Friends On Friday-FoF

Friends On Friday-FoF Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Friends On Friday-FoF, Dar-es-Salaam, Arusha, Dodoma, Tanzania nzima tutafika, Dar es Salaam.

Friends on Friday is the Christian Business Networking event held on every first Friday of the month where various professionals meet for dinner, live Christian music, comedy, talks(presentations or exclusive interviews).

Yule asikiaye Kiu aje anywe.....Kuna KIU ya maendeleo, Kuna KIU ya mafanikio, Kuna KIU kufaulu masomo, Kuna KIU ya Kuoa ...
22/05/2015

Yule asikiaye Kiu aje anywe.....Kuna KIU ya maendeleo, Kuna KIU ya mafanikio, Kuna KIU kufaulu masomo, Kuna KIU ya Kuoa ama Kuolewa "VIU" hivi vyote hutosherezwa na juhudi za binadamu lakini KIU moja tu ya Kumwabudu Mungu hukatwa na yeye pekee.
Yesu Akasimama, Akapaza Sauti yake akasema "Mtu Akiona Kiu, na Aje kwangu anywe".
Tukutane VCCT tarehe 14 June.....Tukate KIU.

K**a uko au una rafiki ambaye yuko Mwanza basi k**ata hii
13/03/2015

K**a uko au una rafiki ambaye yuko Mwanza basi k**ata hii

Papaa On Tuesday.....Pakacha Pakachuka.....Kuvuja kwa Pakacha Ni Nafuu ya Mchukuzi.....Wapo baadhi ya watu wamewabeba wa...
06/05/2014

Papaa On Tuesday.....Pakacha Pakachuka.....Kuvuja kwa Pakacha Ni Nafuu ya Mchukuzi.....Wapo baadhi ya watu wamewabeba watu ndani ya mioyo yao, wapo watu wamewabeba wapenzi wao wa zamani, wapo watu wamebeba ma boss zao waliosababisha wao kufukuzwa kazi, wapo waliowabeba wazazi wao, wapo waliobeba watu waliowakosesha fursa za kwenda kusoma, wapo waliobeba Kero za tabia mbaya za Waume zao wama wake zao, wapo ambao mioyo yao imebeba uchungu wenye maumivu wa yale yaliyowahi tokea kwao. Swali la kujiuliza utabeba mpaka lini?ama umevibeba hivyo vyote mpaka lini, ukiyaruhusu haya mambo yakaondoka kwako utashangaa afya yako inarejea, unashangaa ule ung’aavu wa sura yako unarudi, utashangaa tabasamu lako linarejea natambua kuwa maumivu ni makali lakini umewahi jaribu njia nyingine mbadala wa hiyo unayotumia sasa. K**a umelia muda mrefu embu jaribu kunyamaza pengine katika kunyamaza unaweza pata suluhu ya lile ulilo nalo.

Huzuni haijawahi msaidia mtu kwenye maisha. Huzuni inasababishwa sana na majuto, na waswahili wanasema Majuto ni Mjukuu na k**a ni Mjukuu lazima ana babu yake ama bibi yake anayeitwa Matendo na Mzazi anayeitwa Maamuzi. Unapoamua jambo na Ukafanya lile jambo majuto huwa yanakuja baada ya Matokeo yale uliyotarajia kutokuwepo. K**a mtu alitarajia akifanya ngono zembe atapata mimba hawezi juta, ila majuto yanakuja iwapo kile ulichotarajia sicho kilichokuja, badala mtu kujifunza unakuta mtu anaanza kujilaumu ana juta kwa kile kilichotokea, ukishaanza kujuta kuna mtoto anazaliwa anaitwa huzuni, huzini na majuto vinakufanya wewe ujione useless, vinakufanya wewe ujione hufai, vinakufanya wewe ujione ni mjinga wa wajinga, ukishaanza kujiona mjinga wa wajinga unakosa furaha unakosa ujasiri, unapoteza uwezo wako wa kufanya mambo mengi sana badala ya kunyanyuka baada ya kuanguka unaanza kulalamika aliyeweka jiwe chini wewe ukajikwaa, unaanza kulaumu aliyesababisha wewe uanguke. Mwisho wa siku unajikuta umebeba watu ndani ya maisha yako hasa wale walisababisha wewe kuingia kwenye majuto uliyonayo. Ok ni sahihi kubeba k**a mwanadamu wa kawaida je utabeba mpaka lini?na unabeba ili iweje?.....gonga hapa kusoma zaidi...http://samsasali.blogspot.com/2014/05/papaa-on-tuesdaypakacha-pakachukakuvuja.html

