Mzambarauni - Seventhday Adventist Church

Mzambarauni - Seventhday Adventist Church Mzambarauni - Seventh-Day adventist church
Dar es Salaam

30/12/2017

KISHA LA ASUBUHI
JUMAMOSI (Siku ya Sabato)
Tarehe 30- Disemba - 2017

SOMO :MAMBO ya KWANZA KUWA ya KWANZA

Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Mathayo 6:33.

Ahadi hii haitashindwa kamwe. Hatuwezi kufurahia fadhila za Mungu k**a hatutakubaliana na masharti ambayo kwa hayo fadhila zake zimetolewa. Kwa kufanya hivyo, itatujia amani, ridhaa na hekima ambayo dunia haiwezi kutoa wala kuiondoa….Akili nyenyekevu na moyo wenye shukrani vitatuinua juu ya majaribu madogo madogo na changamoto hakika. Kadiri tunavyopungua katika ari, nguvu na kuwa macho katika utumishi wa Bwana, ndivyo akili itakavyozidi kudumu katika nafsi, ikikuza vichuguu na kuvifanya milima ya matatizo…

Mzigo wa kazi ya Mungu, ambao uliwekwa mabegani mwa Musa, ulimfanya yeye awe mtu wa nguvu. Kwa miaka mingi, alipokuwa akitunza mifugo ya Yethro, alipata uzoefu uliomfundisha unyenyekevu wa kweli… Agizo la kwenda kuikomboa Israeli lilionekana kuwa kubwa sana; lakini, kutokana na kumcha Mungu, Musa alikubali amana. Tambua matokeo: Hakuishusha kazi hadi kwenye udhaifu wake; bali kwa nguvu ya Mungu aliweka jitihada ya dhati kujiadilisha na kujitakasa kwa ajili ya utume wake mtakatifu.

Kamwe Musa asingeandaliwa kwa ajili ya nafasi hii ya kuaminiwa k**a angemngojea Mungu kuifanya kazi kwa ajili yake. Nuru kutoka mbinguni itawajia wale wanaojisikia kuihitaji na ambao wanaitafuta k**a kutafuta hazina iliyofichwa. Lakini ikiwa tutazama hadi kwenye hali ya kutoshughulika, tukiruhusu udhibiti wa nguvu ya Shetani, Mungu hatatuletea uvuvio wake. Tusipotumia nguvu zetu zote ambazo ametupatia, daima tutabaki kuwa dhaifu na wazembe. Maombi mengi na zoezi kali la akili ni muhimu k**a tunataka kuandaliwa kufanya kazi ambayo Mungu ametuaminia. Wengi hawafikii kamwe nafasi ambazo wangeweza kuzishika, kwa sababu wanamngoja Mungu awatendee kile ambacho amewapa uwezo wajifanyie wenyewe. Wale wote ambao wameandaliwa kutumika, katika maisha haya ni lazima waandaliwe kwa kunidhamishwa vikali kiakili na kimaadili na kisha Mungu atawasaidia kwa kuunganisha nguvu ya kimbingu na jitihada ya kibinadamu…

Mazoea mabaya hayashindwi kwa juhudi ya namna moja. Nafsi inaweza tu kutawaliwa kwa kupitia kwenye pambano refu na kali.

29/12/2017

*KESHA LA ASUBUHI*

_IJUMAA DISEMBA 29, 2017_

*Mungu Anawakumbuka Walio Wake*

_Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu. Ufunuo 12 :12._

📚 Katika karne zote, mashahidi walioteuliwa na Mungu wamejiweka wenyewe katika mazingira ya kushutumiwa na kuteswa kwa ajili ya ile kweli. Yusufu alitengwa na kuteswa…Daudi, mjumbe aliyechaguliwa na Mungu, aliwindwa k**a mnyama – windo la maadui zake…..Stefano alipigwa mawe kwa sababu alihubiri juu ya Kristo, Yeye aliyesulubiwa. Paulo alifungwa, akapigwa kwa viboko, alipigwa mawe, na hatimaye aliuawa…

📚 Yohana alifungiwa kwenye kisima cha Patmo “kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda” wa Yesu Kristo. Mifano hii ya uthabiti wa wanadamu inashuhudia juu ya uaminifu wa ahadi za Mungu – juu ya kuwepo kwake kwa kudumu na neema yake inayotushikilia. Inathibitisha juu ya nguvu ya imani iwezayo kusimama dhidi ya nguvu ya dunia.

