Roho wa Neema na Madhabahu

Roho wa Neema na Madhabahu "Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu."
1 Kor 4:1 SUV

Merry Christmas and Happy New Year 🎆🎆🎆🎆
25/12/2025

Merry Christmas and Happy New Year 🎆🎆🎆🎆

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 09MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
06/01/2025

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 09

MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom Mwana wa Mungu Baba katika Kristo Yesu. Ninamtukuza Mungu Baba kwa ajili yako wewe ambaye umepata neema hii ya kujifunza na kufundishika juu ya Karama hii ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu hapa duniani.

TAMKO
Natamka kwa jina la Yesu Kristo, kwamba macho ya moyo wako yametiwa nuru, nawe umeuona na kuujua upendo wa Mungu Baba uliowekwa wazi kwako ktika Kristo Yesu, na ufahamu wa Kristo na maarifa ya kiungu yapitayo ya dunia hii. Umethibitika katika Hekima ya Kiungu na Unatembea katika utukufu wa ufahamu wa Mungu wewe na uzao wako katika Kristo Yesu hapa duniani. AMEN

Karibu tuendelee na Darasa letu na Roho Mtakatifu Mwalimu wetu na kiongozi wetu katika somo letu hili la Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani

Kuwa na ufahamu sahihi wa ufalme wa Mungu ni kufunuliwa karama ya Muda, Hekima, na Fedha ndani ya ufalme wa Mungu. Kwani ufahamu wa Mungu ndani ya Ufalme ndio ufunguo na kanuni ya kwanza katika kufanya jambo lolote lile kwa Mwana wa Mungu.

Gods understanding it is the insight to understand about God and His Kingdom and His Time, wisdom and Money na kuishi hapo.(Ufahamu wa Kiungu ni muono wa ndani tunaofunuliwa na Roho Mtakatifu kumuelewa Mungu Baba, Ufalme wake, muda, hekima na fedha na kuuishi katika damu na nyama hapa duniani.) Hauwezi kutawala hapa duniani k**a hauna ufahamu sahihi wa ufalme wa Mungu.

NB, Kuwa na ufahamu sahihi ni kuishi sahihi.

Mungu Baba kumwambia Adamu wa kwanza kuwa aende akazae, akaongezeke, akatiishe, na kutawala juu ya nchi alimtaka kwanza atambue neema ambayo Mungu ameiachilia kwake kwamba siyo kwa nguvu zake katika hayo yote, Bali inamuhitaji ajifunze na kuthibitika katika ufahamu wa Mungu ndipo ataweza kufanikiwa katika hayo yote. Na ndiyo maana alimuweka Edeni.
K**a ilivyo kwa mkulima ndivyo ilivyo kwa Mwana wa Mungu kwamba kuna kipindi cha kuandaa shamba na mbegu, kuna kipindi cha kupanda, na kuna kipindi cha mavuno(kula matunda) ndivyo ilivyo kwa Mwana wa Mungu ndani ya ufalme wa Mungu. Hauwezi ukayaishi Maisha ya Mungu pasipo kuwa na ufahamu sahihi ambao Mungu ameufunua kwako ukauthamini na ukaamua kuushi.
Katika vipindi hivi vyote Mungu Baba amevifungamanisha katika Karama ya Muda, Hekima na Fedha, hivyo hututaka sisi kuendelea kujifunza na kupata ufahamu zaidi wa ufalme wa Mungu na kuthibitika katika huo. Ni kipindi cha kukubaliana na ufahamu wa Mungu, wazo la Mungu na kulithamini na kuliishi. Yaani kuishi k**a Mungu, kuona k**a Mungu, kusema k**a Mungu na kufanya k**a Mungu.

SOMA ZAIDI
Mwanzo 1:28, 2 :15, Rumi 12:1-2, Efeso 5:15-17

Itaendelea…

Na nabii Tumikiael Nassary

# Roho wa Neema na Madhabahu

                                                         # Roho wa Neema na Madhabahu
27/12/2024

# Roho wa Neema na Madhabahu

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 08MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
20/12/2024

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 08

MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom Mwana wa Mungu Baba katika Kristo Yesu. Ninamtukuza Mungu Baba kwa ajili yako wewe ambaye umepata neema hii ya kujifunza na kufundishika juu ya Karama hii ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu hapa duniani.

