Upendo wa Yesu

Upendo wa Yesu Hakuna Upendo pasipo Mungu maana Mungu ni Upendo wenyewe. Twajifunza kwa Kristo Upendo na Uvumilivu.

MAANA YA KWELI YA IBADAAndiko Kuu: Yohana 4:23–24Kichwa cha Somo: Ibada si Desturi, ni MahusianoUTANGULIZINdugu wapendwa...
29/12/2025

MAANA YA KWELI YA IBADA

Andiko Kuu: Yohana 4:23–24
Kichwa cha Somo: Ibada si Desturi, ni Mahusiano

UTANGULIZI

Ndugu wapendwa, wengi wetu tunaposema ibada tunafikiria:

Kuimba Nyimbo

Kupiga Makofi

Ratiba ya Kanisa

Lakini Yesu anatufundisha kuwa ibada ni jambo la rohoni zaidi kuliko la nje. Ndiyo maana leo tunajifunza maana ya kweli ya ibada

1. IBADA NI KUKUTANA NA MUNGU ALIYE HAI

> “…waabuduo wa kweli watamwabudu Baba katika roho na kweli” (Yohana 4:23)

Ibada si programu, bali ni mkutano:

Kati ya Mungu na mwanadamu

Kati ya Muumba na Kiumbe Wake

➡️ Ukija kanisani bila kukutana na Mungu, umehudhuria ibada lakini hujafanya ibada.

Mfano wa Biblia:
Musa hakufanya ibada kwa kuimba, bali kwa kusujudu mbele ya uwepo wa Mungu (K*toka 3:5–6).

2. IBADA HUANZA NDANI, SIO NJE

> “Mungu ni Roho…” (Yohana 4:24)

Ibada ya kweli:

Huanzia moyoni

Hutoka katika Roho iliyonyenyekea

Si sauti kubwa pekee, Bali moyo ulio safi

➡️ Unaweza kuimba vizuri lakini bila moyo wa ibada.
➡️ Unaweza kuwa kimya lakini unamwabudu Mungu kwa kweli.

Daudi alisema:

> “Moyo safi uumba ndani yangu ee Mungu” (Zaburi 51:10)

3. IBADA NI MAISHA, SIO SAA MOJA KANISANI

> “Mtoeeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai” (Warumi 12:1)

Ibada:

Haishii Jumapili

Inaonekana kwenye mwenendo wetu

Inaonekana kwenye maamuzi yetu

➡️ Namwabudu Mungu:

Ninapokataa dhambi

Ninapotenda haki

Ninapomtii Mungu hata nikiumia

Ibada ya kweli inaonekana kwenye tabia, si madhabahuni tu.

4. IBADA YA KWELI HUACHA MATOKEO

Ibada ya kweli:

Hubadilisha mioyo

Huleta toba

Huleta upako

Huachilia nguvu za Mungu

“Palipo na Roho wa Bwana, hapo pana uhuru” (2 Wakorintho 3:17)

➡️ K**a hakuna mabadiliko, basi tujiulize:
Je, tulikuwa tunaabudu au tulikuwa tunaburudika?

5. IBADA YA WOKOVU NA ROHO MTAKATIFU

Ibada ya Kipentekoste:

ina uhuru wa Roho Mtakatifu

inaruhusu karama za Roho

inampa Roho nafasi ya kuongoza

> “Nao wote wakajazwa Roho Mtakatifu…” (Matendo 2:4)

➡️ Ibada bila Roho Mtakatifu ni k**a mwili bila pumzi.

HITIMISHO

Ibada si:

nyimbo peke yake

ratiba

desturi

Ibada ni:

kujitoa kwa Mungu

kuishi kwa kumpendeza Mungu

kukutana na Mungu kwa rohoni

WITO

Leo Mungu anatafuta:

> “Waabuduo wa kweli”

Je, wewe unaabudu:

kwa midomo au kwa moyo?

kanisani tu au kwa maisha yako yote?

🙏 Mwite Roho Mtakatifu akusaidie uwe mwabudu wa kweli.

Mch salvatory Mngofi

Huwezi kuizuia Injili ya Kristo hasa kwa nyakati hizi za mwisho tulizonazo.Kristo yu karibu sana kurudi. Lazima Injili i...
08/10/2025

Huwezi kuizuia Injili ya Kristo hasa kwa nyakati hizi za mwisho tulizonazo.

Kristo yu karibu sana kurudi. Lazima Injili ihubiriwe kwa mataifa yote watu wamjue Mungu waokolewe.

Usinyamaze Mwanafunzi!
Narudia tena Usinyamaze! Paza sauti yako, piga kelele watu watubu na kumwamini Kristo. Ujumbe ni ule ule "Tubuni! Kwa maana Ufalme wa Mungu umekaribia".

