Bishop Sunbella Kyando

Bishop Sunbella Kyando Karibu Tujifunze kwa pamoja Mambo ambayo Roho Mtakatifu kwa Neema yake anapenda Tujifunze kwa pamoja.

29/05/2026

Unachovaa kinabeba utambulisho wako, kabla hujavaa aina hiyo ya mavazi jiulize kwanza..."wewe ungekutana na mtu kavaa k**a hivyo unavyotaka kuvaa ungemuona ni mtu wa aina gani?"
Maana hivyo ndivyo pia hata watu wengine watakavyokuona.

Kuna msemo mzuri sana ambao huwa naupenda sana, unasema;
"Dress as you desire to be addressed"...watu hawana X-Ray ya kuangalia tabia, hata k**a una tabia nzuri vipi, mavazi yako yanaweza kukufanya ukaonekana una tabia zisizofaa.

25/05/2026

Ni muhimu sana kufahamu vitu hivi vitatu wakati wowote ambapo unapitia kukwama...

21/05/2026

Kila mtu aliye duniani ana hatma ambayo Mungu amemuumbia, kuna wanaojua kusudi lao na kuna wasiojua bado. Na kitu shetani anafanya ni kuhakikisha anawatoa watu kwenye kusudi lao maana nje ya kusudi la Mungu hakuna mafanikio

04/05/2026

Tembea na maombi haya mwezi huu wa tano, na kila kilichotamkwa hapa kikawe halisi kwako kwa Jina la Yesu Kristo!
Kwa pamoja tuseme Amen.

Mtag mtu ambaye unatamani maombi haya yamfikie pia.

29/04/2026

Kuna umuhimu mkubwa sana katika kupambanua roho, sio kila sauti au maono yametoka kwa Mungu..ukiwa kila unachokiona au kusikia unakichukua basi ni rahisi sana kuingia kwenye mtego wa shetani.
Hata maandiko yanasema kuwa msiziamini kila roho, pimeni.

26/04/2026

Kuna vitu muhimu vitatu vya kuvifahamu na kuweza kuvitofautisha ili uweze kutoka kwenye hilo unalopitia.
Na hii sio kwa waamini peke yake, hata Watumishi wa Mungu pia wanatakiwa kuvijua hivi maana ukishindwa kuvitofautisha basi ni ngumu sana kupata yale matokeo yaliyotarajiwa.

20/04/2026

Hakuna aliyepewa kufanya kazi ya Mungu yote, kila mtu kapewa kwa sehemu, na kwa sehemu hizo watu wote tunahusika katika kuujenga mwili wa Kristo.

Kwa ufupi watu wote tunategemeana, ulichopewa wewe sicho alichopewa mwingine na alichopewa mwingine sicho ulichopewa wewe. Jifunze kuheshimu huduma aliyopewa mwingine na wakati huohuo ukiwa unatimiza huduma yako.

18/04/2026

Ulishawahi kujiuliza kwanini unatumia nguvu kubwa sana kufanya vitu lakini huoni matokeo? Au unayaona kwa udogo sana ukilinganisha na nguvu uliyowekeza?
Unaishi maisha yanayojirudia na hujui chanzo ni nini? Unapoteza kazi kwa namna ileile, mahusiano yako yanakufa kwa style ileile? nk

Hakikisha Jumapili hii hukosi hii ibada maana tutakuwa na muendelezo wa somo zuri sana ambalo tulianza nalo wiki iliyopita. Kupitia somo hili Mungu kupitia Mtumishi Wake Bishop Sunbella Kyando ataenda kukufunulia chanzo cha yote na kukupa namna ya kutoka.

Usipange kukosa na Mungu akubariki sana.




Hakuna aliyewahi kumu_encounter Mungu na akabaki k**a alivyo, hakuna ambaye alipokea Neno la Mungu na lisifanye mabadili...
15/04/2026

Hakuna aliyewahi kumu_encounter Mungu na akabaki k**a alivyo, hakuna ambaye alipokea Neno la Mungu na lisifanye mabadiliko kwenye maisha yake.

Tukutane leo hii kupitia ukurasa wa YouTube wenye jina BISHOP SUNBELLA KYANDO kuanzia saa tatu kamili usiku kwa ajili ya somo litakalobadilisha maisha yako na kukutoa kwenye vifungo vinavyokushikilia. Tutajifunza somo zuri sana linaloitwa "Wakati wa kufunguliwa kwako"

Usikose kushiriki ibada hii na Mungu akubariki sana.

17/09/2025

Matendo ya Mitume 17:10 l

Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.

11.Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.

12.Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.

Address

Sinza Mori
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bishop Sunbella Kyando posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Bishop Sunbella Kyando:

Share