📚 Kipindi cha dhiki na mateso kilicho mbele yetu kitahitaji imani itakayostahimili udhaifu, kuchelewa na njaa – imani ambayo haitadhoofika hata ikijaribiwa vikali. Watu wengi wa mataifa yote na wa tabaka zote, wa hali ya juu na wa hali ya chini, matajiri na maskini, weusi na weupe, watatupwa kwenye utumwa wa uonevu na wa kikatili kabisa.

📚 Wapenzi wa Mungu hupita kwenye siku za fadhaa, wakiwa wamefungwa minyororo, wakizuiwa kwa nondo zilizozinga magereza, wakiwa wamehukumiwa kuuawa, inavyoonekana wengine wanaachwa wafe kwa njaa kwenye magereza ya chini ya ardhi yenye giza na ya kuchukiza…ambapo hakuna mkono wa kibinadamu ulio tayari kuwasaidia.

Je, Bwana atasahau watu wake kwenye saa hii ya jaribu? Alimsahau Nuhu mwaminifu wakati hukumu iliposhushwa kwenye dunia wakati wa gharika? Alimsahau Lutu wakati moto uliposhuka kutoka mbinguni kuiangamiza miji ya eneo lile tambarare?.... Alimsahau Eliya wakati Yezebeli alipomtisha kutokana na hatima ya manabii wa Baali? Alimsahau Yeremia kwenye shimo lenye giza na la kusikitisha la gereza lake? Aliwasahau wale watatu kwenye tanuru la moto? Au Danieli kwenye tundu la simba?...

📚 Japo maadui wawatupe gerezani, hata hivyo, kuta za magereza ya chini ya ardhi haziwezi kuvunja mawasiliano kati ya roho zao na Kristo. Yeye aonaye kila udhaifu walio nao, yeye ajuaye kila jaribu, yeye yuko juu ya mamlaka zote za kidunia; na malaika watawajia kwenye vyumba vyao vya magereza vilivyo pweke, akiwaletea nuru na amani kutoka mbinguni.

*_TAFAKARI NJEMA NA MUNGU AKUBARIKI MWANA WA MFALME_*

03/10/2017

*_KESHA LA ASUBUHI_*

♻.Jumanne

🌲October.03/2017

*_KUWA WANAFUNZI WA KRISTO_*
_______________________

*_📖✍🏽👉🏽Yesu akawaambia, Njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. Marko 1:17, 18._*

___,,,,__,,,,,______,,,,______

✍🏽📚📖

_*H*awa walikuwa watu wanyenyekevu na wasio na elimu, wale wavuvi wa Galilaya; lakini Kristo, nuru ya ulimwengu, alikuwa na uwezo mwingi kuwafanya wawe bora kwa ajili ya nafasi ambazo kwazo aliwachagua. Mwokozi hakudharau elimu; kwani tunapotawaliwa na upendo wa Mungu na kujitoa kwa huduma yake, kuendeleza tabia ni baraka. Lakini alipita wenye hekima wa wakati wake, kwa sababu walikuwa na hali ya kujiamini kiasi ambacho wasingeweza kuhurumia binadamu wanaoteseka na kuwa watendakazi pamoja na mtu wa Nazareti. Katika hali ya kuwa na imani kali, walidharau kufundishwa na Kristo. Bwana Yesu anataka ushirikiano wa wale watakaokuwa mifereji ambayo haitazuiwa kwa ajili ya ushirika wa neema yake…_

