31/08/2018
WAHI KUTUBU ILI MAPIGO YALIYO ACHILIWA KWAKO YASIKUPATE TENA
1Samwel 7:9-10
9 Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa nzima; Samweli akamlilia Bwana kwa ajili ya Israeli; Bwana akamwitikia.
10 Hata Samweli alipokuwa akiitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakakaribia ili kupigana na Israeli; walakini Bwana akapiga ngurumo, mshindo mkubwa sana, juu ya Wafilisti siku ile, akawafadhaisha; nao wakaangamizwa mbele ya Israeli.
Bwana Yesu asifiwe mwana wa Mungu.
Hakuna kitu kibaya k**a dhambi, dhambi inaondoa uhalali wa mtu kumiliki, kutawala, kutiisha, Dhambi inaondoa ushirika wako na Mungu, dhambi inazuia ulinzi wa Mungu kusimama juu yako
Hapo ndipo utaona madhara makubwa ya dhambi, watu wengi leo wamezizoea dhambi kiasi kwamba wameishia kwenye utumwa mkubwa na mbaya maishan mwao, magonjwa, taabu umaskin na mabaya yafananayo na hayo vimewashikilia watu kiasi kwamba furaha ya maisha inakosekana kwenye familia na watu binafsi.
Kukosa aman ndani ya moyo, mahangaiko makubwa kwenye mioyo ya watu imepelekea watu kuyachukia maisha yao, ukitazama tatizo ni dhambi ambazo amezitenda.
Neno la Mungu linatuambia wana wa Israel walikaa kwenye utumwa mkubwa sababu ya dhambi walizokua wamemtenda Bwana, kiasi kwamba wakalipoteza sanduku la Agano la Bwana, Neno pia linatuambia ukianza kusoma mstari wa kwanza kuwa Wafirist waliwatesa, kuwapiga na kuwa tawala kwa muda mrefu sababu ya dhambi na uasi wao kwa Mungu.
Dhambi ina ondoa ulinzi wa Mungu kwa mtenda dhambi, na Mungu ndie alie tuumba maana yake pasipo yeye maisha yetu yanakua hatarini,
Ndio maana Mungu amesema na watumishi mbali mbali juu ya kuikataa na kuikimbia dhambi ili kuimarisha uhusiano na yeye kwakiwango kikubwa.
Nami nakusii mwana wa Mungu kaa mbali na dhambi, ikimbie dhambi, usiisogelee dhambi, sio kwamba dhambi itakaa mbali na wewe, itakutafuta ila ukiona ishara zake ikatae na ikimbize mbali nawe kwa jina la Yesu
Neno la Mungu linasema wana wa Israel wakamwambia Nabii samwel ili awaombee toba kwa Mungu, zaman watumishi ndio walikua wapo kusimama na Mungu kuwaombea toba watu, lakini Yesu alivunja kiambaza hivyo kila mtu anauhalali wa kumwendea Mungu na kupeleka hoja zake, hivyo mlilie Mungu kwaajili ya dhambi zako ili akusamehe na utoke utumwan
Mtumishi wa Mungu Samweli akawaombea toba kwa Mungu na Mungu akawasamehe, sasa ona kitu hapa, adui ambao wafirist wakajua kuwa Israel si lolote wakaenda kupigana, Biblia inasema Wafirist walipigwa vibaya na Mungu na badae na wana wa Israel, nataka kusema nini hapo, unapo fanya toba hata k**a uliteswa miaka mingap mateso yanakuachia na ulinzi wa Bwana unakua juu yako na Bwana ndie anaepigana na adui zako
Kuna maadui wengi sana sirin ambao wanakupinga pasipo wewe kujua au ukiwa unajua, lakini wanapata nafasi kwakua, umewapa nafasi ya kukutawala, lakini utakapofanya toba hawataweza kukutesa tena bali watapigwa na Bwana.
Ukiona umeomba toba lakin mateso bado, usikate tamaa endelea kuomba toba kwa iman na bidii, omba mpaka usikie aman ya tofauti ndani yako, kadiri unapofanya toba kuna mambo yabaya yanaanza kukuachia, na mwisho mateso yote yanaondoka kwako
Neno linatuambia kuomba kwake mwenye haki yafaa sana akiomba kwa bidii, maana yake usiache kuomba na bidii yako isirudi nyuma. Yakobo 5:16-18
Omba huku ukijitenga na dhambi, ukiichekea dhambi itakuachilia mauti, mauti ya kila kitu utakachokua unafanya.
Amua leo kumrudia Bwana ili akutoe utumwan.
Nyumba Ya Sala Kwa Mataifa Yote. 969 likes · 80 talking about this. Religious Organization