21/04/2022
DHARAHU AIBU ILIYO MBELE YAKO, KWA AJILI YA FURAHA KUU ILIYOWEKWA MBELE YAKO!
WAEBRANIA 12:2
Tukimtazama Yesu, mwenyewe kuianzisha na kuitimiza Imani yetu, ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake, aliustahimili msalabani na kuidharahu aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti chaenzi cha Mungu.
HALLELUJAH! HALLELUJAH!
Watu wengi wameshindwa kuifikia furaha kuu iliyowekwa mbele yao kwa sababu ya kuogopa aibu.
Wanashindwa kuanzisha Jambo fulani, wanajisemea wenyewe, nitaonekanaje mbele za watu!
Sikiliza mpendwa wangu! Bwana Yesu, alikuwa anakabiliwa na Mambo makubwa ya aibu! K**a kuvuliwa nguo na kuwa uchi mbele ya mama yake, na ndugu zake, na watu wote waliokuwa wamemzunguka.
Lakini pamoja na kwamba aibu ilikuwa imemsonga, aliiangalia ile Furaha iliyokuwa mbele yake, hivyo akaona ile aibu si kitu mbele ya ile Furaha iliyo wekwa mbele yake.
Bwana Yesu hakuendelea kuiangalia ile aibu, bali jicho lake lilikuwa linaitazama Ile furaha itakayo kuja baada ya kuaibishwa.
Mpendwa wangu, usiiangalie aibu unayopitia, bali, angalia ile furaha iliyowekwa mbele yako.
✍️ Pokea neema hii ya kuidharahu aibu katika jina la Yesu Kristo.
✍️ Ninakuombea Neema ya kusonga mbele pasipo kuangalia hiyo aibu, katika jina la Yesu Kristo.
✍️ Pokea Neema ya kuifikia Ile furaha kuu iliyowekwa mbele yako, katika jina la Yesu Kristo.
Chukua hatua, anza kutimiza hayo maono uliyo nayo, pasipo kuangalia utaonekanaje mbele ya watu,maana mbele kuna utukufu wakooo🙏
Mungu akubariki Sana wewe uliyesoma ujumbe huu mpaka mwisho! Mungu akujibu sawasawa na uhutaji wako. Amen!