Luka anaandika katika 19:39-40
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako. Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele.

Mwanafunzi wa Kristo ukinyamaza wewe mawe yatapiga kelele. Mungu atampa mwingine(mawe) ujumbe uleule nao watapiga kelele ileile. Heri ulimi usionyamaza, heri midomo isiyokaa kimya kuhubiri Injili.

Maandiko yanasema ni mizuri k**a nini miguu yao wapelekao habari njema. Tumia privilege (neema) hiyo hiyo kumhubiri Kristo kazini kwako, mtaani kwako, kwa marafiki zako n.k. Usinyamaze.!

Panda mbegu ya Ufalme wa Mungu kila wakati. Usinyamaze!

03/10/2025
Huwafanyia hukumu walioonewa, Huwapa wenye njaa chakula; BWANA hufungua waliofungwa; BWANA huwafumbua macho waliopofuka;...
27/09/2025

Huwafanyia hukumu walioonewa,
Huwapa wenye njaa chakula;
BWANA hufungua waliofungwa;

BWANA huwafumbua macho waliopofuka;
BWANA huwainua walioinama;
BWANA huwapenda wenye haki;

Zaburi 146:7-8

Usiwe na Uchungu na WatuSehemu mojawapo ya mafunzo ya huduma ni kujifunza kutokuwa na uchungu na watu… unajiandaa kusame...
20/05/2025

Usiwe na Uchungu na Watu

Sehemu mojawapo ya mafunzo ya huduma ni kujifunza kutokuwa na uchungu na watu… unajiandaa kusamehe kabla ya kukosewa… unajiandaa kuachwa kabla hujaachwa… unajiandaa kuwaamini watu tena baada ya wale uliowaamini kuwa maadui na kutumia vibaya nafasi….mtu ambaye unajua hakupendi akija kwako unamfundisha k**a mwanao kipenzi. Inabidi ujifunze kufa ili uishi. Watu wawe maadui zako ila wewe usiwe adui na mtu. Yaani hili ujue mapema na likuelee.
—Global Family Gatherings
“God’s Standards”

UTENDAJI KAZI WA TOBA NA BADILIKO LA MWAMINIPart 02Lazima utambua kuwa ukiingia katika wokovu umeyakana maisha ya kale u...
23/04/2025

UTENDAJI KAZI WA TOBA NA BADILIKO LA MWAMINI

Part 02

Lazima utambua kuwa ukiingia katika wokovu umeyakana maisha ya kale umeyaingia maisha mapya. Usijaribu kuishi maisha mapya na attachment (maunganiko) ya maisha ya kale.

Neno la Mungu linasema hivi kupitia Paulo kwa Wakorintho "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya."
2 Wakorintho 5:17

Upya huletwa na Mungu kupitia Neema ya Wokovu. Upya wa maisha hutegemea na utayari wa kuitii Neema uliyopokea. Na Mungu aliweka hii iwe amri ya kwanza inasomeka hivi katika Kitabu cha Marko
Yesu akamjibu, "Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote." Marko 12:29-30

Neema huja na Upendo.Mungu amekupenda, amekuchagua ili uungane na Ufalme wa mwanae Yesu Kristo. Ni juu yako kuchagua kumpenda au la. Upendo wako kwa Mungu utaamua kiasi cha utii wa Neema ya Wokovu uliyopokea. Huwezi kutembea katika mtembeo mpya katika msimu wako mpya kwa akili ileile ya maisha ya zamani. Lazima kufikilia toba kwanza.

Toba ni nini? Kwa ufupi toba neno la Kigiriki "metanoia" maana yake ni "changing ones mind". Kubadili mtazamo, uelekeo au msimamo.

Kwa neno la Kiebrania Toba linatamkwa "teshuvah" ambalo lina maana ya "rudi/rejea" k**a kurejelea/kurudi sehemu au mahali ulipotakiwa kuwa lakini ukapaacha.

Usipoelewa maana iliyo katika sala ya toba unaweza usipate Neema halisi inayoambatana na hiyo sala. Mungu anajua mioyo kwahiyo k**a hujamaanisha hiyo sala ulipoikiri Mungu anajua na shetani anajua vilevile.

Maisha mapya katika Kristo hutegemea utayari, bidii, nidhamu na utii. Usiokoke kwa sababu unataka muujiza, au unataka tu faraja, au mafanikio ya mwilini, au unataka kuvunja laana za ukoo wako na sababu nyingine. Wokovu ni tendo la imani la kumchagua Mungu juu ya kitu chochote na kumpenda. Okoka kwa sababu umechagua kumpenda Mungu.