TAMKO
Natamka kwa jina la Yesu Kristo, kwamba macho ya moyo wako yametiwa nuru, nawe umeuona na kuujua upendo wa Mungu Baba uliowekwa wazi kwako ktika Kristo Yesu, na ufahamu wa Kristo na maarifa ya kiungu yapitayo ya dunia hii. Umethibitika katika Hekima ya Kiungu na Unatembea katika utukufu wa ufahamu wa Mungu wewe na uzao wako katika Kristo Yesu hapa duniani. AMEN

Karibu tuendelee na Darasa letu na Roho Mtakatifu Mwalimu wetu na kiongozi wetu katika somo letu hili la Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Katika Somo lililopita tulijifunza na kuona kuwa watu sahihi ndani ya ufalme wa Mungu Baba ni wana wa Mungu ambao Mungu Baba huwaleta kwetu kwa ajili ya;

Mosi; ku-support(kushiriki) katika Maono ambayo Mungu Baba ametupatia katika Kristo Yesu.
Pili; kwa ajili ya kuthibitisha maono hayo aliyokupatia Mungu Baba.

Swali; Kuthibitisha maana yake ni nini
• Ni hakikisho, Imarisha, kukufanya usimame.

Hivyo, watu sahihi ambao Mungu Baba hutupatia wanapokuja huzungumza kile ambacho Bwana alikwisha kuzungumza na wewe mwenyewe iwe katika ndoto, maono, neno lake, au Bwana kwa kupitia mtumishi wake, au watumishi wake alikwisha kuzungumza na wewe.

Watu sahihi huja Katika majira sahihi na nyakati ya Mungu. Nao huzungumza hayo Maono(maono ndo yanakuwa lugha yetu na wao), hufikiri Maono, Huona Maono, na husimama katika Maono(yaani huhakikisha kwamba tumesimama na kufanya kile alichotupatia Bwana).

NB; Watu hawa mara nyingi hujitoa wao wenyewe na kwa mali zao kwa ajili ya hayo Maono ya Bwana.

Ni muhimu kwetu sisi wana wa Mungu kuwa na ufahamu wa sahihi wa Ufalme wa Mungu Baba ambao tumeupokea kupitia Yesu Kristo na kazi yake Kamilifu ya Msalabani ambao katika huo tunafunuliwa Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Pamoja na watu sahihi ambao Mungu Baba ametupatia.

SOMA ZAIDI;
Efeso 1:17-23, Mwanzo 37, Mithali 27:17, 2 Wakorinto 8:3-5,

Itaendelea…
Na nabii Tumikiael Nassary

# Roho wa Neema na Madhabahu

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 07MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
16/12/2024

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 07

MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom Mwana wa Mungu Baba katika Kristo Yesu. Ninamtukuza Mungu Baba kwa ajili yako wewe ambaye umepata neema hii ya kujifunza na kufundishika juu ya Karama hii ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu hapa duniani.

Karibu tuendelee na Darasa letu na Roho Mtakatifu Mwalimu wetu na kiongozi wetu katika somo letu hili la Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Katika somo lililopita tulijifunza na kufahamu sifa za muda sahihi na mahali sahihi ndani ya Ufalme wa Mungu; kwamba Mungu Baba kutupatia Muda wake (Kristo) ili tuwe na Ushirika naye na tuwe na Ufahamu wake ndani ya Ufalme wake. Hivyo mahali sahihi ni mahali ambapo tunafunuliwa kuhusu ushirika na Mungu Baba, na panatufanya tuongezeke katika ufahamu na maarifa zaidi katika Maono na vyote tuliyopewa na Mungu Baba.

3. Watu sahihi ndani ya ufalme wa Mungu Baba ni wana wa Mungu ambao Munngu Baba huwaleta kwetu kwa ajili ya ku-support(kushiriki) au kuhakikisha Maono ambayo Mungu Baba ametupatia yanazaa, yanaongezeka, yanajaza nchi, yanatiisha na kutawala juu ya nchi.

Watu sahihi huzungumza sawa na Maono tuliyo nayo, yaani Maono ndiyo lugha yetu, kauli yetu,furaha yetu na ndiyo yanayotuweka Pamoja na katika umoja.

Hivyo, ni muhimu kutambua kuwa, Mungu Baba anapotuletea watu sahihi katika maisha yetu ni kwa ajili ya kutujenga na kutuimarisha katika Maono Yake na katika msingi ambao ni Kristo. Kristo ndiye Bwana wa Maono yote ndani ya ufalme wa Mungu.

Kwasababu hiyo, Maono ambayo Mungu Baba ametupatia yamebeba Muda wa Mungu, Hekima, ya Mungu na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu. Hivyo, watu sahihi ambao Mungu Baba ametupatia wanapokuja kwetu kupitia Maono hayo hutufunulia kufahamu zaidi kazi kamilifu ya Yesu Kristo ya Msalabani na matokeo yake.

