutiisha, Dhambi inaondoa ushirika wako na Mungu, dhambi inazuia ulinzi wa Mungu kusimama juu yako

Hapo ndipo utaona madhara makubwa ya dhambi, watu wengi leo wamezizoea dhambi kiasi kwamba wameishia kwenye utumwa mkubwa na mbaya maishan mwao, magonjwa, taabu umaskin na mabaya yafananayo na hayo vimewashikilia watu kiasi kwamba furaha ya maisha inakosekana kwenye familia na watu binafsi.

Kukosa aman ndani ya moyo, mahangaiko makubwa kwenye mioyo ya watu imepelekea watu kuyachukia maisha yao, ukitazama tatizo ni dhambi ambazo amezitenda.

Neno la Mungu linatuambia wana wa Israel walikaa kwenye utumwa mkubwa sababu ya dhambi walizokua wamemtenda Bwana, kiasi kwamba wakalipoteza sanduku la Agano la Bwana, Neno pia linatuambia ukianza kusoma mstari wa kwanza kuwa Wafirist waliwatesa, kuwapiga na kuwa tawala kwa muda mrefu sababu ya dhambi na uasi wao kwa Mungu.

Dhambi ina ondoa ulinzi wa Mungu kwa mtenda dhambi, na Mungu ndie alie tuumba maana yake pasipo yeye maisha yetu yanakua hatarini,

Ndio maana Mungu amesema na watumishi mbali mbali juu ya kuikataa na kuikimbia dhambi ili kuimarisha uhusiano na yeye kwakiwango kikubwa.

Nami nakusii mwana wa Mungu kaa mbali na dhambi, ikimbie dhambi, usiisogelee dhambi, sio kwamba dhambi itakaa mbali na wewe, itakutafuta ila ukiona ishara zake ikatae na ikimbize mbali nawe kwa jina la Yesu

Neno la Mungu linasema wana wa Israel wakamwambia Nabii samwel ili awaombee toba kwa Mungu, zaman watumishi ndio walikua wapo kusimama na Mungu kuwaombea toba watu, lakini Yesu alivunja kiambaza hivyo kila mtu anauhalali wa kumwendea Mungu na kupeleka hoja zake, hivyo mlilie Mungu kwaajili ya dhambi zako ili akusamehe na utoke utumwan

Mtumishi wa Mungu Samweli akawaombea toba kwa Mungu na Mungu akawasamehe, sasa ona kitu hapa, adui ambao wafirist wakajua kuwa Israel si lolote wakaenda kupigana, Biblia inasema Wafirist walipigwa vibaya na Mungu na badae na wana wa Israel, nataka kusema nini hapo, unapo fanya toba hata k**a uliteswa miaka mingap mateso yanakuachia na ulinzi wa Bwana unakua juu yako na Bwana ndie anaepigana na adui zako

Kuna maadui wengi sana sirin ambao wanakupinga pasipo wewe kujua au ukiwa unajua, lakini wanapata nafasi kwakua, umewapa nafasi ya kukutawala, lakini utakapofanya toba hawataweza kukutesa tena bali watapigwa na Bwana.

Ukiona umeomba toba lakin mateso bado, usikate tamaa endelea kuomba toba kwa iman na bidii, omba mpaka usikie aman ya tofauti ndani yako, kadiri unapofanya toba kuna mambo yabaya yanaanza kukuachia, na mwisho mateso yote yanaondoka kwako

Neno linatuambia kuomba kwake mwenye haki yafaa sana akiomba kwa bidii, maana yake usiache kuomba na bidii yako isirudi nyuma. Yakobo 5:16-18

Omba huku ukijitenga na dhambi, ukiichekea dhambi itakuachilia mauti, mauti ya kila kitu utakachokua unafanya.

Amua leo kumrudia Bwana ili akutoe utumwan.

Nyumba Ya Sala Kwa Mataifa Yote. 969 likes · 80 talking about this. Religious Organization

31/08/2018

*HII INAKUHUSU WEWE.*
UNAWEZA NA INAWEZEKANA

✍Haijalishi umepitia maisha magumu kiasi gani, bado una uwezo wa kufanya makubwa kwenye maisha yako. Usiangalie sana ulikotoka, bali angalia unakotaka kufika.

✍Kuanza kidogo haimaanishi utaendelea kuwa hapo, kuwa na ndoto kubwa lakini anzia chini na endelea kukua.

✍K**a huna pa kuanzia, anzia chini kabisa, jifunze kwa kila unachofanya na kuwa na ndoto kubwa zaidi ya ulipo sasa.
✍Unapokuwa na ndoto kubwa, ifanyie kazi, hata k**a kila mtu yupo kinyume na wewe.

✍watu wengi wamekuwa wanashindwa kuingia kwenye biashara kwa sababu wanajiona hawajawa na wazo kamili. Ni bora kuanza, utaendelea kurekebisha wazo lako kadiri unavyokwenda.

