Efatha Church Makabe

Efatha Church Makabe Christian Church
Efatha Makabe is located at Mbezi Mwisho,Makabe Road near Makabe Police Station

07/06/2026

Somo:IBADA  YA SHUKURANIMchungaji :FELX SECHU Ni wajibu wa kila mtu kumshukuru Mungu kwasababu yeye ndiye chanzo cha kuu...
07/06/2026

Somo:IBADA YA SHUKURANI
Mchungaji :FELX SECHU

Ni wajibu wa kila mtu kumshukuru Mungu kwasababu yeye ndiye chanzo cha kuumbwa
-unakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa neema yake ya milele mfano viungo vyote unavyo huna kilema , mshukuru Mungu kwa kukupa chakula maana kunawengine wanalala njaa, mshukuru Mungu kwajili ya familia uliyo nayo

_Wimbo wa shukrani unaimbwa sawa sawa na kipawa na karama aliyokupa Mungu, namnaunavyotumia kipawa na karama aliyokupa Mungu nafasi hiyo kumshukuru Mungu inamaana unamshukuru Mungu kwa kazi hiyo aliyokupa

Mathayo 25:14-30
Maana ni mfano wa mtu atakaye kusafiri, aliwaita watumwa wake, akaweka kwao mali zake.Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja;

*Lazima utumie nafasi uliyopewa sawasawa ili Mungu asikunyang'anye
Kwahiyo ni lazima uheshimu nafasi uliyopewa na Mungu na utumie sawasawa
-Ni ratiba ya Mungu kuona watu wanamshukuru
Luka 17:12-19
Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali;wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.

-Mungu anapokutendea anapenda kushukuliwa .Mungu anaweza akakuponya na asikuokoe lakini anaweza kukuponya na akakuokoa k**a yule mkoma ambaye alirudi kumshukuru ndiye aliye okolewa na akapewa nyongeza ya wokovu kwahiyo ni vizuri kwenda mbele za Mungu kwa shukurani

Njia zakumshukulu Mungu
1.Kumshukuru Mungu kwa njia ya kusifu
2.kumshukuru Mungu kwa nyimbo
3.kumshukuru Mungu kwa MATOLEO yako
- Agizo la Bwana linapokuja kwako na ukalifanya kwa bidii lazima upokee majibu kwa sababu umelifanya kwa moyo wa shukrani
-sadaka ya shukrani ni muhimu uwe umepata baya ama zuri jifunze kumshukuru

Zaburi 138:1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.

Mfalme daudi hakuangalia mazingira yaliyomzunguka ndomana akasema mbele ya Miungu nitakuimbia zaburi .Mungu lazima ashukuriwe mtu mwenye moyo wa shukrani kesho yake ni ya dhahabu anakuwa anawaza mbele anaamini Mungu atafanya tena
*Anayestahili kupewa sifa na utukufu ni Mungu pekee piaMungu anapenda tumshukuru kwa sifa kwahiyo jifunze kumshukuru kwa kusifu

Nini kinatokea unapo mshukuru Mungu
Ayubu 35:7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?

Nikawaida ya Mungu kupokea kitu kutoka kwa mwanadamu

*Shukrani inamaanisha kwamba unatambua uwepo wa Mungu na kwamba jinsi ulivyo ni Mungu ameyafanya

*Shukrani inamaanisha kwamba Mungu anastahili kupewa ama kupokea tena

Ufunuo wa Yohana 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.
-unapotoa sadaka ya shukrani unamshinda adui,sadaka ya shukrani ni njia ya kumshinda adui pia kunasiri katika kumshukuru Mungu lakini ukinung'unika unampa adui nafasi ya kukushikilia

2 Mambo ya Nyakati 29:31 Ndipo Hezekia akajibu, akasema, Sasa mmejifanya wakfu kwa Bwana, karibuni mkalete dhabihu na matoleo ya shukrani nyumbani mwa Bwana. Basi kusanyiko wakaleta dhabihu na matoleo ya shukrani; na wote wenye moyo wa ukarimu, wakaleta sadaka za kuteketezwa.
-Unapitoa sadaka ya shukrani unaonesha moyo wa ukarimu unaaminiwa na Mungu pia unajiweka wakfu na kufanywa kuwa wa Bwana

-Mungu anapendezwa na moyo wa ukarimu, ukiwa na ukarimu unakuwa na utayari ukishakuwa na utayari unapata nafasi kwa Mungu na unaruhusu Mungu akutumie

Mungu anapendezwa nawewe kuona unamshukuru

IBADA YA MATOLEOMT:Roselyn Mwanzo  8:15-22Mungu akamwambia Nuhu, akisema,Toka katika safina, wewe, na mkeo, na wanao, na...
07/06/2026