Usipoelewa na kutambua sababu ya kuokoka kwako utarudi nyuma kirahisi.

Jiulize kwanza! Wewe ni nani katika Kristo. Marafiki zako ni kina nani? Unazungumza nini na nani na unafanya nini na nani? Unatazama na kusikiliza nini, wakati gani ? Umezingukwa na kina nani na kwa kusudi gani? Unafikiri nini? Kwa ajili ya nini na nini ni vipaumbele vyako. K**a kipaumbele chao sio Mungu kwanza your in trouble.
Haijalishi unajiona uko salama kiasi gani kiuhalisia hauko salama k**a huna Mungu.

Maana Ibilisi hakujii ndotoni anakuja mwilini. Kwenye maisha ya kawaida ya kila siku. Maisha ya wokovu ni maisha ya nidhamu na utii sio mtindo wa kuingia na kutegemea kukutana tu na muujiza kwamba ghafla tu umekuwa safi na mtakatifu. Noop!

Wokovu ni hatua kwa hatua.

Kwanza unza toba. Toba ni mlango wa kumfungulia Kristo aingie maishani mwako. Iko hivi "atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi."

Kristo amekuja na amedhihirishwa kusudi azivunje kazi za Ibilisi. Ibilisi anafanya vita na mwili uli usitii Neema ya Mungu katika Kristo ili kuleta mauti. Kuvunjwa kwa kazi za Ibilisi na Kristo ni kuvunja nia ya Ibilisi.

Nataka kuzungumza na Mtu aliyeacha Wokovu na kugeukia maisha mengine. Na mtu ambaye anapinga wokovu kwa nguvu zote hataki kusikia wala kujua. Mtu ambaye anasema sikuwa ninajua wokovo leo nimepata NURU sema pamoja nami sala hii kwa kumaanisha. Sema

BWANA YESU! NINAKUJA KWAKO MIMI MKOSEFU NIMETENDA DHAMBI. NIMEJUA MIMI MAKOSA YANGU NA KWAMBA NAKUHITAJI WEWE. NAOMBA UNISAMEHE DHAMBI ZANGU NA MAOVU YANGU YOTE. FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU ANDIKA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA. NAKUPOKEA LEO UWE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU! Amina!

JINSI PASAKA INAVYOTIMIA  KWA KILA MKRISTO MMOJA MMOJAUtanguliziPasaka ilianzia katika historia ya kale ya Waisraeli na ...
22/04/2025

JINSI PASAKA INAVYOTIMIA KWA KILA MKRISTO MMOJA MMOJA

Utangulizi
Pasaka ilianzia katika historia ya kale ya Waisraeli na baadaye ikapata maana mpya kwa Wakristo.

1. Pasaka ya Kiyahudi (Asili ya kwanza)
Pasaka ya kwanza ilianzia Misri, wakati Waisraeli walikuwa watumwa. Mungu aliwaamuru kusherehekea Pasaka (kwa Kiebrania: Pesach) k**a kumbukumbu ya kuokolewa kutoka utumwa. Katika Kitabu cha K*toka (K*toka 12):

Mungu alileta mapigo kumi juu ya Wamisri ili kuwaachilia Waisraeli.

Pigo la mwisho lilikuwa kuua wazaliwa wa kwanza wa Wamisri.

Mungu aliwaagiza Waisraeli wachinje mwana-kondoo asiye na doa na wapake damu yake milangoni mwao ili “malaika wa mauti” apite juu yao bila kuwaangamiza – hapa ndipo jina Pasaka linatoka, yaani “kupita juu” (pass over).
Tangu hapo, Pasaka ikawa sikukuu ya kila mwaka kwa Wayahudi.

2. Pasaka ya Kikristo
Kwa Wakristo, Pasaka ina maana mpya:
Yesu alikufa na kufufuka wakati wa Pasaka ya Kiyahudi.

Wakristo tuiona k**a ukombozi wa kiroho – Yesu ni “Mwana-Kondoo wa Mungu” aliyechinjwa kwa ajili ya dhambi za wanadamu.

Pasaka ya Kikristo huadhimisha kifo na ufufuo wa Yesu Kristo, na ndio sikukuu kuu katika imani ya Kikristo.

3.Pasaka ya mtu mmoja mmoja
Hii pasaka hutimia pale mtu mmoja anapookoka na kumkubali Yesu kuwa BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA yake maana yake ametoka katika hali ya utumwa na kuja kwa Yesu

Tuangalie

JINSI PASAKA INAVYOTIMIA AU KUTIMIA KWA KILA MKRISTO MMOJA MMOJA

1. Kupokea wokovu kwa imani
Pasaka inatimia kwa mtu mmoja mmoja wakati mtu anamwamini Yesu Kristo k**a Mwokozi wake binafsi.
Waefeso 2:8
Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

2. Toba ya dhambi na maisha mapya
K**a Waisraeli walivyokombolewa kutoka utumwa wa Misri, Mkristo naye hukombolewa kutoka dhambi, na huanza maisha mapya.