✍Uwekezaji unakuwezesha kutengeneza utajiri mkubwa bila ya kufanya kazi moja kwa moja, hasa pale unapochagua vizuri na kuwekeza mapema

✍Upo uwezekano wa kufanya makubwa kuliko wengi walivyozoea, fikiria makubwa, hata k**a hakuna mwingine anayeona hivyo.

✍Hakuna mafanikio bila ya kushindwa,Muda mwingine unaweza ukapata hasara kwenye biashara,kilimo au uwekezaji wako.usikate tamaa piga hatua mbele zaidi(Aluta continua)

✍Elewa kuwa tunajifunza kupitia Changamoto tunazokutana nazo katika kilimo,biashara na uwekezaji hivyo usichukulie Changamoto k**a tatizo Bali k**a njia ya kukupa mbinu mpya ili kuondokana nayo kwa Mara nyingine

✍Tengeneza nidhamu katika usimamizi wa muda(Time management discipline) ili kufikia ndoto,Maono malengo uliyojiwekea

✅Endelea kupambana mpaka kieleweke

*Usikate tamaa acha tamaa ijakate yenyewe*

*Mtangulize Mungu kwa kuombea mipango yako na kujiombea ujasiri wa kusonga mbele.
Wafilipi 4:6 "msijisumbue kwa neno lolote bali kwa kila neno kwa kusali na kuomba...

28/07/2018

*USHAURI KWA WATUMISHI VIJANA*

Wale mnaoanza huduma, watumishi vijana k**a Mimi, kuna kitu kinaitwa MINISTERIAL ETHICS ambazo lazima uzifuate hasa unapoalikwa kuhudumu kwenye madhabahu anayoisimamia mtu mwingine k**a unataka kulinda heshima yako na usijifungie milango.
Nitasema vichache;

🔥Unapofika kwenye madhabahu ya mtu mwingine ni sawa na umeenda kwenye nyumba ya mtu mwingine ambayo sio Nyumbani kwako. Kila nyumba ina UTARATIBU WAKE na ina NAMNA YAKE ya kuendesha mambo. Pamoja na kuongozwa na Roho, tafuta kujua taratibu za madhabahu hiyo na zifuate hasa k**a haziko kinyume na neno la Mungu. Na ikibidi kufanya jambo ambalo sio kawaida ya mahali hapo omba kibali au shauriana kwanza na mwenyeji aliyekuita. Usije na utaratibu wako kwenye nyumba ya mtu mwingine ukisingizia ni ratiba za Roho Mtakatifu,Ni kukosa adabu Roho Mtakatifu ni wa utaratibu hakosi adabu.

🔥Unapofika kwenye madhabahu ya mtu muheshimishe kiongozi mwenye madhabahu hiyo kwa watu wake. K**a wanamuita Baba/Mama wewe hutakiwi kuwaonyesha kwamba hastahili kuitwa hivyo wanavyomuita. Badala yake sisitiza wamuheshimu zaidi, mseme vizuri kwa watu anawaongoza na mjenge mbele za macho ya watu Mungu aliowaweka chini yake. Unapoitwa mahali siku unayoondoka heshima ya aliyekuita inatakiwa kuwa imeongezeka zaidi. Unatakiwa kuwa umeijenga Image yake vizuri zaidi kuliko kuibomoa. Mshukuru aliyekuita, hata k**a umemzidi chochote wakati huo ukiwa kwake yeye ni Boss wako. Ni makosa kufika kwenye madhabahu ya mtu na ukajaribu kuwaonyesha washirika kwamba wewe ni bora kuliko mwenyeji aliyekuita ambaye ni kiongozi wao.

🔥Ni makosa kufika kwenye madhabahu ya mtu na ukaanza kujisifia utajiri, Mali, elimu au chochote ulichonacho. Let it be all about God and His word na ikibidi kusema sema with all humility na sema vile ambavyo unaona vitajenga watu au watu watajifunza kwavyo.

🔥Usiite washirika hotelini/mahali mwenyeji alipokuandalia pa kupumzika hasa wa jinsia tofauti na ikibidi waje basi mwenyeji wako awe na taarifa na k**a ni msichana na wewe ni mwanaume asije peke yake na hata akija peke yake msiongelee chumbani kaeni kwenye mahali pa wazi hata k**a ni hapo hapo hotelini ili UJILINDE na chochote ambacho shetani anaweza kutaka kukifanya kuaibisha na kuharibu utumishi wako.

🔥Usichukue namba za simu za washirika na kuwapigia kwa siri bila mwenyeji wako kufahamu. Na mshirika asichukue namba yako ya simu bila mwenyeji kujua, wakati mwingine ni Salama zaidi wanapokuja kukuomba namba waelekeze waichukue kwa Mchungaji au kiongozi wao aliyekuita. Yeye anawajua watu wake vizuri zaidi na anajua intentions au nia zao kwa sababu amekaa nao kwa muda kuliko wewe. Kuna wengine ambao wewe ungewapa namba lakini wangeenda kwake angewanyima kwa sababu anawajua sio watu Salama sana kupata mawasiliano ya Mtumishi.

