11/06/2026
KUTOKA MASHAKA NA KUTOKUAMINI HADI KUFIKIA IMANI YA KWELI KATIKA KRISTO
Huu ni ushuhuda huu wenye nguvu sana, ambapo Joan anasimulia safari yake kutoka kwenye mashaka na kutokuamini hadi kufikia imani ya kweli kwa Kristo, akieleza jinsi alivyokutana na Mungu katikati ya ugonjwa mkali na maswali mengi moyoni mwake.
Licha ya kujaribu kuupinga ukweli na kuuthibitisha Ukristo kuwa si wa kweli, Joan anapitia mabadiliko makubwa ya ndani baada ya kutambua ukweli kuhusu Yehoshua (Yesu) kuwa ndiye Masihi wa Ulimwengu na Wayahudi wote.
Akiwa anakabiliana na magonjwa zaidi ya 75 yaliyokuwa yakimdhoofisha, pamoja na saratani ya endometria, Joan hatimaye anapata uponyaji kupitia maombi na toba ya kweli. Leo hii, ana shauku kubwa ya kuwafundisha wengine kuhusu Israeli na imani yake, huku akiendelea kushikilia urithi wake wa Kiyahudi kwa kina na wakati huo huo akimkubali Yeshua k**a Masihi wake.
Ushuhuda wa Joan ni ushuhuda uliobeba nguvu ya uponyaji ya Mungu na namna kukutana na ukweli wake kunavyoweza kubadilisha maisha kabisa.
Alikuwa amekonda sana kiasi kwamba hata kuinua kichwa chake kitandani ilikuwa shida. Mwili wake ulikuwa umechoka sana. Nguvu zote zilikuwa zimeisha. Na sasa madaktari walikuwa wanamwambia:
“Una saratani mbaya sana. Utahitaji miezi sita ya chemotherapy yenye nguvu sana, na wiki sita za mionzi kila siku.”
Aliposikia hayo, kitu pekee kilichokuwa kichwani mwake ni:
“Hii tiba itanua.”
Lakini kabla ya kufika kwenye kitanda hicho cha hospitali, kulikuwa na safari ndefu sana iliyomfikisha hapo.
Joan alizaliwa na kukulia Southern California katika Familia ya Kiyahudi katika mila na tamaduni zao. Kumbuka Wayahudi wako strict sana kwenye mila na taratibu zao. Kila wiki walikwenda katika sinagogi zao kwa masomo ya dini, na wakishiriki sikukuu zote muhimu za Kiyahudi.
Akiwa na miaka 12, familia yao ilisafiri kwenda Israel huo ni mwaka 1966. miezi mitano kabla ya vita vya mwaka 1967.
Anakumbuka siku moja akiwa sehemu ya juu akiangalia mbali, mwongoza watalii akiwaambia:
“Huo ndio mji wa kale… lakini haturuhusiwi kwenda huko.”
Akasimama akitazama kwa mbali na kujiuliza
“Ingekuwaje k**a tungeruhusiwa kuingia huko?”
Mama yake alikuwa ameishi Israel tangu akiwa na miaka 12 mpaka 24. Alikuwa sehemu ya harakati za siri za Israeli, akafanya kazi k**a jasusi kwa Waingereza.
Kwa hiyo, hata akiwa anaishi California, Israel ilikuwa katika damu yake. Kadri alivyokuwa anakua, alitamani kuielewa zaidi dini yake ya Kiyahudi. Walifundishwa hadithi za Nuhu, Musa na Kutoka Misri, lakini hakuwahi kuona picha nzima ya mpango wa Mungu kwa taifa la Israeli kuanzia mwanzo mpaka mwisho.Kuna kitu hakikuwa kinaungana pamoja moyoni mwake.
Shuleni kwao alikuwa Myahudi pekee. Walipoimba nyimbo za Krismasi na jina “Yesu” lilipotajwa, kwa namna fulani alijisemaea,
“Hilo jina halipaswi kutoka kinywani mwangu.”
Kwa hiyo kila walipolitaja, alikuwa anafunga mdomo wake.
Mpaka alipofika chuo kikuu. Huko alipata roommate Mkristo mwaka wa kwanza. Kwa macho yake, Wakristo walikuwa watu dhaifu tu waliotafuta kitu cha kuwafariji kihisia. Aliamini hawakuwa na msingi wa kweli wa kile walichokiamini.
