Efatha Church Yerusalem

Efatha Church Yerusalem WE BRING THE WORLD TO JESUS

Matukio katika picha IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE
18/08/2024

Matukio katika picha

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

SOMO; MaamuziHauwezi kufika mahali popote bila ya kuwa na maamuzi, sababu ni Muhimu sana katika maisha ya mwamini..Maamu...
18/08/2024

SOMO; Maamuzi

Hauwezi kufika mahali popote bila ya kuwa na maamuzi, sababu ni Muhimu sana katika maisha ya mwamini..Maamuzi ya mtu yapo katika AKILI na MOYO hivyo tunazungumzia NAFSI na ndani yake ndipo kulipo kuzingatia

Mwamini akili Yako unatakiwa kuilisha Neno la Mungu na si vinginevyo ili uweze kufanya maamuzi yaliyo sahihi

Nini umeweka Moyoni mwako hicho ndicho kinachokufanya uamue nini,Vile unavyosikia ndivyo inakufikisha katika ukuu wako.

Mda mwengine ukiona mambo Yako hayaendi Rudi iulize akili yako na ipeleke taarifa kwenye moyo wako ili uweze kufanya maamuzi yaliyo sahihi juu ya jambo fulani

Ili uwe na maamuzi sahihi lazima uwe na uponyaji wa NAFSI, Hatufiki hapa tunapotakiwa kufika kwa urahisi kuna changamoto nyingi.

Wafilipi 4;8 "Hatimaye,ndugu zangu,mambo yo yote yaliyo ya kweli,yo yote yaliyo ya staha,yo yote yaliyo ya haki,yo yote yaliyo safi,yo yote yenye kupendeza yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote,ikiwapo sifa nzuri yo yote,yayafakarini hayo."

Maamuzi yamebeba kushinda au kushindwa (mabadiriko) kwa mtu.

Mwanzo 11;6 " BWANA akasema ,Tazama, watu Hawa ni taifa Moja, na lugha Yao ni Moja na haya ndio wanayoanza kuyafanya ,Wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya"

K**a tukifika sehemu ya kuamua chochote hakuna kitu kitakachokuzuilia, kuokoka MUNGU Alikuamulia ili kutembea katika wokovu ni wewe mwenyewe

Ayubu 22;28 "Nawe utakusudia Neno,nalo litathibitika kwako, Na mwanga utazitimiliza nadhiri zako"

Mwanzo 4;7 "K**a ukitenda vyema ,hautapata kibali.? Usipotenda vyema dhambi Iko,inakuotea mlangoni,nayo inakutamani wewe,lakini yapasa uishinde"

1 Wafalme 11;38 " Tena utakuwa,ukiyasikia yote nitakayokuamuru, na kuenenda katika njia zangu ,na kutenda yaliyo mema machoni pangu,ili kuzishika amri zangu na hukumu zangu k**a Daudi mtumishi wangu alivyotenda, basi, nitakuwa pamoja nawe, nitakujengea nyumba iliyo imara ,k**a nilivyomjengea Daudi ,nami nitakupa wewe Israel"

©Mtumishi; EINHARD NDOMBA

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

IBADA YA MATOLEO KATIBU; SABASTIAN MRAYMatendo ya mitume 5;11 " Lakini mtu Mmoja Anania,pamoja na Safira mkewe aliuza Ma...
18/08/2024

IBADA YA MATOLEO
KATIBU; SABASTIAN MRAY

Matendo ya mitume 5;11 " Lakini mtu Mmoja Anania,pamoja na Safira mkewe aliuza Mali.
Akazuia kwa Siri sehemu ya thamani yake,Mkewe naye akijua haya,akaleta fungu Moja akaliweka miguuni pa mitume..."

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

USHUHUDA Anaitwa SESILIA PIUS  yupo hapa kumshukuru MUNGU Kwa kumlinda dhidi ya ajali ya moto nyumbani kwake mwishoni mw...
18/08/2024

USHUHUDA

Anaitwa SESILIA PIUS yupo hapa kumshukuru MUNGU Kwa kumlinda dhidi ya ajali ya moto nyumbani kwake mwishoni mwa wiki hii. Alivyokuwa nyumbani anaandaa chakula kwa ajili ya familia gesi ilileta changamoto kwenye uzimaji wake had kuzua taharuki ndani ya nyumba sababu hofu tayar ilikuwa imeshatanda ila kwa kuwa anae Mungu wa efatha na k**a neno lisemavyo kupitia mpaka mafuta wa BWANA hatutakufa kwa ajali na atatulinda na mabaya yote pamoja na ajali zote juu yetu ndipo akafanya njia pasipo na njia na kumuepusha na ajali ya moto wa gesi na jiko lile likazima pasipo leta madhara yeyote ndani ya nyumba

