Gospel Of Thomas Unveiled

Gospel Of Thomas Unveiled Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Gospel Of Thomas Unveiled, Religious organisation, DAR ES SALAAM, Dar es Salaam.

Watu wengi wanaogopa kifo. Sio kwasababu wao ni dhaifu. Hasa ni kwasababu hajielewi, hawajitambui hawajui nafsi zao.Wana...
05/10/2025

Watu wengi wanaogopa kifo. Sio kwasababu wao ni dhaifu. Hasa ni kwasababu hajielewi, hawajitambui hawajui nafsi zao.

Wanacho kijua ni milango mitano ya ufahamu ya kibinadamu (kusikia, kuona, kuhisi kuonja n.k)Wanaishi maisha yao kupitia ulimwengu wa kifizikia , ulimwengu wa vitu vya mwilini ulimwengu wa nje.

Lakini utambuzi wa kweli ama uelewa wa kweli (wa maisha) huja kwa kujifunza kuhusu nafsi yako.

Utakapo geukia ndani yako, siri zitaanza kufunuliwa.

Ni ukosefu wa maarifa na ujuzi wa nafsi zetu ndio husababisha hofu. Mara tu, utakapo jitambua hofu huyeyuka.

Na maisha hubadilika na huwa ya kushangaza yasiyo ya kawaida.

"mtakapo jitambua ndipo mtakapo julikana...na k**a hamto jitambua mtakuwamnakaa jatika umasikini (mwilini -gizani) na ninyi wenyewe ndio huo umasikini (mwili, giza)".

Ijue nafsi yako.

INJILI YA TOMASO NA MAANA YAKE ILIYO FUNULIWA.Na akasema, Yeyote anayesikia hayamaneno (na) kupata maana yake na kukubal...
04/12/2024

INJILI YA TOMASO NA MAANA YAKE ILIYO FUNULIWA.

Na akasema, Yeyote anayesikia haya
maneno (na) kupata maana yake na kukubali kuihangaika juu ya maneno yale ( hatapoteza maana/siri ya maneno yale yaliyo katika mafumbo)

2)Yesu akasema, Mtu atafutaye (maana ya maneno haya) maneno haya bila kuchoka na kuendelea kutafuta maneno ( maana) mpaka akayapata ( maana halisi)na atakapo yapata ( maana halisi ya ukweli) hato hangaishwa (hatakuwa kwenye Illusion yenye fedheha na udanganyifu wa maana nzima ya maneno yale) na atashangaa kwa hamaki kubwa- verse 58 na atakuwa mtu mwenye kuujua ukweli wa mambo yote kwani nguvu ya kukaa katika kiti cha enzi chenye mamlaka makuu ya kutawala ulimwengu vitakuwa mikononi mwake.

➖MISEMO YA SIRI YA YESU NA MAANA ZAKE KATIKA INJILI YA THOMASO.Injili ya Tomaso :- Msemo '01➖1.Haya ndiyo maneno ya siri...
03/12/2024

➖MISEMO YA SIRI YA YESU NA MAANA ZAKE KATIKA INJILI YA THOMASO.

Injili ya Tomaso :- Msemo '01

➖1.Haya ndiyo maneno ya siri aliyo sema Yesu aliye hai ambayo Didmos Yuda ambaye ni Thomaso aliyaandika.

"Naye akasema, yeyote atakaye pata tafairi ya maneno haya hataona mauti"'

➖MAANA YA MSEMO NO 1

➖Haya ndiyo maneno ya mafumbo aliyo sema Yesu, Aliye hai, na Didymos (yule pacha) Yuda, aitwaye Thomaso, aliandika.

"Akasema, yeyote asikiaye maneno haya (na) akagundua na kupata maana yake (Ya kweli na kisha kufanyia kazi na kupata uzima) hata onja mauti milele (kupotea kwa maana ya maneno haya).

➖MSEMO NAMBA 2

Yesu alisema, "Anaye tafuta na asiache kutafuta mpaka apate. Na atakapo pata atasumbuliwa, (na) atakapo sumbuliwa, atastaajabu na atatawala juu ya wote.

➖MAANA YA MSEMO NAMBA 2 (Unveilled).

Ysu alisema, Anayetafuta (maana ya maneno haya), asiache, (bali) aendelee kutafuta (kwa ajili yake) mpaka aipate (Siri). Atakapo pata (Maana, Siri) atafadhaika (atahangaika na kufanyia kazi kisha kupata uzima) (na) atastaajabu. Atakapo taabika (na) anapo staajabu, basi atashangaa, (maana) atatawala (juu ya dunia) (na) atatawala juu ya wote. Na atakapo tawala basi atapumzika (Pumziko la Sabato katika Millenia ya 7).

