07/06/2026
Somo:IBADA YA SHUKURANI
Mchungaji :FELX SECHU
Ni wajibu wa kila mtu kumshukuru Mungu kwasababu yeye ndiye chanzo cha kuumbwa
-unakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa neema yake ya milele mfano viungo vyote unavyo huna kilema , mshukuru Mungu kwa kukupa chakula maana kunawengine wanalala njaa, mshukuru Mungu kwajili ya familia uliyo nayo
_Wimbo wa shukrani unaimbwa sawa sawa na kipawa na karama aliyokupa Mungu, namnaunavyotumia kipawa na karama aliyokupa Mungu nafasi hiyo kumshukuru Mungu inamaana unamshukuru Mungu kwa kazi hiyo aliyokupa
Mathayo 25:14-30
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake.Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja;
*Lazima utumie nafasi uliyopewa sawasawa ili Mungu asikunyang'anye
Kwahiyo ni lazima uheshimu nafasi uliyopewa na Mungu na utumie sawasawa
-Ni ratiba ya Mungu kuona watu wanamshukuru
Luka 17:12-19
Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali;wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
-Mungu anapokutendea anapenda kushukuliwa .Mungu anaweza akakuponya na asikuokoe lakini anaweza kukuponya na akakuokoa k**a yule mkoma ambaye alirudi kumshukuru ndiye aliye okolewa na akapewa nyongeza ya wokovu kwahiyo ni vizuri kwenda mbele za Mungu kwa shukurani
Njia zakumshukulu Mungu
1.Kumshukuru Mungu kwa njia ya kusifu
2.kumshukuru Mungu kwa nyimbo
3.kumshukuru Mungu kwa MATOLEO yako
- Agizo la Bwana linapokuja kwako na ukalifanya kwa bidii lazima upokee majibu kwa sababu umelifanya kwa moyo wa shukrani
-sadaka ya shukrani ni muhimu uwe umepata baya ama zuri jifunze kumshukuru
Zaburi 138:1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Mfalme daudi hakuangalia mazingira yaliyomzunguka ndomana akasema mbele ya Miungu nitakuimbia zaburi .Mungu lazima ashukuriwe mtu mwenye moyo wa shukrani kesho yake ni ya dhahabu anakuwa anawaza mbele anaamini Mungu atafanya tena
*Anayestahili kupewa sifa na utukufu ni Mungu pekee piaMungu anapenda tumshukuru kwa sifa kwahiyo jifunze kumshukuru kwa kusifu
Nini kinatokea unapo mshukuru Mungu
Ayubu 35:7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
Nikawaida ya Mungu kupokea kitu kutoka kwa mwanadamu
*Shukrani inamaanisha kwamba unatambua uwepo wa Mungu na kwamba jinsi ulivyo ni Mungu ameyafanya
*Shukrani inamaanisha kwamba Mungu anastahili kupewa ama kupokea tena
Ufunuo wa Yohana 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.
-unapotoa sadaka ya shukrani unamshinda adui,sadaka ya shukrani ni njia ya kumshinda adui pia kunasiri katika kumshukuru Mungu lakini ukinung'unika unampa adui nafasi ya kukushikilia
2 Mambo ya Nyakati 29:31 Ndipo Hezekia akajibu, akasema, Sasa mmejifanya wakfu kwa Bwana, karibuni mkalete dhabihu na matoleo ya shukrani nyumbani mwa Bwana. Basi kusanyiko wakaleta dhabihu na matoleo ya shukrani; na wote wenye moyo wa ukarimu, wakaleta sadaka za kuteketezwa.
-Unapitoa sadaka ya shukrani unaonesha moyo wa ukarimu unaaminiwa na Mungu pia unajiweka wakfu na kufanywa kuwa wa Bwana
-Mungu anapendezwa na moyo wa ukarimu, ukiwa na ukarimu unakuwa na utayari ukishakuwa na utayari unapata nafasi kwa Mungu na unaruhusu Mungu akutumie
Mungu anapendezwa nawewe kuona unamshukuru