✍🏽📚📖

_*Y*esu alichagua wavuvi ambao hawakuwa na elimu kwa sababu hawakuwa wamefundishwa katika desturi na utamaduni wenye makosa wa wakati wao. Hawa walikuwa watu wenye uwezo wa asili na walikuwa wanyenyekevu na wanaofundishika, -- Watu ambao angeweza kuwaelimisha kwa ajili ya kazi yake. Katika maisha ya kawaida, kuna watu wengi ambao kwa uvumilivu huwa kuna wengi wanaotembea katika mzunguko wa kazi ngumu za kila siku, bila kujua kwamba wanao uwezo ambao ukiwekwa katika vitendo, utamuinua hadi kufikia katika usawa na watu wa dunia wenye heshima kubwa zaidi. Mguso wa mkono ulio stadi unahitajika ili kuinua uwezo huo uliolala. Walikuwa watu wa namna hiyo ambao Yesu aliwaita ili wawe watendakazi wake wenza; naye akawapa faida ya kushirikiana naye mwenyewe. Kamwe wakuu wa ulimwengu hawakuwa wamewahi kuwa na mwalimu wa namna hiyo. Wanafunzi walipotoka kwenye mafunzo ya Mwokozi, hawakuwa wajinga tena na wasiostaarabika. Walikuwa sasa k**a yeye kwa mawazo na tabia na watu waliwatambua kwamba hawa walikuwa pamoja na Yesu._

✍🏽📚📖

_*Y*eye aliyewaita wavuvi wa Galilaya bado anaita watu kwa ajili ya utumishi wake. Naye yuko tayari kudhihirisha uwezo wake kupitia kwetu k**a alivyofanya kupitia kwa wanafunzi wa kwanza. Bila kujali kuwa sisi ni waovu na wapungufu kiasi gani, Bwana anatupatia nafasi ya kuwa na ubia pamoja naye mwenyewe, nafasi ya kuwa wanafunzi kwenye shule ya Kristo. Anatualika kuja chini ya maelekezo ya kimbingu, ili, tunapounganika na Kristo, tupate kuzitenda kazi za Mungu._

________________________

*_tafakari.... njema_*
..
.

12/02/2017

NYUMBA AMBAYO MUNGU ANAWEZA KUIBARIKI

Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu. Mwanzo 18:19.

Machoni pa Mungu, mwanamume anapimwa kwa namna alivyo kwenye familia yake. Maisha ya Ibrahimu, rafiki wa Mungu, yalitambulika kutokana na heshima ya juu kwa Neno la Bwana. Aliendeleza dini ya nyumbani. Hofu ya Mungu ilipenya nyumbani kwake. Yeye alikuwa kuhani wa nyumba yake. Aliitazama familia yake k**a amana takatifu. Nyumba yake ilikuwa na watu zaidi ya elfu moja na aliwaelekeza wote, wazazi na watoto kwa Mungu Mwenye enzi. Hakukubali namna yoyote ya ukandamizaji wa wazazi kwa upande mmoja au kutotii kwa watoto kwa upande mwingine. Kwa muunganiko wa mvuto wa upendo na haki, aliitawala nyumba yake katika kicho cha Mungu na Bwana alishuhudia uaminifu wake.

Yeye, “atawaamuru…nyumba yake.” Hapakuwa na uzembe wa uovu katika kudhibiti tabia ya uovu ya watoto wake, hapakuwa na upendeleo dhaifu, usio wa hekima, unaodekeza, wala kukubali kuacha kuwajibika kwa ajili ya upendo usiostahili. Ibrahimu hakutoa tu maelekezo sahihi, lakini angelidumisha mamlaka ya sheria za haki na uadilifu.

Wapo wachache sana katika siku zetu ambao wanafuata mfano huu. Kwa upande wa wazazi wetu wengi sana ipo hali ya kuongozwa na hisia zinazopofusha au za kibinafsi, hali inayodhihirika katika kuacha watoto ambao hawajaweza kufanya uamuzi na kunidhamisha shauku zao, waendeshwe na nia zao wenyewe. Huu ni ukatili mbaya kuliko wowote kwa vijana na kosa kubwa kwa dunia. Upole kupita kiasi kwa upande wa wazazi husababisha kukosekana kwa utaratibu kwenye familia na katika jamii. Hiyo huwathibitisha vijana katika tamaa ya kufuata mwelekeo wao, badala ya kujisalimisha kwa masharti ya Mungu.

