Polycarp - The Bibliophile

Polycarp - The Bibliophile PASO CORTO, VISTA LAGA

07/03/2026

Video ya kwanza imeonekana ikionyesha Marekani ikirusha kwa mara ya kwanza kombora lake jipya la Precision Strike Missile.

Video hiyo inaonyesha mfumo wa roketi wa M142 HIMARS uliopo nchini Bahrain ukirusha kombora la PrSM kuelekea maeneo yaliyopo Iran, kuvuka Persian Gulf.

Mfumo huu wa silaha ni kombora la kisasa la kizazi kipya la ardhini-kwa-ardhini (surface-to-surface ballistic missile) lililoundwa kuchukua nafasi ya mfumo wa zamani wa ATACMS.

Kombora hili lina uwezo wa kufika umbali wa zaidi ya kilomita 500 (ikilinganishwa na takribani kilomita 300 za mfumo wa zamani wa ATACMS zinazotumiwa na HIMARS), huku matoleo yajayo yakipangwa kufikia hadi kilomita 1000.

Kichwa cha kombora (payload) kina takribani uzito wa kilo 91 za vilipuzi vinavyogawanyika vipande vipande (high-explosive fragmentation unitary warhead).

07/03/2026

Rubani wa Jeshi la Anga la Israel alirekodi ujumbe huu akiwa angani juu ya Iran akisema:

“Tunaendelea kupigana k**a inavyohitajika, mchana na usiku bila kupumzika, na tunahisi msaada wenu wakati wote, Tunawatakia ninyi, wananchi wa Israel, Sabato salama na yenye utulivu.”

Sabato/Shabbat ni siku takatifu ya mapumziko kwa Wayahudi inayoadhimishwa kuanzia Ijumaa jioni hadi Jumamosi jioni.

Cc: Yeshiva World News

🚨 Kikosi cha meli za kivita kinachoongozwa na manowari ya kubeba ndege USS George H.W. Bush (CVN‑77) kinaelekea katika B...
07/03/2026

🚨 Kikosi cha meli za kivita kinachoongozwa na manowari ya kubeba ndege USS George H.W. Bush (CVN‑77) kinaelekea katika Bahari ya Mediterranean Sea.

Hii ni manowari ya tatu kubwa ya Marekani (supercarrier) kupelekwa katika eneo hilo, ikiwa ni sehemu ya nguvu kubwa ya kijeshi inayolenga kukabiliana na utawala wa Iran.

“Watu wanapozungumza, dunia inapaswa kusikiliza! Uhuru haupaswi kunyamazishwa! Waungeni mkono wananchi wa Iran!”Ndivyo u...
06/03/2026

“Watu wanapozungumza, dunia inapaswa kusikiliza! Uhuru haupaswi kunyamazishwa! Waungeni mkono wananchi wa Iran!”

Ndivyo ulivyo ujumbe uliokuwa umeandikwa kwenye bango la matangazo lililoonekana mjini Paris, nchini France, likitoa ujumbe wa kuunga mkono wanawake wa Iran.

“Sisi hapa tuko huru! Watu huko Iran hawako huru!”Ndivyo ilivyoandikwa kwenye bango la matangazo lililoonekana katika mj...
06/03/2026

“Sisi hapa tuko huru! Watu huko Iran hawako huru!”

Ndivyo ilivyoandikwa kwenye bango la matangazo lililoonekana katika mji wa Rome, nchini Italy.

Donald Trump amesema:“Tunaendelea kuwahamisha maelfu ya watu kutoka nchi mbalimbali za Mashariki ya Kati. Operesheni hii...
06/03/2026

Donald Trump amesema:

“Tunaendelea kuwahamisha maelfu ya watu kutoka nchi mbalimbali za Mashariki ya Kati. Operesheni hii inafanyika kimya kimya lakini kwa utaratibu mzuri bila matatizo. Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, chini ya Waziri Marco Rubio, inafanya kazi nzuri sana.”

06/03/2026

Jeshi la Israel (IDF) limechapisha mchoro unaoonyesha Handaki chini ya ardhi katika ofisi ya Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei,

Bunker hiyo iliyokuwa chini ya majengo ya uongozi wa Iran, ambayo iliharibiwa katika shambulizi la anga la IDF.

06/03/2026

🚨 Taliban wameshambulia kituo cha Jeshi la Pakistan kilichopo mpakani kwa kutumia kombora la kisasa linaloongozwa (self propelled guided missile), silaha ambayo hutumika mara chache katika mashambulizi ya aina hiyo.

06/03/2026

Ukraine imefanikiwa kuwarejesha watu 200 kutoka kifungoni Russia jana, na wengine 300 leo.

Miongoni mwa walioachiwa huru wapo wanajeshi wa Vikosi vya Ulinzi vya Ukraine, walinzi wa National Guard of Ukraine, pamoja na maafisa wa State Border Guard Service of Ukraine.

Wengi wao walikuwa wamezuiliwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, huku baadhi wakiwa kifungoni tangu mwaka 2022.

Raia wawili pia ni miongoni mwa walioachiliwa huru.

Chanzo:

Address

5529
Dar Es Salaam
14107

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Polycarp - The Bibliophile posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Polycarp - The Bibliophile:

Share