SIFA ZA WATU SAHIHI
âś…Huja kuthibitisha kile ambacho Bwana amesema na sisi
âś…Wana Imani moja pamoja na sisi(wanaamini sawa na sisi).
âś…Wana ufahamu na maarifa ya Ufalme wa Mungu.
âś…Wanazijua kanuni na sheria za ufalme wa Mungu.

SOMA ZAIDI;
Mwanzo 1:27-28, Mwanzo 22, Kutoka 3, Amosi 3:3, Mithali 27:17, Yoh 3:27, Mdo7,

Itaendelea…
Na nabii Tumikiael Nassary

# Roho wa Neema na Madhabahu

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 06MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
13/12/2024

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 06

MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom Mwana wa Mungu Baba katika Kristo Yesu. Ninamtukuza Mungu Baba kwa ajili yako wewe ambaye umepata neema hii ya kujifunza na kufundishika juu ya Karama hii ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu hapa duniani.

Karibu tuendelee na Darasa letu na Roho Mtakatifu Mwalimu wetu na kiongozi wetu katika somo letu hili la Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Katika somo lililopita tulijifunza kuwa Mafanikio kwa Mwana wa Mungu yapo pale anapokuwa mahali sahihi, kwa Muda sahihi na kwa watu sahihi ambapo ni katika Mwili wa Kristo; kwasababu Bwana ameachilia Roho wa Neema mbalimbali kwa ajili ya kutujenga, kutuimarisha na kutuinua katika majira sahihi na nyakati sahihi ya Mungu Baba juu ya mwili wa Kristo.

Kwanini mahali sahihi, muda sahihi na watu sahihi?

1.Mahali sahihi(Mwili wa Kristo);
Ni mahali au ni familia ya Mungu, ambapo Mungu Baba hutuweka kwa ajili yake, hivyo hutuhudumia kwa neno lake na kutufunulia zaidi kuhusu maono yake.

Ni mahali ambapo hutufanya tukue na kuimarishwa katika maono ambayo Mungu Baba ametupatia katika Kristo Yesu.

Ni mahali ambapo inatufanya kuwa hayo maono tuliyopatiwa na Mungu Baba.

Ni mahali ambapo panatufanya tuongezeke katika ufahamu na maarifa zaidi katika maono.

Mungu Baba ametupatia Familia yake ambayo ni mwili wa Kristo (mahali sahihi) kwa ajili ya kutujenga, kutuimarisha na kutufanya tukue katika maono na wazo lake alilotufunulia katika Kristo Yesu.

2. Muda sahihi,
Muda sahihi hutokana na Ufahamu sahihi wa Yesu Kristo na Kazi yake Kamilifu ya msalabani. Na ni mahali pa Ushirika Zaidi, ambapo tunafunuliwa hazina zote za Ufalme wa Mungu Baba, tunafundishwa na kujifunza kwasababu tunamuona na kumsikia Baba.

Hivyo, Mungu Baba kutupatia Muda wake (Kristo) ni ili tuwe na Ushirika naye na tuwe na Ufahamu wake na wa ndani ya Ufalme wake.

SOMA ZAIDI
Mwanzo 2:15, 47:27, Zaburi 133:1, Isaya 45:3, Yoh 5:19, Mdo 15:35,

Itaendelea…
Na nabii Tumikiael Nassary

# Roho wa Neema na Madhabahu

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 05MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
09/12/2024

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 05
MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom mwana wa Mungu Baba na Urithi wa Mungu Baba Katika Kristo Yesu. Hongera sana kwa kuendelea kujifunza, Umebarikiwa wewe na uzao wako na vizazi vyako vyote.

Karibu tuendelee na somo letu la Karama ya Muda, Hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Katika SOMO lililopita tulijifunza kuwa kumfahamu sana Kristo ni kuyafahamu majira na nyakati ya Mungu Baba. Pia, Muda wa Mungu Umebeba watu sahihi na mahali sahihi katika kila jambo, ambapo mahali sahihi na watu sahihi ni MWILI WA KRISTO hapa duniani.

Hivyo, Mwana wa Mungu tunapaswa kuufurahia mno Mwili wa Kristo kwasababu ndipo mahali ambapo Kristo amewekeza utajiri wa Roho wake wa Hekima, Maarifa na Ufahamu wa vizazi hata vizazi. Mwili wa Kristo unapopata ufahamu sahihi wa karama hii ya Muda, Wana na Urithi wa Mungu huona na kufurahia kuwapo katika kusanyiko pasipo kusukumwa au kulazimishwa.