Lakini boyfriend wa roommate wake alikuwa kijana mtulivu aitwaye Gary. Mara nyingi alikuwa anazungumza naye kuhusu Mungu.
Siku moja akamwambia:
“Gary, nitathibitisha kwamba kile mnachoamini hakina msingi wowote.”
Gary akamjibu kwa utulivu: “Sawa. Lakini kabla hujaanza safari yako, naomba usome kitabu kimoja.” Akakubali.
Kitabu kile kilikuwa kinaitwa Late Great Planet Earth. Na hicho ndicho kilibadilisha kila kitu. Kwa mara ya kwanza maishani mwake, alianza kuona picha kubwa ya historia ya Wayahudi kuanzia Mwanzo hadi mwisho wa mpango wa Mungu.Kilichomshtua zaidi kilikuwa unabii. Hakuwahi kufundishwa unabii kwenye sinagogi.
Lakini sasa alikuwa anaona jinsi Mungu alivyotoa utabiri maalum mamia na maelfu ya miaka kabla na mambo hayo yakatokea sawasawa kabisa. Na unabii huo wote ulikuwa unaelekeza kwa mtu mmoja Yehoshua (Yesu).
Jambo hilo lilimkasirisha sana.Kwa sababu kitu cha mwisho kabisa alichotaka maishani mwake… kilikuwa kuwa Mkristo.
Akaenda kwa rabbi wake na kumuuliza:
“Naomba unielezee Isaya 53. Kwa sababu hii inaonekana kabisa k**a Masihi wa Agano Jipya.”
Rabbi aliiangalia ile sura.
Halafu akasema kwa uaminifu:
“Samahani… siwezi kukuelezea. Sijui.”
Kadri alivyoendelea kusoma, kila kitu kilikuwa kinaonyesha upande mmoja tu. Kwamba Yeshua ndiye Masihi wa Wayahudi.Na jambo hilo lilimvuruga sana kwa sababu lengo lake tangu mwanzo lilikuwa kupinga hilo.Usiku mmoja akiwa amelala kitandani, akiwa amechanganyikiwa kabisa, alimlilia Mungu.
“Mungu… sitaki kuwa Mkristo.”
Halafu akaongeza:
“Lakini k**a kweli unataka kuniokoa… basi fanya utakavyo.”
Ndani yake alifikiri:
“Sawa. Hakuna kitakachotokea.”
Lakini ghafla…akaanza kuhisi kitu kinatembea kuanzia kichwani mwake. Kana kwamba uwepo fulani ulikuwa ukimwambia kuwa Mungu alikuwa anamsafisha dhambi zake.Hali ile ikatembea kutoka kichwani taratibu… ikashuka mwilini mpaka miguuni.
Usiku huo alilala vizuri.Na alipoamka asubuhi…alikuwa mtu tofauti kabisa. Nia yake ilibadilika. Sababu za kuishi zikabadilika.
Yule msichana aliyekuwa anaogopa hata kutamka jina la Yesu sasa alikuwa anasimama kwenye stage (mimbari) chuoni mbele ya mamia ya watu akishuhudia:
“Mungu ni halisi. Na Yesu ndiye Masihi wa Wayahudi.”
Miaka ikapita. Akaolewa. Baadaye ndoa yake ikaishia kwenye talaka baada ya miaka mingi.Kisha maisha yakaanza kubadilika tena na safari hii kwa maumivu makali.
Alipata fibromyalgia. Chronic fatigue syndrome. Mwili wake ulikuwa unateseka kila siku kwa miaka karibu nane.Hali ilizidi kuwa mbaya.Halafu madaktari wakampa habari nyingine mbaya zaidi kuwa ana Saratani ya kizazi. Stage 3C.
Walimwambia:
“Una nafasi nzuri ya kupona ikiwa utapitia chemotherapy kali kwa miezi sita, halafu tiba mionzi kila siku kwa wiki sita.”
Alishtuka sana.
Kwa sababu tayari alikuwa dhaifu sana.
Alikuwa amekonda kupita kiasi. Hata kutembea hadi kwenye mailbox ya nyumba yake ilikuwa kazi kubwa.