Matendo ya Mitume 3:19
Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

2 Wakorintho 5:17
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

3. Kuweka imani kwa damu ya Kristo k**a kinga ya maisha ya kiroho
K**a Waisraeli walivyopaka damu ya mwana-kondoo, Mkristo hupokea damu ya Yesu k**a kinga dhidi ya hukumu ya kiroho.
Warumi 5:9
Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye.

4. Uhusiano wa karibu na Mungu.
Pasaka humfungulia mtu mlango wa kuingia kwenye agano jipya na Mungu, kupitia Yesu Kristo. Hii huleta maombi, ibada ya kweli, na ushuhuda wa kiroho.

Waebrania 10:19
Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,

5. Tumaini la ufufuo na uzima wa milele.
Ufufuo wa Yesu unampa kila Mkristo tumaini kwamba hata yeye atafufuka na kuishi milele.
Andiko:

Yohana 11:25
Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

Mwl Joshua Mwiketege

[email protected]" rel="ugc" target="_blank">[email protected]
0622662463

UTENDAJI WA TOBA NA BADILIKO LA MWAMINIPART 01Kuna sababu ipo nyuma ya roho chafu inayomtesa mtu. Roho ya ulevi, uzinzi,...
17/04/2025

UTENDAJI WA TOBA NA BADILIKO LA MWAMINI

PART 01

Kuna sababu ipo nyuma ya roho chafu inayomtesa mtu. Roho ya ulevi, uzinzi, wizi, punyeto, chuki, n.k.

Ukisoma Yohana 6:63 imeandikwa 'Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima."

Sasa kuna hiyo roho na nyuma yake kuna nguvu inayoifanya Roho iwe na uwezo wa kumtesa mtu. Nguvu ipo katika mwili.

Biblia inasema katika Warumi 8:7 kuwa "Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii."

Usipoelewa hila ya shetani ni rahisi sana kuteswa na hiyo roho na ikaharibu destiny yako aliyokupangia Mungu. Mwili una hatari sana ya kuzuia ukuaji wa Roho yako. Biblia inasema "Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu."Warumi 8:8

Wakati unashindana na tabia(matokeo) lazima kwanza ushughulike na roho (chanzo) kinachofanya kazi na nguvu (mwili) iliyo nyuma yake.

Ulishawahi kuona mtu ameokoka leo na hapohapo akaacha ulevi na akastawi kutoka hapo. Na mwingine ameokoka lakini baada ya muda akarudia ulevi na uzinzi aliokuwa anaufanya kwa kasi zaidi.

Maagizo ya Torati hayawezi kutimizwa ndani ya mtu asipoyakana mambo ya mwili na kutafuta kuyaishi maisha ya rohoni. Biblia inasema katika Warumi 8:5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.

Lazima mwili ufe kwa habari ya mambo ya mwili na usidhani ni kitu chepesi. Inachukua muda na nidhamu ya hali ya juu. Biblia inaandika hivi katika Wagalatia 5:19-21 "Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, k**a nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu."

Unakufaje katika mwili? Biblia inasema wazi kuwa "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya." 2 Wakorintho 5:17

Wokovu ni Neema anayopata mtu kutoka kwa Mungu ambayo usipoipokea kwa dhati na kujikana ipasavyo huwezi kutoboa. Unaweza kustruggle lakini kitakachoamua ukaaji wako kwenye wokovu ni utayari wako wa kutii. Ipo neema ya kukusaidia lakini inategemea utayari wako.

Umempokea Yesu ndio! Anakaa ndani yako ndio! Ya kale yamepita ndio! Yamekuwa mapya ndio! Lakini je, umejitambua? Unajua thamani ya Neema uliyopokea?K**a ya kale yamepita mbona huyu ameyarudia ya kale.

Tutaendelea na part 02 kesho
.................

10/01/2025

NIMESAMEHEWA DHAMBI ZANGU ZOTE Part 2
Copy and Paste

K*toka Kwa Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church

Waefeso 1:7

[7] Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.

Katika Kristo kwa damu yake tunao msamaha ya dhambi.

Wakolosai 1:13-14

[13] Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

[14] ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

Mwamini hasubiri kusamehewa, ANAO msamaha wa dhambi. Msingi wa msamaha wa dhambi zetu ni dhabihu yake Yesu Kristo au damu yake.