➖MSEMO NAMBA 3.

Yesu alisema, "Ikiwa viongozi wenu wakiwaambia, " Tazama, Ufalme uko mbinguni",!basi ndege wa angani watawatangulia. Ikiwa watakwambia, "Uko baharini; basi Samaki watafika hapo kabla yenu.

- " Bali Ufalme umo ndani yako na nje yako. Mtakapo jitambua wenyewe, ndipo mtakapo julikana, na kufahamu ya kuwa ninyi ni wana wa Baba aliye hai. Lakini ikiwa hamjitambui, basi mnaishi katika umasikini na ninyi ndiyo huo umasikini -Umasikini ulio fanyika mwili

➖MAANA YAMSEMO NAMBA 3.

Yesu alisema, wale wanao kuongoza wakikujaribu kwa dhihaka (na) kusema, "Tazama Ufalme upo angani/mbinguni (kwamba viongozi wa kidini pekee ndio wenye uwezo wa kuuelewa na kuufikia). Basi ndege wa angani (ambao ni viongozi wa kidini, walio kula mbegu au neno la mungu) wangekutangulia (wameficha funguo na kukukataza ninyi kuzifikia kwa kuwaambia mafunuo haya ya siri ni ushetani)

Na k**a pia wakikwambia upo chini ya ardhi, (kwamba unapatikana kwa kusoma sana elimu ya kidunia au kuwa mwanazuoni), (Au) upo baharini (Unapatikana chini ya mafundisho ya kanisa), (k**a ni hivyo) basi samaki wa baharini (viongozi wa kikristo) wangekupiga kwa hilo.

Badala yake ni kwamba Ufalme upo ndani yako na nje yako (Huitaji viongozi ili kuuona). Wale watakao jitambua wenyewe (uzima, nuru , mamlaka na ukweli) watajua kupitia (kujitaabisha na kufanyia kazI, na kutafuta uzima) kwamba hii ni kweli. Utakapo jitambua wewe ni nani, ndipo utakapo julikana. (katika mantiki ya kibiblia ni pale yesu atakapo kuwa wewe fungu la 108), na utatambua kuwa ninyi ndiyo wana wa Baba aliye hai (Fungu la 106).

Lakini k**a hamto jitambua, mtakuwa mnakaa katika umasikini wa (mwili) na ninyi wenyewe ni umasikini huo (mwili).

GOSPEL OF THOMAS SAYING NO 71Yesu akasema, Nitaibomoa nyumba hii, wala hakuna mtu atakayeweza kuijenga tena.MAANA👉Yesu a...
02/12/2024

GOSPEL OF THOMAS SAYING NO 71

Yesu akasema, Nitaibomoa nyumba hii, wala hakuna mtu atakayeweza kuijenga tena.

MAANA

👉Yesu alisema, Nitaibomoa nyumba hii, (Yerusalemu ya kale; Dini ya Uyahudi na Ukristo; ambayo ni mzabibu ulio pandwa mbali na Baba) na hakuna mtu atakaye weza kuijenga tena (Kwasababu Uwongo walio jengea nyumba yao -dini yao utafichuliwa kwa wakati.)

GOSPEL OF THOMAS SAYING NO. 69“Heri walioudhiwa mioyoni mwao; (kwa maana) wanamjua Baba kweli.“Heri wenye njaa,kwa maana...
02/12/2024

GOSPEL OF THOMAS SAYING NO. 69

“Heri walioudhiwa mioyoni mwao; (kwa maana)
wanamjua Baba kweli.
“Heri wenye njaa,
kwa maana tumbo la mwenye njaa litajazwa.

👉Heri wale walio teswa - walio teseka ndani yao wenyewe (kutokana na mafundisho ya uongo).Ni wale ambao wamemjua Baba kweli (Msipokee kile ambacho mwili na damu husema, bali Baba). Heri wenye njaa (Kwaajili ya aikukuu ya neno la Mungu), Kwa maana tumbo la yule anayetaka (kujua kweli, Funguo) litajazwa kwa (ujuzi wa wa siri / maarifa ya siri).

UNVEILED GOSPEL THOMAS."Kwa maana hakuna kilichofichwa (K**a funguo) ambacho hakitadhihirishwa, na hakuna kilichofichwa ...
03/03/2023

UNVEILED GOSPEL THOMAS.

"Kwa maana hakuna kilichofichwa (K**a funguo) ambacho hakitadhihirishwa, na hakuna kilichofichwa (Na waandishi, Mafarisayo na baadaye, Wakristo) ambacho hakitafichuliwa (Na Wateule)"

~Gospel Of Thomas

Address

DAR ES SALAAM
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gospel Of Thomas Unveiled posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share