Ndani yake alifikiri:
“Tiba hii itanua.”
Lakini badala ya kukata tamaa, alianza safari nyingine.Safari ya toba.Usiku mmoja wa Mkesha wa Mwaka Mpya, alimwaga moyo wake mbele za Mungu huku analia.
“Bwana… unisamehe. Sikujua hata jinsi moyo wangu ulivyokuwa wenye dhambi.”
Akamwambia Mungu:
“Nitakesha mpaka unionyeshe kuwa uko pamoja nami.” Aliendelea kukesha mpaka saa tisa za usiku. Hakuhisi chochote. Lakini hakukata tamaa.
Kila siku aliendelea kudumu katika kuomba. Kuendelea kutubu. Kuendelea kumtafuta Mungu.Na polepole kila kitu kilianza kubadilika ndani yake.Alianza kusoma Biblia kwa namna ambayo hajawahi kufanya kabla.Alikesha mpaka saa nane au saa tisa usiku akisoma.
Anasema:
“Kila neno lilionekana k**a pumzi halisi ya Mungu.” Wakati huo huo alianza kula vitu ambavyo zamani vilikuwa vinamfanya awe mgonjwa k**a ice cream, dairy, gluten, chips lakini safari hii mwili wake haukupata shida k**a zamani.
Siku moja akasema:
“Lazima nijaribu kutembea hadi kwenye mailbox.”
Na akafanikiwa.Bila maumivu makali. Polepole, ndani ya miezi nane mpaka mwaka mmoja… Mungu alimponya.Si saratani tu.
Lakini pia karibu magonjwa 75 aliyokuwa nayo.
Na kitu kikubwa zaidi ambacho alikuwa amepambana nacho tangu akiwa mtoto mdogo ni Hofu kali na wasiwasi.
Anasema:
“Nilikuwa na nguvu. Sikuhofia tena. Kwa sababu nilijua Mungu wa ulimwengu wote alikuwa upande wangu.”
Halafu akaeleza jambo ambalo lilikuwa muhimu sana kwake;
“Hapana, sikugeuka kutoka kuwa Myahudi kwenda dini nyingine.”
Wayahudi wamekuwa wakimsubiri Masihi kwa maelfu ya miaka.Na yeye aliamini kuwa amempata.Yeshua.Masihi wa Wayahudi.
Mwaka 2012 aliporudi Israel, alipouona Mji wa Kale kwa macho yake mwenyewe, aliona k**a amerudi nyumbani.
Baadaye akaandika travel guide kuhusu Israel kwa ajili ya waamini, akaanza kupeleka vikundi Israel, na akaanzisha taisisi ya kusaidia kuelimisha watu kuhusu umuhimu wa Israel na kusaidia manusura wa Holocaust.
Na kila alipofikiria maisha yake…...alijawa na shukrani. Kwa sababu Mungu alimtoa kutoka mahali pa maumivu, hofu, ugonjwa, na kukata tamaa… na kumpa maisha mapya.
Hapa kuna la Kujifunza;
Yesu bado anaokoa watu wake. Hakuna wokovu mkuu namna hii. Tafuta taaluma zote na unajimu wa maarifa ya kila kitu bado Yesu atabaki kuwa Mungu katika nia ileile kuwaokoa waliopotea na kuwarejesha.
Wakati mwingine Mungu hukuruhusu ufikie mwisho wa nguvu zako ili ujue kwamba tumaini la kweli halipo kwenye uwezo wako, afya yako, au mipango yako, mwenza wako bali kwake pekee.
Pia, si kila mtu anayemtafuta Mungu anaanza akiwa tayari kuamini. Wengine wanaanza safari yao wakitaka kupinga ukweli. Lakini ukweli unapokuwa wa kweli, una nguvu ya kugusa moyo hata wa mtu aliyepinga zaidi.
Na jambo kubwa zaidi: Usikate tamaa hata hali yako inaonekana imefika mwisho. Ukiwa bado unapumua, bado kuna tumaini. Mungu anaweza kubadilisha moyo, kuponya maisha, na kuleta nuru hata katikati ya giza kubwa kabisa.
Natamani Mtu mmoja aokoke leo. Ikiwa uko tayari komenti hapa chini
Upendo wa Yesu