Tazama 1 Yohana 2:1-2

[1] Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na k**a mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,

[2] naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.

Zingatia matumizi ya nyakati hapa…tunaye mwombezi… Neno kipatanisho ni neno la Kigiriki "hilasmos" lenye maana ya sadaka iletayo utakaso. Yesu ni kipatanisho kwa dhambi za wanadamu, Yeye ndiye sadaka iliyotolewa, hata sasa na milele na anabaki kuwa sadaka ambayo kwayo tumepata UTAKASO. Hakuna alichosaza.

Waebrania 8:10-12

[10] Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.

[11] Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.

[12] Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.
Kwenye Agano hili, dhambi na uovu wetu haukumbukwi tena.

Chini ya Sheria, kulikuwa na kumbukumbu la dhambi na sadaka zilizotolewa ni za wanyama. Kwenye Agano jipya, Yesu mwenyewe amejitoa kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu.

Tazama Waebrania 10:3-4

[3] Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.

[4] Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

Dhabihu za mahafali na mbuzi hazijawahi kumsaidia yeyote, lakini Yesu kwa kujitoa kwake kuwa dhabihu kwa ajili yetu amefanya kazi timilifu.

Waebrania 10:10

[10] katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.

Tazama, ni kwa kutolewa mwili ya Yesu Kristo MARA MOJA TU. Si kila mwaka. Yeye si k**a sadaka za Wanyama.

Waebrania 10:11-12

[11] Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.

[12] Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;

Yesu hasimami KILA SIKU akifanya ibada, mara moja ALIMALIZA. Ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Kazi yake ameimaliza. KWA DHABIHU MOJA IDUMUYO HATA MILELE AMEWAKAMILISHA HAO WANAOTAKASWA. AMETUKAMILISHA.

Tazama utofauti uliopo kati ya dhabihu ya Yesu na dhabihu za Wanyama.

Waebrania 9:13-14 inandika

[13] Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili;

[14] basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?

Tazama maneno haya KWA ROHO WA MILELE…SADAKA ISIYO NA MAWAA…ITAWASAFISHA DHAMIRA ZENU. Huu ndio urefu na kimo ambacho dhabihu hii hutenda.Dhambi huondolewa au husamehewa kwa imani katika dhabihu ya Yesu Kristo. Mungu hana kumbukumbu la dhambi na uovu kwenye Agano la Kristo. Hivyo, mwamini amekamilishwa milele na imefanyika hivyo mara moja.

Msamaha wa dhambi hivyo ni zawadi. Hii haina vigezo na masharti. Msamaha wa dhambi pia sio jambo ambalo Mungu atafanya, ni jambo ambalo Mungu ameshafanya ndani ya Kristo. Mungu haendi kumsamehe mtu kesho au baadae. Kristo – sadaka toshelevu amekwishatolewa, mtu anahitaji kuamini tu na kupokea msamaha wa dhambi.

Zingatia nyakati Paulo anazotumia akizungumzia msamaha wa dhambi kwa waamini hapa;

Waefeso 4:32 [32] tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane k**a na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
MKASAMEHEANE K**A NA MUNGU KATIKA KRISTO ALIVYOWASAMEHE NINYI.

Tena, Warumi 4:7 [7] Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao.
MAKOSA YAMESAMEHEWA, DHAMBI ZIMESITIRIWA. Heri hapa ni kubarikiwa. Wamekwishabarikiwa.

Wakolosai 1:13-14 inaandika

[13] Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

[14] ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

MUNGU AMETUOKOA KATIKA NGUVU ZA GIZA…AMETUHAMISHA KUJA KWENYE UFALME WAKE…TUNAO UKOMBOZI NDANI YAKE YAANI MSAMAHA WA DHAMBI.

Wakolosai 2:13

[13] Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;
AMETUFANYA HAI PAMOJA NAYE, AKIISHA KUTUSAMEHE MAKOSA YOTE.

Wakolosai 3:13 [13] mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; k**a Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
BWANA AMETUSAMEHE, VIVYO NASI TUNAWASAMEHE WENGINE.

1 Yohana 2:12 [12] Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake.ANAWAANDIKIA WAJUE KUWA WAMESAMEHEWA DHAMBI ZAO, KWA AJILI YA JINA LAKE YESU.

Isaya nabii ameweka wazi hili pia…Isaya 43:25 [25] Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako. MUNGU HUFUTA MAKOSA KWA AJILI YAKE MWENYEWE.