Zifahamu sababu za Wasichana kuchelewa Kuolewa....Kwenye Kizazi chetu wanawake wengi sana hawapendi kunyanyasika, wengi ...
30/04/2014

Zifahamu sababu za Wasichana kuchelewa Kuolewa....Kwenye Kizazi chetu wanawake wengi sana hawapendi kunyanyasika, wengi wamekuwa enlighten kupitia televisions, wanaharakati wa kutetea haki za wanawake. Mama zetu wakati wanaolewa tangu wakiwa mabinti walikuwa wanaandaliwa kuwa “wake za watu”. Ndio maana kwenye jando na Unyago mafunzo yao yalikuwa ni kumtengeneza mwanamke kwa ajili ya familia na Mwanaume kuwa baba wa familia. Kwenye mafunzo hayo asilimia kubwa ya wanawake walikuwa wanaandaliwa kisaikolojia kuwa watii ambapo siku hizi ni k**a tunaona walikuwa wanaandaliwa kuwa Watumwa wa ndoa zao. Kizazi chetu kimebadilika unaoa mwanamke anajua katiba ya nchi kuliko Biblia utamwambia nini. Ndio maana ukichukua level of development kati ya mwanamke na mwanaume waliokuwa pamoja tangu utotoni Mwanamke anakuwa na maendeleo ya haraka kuliko mwanaume. Wanawake wa kizazi chetu hawapendi hali ya Utegemezi kwa Wanaume. Wanatamani kuwa na kazi zao kuwa na miradi yao, kuwa na vyanzo vyao vya fedha tofauti na mama zetu ambao wengi wakiamka asubuhi, wataomba hela ya mafuta ya taa, wataomba vocha, wataomba kila kitu na hali hiyo ya utegemezi Kisaikolojia ilikuwa inawafanya wanaume wengi wajisikie kuwa wao ndo wanaume. Kati ya Wanawake na Wanaume, Wanaume wengi ni Money & Material Conscious kuliko wanawake inapofika suala la matumizi hasa kwa mtu fulani. Ndio maana watu wengi sana wanapoachana utakuta mwanaume anadai hela zake ama mali zake. Utasikia nipe simu yangu, nipe hela zangu na anasahau kuwa huyo mwanamke alikuwa anampa “pukuchuku” yake sasa nae amdai?.

Sio kwamba hawapendwi, Ila By nature Mwanaume anapenda kuwa juu ya Mwanamke katika Kila hali. Wanawake wenye uwezo wa chini na Wakati kiuchumi ndio waliopiga bao. Ni saikolojia ya kitoto sana kwa mwanaume kupenda kwa ajili ya mwanamke. By nature mwanaume anapenda kufanya kwa ajili ya mwanamke, anataka amsomeshe, amtafutie kazi,amnunulie gari ndio wanaume huona k**a wao ni wanaume, sasa wao wanaona kuoa mwanamke ana degree 3, ana mashamba 6, ana viwanja 2, ana gari 2 kwenye akili yake anaonekana k**a vile “ataonekana” amefuata mali za mwanamke. Swali la Kujiuliza Je Wanawake wabaki nyuma kimaendeleo ili waolewe?la hasha ila tafiti inaonesha kuwa maendeleo hayo yana uzuri wake na changamoto zake. …..Financial Freedom.....kusoma zaidi gonga....http://samsasali.blogspot.com/2014/04/baadhi-ya-sababu-zinazosababisha.html

Mtumishi Wa Mungu Mch. Antony Lusekelo alimaarufu k**a Mzee wa Upako a.k.a Transformer wiki iliyopita aliibua mjadala mz...
06/01/2014

Mtumishi Wa Mungu Mch. Antony Lusekelo alimaarufu k**a Mzee wa Upako a.k.a Transformer wiki iliyopita aliibua mjadala mzito kwenye mitandao ya Kijamii hususan kwenye facebook wakristo na wasio Wakristo wakihoji uhajali wa Mtumishi wa Mungu huyu kwenda kwenye Kipindi Cha Mkasi kilicho chini ya Salama Jabir Mtangazaji nambari One wa Kipindi hicho.