Karama ya muda humfunua Mwana wa Mungu kuwa anaishi na kutembea katika majira na nyakati ya Mungu na siyo kutokea kwenye kalenda ya warumi kwasababu anaufahamu wa vitu vyote vya thamani alivyonavyo ndani yake Kristo.

Mwana ambaye anaongozwa na kalenda ya warumi na siyo Muda wa Mungu, siku zote hutamani zaidi matokeo ya nje au utajiri wa nje zaidi kuliko ule wa Rohoni(vipawa tulivyovipokea katika Kristo Yesu), hii ni kwasababu ya kutoielewa vizuri kazi kamilifu ya Yesu Kristo ya Msalabani na matokeo yake. Kuielewa kazi kamilifu ya msalabani ya Yesu Kristo ni kujua muda wa Mungu na kuutambua umuhimu wa Mwili wa Kristo na kuuthamini.

Mafanikio kwa Mwana wa Mungu yapo pale anapokuwa mahali sahihi, kwa Muda sahihi na kwa watu sahihi ambapo ni katika Mwili wa Kristo. Katika mwili wa Kristo ndipo Bwana ameachilia Roho wa Neema mbalimbali kwa ajili ya kutujenga, kutuimarisha na kutuinua katika majira sahihi na nyakati sahihi ya Mungu Baba.

SOMA ZAIDI;
Kolosai 3:1-3, Efeso 1:3,1Korinto 1:10
Itaendelea…

Na nabii Tumikiael Nassary
# Roho wa Neema na Madhabahu

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 03MHUBIRI 3:1-11.“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa ki...
02/12/2024

KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 03
MHUBIRI 3:1-11.
“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”

Shalom mwana wa Mungu Baba, hakika ni jambo jema na la muhimu kuchagua na kupenda maarifa na ufahamu. Kwani ufahamu sahihi wa ufalme wa Mungu ndio utufanya tuishi sahihi na haya ndiyo Maisha ya mwana wa Mungu hapa duniani(kufahamu sahihi ni kuishi sahihi). Hongera sana wewe ambaye unaendelea kufuatilia mfululizo wa somo hili, na Bwana amekuthibitisha katika ufahamu wake na unaishi katika huo.

Karibu tuendelee na somo letu la Karama ya muda, hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Mwana wa Mungu k**a ambavyo katika somo lililopita tuliona na kujifunza kuwa leo hii Hekima ya Mungu duniani inaonekana au imefunuliwa katika mwili wa Kristo duniani. Hii ikiwa na maana kwamba mwili wa Kristo duniani hutambua majira na nyakati ya Mungu Baba hapa duniani kwasababu yeye Mungu yupo Katikati yetu daima. Ni roho wa hekima ya Mungu Baba ndiye hufunua majira sahihi, eneo sahihi, na watu sahihi ambao Mungu Baba huwaleta kwetu, ama ametupatia. Hivyo Mungu Baba kutupatia Hekima yake maana yake ametupatia ukamilifu wake wote.

Je? fedha ni nini ndani ya ufalme wa Mungu?

FEDHA ndani ya ufalme wa Mungu ni Ufahamu wa vitu vyote vya thamani(VIPAWA) ambavyo Mungu Baba amewekeza ndani yetu katika Kristo Yesu na kuvitumia huku tukiwa na ufahmu kuwa hakuna mtu yeyote anayeweza kutunyang’anya.

Ni Mawazo yote ya kiungu tunayoyapokea ndani ya ufalme wa Mungu Baba kwa ajili ya kuleta majibu kwa watu wote.

JE MWANA WA MUNGU UNAJUA KIPAWA ULICHO NACHO, AU VIPAWA ULIVYONAVYO KATIKA KRISTO YESU? Ni kipawa ndicho ututofautisha. Kipawa ndicho utufanya tuone tofauti na kufanya tofauti na watu wengine walivyozoea ua mazingira yetu. Mtume Paulo anatuambia katika Warumi 14:5, kuwa kuona tofauti na kufanya tofauti kati ya siku na siku hutokana na ufahamu sahihi wa nini Mungu Baba amewekeza ndani yako katika Kristo Yesu na kukiishi.

