31/05/2026
Maonyesho ya Biashara katika BUSINESS GALA REVIVAL
Ilikuwa ni zaidi ya maonesho ya bidhaa na huduma. Mtumishi wa Mungu alipata nafasi ya kutembelea meza moja baada ya nyingine, akitoa ushauri wa kitaalamu, maelekezo ya kimkakati na maombi kwa kila biashara.
Tulijifunza kuwa biashara haihitaji mtaji pekee, bali pia inahitaji hekima, maono na uongozi wa Mungu ili ikue na kustawi. Kila meza iliguswa na neno, maombi na maelekezo yaliyoleta matumaini mapya kwa wajasiriamali.
Tunaamini mbegu zilizopandwa katika BUSINESS GALA REVIVAL zitazaa matunda makubwa katika biashara zetu na kuleta ushuhuda wa ukuu wa Mungu.