Katika watu waliotazama Mahojiano hayo walimsifu sana Mzee wa Upako jinsi alivyoweza kujibu maswali yote kwa hekima kubwa tofauti na watu wengi walivyokuwa wakimchukulia Mzee wa Upako kuwa angechemka.

Huwa ninamkubali sana Mzee wa Upako kwa sababu yeye ni mtumishi aliyewekwa maalum kwa ajili ya watu Mtaani kabisa yaani "Gospel Kitaa". K**a huku bahatika kutazama mahojiano hayo gonga hapa...http://samsasali.blogspot.com/2014/01/mzee-wa-upako-ndani-ya-kipindi-cha-mkasi.html

08/09/2013
22/08/2013

Friends On Friday Maridadi

Papaa On Tuesday....Makovu Yasiyokuwa na Hisia...Wengine wamekuwa wakihangaika na matumizi mabaya ya fedha kiasi kwamba ...
30/07/2013

Papaa On Tuesday....Makovu Yasiyokuwa na Hisia...Wengine wamekuwa wakihangaika na matumizi mabaya ya fedha kiasi kwamba wanajitahidi kujidhibiti wanashindwa, kosa alilofanya mwezi uliopita amejikuta na mwezi huu amelifanya, wengine wamejitahidi kuacha matumizi ya hovyo lakini imeshindikana kilichotokea wamekubali kuwa hawawezi kubadilika, ilipoanza ni k**a haikuwa na madhara lakini wengine sasa its too mucha na still hawaoni k**a watasaidika katika hilo, wamekubali matokeo. Wengine tabia za kuzira, ajabu unakuta mtu mkubwa kabisa eti anazira, lakini hakuanza leo tabia hii imekuwa polepole bila ya watu wenyewe kujijua imejijenga ndani yao. Wengine ni hofu, wamejawa na hofu mpaka unnecessary. Kuna rafiki yangu yeye kila kitu anaogopa hasa inapofika suala la ndoa yale aliyoyasikia kutoka kwa watu na aliyoyapitia yamemjaza hofu kuwa katika dunia hii k**a kuna mwanaume ambaye yupo kabisa hawezi cheat na akabaki kuwa mwaminifu kwake peke yake. Hofu anabadili namna ya kutazama mambo, hofu inamadili namna ya kuishi na kuongea na kuamua mambo mengi, hofu ikikujaa unaweza ukaufunga hata uwezo wako wa kuwaza na kupambanua mambo, hofu inatawala.

Inawezekana kuna jambo ulishawahi dhani umelisamehe na kuliachilia lakini kila lile jambo linapotajwa kuna mkwaruzo ndani ya moyo wako hutokea, k**a umewahi umizwa na mapenzi ukiwasikia watu wanaongelea mapenzi unatamani usimkumbuke mtu aliyekutenda, ikitokea umemuona njiani anakuja unatamani kubadilisha njia, yamkini uliwahi dhurumiwa ama pata hasara ya biashara yale maumivu bado yameganda kwenye nafsi, inawezekana ni ofisi waliyokufukuza sometimes back ukisikia jina la ofisi moyo unakuuma. Makovu haya ya nafsi hu-develop tabia ambayo yamkini hukuwa nayo hapo awali. Umejengeka na kuto samahe, umejengeka kuwa na tahadhari nyingi zaidi, Umejengeka kuto amini amini mwenzi wako akishika tu simu unajua anachat na wanawake wake unatamani kumwamini lakini nafsi yako imesha develop tabia iliyotengenezwa kutokana na jeraha. Ukimsikia mtu anasema "wanaume wenyewe wote vimeo" jua ana jeraha ama ukisikia mtu anasema "wanawake wote wanafanana" jua ana jeraha lake la kwenye nafsi kila mtu amejawa na hofu ya kuogopa kutoneshwa jeraha la nafsi alilowahi kupitia hapo kabla....kwa habari ziidi gonga......http://samsasali.blogspot.com/2013/07/papaa-on-tuesdaywengi-tu-waathirika-wa.html