🔥Sio tabia nzuri kukusanya sadaka kwenye madhabahu ya mtu halafu ukazibeba hapohapo. Acha chochote kinachopatikana mwenyeji akupe kulingana na matakwa yake au alivyopanga na uongozi wake. Usijikusanyie halafu baada ya ibada ukaziokota ukaweka kwenye pochi ukasepa nazo. Labda wakuruhusu wenyewe au wakupe wenyewe lakini otherwise Ni kuonyesha tabia ya ulafi na uroho. Ni kukosa adabu kwenye madhabahu ya mtu. Paycheck yako inatoka kwa Mungu. Usiangalie kapu la sadaka au kinachokusanywa. Mimi na Mume wangu tumewahi kufanya kazi na unaondoka mwenyeji anakupa mkono tunamshukuru Mungu tunaendelea na Maisha. Na mara nyingi Mungu amejua kutulipa kwa njia tusizotarajia na ametulipa vikubwa zaidi kuliko kile ambacho pengine tungepewa na watu. Ukijifunza kuwaza hivi utafanya huduma bila manung'uniko na kwa Uhuru sana.

🔥Usiwe TOO DEMANDING unachosha watu. Kuwa simple na mruhusu mwenyeji akuhudumie kulingana na UWEZO WAKE. Usiwe mtu ambaye mtu akikualika kwake atajuta yaani anatamani tu uondoke kwa jinsi ulivyo msumbufu. Mara unataka hiki, Mara huli hiki, Mara huwezi kulala mahali Fulani (wakati kwako unalala pabaya kuliko hapo), Maintain standards yes lakini USICHOSHE WATU...

🔥Heshimu MUDA uliopewa. Usijiongezee muda huku unasema ni Roho Mtakatifu. Na hata ikiwa ni Roho Mtakatifu mwenyeji atajua na atakuruhusu kuendelea, acha wenyewe wakuruhusu. Usiambiwe uimbe wimbo mmoja ukasimama ukahubiri kwanza ndio ukaimba mbili na mwenyeji akisimama anataka Mic ndio unajifanya uko deep huoni na macho unafunga, usijiongezee muda na hawajakuruhusu, usipewe lisaa limoja LA kuhubiri/kufundisha ukanogewa ukapiga mawili huku mwenyeji anakuandikia vikaratasi kila Saa na unajifanya umechemka huvioni. Siku nyingine hawatakuita. Heshimu MUDA.

🔥Ukiona tatizo lolote ndani ya huduma ya mtu au mahali ulipoitwa kabla ya kuliadress publicly liaddress privately na mwenyeji aliyekuita. Akikuruhusu kulishughulikia publicly lishughulikie. Other wise Fanya kilichokupeleka matatizo yao waachie wenyewe.

🔥Mara nyingi tafuta kujua MATARAJIO ya aliyekuita. Mimi huwa nauliza wenyeji what do you want kiwe kimekua accomplished baada ya mkutano huu, matarajio yenu ni nini, malengo yenu ya kuandaa mkutano/semina/workshop hii ni nini.....Nikishayajua yananisaidia kujua k**a nafanya kazi napiga mpaka wapi.

🔥Sio vibaya kupokea zawadi kutoka kwa washirika lakini ni vizuri na ni Salama mwenyeji akijua hasa vinapokua vitu vikubwa k**a nyumba, magari, viwanja etc.

🔥Usiende kwenye nyumba/biashara za washirika bila mwenyeji kuwa na taarifa na ikiwezekana nenda nae.
🔥Usichukue mawasiliano ya washirika wa mtu kwa siri hasa wenye vyeo na pesa na ukaanza kuwaambia wakuletee sadaka. Ni kujidhalilisha na ni kuonyesha umejaa njaa. Katika hali zote jua kwamba wewe ni Mtumishi wa Mungu na cheo au pesa ya mtu visikubabaishe. Fanya kazi ya Mungu kwa uaminifu mengine muachie Mungu mwenyewe afanye.

🔥Usiambie mshirika yeyote wa mwenyeji aliyekualika MADHAIFU ya kiongozi wao hata k**a yakoje. Wala usikae na washirika ukaanza kudiscus matatizo ya kiongozi/viongozi wao. Ni kuwashusha hadhi, kuwadhalilisha na kuwavua Nguo kwa Watoto wao wenyewe.

Kumbuka unachokipanda utavuna.

*©NGUVU YA NENO NA MAOMBI*

Baadhi ya picha za matukio ya Graduation ya TANZANIA PRAYER WARRIORS ya wahitim wa kidato cha sita, Kazima sec April 201...
22/04/2018

Baadhi ya picha za matukio ya Graduation ya TANZANIA PRAYER WARRIORS ya wahitim wa kidato cha sita, Kazima sec April 2018.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

0719852634

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania Prayer Warriors posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share