Hivyo, msamaha wa dhambi sio jambo la mtu kuomba asamehewe. Asiyeamini anapaswa kupokea msamaha kwa imani na mwamini anapaswa kuwa na uhakika kuwa amesamehewa; dhambi hazitawekwa juu yake kamwe. Mwamini anao (anamiliki) msamaha wa dhambi. Uzuri zaidi ni kwamba; waamini hatujasamehewa tu dhambi bali pia tumeokolewa katika dhamiri ya kujiona wenye dhambi kila wakati. Dhabihu za Wanyama ziliwafanya waendelee kujiona wenye dhambi lakini dhabihu ya Yesu imetuweka huru na dhambi na dhamira ya dhambi. HALELUYA!

Hivyo, MWAMINI ANAO MSAMAHA WA DHAMBI.

Apostle Shemeji Melayeki
Global Family Gatherings
“God’s Standards”

MATOKEO MAKUBWA SASACopy and Paste kutoka kwa Pastor Carlos Ricky Wilson Kirimbai Hii kitu inawagharimu sana watu wengi....
09/01/2025

MATOKEO MAKUBWA SASA

Copy and Paste kutoka kwa Pastor Carlos Ricky Wilson Kirimbai

Hii kitu inawagharimu sana watu wengi.

Wanapenda kuona matokeo ya ghafla pasipo kulipa gharama.

Ndiyo maana wanadanganyika kirahisi.

Anadhani anaweza kwenda kwenye ibada, au semina au kongamano akapokea matamshi ya mtumishi, akaombewa, akatoa sadaka yake alafu akaona badiliko immediately.

Mungu hayupo hivyo.

Mafanikio na ustawi hutaka kanuni.

Kanuni zinataka uvumilivu na saburi sio vitu vya vu bin ghafla.

Ndiyo maana tunakutana na maandiko k**a haya yafuatayo katika bibilia:

Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. (Gal 6:9 SUV).

K**a maandiko yanasema habari ya kutokuchoka katika kutenda mema basi uwe na uhakika hapa hapazungumziwi habari ya matokeo makubwa sasa bali ni kuinuka hatua kwa hatua k**a matokeo ya kutenda mema na sio kuombewa au kutamkiwa.

Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho; ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu. (Ebr 6:11‭-‬12 SUV).

K**a maandiko yanazungumzia kuhusu bidii na kuwa na uvumilivu wa matumaini mpaka mwisho uwe na uhakika hamna kitu k**a MATOKEO MAKUBWA SASA ila utatakiwa kuwa na bidii katika kufanya kilicho sahihi pasipo kuchoka mpaka uyaone matokeo.

Imani haitoshi lazima kuwe na uvumilivu na ukishaona neno uvumilivu jua tu hamna kitu k**a matokeo makubwa sasa.

Huwezi ombewa na kutamkiwa alafu hufanyi bidii, sio mvumilivu alafu uje uonage matokeo.

UTAENDELEA KUIBIWA TU.

SADAKA SIO KIZALISHA MATOKEO BALI NI SHUKURANI YAKO KWA MUNGU KWA SABABU YA MATOKEO.

KANUNI NDO KIZALISHA MATOKEO.

Basi Yeye atufanyaye imara pamoja nanyi katika Kristo, na kututia mafuta, ni Mungu, (2 Kor 1:21 SUV).

Kufanywa imara sio kitu cha kuombewa na kutamkiwa ndugu yangu ni kitu ambacho kinataka hatua yako binafsi katika kutenda kilicho sahihi tena kwa muda mrefu pasipo kuacha ndipo unafanywa imara alafu mafuta ya Mungu yanakuja juu yako kukuwezesha kufanikiwa na kustawi.

Unakwepa kufanya vitu vya kukuimarisha unahangaika tu na mambo ya kutamkiwa na kuombewa alafu unadanganywa ukitoa sadaka mambo yatakuwa sawa.

HAMNA KITU K**A HICHO NDUGU YANGU.

Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu.
2 Fal 19:30 SUV

Unatakaje kuzaa matunda katika maisha yako pasipo kwanza kudhibitika kwa kutia mizizi chini na je jambo la kutia mizizi chini unafikiri ni jambo la kuombewa na kutamkiwa na kulitolea sadaka?

Hii inataka bidii na jitihada zako binafsi.

Hiiiviiiii!!!

Unaweza ukaenda kuombewa na kutamkiwa na kutoa sadaka ili mwili wako uimarike kwa misuli kuwa imara pasipo kuchukua hatua ya kufanya mazoezi kwa nidhamu mtu wa Mungu?

Unaamini kabisa ukienda mahali ukawa unapiga kelele "NAPOKEA (I RECIEVE), NAJIUNGAMANISHA (I CONNECT), NAAMINI (I BELIEVE) basi mambo yatabadilika?

UTANEDELEA KUIBIWA NDUGU YANGU.