K**a walivyo wazazi ndivyo ilivyo kwa watoto kuwa ni wa Mungu ili awatawale. Kwa muunganiko wa upendo na mamlaka, Ibrahimu aliitawala nyumba yake. Neno la Mungu limetupatia kanuni kwa ajili ya kutuongoza. Kanuni hizi hutengeneza kiwango ambacho katika hicho hatuwezi kuyumba k**a tunadumu katika njia ya Bwana. Lazima mapenzi ya Mungu yawe ndiyo yenye umuhimu mkubwa. Swali ambalo inatupasa tuulize siyo: Wengine wamefanya nini? Ndugu zangu watafikiri nini? Au, watasema nini juu yangu k**a nikichukua mwelekeo huu? Lakini swali liwe, Mungu amesema nini? Hakuna mtoto wala mzazi anayeweza kufanikiwa kweli katika mwelekeo wowote isipokuwa katika njia ya Bwana.

30/01/2017

MUONGOZO WA KUJIFUNZA BIBLIA

TAREHE 30-01-2017

Kujazwa Roho Mtakatifu

Soma Waefeso 5:18, Matendo 13:52, na Warumi 8:9. Je, kujazwa Roho Mtakatifu humaanisha nini? Kujazwa Roho hutokeaje katika maisha yetu?

Mara tunapobatizwa na kuwa wafuasi wa Kristo, tunapaswa kuishi katika uwezo wa Roho. Ili hili liweze kutokea lazima tujazwe na Roho. Kuna rejea nyingi katika Agano Jipya ambapo watu wanajazwa Roho (Lk. 1:41, 67; Mdo. 2:4; 4:8, 31; 9:17;21 13:9). Mtume Paulo anatumia neno kujazwa ili kusema kuwa mtu amejisalimisha kikamilifu kwa Mungu na yuko tayari kwa ajili ya mvuto wa uongozi wa Roho Mtakatifu ili kazi ya Mungu mwenyewe iweze kutimizwa katika maisha ya mtu huyo.

K**a tukijisalimisha chini ya mvuto wa ulevi wa pombe, mwenendo wetu, mazungumzo yetu, na mawazo yataathiriwa vibaya. Tunapojazwa na Roho Mtakatifu, tunasalimisha kila sehemu ya maisha yetu kwa mvuto ubadilishao wa ukiwa na matokeo kuwa mwenendo wetu, mazungumzo, na mawazo yatamwakisi Yesu.

Wakati ambapo Roho huletwa kwetu kwa njia ya kusikia kunakotokana na imani (Gal. 3:2) na anapokelewa kupitia imani (Gal. 3:14) katika ubatizo wetu (Tito 3:5, 6), tunahitaji kutafuta kujazwa na Roho Mtakatifu kila siku. Hatuwezi kutegemea uzoefu mkubwa tuliokuwa nao mwaka uliopita, au mwezi uliopita, au hata jana. Tunahitaji ujazo wa Roho Mtakatifu kila siku, kwa maana kila siku huleta changamoto zake.

Katika lugha ya Kiyunani iliyotumika kwenye Matendo 13:52, neno walijaa Roho liko katika kauli ya wakati usiotimilifu, ikidokeza juu ya tendo endelevu. Humaanisha, kwa fasiri ya moja kwa moja: “kuwa katika hali ya kuendelea (daima) kujazwa.” Kuendelea kujazwa Roho siyo tukio la wakati mmoja. Ni kitu fulani ambacho tunapaswa kukitafuta na kukipokea kila siku. Kujazwa huku kunapaswa kurudiwa ili kwamba kila kipengele cha maisha yetu kiweze kujazwa na uwepo Wake, na kwa hiyo tunawezeshwa kuishi tunavyopaswa.

Kujazwa Roho Mtakatifu haimaanishi sana tunamiliki kiasi kikubwa cha Roho bali kwamba Yeye ndiye anatumiliki sisi zaidi. Ni pale tu tunapokuwa tumemkabidhi Roho vipengele vyote vya maisha yetu kila siku ndipo anapoweza kututumia kwa utukufu Wake. “Ninatamani kuwasisitizia ukweli kuwa wale ambao Yesu amekaa moyoni mwao kwa imani, kwa hakika wamempokea Roho Mtakatifu. Kila mtu anayempokea Yesu k**a Mwokozi wake binafsi, kwa hakika anampokea Roho Mtakatifu kuwa Mshauri, Mtakasaji, Kiongozi, na Shuhuda wake.”—Ellen G. White, Manuscript Releases, vol. 14, uk. 71

22/01/2017

ALITEMBEA PAMOJA NA MUNGU

Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu. Mwanzo 5:21, 22.