Papaa On Tuesday...Shida haina Mjuzi....Kila mtu ana shida na changamoto zake shida haina mjuzi wala mwenyewe unaweza uk...
09/07/2013

Papaa On Tuesday...Shida haina Mjuzi....Kila mtu ana shida na changamoto zake shida haina mjuzi wala mwenyewe unaweza ukawa na Kila kItu kwenye maisha ukawa na fedha ukawa na gari ukawa na mavazi mazuri na mke ama mume mzuri lakini hakuna amani ndani ya ndoa, unaweza kuwa na mshahara mzuri na nyumba nzuri lakini hauna inner satisfaction, inawezekana ukawa unafanya biashara unapata fedha kila siku lakini una ugonjwa unaokutesa, unaweza kuwa na elimu nzuri sana na akili njema sana ajabu hupati Usingizi na unakunywa mpaka madawa na sindano, yawezekana una umbile zuri sana na raha sana lakini ukiwa period mpaka hauoni thamani ya kuishi unatamani kufa, pengine una kila kitu unachodhani unapaswa kuwa nacho lakini unajiuliza kwanini wanaume wanakukimbia, asikuambie mtu shida haina mjuzi wala haina mwenyewe. Kuna mambo kadha wa kadha ambayo kwa watu wasiotujua kwa vile tumeamua kuyaficha tunaonekana tuko pouwa sana lakini k**a leo ingekuwa kila mtu shida yake inaonekana Live Live k**a CCTV ndipo ungejua kuwa shida haina mwenyewe wala haina mjuzi maana wewe unaloliweza mwingine linamshinda lile linalokushinda yeye analiweza unatamani mbadilishane lakini sasa sio fungu lake wala lako la kugawa shida hizo....zaidi soma hapa...www.samsasali.com

Papaa On Tuesday...Tofauti Ya Kuweza na Kutokuweza Ipo Kwenye KUAMUA......Kinachofanywa na Serikali ya Tanzania ni Refle...
02/07/2013

Papaa On Tuesday...Tofauti Ya Kuweza na Kutokuweza Ipo Kwenye KUAMUA......Kinachofanywa na Serikali ya Tanzania ni Reflection ya Maisha halisi ya Watanzania k**a sio Waafrika kwa Ujumla. Nakumbuka Wakati ninasoma mpaka Chuo Kikuu ile wiki ya Kuelekea kwenye Mitihani ndipo unaona watu sasa ndo wanashika vitabu kisawasawa kumbe unajiuliza swali kwanini mtu anakesha namna hii kumbe alikuwa hajaamua kusoma, k**a angeanza semester wakati inaanza yamkini maisha yake ya kusoma yangekuwa yako mbali uwezo na upeo wake ungekuwa wa kutisha lakini ajabu ng'ombe analishwa siku ya mnada. Sisi ni watu ambao kwenye nyumba zetu kuna vyombo ambavyo havitumiki mpaka waje wageni, hata k**a mtakuwa hamna wageni miaka 800 lakini kuna glass ziko kwenye kabati, kuna sahani ziko kwenye kabati ambazo wenyeji hawazitumii mpaka aje mgeni utashangaa mgeni akija nyumbani ndipo siku hiyo mtakunywa na soda, ndipo siku hiyo mtatumia sahani nzuri, ndipo siku hiyo mtapelekwa kuoga mchana, ndipo siku hiyo utaona mpaka goti la mkeo ama mama akiwakaribisha wageni kwenda kuchukua chakula ajabu ni kwamba Mgeni ama wageni wakisha ondoka tunarudi katika maisha yetu yale yale ya sahani za plastiki na soda za sikukuu kumbe kuna siku tukiamua k**a familia tunaweza kula k**a kuna wageni na hakuna madhara.