Mtu wa pekee ambaye alipataga mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu alikuwa Mariamu mama Yake Yesu.

Wengine wote wakiahidiwa watoto ilibidi wawajibike na wenzi wao kwa kukutana kimwili kwenye tendo la ndoa ndipo Mungu akawapa watoto.

HAKUNA KITU K**A BARAKA ZAKUOMBEWA NA KUTAMKIWA.

Fanya kazi na Mungu atabariki kazi za mikono yako na sio vu bin ghafla, utalipa gharama ya uvumilivu na kutenda mema pasipo kuchoka.

Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. (Ebr 10:36 SUV).

Yapo mapenzi ya Mungu ya kuyafanya tena kwa saburi ambayo ndo yatakuleta kwenye uhalisia wa ahadi za Mungu katika maisha yako.

ACHA KUENDELEA KUDANGANYWA NA KUIBIWA.

Unaishi kiholela alafu uwende tu kwenye kongamano, semina, mkutano utamkiwe, uombewe ujisemee I RECIEVE, I CONNECT alafu eti mambo yabadilike pasipo kubadilisha namna unavyoenenda na kuishi?

SAHAU.

KUNA CHA KUFANYA ILI UFANIKIWE NA KUSTAWI NA SIO CHA KUSEMA.

IMANI INADAI MATENDO ILI IZAE MATUNDA SIO KUTAMKA TAMKA TU PASIPO KUFANYA KILICHO SAHIHI ALAFU UONE MAFANIKIO NA USTAWI.

Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia. (Lk 8:15 SUV).

Neno la Mungu unalosikia linadai hatua.

Lipokee kwanza alafu chukua hatua tena kwa uvumilivu ndipo utaona matokeo.

Hata Mariamu baada ya kupokea Neno la malaika alisubiri miezi tisa kabla mtoto Yesu hajazaliwa.

MUNGU NI MTENDA MIUJIZA SIO MFANYA MAZINGAOMBWE.

Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao. Nami nitapeleka mavu mbele yako, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako. Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua. Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, hata utakapoongezeka wewe, na kuirithi hiyo nchi. (K*t 23:27‭-‬30 SUV).

Ndiyo Mungu ameahidi kushughulika na adui zako, changamoto zako, matatizo yako na shida zako ila sio mara moja na sio pasipo kukuhusisha wewe.

Hatawaondoa mara moja au katika mwaka moja bali kidogo kidogo kwa kadiri wewe unavyoongezeka

ACHA UKRISTO WA MAZINGAOMBWE KUWA MKRISTO WA BIBILIA, MKRISTO WA KANUNI.

ASOMAYE AFAHAMU.

NIMESAMEHEWA DHAMBI ZANGU ZOTE Part 1 Copy & Paste Chukua Hii K*toka Kwa Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gather...
08/01/2025

NIMESAMEHEWA DHAMBI ZANGU ZOTE Part 1
Copy & Paste

Chukua Hii K*toka Kwa Apostle Shemeji Melayeki - Global Family Gatherings Church

Malaika alimtokea Yusufu na kumwambia…

Mathayo 1:20-21
[20] Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

[21] Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake YESU, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao
Tazama Luka 24:44-49
[44] Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.

[45] Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.

[46] Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

[47] na kwamba mataifa yote WATAHUBIRIWA kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.

[48] Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

[49] Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.

Ujumbe wa Injili unaweza kuelezwa k**a AHADI KWENYE VITABU VYA AGANO LA KALE AMBAYO KRISTO ATAKUJA NA KUITIMIZA KWA KUPATA MATESO, KUFA NA KUFUFUKA KWAKE NA KWA SABABU HIYO TOBA NA MSAMAHA WA DHAMBI KUHUBIRIWA. Hii ndio sababu Injili inahubiriwa.

Je, toba ni nini?

Toba ni neno la Kigiriki metanoia lenye maana badiliko la fikra na mwelekeo na hii hutokea zaidi baada ya kusikia ujumbe. Hebu tutazame namna neno hili metanoia lilivyotumika katika Biblia. Mzizi wa neno metanoia ni metanoeō lenye maana ya kufikiri tofauti baadae.

Marko 1:15 [15] akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili. "…tubuni na kuiamini Injili". Maana yake Kubadili fikra kwa kuiamini Injili.

Mathayo 12:41
[41] Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.
…kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; walibadilika katika fikra zao, walisadiki ujumbe wake.

KUTUBU NI KUPOKEA UJUMBE.
Neno kutubu limekuwa likitumika kwa umaarufu katika jamii yetu k**a KUOMBA MSAMAHA BAADA YA KUFANYA KOSA. Maana ya Biblia ya kutubu sio hii kabisa. K*tubu sio matokeo ya kukosea kwa mtu bali ujumbe aliosikia (Injili).