Kuhusu Henoko imeandikwa kwamba aliishi miaka sitini na mitano, akazaa mwana… Katika miaka hii ya awali Henoko alikuwa amempenda na kumcha Mungu na alikuwa amezishika amri zake… Lakini baada ya kuzaliwa kwa mwana wake wa kwanza, Henoko alifikia kiwango cha juu zaidi cha uzoefu; alivutwa kuwa katika uhusiano wa karibu zaidi na Mungu. Kwa ukamilifu zaidi alitambua majukumu yake binafsi na wajibu k**a mwana wa Mungu. Alipoona upendo wa mwana kwa baba yake, usahili wake wa kutegemea ulinzi wake; alipojisikia upendo wenye shauku, wenye kina uliotoka moyoni mwake kwa ajili ya mwana wake wa kwanza, alijifunza somo la pekee la upendo wa ajabu wa Mungu kwa watu katika karama ya Mwana wake na ujasiri ambao watoto wa Mungu wanaweza kuwa nao katika Baba yao wa mbinguni. Upendo usio na mwisho, usioelezeka wa Mungu kupitia kwa Kristo ukawa suala la kutafakari mchana na usiku; na kwa hamasa yote ya nafsi yake alitafuta namna ya kudhihirisha upendo huo kwa watu alioishi kati yao.

Kwa Henoko kutembea na Mungu hakukuwa katika hali ya kuzubaa, kuota au njozi, lakini katika majukumu ya maisha ya kila siku. Hakuwa mtawa, akijitenga mwenyewe na ulimwengu kabisa; kwani alikuwa na kazi ya kufanya kwa ajili ya Mungu hapa duniani. Katika familia na katika muingiliano wake na watu, k**a mume na baba, k**a rafiki, raia, alikuwa mtumishi wa Bwana aliye thabiti asiyeyumba…. Tena kutembea huku kwa utakatifu kuliendelea kwa miaka mia tatu. Wapo Wakristo wachache ambao wangekuwa makini na wangejitoa sana k**a wangejua kwamba wanao muda mfupi wa kuishi, au kwamba kuja kwa Kristo kumekaribia sana. Lakini imani ya Henoko ilizidi kuwa na nguvu, upendo wake ulizidi kadiri karne zilivyoendelea kupita.

Yeye [Henoko] alikuwa na nia moja na Mungu… tukinia mamoja na Mungu, nia zetu zitamezwa na nia yake nasi tutafuata popote atakapotuongoza. K**a mtoto mwenye upendo anavyoweka mkono wake kwa ule wa baba yake na kutembea pamoja naye akiwa na tegemeo kamili iwe ni usiku au mchana, vivyo hivyo inawapasa wana na mabinti wa Mungu watembee pamoja na Yesu wapitapo katika furaha au huzuni.

19/01/2017

MUONGOZO WA KUJIFUNDISHA BIBLIA

Tarehe 19-01-2017

ALHAMISI

UMUHIMU WA UUNGU WAKE

Nini kingelikosekana ikiwa Roho Mtakatifu hakuwa Mungu? K**a Roho Mtakatifu siyo Mungu kamili, basi matokeo yake kwa wokovu na ibada ni ya hatari. Biblia inatuambia kuwa Roho Mtakatifu anawajibika kwa ajili ya kuwaumba upya waumini. Anakaa ndani yao na kuwajaza. Hurekebisha fikra zetu hubadilisha tabia zetu. Anao uwezo wa kufufua. Huwafanya wafuasi wa Kristo kuwa k**a alivyo Mungu: watakatifu. Ikiwa Roho Mtakatifu si Mungu, tunaweza kuwaje na hakika kwamba anaweza kufanya lolote miongoni mwa mambo haya na kuyafanya katika namna ambayo yanakubalika kwa Mungu?

Soma 1 Petro 1:2; 2 Wakorintho 13:14; na Mathayo 28:18, 19. Je, ukweli kuwa Roho Mtakatifu anatajwa pamoja na Mungu Baba, na Yesu Kristo, Mwana, katika ubatizo na baraka hutuambia nini kuhusu nafasi ya Roho Mtakatifu katika kusifu na ibada ya Mungu?

