08/01/2025
NIMESAMEHEWA DHAMBI ZANGU ZOTE Part 1
Copy & Paste
Chukua Hii K*toka Kwa Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church
Malaika alimtokea Yusufu na kumwambia…
Mathayo 1:20-21
[20] Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
[21] Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake YESU, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao
Tazama Luka 24:44-49
[44] Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.
[45] Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
[46] Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
[47] na kwamba mataifa yote WATAHUBIRIWA kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
[48] Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.
[49] Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
Ujumbe wa Injili unaweza kuelezwa k**a AHADI KWENYE VITABU VYA AGANO LA KALE AMBAYO KRISTO ATAKUJA NA KUITIMIZA KWA KUPATA MATESO, KUFA NA KUFUFUKA KWAKE NA KWA SABABU HIYO TOBA NA MSAMAHA WA DHAMBI KUHUBIRIWA. Hii ndio sababu Injili inahubiriwa.
Je, toba ni nini?
Toba ni neno la Kigiriki metanoia lenye maana badiliko la fikra na mwelekeo na hii hutokea zaidi baada ya kusikia ujumbe. Hebu tutazame namna neno hili metanoia lilivyotumika katika Biblia. Mzizi wa neno metanoia ni metanoeō lenye maana ya kufikiri tofauti baadae.
Marko 1:15 [15] akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili. "…tubuni na kuiamini Injili". Maana yake Kubadili fikra kwa kuiamini Injili.
Mathayo 12:41
[41] Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.
…kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; walibadilika katika fikra zao, walisadiki ujumbe wake.
KUTUBU NI KUPOKEA UJUMBE.
Neno kutubu limekuwa likitumika kwa umaarufu katika jamii yetu k**a KUOMBA MSAMAHA BAADA YA KUFANYA KOSA. Maana ya Biblia ya kutubu sio hii kabisa. K*tubu sio matokeo ya kukosea kwa mtu bali ujumbe aliosikia (Injili).
Baada ya mahubiri marefu ya Petro kwenye Matendo 2, anawaagiza wasikilizaji wake kutubu.
Matendo 2:37-38
[37] Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
[38] Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Wakamwambia Petro, tutendeje ndugu zetu? Tubuni mpate ondoleo la dhambi zenu.
Hapa tena baada ya kuhubiri;
Matendo 3:19
[19] Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;
Tubuni ili dhambi zenu zifutwe.
Matendo 5:31
[31] Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.
Matendo 10:43
[43] Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.
Kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.Hapa Petro ametumia maneno KILA AMWAMINIYE ambapo ni sawa na kusema TUBUNI.
Kwa muktadha huu KUTUBU ni kile kinachotokea baada ya mtu kusikia Injili yaani habari za kufa na kufufuka kwa Yesu. Matokeo ya badiliko hili la nia ni kupokea MSAMAHA WA DHAMBI.
Hii ni kwa imani (kwa kuamini Injili).
Msamaha wa dhambi au ondoleo la dhambi ni neno moja la Kigiriki APHESIS ambalo linamzizi kutoka kwenye neno APHIEMI…lenye maana ya (English) -- release from the bo***ge or imprisonment, pardon of sins (letting them go as if they had never been commited), remission of the penalty.
[Kiswahili chake] kuachiliwa au kuondolewa kifungoni, kusamehe au kuziachilia dhambi kana kwamba hayajawahi kufanyika.Huu ndio ubora wa dhabihu ya Yesu Kristo. Hivi ndivyo Mungu anafanya kwa mwamini. Dhambi zake zimeondolewa, zimefutwa.
Maneno yote mawili, MSAMAHA WA DHAMBI na ONDOLEO LA DHAMBI yametafsiriwa kutoka kwenye neno hili moja la Kigiriki APHESIS.
Matendo ya Mitume 5:29-31
[29] Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
[30] Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti.
[31] Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.
Anawataka pia watubu (waamini) katika kufa na kufufuka kwake ili wapokee Msamaha wa dhambi.
Nyuma kwenye sura ya 2, Petro alihubiri vivyo hivyo;
Matendo ya Mitume 2:38
[38] Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Tubuni mpate ondoleo la dhambi zenu. Neno la Kigiriki la ondoleo la dhambi na Msamaha wa dhambi ni moja APHESIS.
Matendo ya Mitume 10:42-43
[42] Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na wafu.
[43] Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.
Kwenye nyumba ya Kornelio pia alihubiri habari za kufa na kufufuka kwake Yesu hivyo kupata ondoleo la dhambi kwa kila aaminiye.
Matendo ya Mitume 13:37-39
[37] Bali huyu aliyefufuliwa na Mungu hakuona uharibifu.
[38] Basi, na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo mnahubiriwa msamaha wa dhambi;
[39] na kwa yeye kila amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa.
Matendo ya Mitume 26:13-18
[13] Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote.
[14] Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
[15] Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.
[16] Lakini inuka, usimame kwa miguu yako, maana nimekutokea kwa sababu hii, nikuweke wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako;
[17] nikikuokoa na watu wako, na watu wa Mataifa, ambao nakutuma kwao;
[18] uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.
Tazama mkazo wa huduma yake…awafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache nguvu za giza na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi (YESU).
Mtume Paulo alijua namna ya kuzishinda nguvu za giza (za shetani); ni kwa kuhubiri Injili inayotoa msamaha wa dhambi kwa imani katika Kristo.Paulo hapa tena, Matendo ya Mitume 26:22-23
[22] Basi kwa kuwa nimeupata msaada utokao kwa Mungu nimesimama hata leo hivi nikiwashuhudia wadogo kwa wakubwa, wala sisemi neno ila yale ambayo manabii na Musa waliyasema, kwamba yatakuwa;
[23] ya kwamba Kristo hana budi kuteswa na ya kwamba yeye kwanza kwa kufufuliwa katika wafu atatangaza habari za nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.
Paulo alibaki katika kiini cha ujumbe wa manabii na Musa, habari za kufa na kufufuka kwa Yesu na watu kupokea Nuru (msamaha wa dhambi au kuhesabiwa haki).
Itaendelea….
Apostle Shemeji Melayeki
Global Family Gatherings
“God’s Standards”