Hivyo; ufahamu wa vipawa tulivyonavyo(alivyotupatia Mungu Baba) na kuvitumia ndivyo pesa au utajiri wa thamani ambao Mungu Baba ametupatia. Kwasababu hiyo mwana wa Mungu kuwa na fedha hizi za makaratasi haimanishi kuwa umetajirika BALI UTAJIRI MKUU NA MKUBWA NA WATHAMANI KWETU MWILI WA KRISTO DUNIANI KUFAHAMU VIPAWA TULIVYO NAVYO NA KUVITUMIA. Kwasababu hiyo pesa za makaratasi kwetu ni matokeo ya ufahamu sahihi wa vipawa tulivyo navyo na kuvitumia.

SOMA ZAIDI
Mith 8:14-21,Kol 1:26-27, Yak 1:17, Rum 14:5

# Roho wa Neema na Madhabahu

Itaendelea…
Imeandaliwa na Nabii Tumikiael Nassary

*KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 02**MHUBIRI 3:1-11.* *“Kila jambo kuna majira yake na wakati...
29/11/2024

*KARAMA YA MUDA, HEKIMA, NA FEDHA NDANI YA UFALME WA MUNGU. 02*

*MHUBIRI 3:1-11.*
*“Kila jambo kuna majira yake na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu…”*

Shalom mwana wa Mungu Baba katika Kristo Yesu unayependwa na kutunzwa na Mungu Baba. Karibu tuendelee na somo letu la Karama ya muda, hekima na Fedha ndani ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.

Tukirejea pale tulipoishia tuliona kuwa mwana wa Mungu ili tuweze kuyafurahia matunda ya muda na nyakati ya Mungu ushirika ni muhimu kabla ya kitu chochote. Kwasababu ni katika ushirika ndipo ambapo sisi wana hufunuliwa utajiri wa muda, na kuzidi kupata maarifa ya namna ya kuusimamia na kuuendeleza utajiri huo kwa ajili ya vizazi hata vizazi.

Ni katika ushirika na Baba ndipo ambapo tunajifunza zaidi na kumsikia Mungu Baba kupia neno lake, Kutenda anayotutaka tuyatende katika majira na nyakati zake, kuishi na kutembea katika utukufu wa muda ambao umefunuliwa kwetu.

Mwana wa Mungu ushirika ni jambo la lazima na la muhimu sana kwa mwili wote wa Kristo duniani, hii ni kwasababu Mungu Baba amekuwa akitupatia ufunuo ambao upo katika majira na nyakati sahihi lakini kwa kukosa kuwa na ushirika wana wengi wamekuwa wakipishana na muda wa Mungu, Na mwisho kuanza kulalamika na kukosa kuwa na shukrani. Shukrani ni matokeo ya ushirika kati ya mwana na Mungu Baba yake, Mwana aliyeona na kutambua majira na nyakati za Mungu Baba na kuyaishi katika damu na nyama.

Mfano tunawaona Abrahamu na Sara wakiwa hemani(mahali pa ushirika na Baba) wanafunuliwa majira na nyakati ya kupokea mwana, na muda ulipotimia walipokea mwana (ISAKA). Pia tunamuona mama mshunami anafunuliwa majira na nyakati ya kupokea mtoto, na majira yalipo wadia alipokea mwana.
Muda ni kanuni au kitu cha msingi sana kwa mwana wa Mungu hapa duniani. Kwasababu muda ndio unao funua Hekima ya Mungu kwetu, na fedha. Yaani muda ndiyo uliobeba Hekima, muda ndiyo uliobeba Fedha.

*Tujiulize swali! Je Hekima ni nini?*

*HEKIMA* ni uwezo wa kiungu/ ufahamu wa kiungu wa kuweza KUFASIRI NA KUKALMAN mambo ya Mungu kwa njia rahisi, kwa muono wa ndani ambao watu wengine hawawezi kuona. Leo hii hekima ya Mungu duniani inaonekana au imefunuliwa katika mwili wa Kristo duniani.


*SOMA ZAIDI*
*Amosi 3:3, mithali 8:12-21, 30-31, Mwanzo 18”1-14, 21:1-3 , 2 wafalme 4:8-17*

Mwana wa Mungu karibu kwa majibu, ya swali letu hapa chini. Nasi tutaanza nalo katika somo lijalo.

*Je? fedha ni nini ndani ya ufalme wa Mungu?*

Itaendelea…
Imeandaliwa na Nabii Tumikiael

Nassary # Roho wa Neema na Madhabahu

                                                         # Roho wa Neema na Madhabahu
28/11/2024

# Roho wa Neema na Madhabahu

Address

Daresalaam
Dar Es Salaam
1428

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Roho wa Neema na Madhabahu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Roho wa Neema na Madhabahu:

Share