Uungu wa Roho Mtakatifu hutusaidia kuhusiana Naye kwa njia sahihi zinazomtambua kwa jinsi alivyo hasa. Uungu Wake ndilo hitaji kwa ajili ya maisha ya kiroho yaliyojikita kwa Mungu. Kanisa la Agano Jipya bila kusita humtaja Roho Mtakatifu pamoja na washirika wawili wa Utatu Mtakatifu. Roho Mtakatifu anachukua cheo na nafasi ileile katika tukio la ubatizo k**a anavyofanya Baba na Mwana. Ubatizo una umuhimu wa kina kiroho na pia ni agizo la ibada ya maana sana. Kile kilicho sahihi katika tendo la ubatizo ni sahihi vilevile kwa baraka ya kitume. Ni ombi la sifa ambapo Roho Mtakatifu anatukuzwa k**a tu ilivyo kwa Baba na Mwana. Nafsi Tatu wote wa Utatu Mtakatifu wametajwa kwa pamoja na wanathibitishwa kwa pamoja.

Roho Mtakatifu anathibitishwa k**a mlengwa wa ibada anayestahili katika Agano Jipya, siyo tu katika ubatizo na katika baraka ya kitume, lakini pia sharti la kudumu kwamba tunamtegemea kwa ajili ya mafanikio bora ya kiroho na tunapaswa kumtii k**a Mwalimu na Mtakasaji wetu wa kiungu. Je, kuna umuhimu wowote kwamba Roho Mtakatifu ni Mungu? Ndiyo, kwa kiasi kikubwa. Tunapofahamu jinsi alivyo hasa, na kutambua na kukiri Uungu Wake, tutaiheshimu kazi Yake na kumtegemea Yeye kwa ajili ya ukuaji na utakaso wetu binafsi.

Hebu fikiria kile kinachomaanishwa kuwa Roho Mtakatifu, Mungu Mwenyewe, anatenda kazi katika maisha yako. Ni ahadi gani kuu zinapatikana hapa kwa ajili yetu katika kujua kuwa ni Mungu ndiye atendaye kazi ndani yako ili kukubadilisha kuwa kile unachoweza kuwa katika Yeye? Kwa nini huu ni kweli unaoinua na kututhibitisha?

23/12/2016

*MORNING DEVOTION WITH JESUS*
🌤😄🌤😄🌤😄🌤😄🌤😄🌤

KEY TEXT:
*"Let not your heart be troubled: ye believe in God, believe also in me. In my Father’s house are many mansions: if it were not so, I would have told you. I go to prepare a place for you. And if I go and prepare a place for you, I will come again, and receive you unto myself; that where I am, there ye may be also"*
John 14:1-3.

Beloved, when Christ lay in the tomb, His disciples called to mind these words. They pondered over them, and wept because they could not fathom the meaning of them.

No faith and hope relieved the brokenhearted disciples. They could only repeat the words, _*“I will come again, and receive you unto myself"*_.

Mansions are prepared for all who have subjected themselves in obedience to the divine law. And in order that the human family might have no excuse because of Satan’s temptations, Christ became one with them. Jesus asks no more of men than that they shall follow in His footsteps.

He was the Majesty of heaven, the King of glory, but for our sakes He became poor that we through His poverty might be made rich.

What a comfort these words should be to us! Think of the work Christ is now doing in heaven, preparing mansions for His children. He wants us to prepare to dwell in these mansions.

God bless us, thank you for reading...

A m e n
❤❤❤❤❤❤❤❤❤❤❤

22/11/2016

*_MUONGOZO WA KUJIFUNDISHA BIBLIA_*

Jumanne 22-11-2016

*VIDOKEZO VYA TUMAINI*

"Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu; Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake’ ” (Ayubu 13:16). Aya hii inafuatia mara baada ya ile tuliyoisoma jana. Aya hii inathibitishaje zaidi dhana ya kwamba, pamoja na yote, Ayubu alikuwa na tumaini, na kwamba tumaini lake lilikuwa kwa Mungu?