IBADA YA MATOLEO
MT:Roselyn
Mwanzo 8:15-22
Mungu akamwambia Nuhu, akisema,Toka katika safina, wewe, na mkeo, na wanao, na wake za wanao pamoja nawe.Utoe pamoja nawe kila kilicho hai kilichomo pamoja nawe, chenye mwili, ndege, na mnyama, na kila kitambaacho, chenye kutambaa juu ya nchi; wajae katika nchi, wawe na uzazi, wakaongezeke katika nchi.Basi Nuhu akatoka, yeye, na wanawe, na mkewe, na wake za wanawe pamoja naye;
kila mnyama, na kila kitambaacho, na kila ndege, kila kinachokwenda juu ya nchi kwa kabila zao, wakatoka katika safina.Nuhu akamjengea Bwana madhabahu;

-Nuhu alimjengea Mungu madhabahu na akamtolea Mungu sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu

*Kwa Yale yote ambayo Mungu ameyafanya kwetu inabidi Umtolee sadaka ya shukrani
Unapotoa sadaka ya shukrani unaonesha alama ya ushindi kwa Yale yote Mungu aliyoyafanya kwako

IBADA YAUFUNGUZIAsk:Severina  MateruMithali 20:27 Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yak...
07/06/2026

IBADA YAUFUNGUZI
Ask:Severina Materu

Mithali 20:27
Pumzi ya mwanadamu ni taa ya Bwana; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.

Zaburi 23:1-6
Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.

MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
01/06/2026

MEZA YA BWANA

Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.

Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.

Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

MEZA YA BWANAYohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.  B...
31/05/2026

MEZA YA BWANA

Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.”

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”

Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”

Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa...
31/05/2026

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Baba anabeba mizigo yote inayohusu watoto, maumivu yote ya watoto, huu ndiyo ubaba; anasimama kwa ajili ya familia yake. Yesu aliye baba wa milele kwetu, alichukua mizigo yetu, maumivu yetu na changamoto zetu zote na akafa nazo msalabani na huu ndiyo ubaba.

Wakolosai 2:14-15 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutush*taki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Yesu k**a baba aliyabeba haya yote kwa ajili yetu mimi na wewe, halafu kuna mtu anasahau kile Yesu Kristo amefanya pale msalabani? Aliyoyafanya Yesu ni kwa ajili yetu.

Wakolosai 2:13 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;”
Tulikuwa tumekufa lakini kwa ajili yake leo hii tupo hai.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Pasipo Imani hauwezi kumpendeza Mungu, k**a haumpendezi YEYE inamaana kuwa unamkosea; utajuaje hivyo? Kwa maana Biblia inasema “huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Wale wanaompendeza Mungu YEYE huwapa mahitaji yao, hii ina maana kuwa wale wasiyompendeza wanateseka na kuzunguka sana, wanaishi na njaa na katika uhitaji ingawa wamezaliwa mara ya pili (wameokoka) kwa nini wanaishi hivyo? Ni kwa sababu hawampendezi YEYE.

Biblia inasema “Kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Hivyo kwanza unapaswa kuelewa kuwa YEYE yupo hai, anakuona na kukutazama, hivyo atatazama kila unachofanya, kile unachokifanya kikimpendeza YEYE anakupa mahitaji ili kukufanya wewe uende mbele, k**a ukifanya vizuri anakupa uzuri ili aweze kukushawishi wewe uende mbele. Vile unavyofanya vizuri inamfurahisha YEYE na YEYE akifurahi anakupa wewe zaidi na zaidi na ndivyo unavyozidi kuwa na kila kitu katika maisha yako, yaani (unakuwa tajiri).

Mwanamke muombe Mungu akupe kuolewa na mwanaume mwenye akili nzuri maana mtu mwenye akili nzuri mara zote anatafuta kumpendeza Mungu. Anaweza kuwa leo hii hana kitu lakini k**a akili yake ni nzuri basi utajua kuwa huyu ana uhakika na anajua wapi anaenda. Mwanaume mwenye imani hata k**a ataanguka lakini Bwana Yesu atamuinua na atampa kusonga mbele.

Wewe mama muangalie mumeo Je! Akianguka anainuka? Ukimuona anaamka na kwenda kanisani usiangalie alichokosea lakini angalia nia aliyonayo, biblia inasema “ataanguka mara saba lakini atainuka,” mwanamke usimkatishe mumeo tamaa maana ana safari na atafika. Mimi k**a baba yao nimeamua kusimama na wababa na sitakaa kimya mpaka wafike wanakotakiwa kufika.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Nay...
31/05/2026

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGUIsaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kif...
31/05/2026

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU

Isaya 9:6
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Address

Mbezi Makabe
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
23:00 - 05:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 07:30 - 17:00

Telephone

+255713402322

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Makabe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share