Baada ya mahubiri marefu ya Petro kwenye Matendo 2, anawaagiza wasikilizaji wake kutubu.

Matendo 2:37-38

[37] Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

[38] Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Wakamwambia Petro, tutendeje ndugu zetu? Tubuni mpate ondoleo la dhambi zenu.

Hapa tena baada ya kuhubiri;

Matendo 3:19
[19] Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;
Tubuni ili dhambi zenu zifutwe.

Matendo 5:31
[31] Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

Matendo 10:43
[43] Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.Hapa Petro ametumia maneno KILA AMWAMINIYE ambapo ni sawa na kusema TUBUNI.

Kwa muktadha huu KUTUBU ni kile kinachotokea baada ya mtu kusikia Injili yaani habari za kufa na kufufuka kwa Yesu. Matokeo ya badiliko hili la nia ni kupokea MSAMAHA WA DHAMBI.

Hii ni kwa imani (kwa kuamini Injili).
Msamaha wa dhambi au ondoleo la dhambi ni neno moja la Kigiriki APHESIS ambalo linamzizi kutoka kwenye neno APHIEMI…lenye maana ya (English) -- release from the bo***ge or imprisonment, pardon of sins (letting them go as if they had never been commited), remission of the penalty.

[Kiswahili chake] kuachiliwa au kuondolewa kifungoni, kusamehe au kuziachilia dhambi kana kwamba hayajawahi kufanyika.Huu ndio ubora wa dhabihu ya Yesu Kristo. Hivi ndivyo Mungu anafanya kwa mwamini. Dhambi zake zimeondolewa, zimefutwa.

Maneno yote mawili, MSAMAHA WA DHAMBI na ONDOLEO LA DHAMBI yametafsiriwa kutoka kwenye neno hili moja la Kigiriki APHESIS.

Matendo ya Mitume 5:29-31

[29] Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.

[30] Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti.

[31] Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

Anawataka pia watubu (waamini) katika kufa na kufufuka kwake ili wapokee Msamaha wa dhambi.

Nyuma kwenye sura ya 2, Petro alihubiri vivyo hivyo;

Matendo ya Mitume 2:38

[38] Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Tubuni mpate ondoleo la dhambi zenu. Neno la Kigiriki la ondoleo la dhambi na Msamaha wa dhambi ni moja APHESIS.

Matendo ya Mitume 10:42-43

[42] Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na wafu.

[43] Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi.

Kwenye nyumba ya Kornelio pia alihubiri habari za kufa na kufufuka kwake Yesu hivyo kupata ondoleo la dhambi kwa kila aaminiye.

Matendo ya Mitume 13:37-39

[37] Bali huyu aliyefufuliwa na Mungu hakuona uharibifu.

[38] Basi, na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo mnahubiriwa msamaha wa dhambi;

[39] na kwa yeye kila amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa.

Matendo ya Mitume 26:13-18

[13] Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote.

[14] Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.

[15] Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.

[16] Lakini inuka, usimame kwa miguu yako, maana nimekutokea kwa sababu hii, nikuweke wewe uwe mtumishi na shahidi wa mambo haya uliyoyaona, na wa mambo ambayo katika hayo nitajidhihirisha kwako;

[17] nikikuokoa na watu wako, na watu wa Mataifa, ambao nakutuma kwao;

[18] uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.

Tazama mkazo wa huduma yake…awafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache nguvu za giza na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi (YESU).

Mtume Paulo alijua namna ya kuzishinda nguvu za giza (za shetani); ni kwa kuhubiri Injili inayotoa msamaha wa dhambi kwa imani katika Kristo.Paulo hapa tena, Matendo ya Mitume 26:22-23

[22] Basi kwa kuwa nimeupata msaada utokao kwa Mungu nimesimama hata leo hivi nikiwashuhudia wadogo kwa wakubwa, wala sisemi neno ila yale ambayo manabii na Musa waliyasema, kwamba yatakuwa;

[23] ya kwamba Kristo hana budi kuteswa na ya kwamba yeye kwanza kwa kufufuliwa katika wafu atatangaza habari za nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.

Paulo alibaki katika kiini cha ujumbe wa manabii na Musa, habari za kufa na kufufuka kwa Yesu na watu kupokea Nuru (msamaha wa dhambi au kuhesabiwa haki).

Itaendelea….

Apostle Shemeji Melayeki
Global Family Gatherings
“God’s Standards”

Address

Kimara
Dar Es Salaam
00000

Telephone

+255768004412

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Upendo wa Yesu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Upendo wa Yesu:

Share