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

Shuhuda na Mtumishi; Theonestina Deus Zaburi 9;1-2 "Nitashukuru BWANA kwa moyo wangu wote,Nitayasimulia matendo Yako yot...
18/08/2024

Shuhuda na Mtumishi; Theonestina Deus
Zaburi 9;1-2 "Nitashukuru BWANA kwa moyo wangu wote,Nitayasimulia matendo Yako yote ya ajabu.
Nitafurahi na kukishangilia wewe; Nitaliimbia Jina lako wewe uliye juu"

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

UFUNGUZI WA IBADA MTUMISHI; DANIEL JOHNTenzi ni 40 (Nasikia kuitwa)IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSAL...
18/08/2024

UFUNGUZI WA IBADA
MTUMISHI; DANIEL JOHN
Tenzi ni 40 (Nasikia kuitwa)

IBADA YA JUMAPILI 18/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

Matukio katika picha IBADA YA JUMAPILI 11/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE
11/08/2024

Matukio katika picha

IBADA YA JUMAPILI 11/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

Matukio katika picha MCHUNGAJI AESTERIA NDOMBA akiwahudumia Wana wa Mungu katika Ibada IBADA YA JUMAPILI 11/08/2024 KANI...
11/08/2024

Matukio katika picha MCHUNGAJI AESTERIA NDOMBA akiwahudumia Wana wa Mungu katika Ibada

IBADA YA JUMAPILI 11/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

ShuhudaNaitwa Tesituta namshukuru Mungu kwa ajili ya mkesha wa viongozi siku ya jumatano, kesho yake siku ya alhamisi ni...
11/08/2024

Shuhuda
Naitwa Tesituta namshukuru Mungu kwa ajili ya mkesha wa viongozi siku ya jumatano, kesho yake siku ya alhamisi nilikuwa na mwaliko kwenda kwenye sherehe ila siku Ile nilijivuta sana na kuchelewa kutoka nyumbani, kumbe, Palikuwa na sababu Mungu ameiweka Mimi kuchelewa . Wakati natoka nje niliona watu wengi walikuwa wametahaluki huku wakiwa wamebeba mtoto,kuwaauliza kuhusu mtoto alikuwa amepata ajali katika michezo Yao na amekauka na kupoteza fahamu mpaka familia yake kujua ya kwamba ameshapoteza uhai.Kupitia Ibada ya mkesha nilitoka na nguvu ya MUNGU nikamsihi anifanye k**a chombo chake kurejesha afya kwa mtoto yule. Basi nilipoweka mikono yangu juu ya mtoto yule alipata fahamu na kuweza kunyanyuka

IBADA YA JUMAPILI 11/08/2024 KANISA LA EFATHA YERUSALEM-MAJOHE

Shuhuda;Halleluya naitwa Aloyce Valonge, Namrudishia Mungu sifa na utukufu kwa ajili ya shamba langu,Mimi ni mkulima na ...
11/08/2024

Shuhuda;
Halleluya naitwa Aloyce Valonge, Namrudishia Mungu sifa na utukufu kwa ajili ya shamba langu,Mimi ni mkulima na mahali shamba langu lilipo lipo karibu na wanyama pori yaani tembo kupita na kula mazao ni jambo la kawaida. Ila kupitia dhabihu (sadaka) ninazomtolea Bwana pamoja na fungu la kumi nilimsihi Mungu anilindie mazao yangu dhidi ya tembo, Hivyo shamba langu liko salama na tembo wakipita kwangu wanapita na kwenda kula mazao kwenye mashamba mengine na kwangu kubakia salama, Hali hii hupelekea wakulima wenzangu kushangaa na kuniomba niwape Siri ya yote haya nam kubakia kuwaambia si kwa uwezo wangu ila Siri ya yote haya ni Yesu tu sababu Tembo hawawezi kula mazao yangu kwa kuwa wao sio waliopanda .

Address

Majohe
Dar Es Salaam

Telephone

+255652153160

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Yerusalem posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share