29/04/2022
UNAJIFUNZA NINI?????
Ndege kubwa aina ya Boeng ilikuwa inafanya safari zake kuelekea nchi za Ulaya ikiwa na abiria wasiopungua 300 ndani yake.
Ghafla Baada ya nusu saa kupita tangu kupaa angani, sauti ilisikika toka chumba cha Rubani kwamba "Ndege imepata itilafu kwenye mfumo wa Engine na Engine moja haifanyi Kazi kabisa ila engine nyingine inafanya KAZI kwa uhafifu na Wakati wowote Ndege itaanguka na kuteketea kabisa.
Hivyo kila mmoja Ndani ya Ndege na afanye ibada ya maombi na kuombana msamaha Ili Hata wakifa Mungu awapokee.
Basi miongoni mwa abiria waliokuwemo ni pamoja na Mume na mke waliokuwa wakielekea jijini Paris Ufaransa.
Mke akaanza kusema: Mume Wangu naomba unisamehe Maana mtoto yule Angle tulienae Sio mtoto wako, pia Wakati unavamiwa na kuporwa pesa ilikuwa ni mpango Wangu Ili kupata pesa za kumsaidia boyfriend Wangu kulipia Ada ya chuo. Hivyo naomba unisamehe Sana mume Wangu.
Mume: Wala usijali mke wangu nami pia nilitembea na wadogo zako wote na kulala nao, pia yule mama Yako mdogo ile mimba ni mimba yangu.
Baada ya muda kupita Sauti nyingine toka chumba cha Rubani ikasikika ikisema, ASANTENI SANA NDG ABIRIA KWA MAOMBI YENU NA MUDA MCHACHE NDEGE YETU ITAWEZA KUTUA KWENYE KIWANJA CHA NDEGE KWA DHARURA.
Basi Abiria wote wakabaki na mshangao mkuu Sana.
UNAJIFUNZA NINI KUPITIA KISA HIKI??????