*Hii ni aya ya kuvutia kufuatia ile iliyotangulia. Hata k**a Ayubu angekufa, hata k**a Mungu angemuua, Bado Ayubu alikuwa anamtegemea Mungu kwa wokovu. Japo kwa upande mmoja kuna wa ajabu, kwa upande mwingine inaleta maana kamili. Hata hivyo wokovu ni nini zaidi ya kukombolewa kutoka kwenye kifo? Na kifo ni nini, angalau kwa waliookolewa, zaidi ya muda mfupi wa kupumzika, usingizi wa haraka, unaofuatiwa na ufufuo wa uzima wa milele? Je, si tumaini hili la ufufuo na kuingia katika uzima wa milele ambalo watu wote wa Mungu wamekuwa wakilitumainia kwa millennia nzima iliyopita? Hili lilikuwa ni tumaini la Ayubu pia.*

_"Soma 1 Wakorintho 15:11-20. Linaelezewa tumaini gani hapa? Bila tumaini hili, kwa nini ni bora tusingekuwa na tumaini kabisa?_

Pia, baada ya uthibitisho huu mkubwa katika wokovu, Ayubu anasema “hanef haitakuja mbele zake.” Mzizi wa neno hili unamaanisha “ovu” au “-siokuwa tauwa,” neno lenye vidokezo hasi katika Kiebrania. Ayubu alikuwa anajua kwamba wokovu wake ungepatikana kwa Mungu tu, katika maisha yaliyosalimishwa kwake kwa utii wa uaminifu. Ndiyo maana mtu mwovu asiyekuwa mtauwa yaani hanef hakuwa na hilo tumaini. Bila shaka Ayubu alikuwa anaelezea alichokuwa anakielewa k**a “uhakika wake wa wokovu.”

Ingawa Ayubu alitoa dhabihu za wanyama kwa uaminifu kwa ajili ya dhambi, hatujui alikuwa anaelewa kiasi gani maana ya dhabihu hizo. Kabla ya msalaba, wafuasi wengi waaminifu wa Bwana k**a vile Ayubu, hawakuwa na uelewa kamili wa wokovu k**a tunaoweza kuwa nao sisi tunaoishi baada ya msalaba. Hata hivyo, Ayubu alikuwa anajua kiasi cha kutosha kujua kwamba tumaini lake la wokovu linapatikanakwa Bwana tu na kwamba zile dhabihu zilikuwa ni kielelezo cha vile

wokovu huo ungepatikana.

16/11/2016

*Muongozo wa kujifunza BIBLIA*

Jumatano 16-11-2016

*YATOSHA KWA SIKU …....*

```“Soma aya zifuatazo kisha ufikirie hatima ya moja kwa moja kwa wale walioelezewa katika mafungu haya. Kisha jiulize swali hili: Je, hali ilikuwa inawatendea haki kwa vipi?```
°

Ayubu 1:18-20; Mwanzo 4:8; Kutoka 12:29,30; 2Sam. 11:17; Yeremia 38:6 ; Mathayo 14:10; Waebrania 11:35-38;

Biblia inaonesha ukweli mgumu katika ulimwengu wetu ulioanguka: uovu na mateso vipo. Usomaji wa juu juu tu wa neno la Mungu, kuchomoa mafungu machache kutoka katika muktadha mzima, ndiko kunaweza kumpatia mtu wazo la kwamba maisha hapa duniani ni ya haki, na mazuri, na kwamba k**a tukiendelea kuwa waaminifu kwa Mungu, mateso hayatakuja. Uaminifu Unaweza kukuletea mema kwa sasa, lakini hiyo haina maana ya kwamba unatoa kinga isiyopenyeka dhidi ya mateso na maumivu. Mwulize Ayubu.

Katika hubiri la mlimani, Yesu alitoa hotuba nzuri juu ya kwa nini tunatakiwa kumwamini Mungu na kutokuwa na wasiwasi juu ya tutakachokula, au kunywa, au kuvaa. Na Yesu alitumia mifano kutoka katika viumbe k**a kielelezo juu ya kwa nini tunaweza kumwamini Mungu kututimizia mahitaji yetu. Kisha alitumia maneno haya maarufu: “Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake” (Mathayo 6:34).

Zingatia kiwamba, yatosha kwa siku maovu yake. Yesu hakuwa anakana kuwapo, tena kila siku, kwa uovu, (kutoka kwenye neno la Kigiriki linaloweza kumaanisha “ubaya,” “upotovu,” na “ubaya”) katika maisha yetu. Sana sana alikuwa anafanya kinyume chake. Alikuwa anakiri na kuenea na kuwapo kwa uovu katika maisha yetu ya kila siku. Asingeweza kufanya vinginevyo. K**a Bwana, alikuwa anajua zaidi kuhusu uovu duniani kuliko ye yote yule kati yetu anavyoweza kujua, nasi sote kwa hakika tunajua mengi tayari.

_*Ni nani ambaye hajaonja kidogo (au sana) wa vile maisha yanavyoweza kuwa bila haki na machungu? Kuzingatia kukiri kwa Yesu juu ya kuwapo kwa uovu kunasaidiaje kutupatia faraja na nguvu wakati wa mateso?*_

06/10/2016

MUONGOZO WA KUJIFUNZA BIBLIA

Alhamisi

06-10-2016

MAJIBU MSALABANI