Hatma ya Maisha yako yanategemeana sana na MAAMUZI unayoyafanya kwenye maisha, ukiamua kubadilika utaona mabadiliko ukipotezea mabadiliko utajipoteza mwenyewe, ukitazama duara lako kubwa la uwezo ulio nao halifanani kabisa na kile ambacho unakifanya na unajua UKIAMUA inawezekana tatizo halipo kwenye kile unachokifanya tatizo lipo kwenye Maamuzi yako ya kuamua kufanya kwa utashi wa ndani kabisa.

Tofauti ya waliofanikiwa na kwenye maisha na wale wasiofanikiwa ipo kwenye KUAMUA. Wengi wetu tumebaki kuwa wachambuzi na wakosoaji na sio watu wenye kuamua, wengi huwa wanasisimka wakisoma Papaa On Tuesday lakini kasheshe iko kwenye Kutendea kazi. Yesu akasema anaheri yule anayesikia na Kutenda. Upo hivyo ulivyo kwa sababu ya aina ya maisha uliyoyaamua na siku ukiamua kufanya utashangaa kwanini ulichelewa kufanya maamuzi sababu kubwa Unaweza kufanya lakini yamkini hujaamua kufanya ingawa unajua ndani ya Moyo wako UKIAMUA kikwelii kufanya unaweza kufanya na kubadilika. Yamkini umekuwa ukitamani kubadilika tabia fulani kwenye maisha yako lakini umekuwa ukiindekeza ili uendelee kuwa nayo huku ukitambua fika tabia hiyo ndiyo imekuwa kikuharibia kila siku kwenye maisha lakini hujaamua tu kubadilika ukiamua inawezekana. Gonga hapa kusoma yote...http://samsasali.blogspot.com/2013/07/papaa-on-tuesdaytofauti-ya-kuweza-na.html

Je wajua??Walio-Mabachelor (Wasiooa na Kuolewa) Hulala Usingizi wa Afya Kuliko Wanandoa??1. Kwanza ni mambo yetu yale ya...
25/06/2013

Je wajua??Walio-Mabachelor (Wasiooa na Kuolewa) Hulala Usingizi wa Afya Kuliko Wanandoa??

1. Kwanza ni mambo yetu yale ya kawaida kwa wanandoa ambapo ukioa linageuka kuwa "Haki Ya Kimsingi".

2. Ujio Wa Style Mpya either ya Ubunifu ama Kuzorotesha pambano. Wanasema k**a siku hiyo mume ama mke amekuja na style mpya ama k**a anakuwa chini ya kiwango basi baada ya hapo ujue kuna Kesi. "Haya niambie hii ya leo umeipata wapi??au mbona leo uko hivyo???

3. Mipango na Mikakati ya Kifamilia. Kutokana na Muda mwingi mchana kutumika kwa ajili ya Mishe mishe. Usiku hutumika k**a muda muafaka wa wanandoa wengi kupanga mikakati kwa ajili ya maendeleo.

4. Usuluhishi wa Migongano. Kesi nyingi sana huongelewa usiku baada ya mmoja kuona ipo haja ya kuamshana na kuongea na kupata utatuzi wa tatizo lililopo. Migogoro ya kwenye ndoa hupelekea vikao vya usiku ili kujaribu kupata suluhu ya tatizo.

5. Mabadiliko Ya Tabia Za Mwenzi Wako. Mfano mpenzi wako anaaanza tabia mpya ya kuongea na simu mbali na wewe ama kunyanyuka kitandani, kuweka password kwenye simu, kuchelewa kurudi tabia hizi hupelekea wivu wa mapenzi kujengeka na kuanza kufatilia mwenendo wa mpenzi wako. Kwa kuwa unakuwa huna amani na tabia hizo mwenzio anajionea sawa anaamua kulala wakati huo wewe unajihoji nini chanzo cha mabadiliko hayo.

gonga hapa kupata sababu 11....http://samsasali.blogspot.com/2013/06/xposed-from-facebookje-ni-kweli-walio.html

Address

Dar-es-Salaam, Arusha, Dodoma, Tanzania Nzima Tutafika
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Friends On Friday-FoF posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Friends On Friday-FoF:

Share