```Kitabu cha Ayubu kinaibua masuala mengi. Lakini mengi kati ya masuala haya hayajibiwi humo. Tunahitaji Biblia yote. Na hata tukiwa na Biblia yote, bado “tunaona kwa kioo, kwa jinsi ya fumbo” (1 Kor. 13:12).```

🌾K**a tulivyoona jana, kwa mfano, kitabu cha Ayubu hakisemi cho chote kuhusu uasi wa Shetani ulivyoanza. Pia hakisemi kitu kuhusu Shetani atakavyoshindwa hatimaye katika pambano kuu. Kusema kweli, pamoja na mchango wake katika yote yanayotokea katika kitabu cha Ayubu—baada ya kuonekana mara mbili tu katika Ayubu (Ayubu 1:6-12, 2:1-7)—Shetani haonekani tena. Anatoweka tu, japo uharibifu aliosababisha unabaki. Sehemu ya kitabu iliyobaki wala haimtaji; badala yake, yanayofuata yote katika kitabu hicho yanamhusu Mungu, si Shetani. Na hiyo inaleta maana kwani, hatimaye, kitabu cha Ayubu ni juu ya Mungu na jinsi alivyo hasa.

🌾Mafungu yafuatayo yanasaidiaje kuelezea jambo ambalo Yesu alilifanya ambalo litaleta mwisho wa pambano kuu? Yn. 12:31, 32; Ufu. 12:10-12; Rum. 3:26; Ebr. 2:14.

🌾Pale msalabani Shetani alidhihirishwa kikamilifu kwa Ulimwengu k**a alivyo hasa, mwuaji. Waliokuwa wanamjua Yesu alipokuwa akitawala mbinguni, bila shaka walishikwa na butwaa kumwona akidhalilishwa kiasi hicho na watumishi wa Shetani. Hiyo ndiyo “hukumu” ya Shetani ambayo Yesu aliizungumzia katika Yohana 12. Pale msalabani, Mwokozi alipokufa kwa ajili ya “dhambi za ulimwengu wote” 1 (Yoh. 2:2), ndipo Mungu angeweza kusema kuwa wokovu sasa umekuja. Hapo ndipo ahadi ya Mungu, iliyoahidiwa kabla ulimwengu haujaanza (1 Tim. 1:9), ilikuwa halisi. Kwa sababu ya mauti yake kwa ajili yetu, Kristo aliweza kuwa “mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yeye amwaminiye” (Rum. 3:26). Yaani, pale msalabani, Yesu alikanusha tuhuma za ibilisi kwamba Mungu asingeweza kudumisha sheria yake (kuwa mwenye haki) na bado aweze kuwaokoa walioivunja hiyo sheria (mwenye kuwahesabia haki). Baada ya Kalvari, kuangamia kwa Shetani kulikuwa hakika.

☀ Tunawezaje kujifunza kufurahia jambo ambalo Kristo alifanya kwa ajili yetu pale msalabani, hata katikati ya majaribu tunayokabiliana nayo katika pambano kuu sasa?

Address

Gongo La Mboto/Ukonga
Dar Es Salaam

Opening Hours

Wednesday 16:00 - 18:37
Friday 16:00 - 18:30
Saturday 07:30 - 18:37

Telephone

0713431401

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mzambarauni - Seventhday Adventist Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share