Gospel Of Thomas Unveiled

Gospel Of Thomas Unveiled Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Gospel Of Thomas Unveiled, Religious organisation, DAR ES SALAAM, Dar es Salaam.

Injili ya Tomaso /Gospel Of Thomas sio kitabu cha masimulizi k**a zilivyo Injili zingine za kikanuni katika Biblia, bali...
23/02/2026

Injili ya Tomaso /Gospel Of Thomas sio kitabu cha masimulizi k**a zilivyo Injili zingine za kikanuni katika Biblia, bali ni mkusanyiko wa kauli zinazo husishwa na Yesu...ni misemo mifupi inayo mualika mtafutaji wa nuru kutazama ndani yake mwenyewe. Tofauti na mafundisho yaliyo ratibiwa na kupangiliwa na kanisa la Mwanzo, Injili ya Tomaso inamuwasilisha Yesu k**a mwalimu wa maarifa ya moja kwa moja ya kiroho yaani Gnosis, ikielezea kwa kina kwamba "Ufalme wa mbinguni" sio eneo la nje bali ni utambuzi unao tokea ndani ya Nafsi.

Moja ya kauli zake zenye uzito mkubwa ipo kwenye kauli ya :3

"Ufalme upo ndani yenu, na upo nje yenu; mtakapo jitambua ndipo mtajulikana, nanyi mtatambua ya kuwa ninyi ndiyo watoto wa Baba aliye hai. Lakini msipojitambua, mnakaa katika umasikini, na ninyi wenyewe ndio huo umasikini".

Hapa yesu anamaanisha kwamba; "Wokovu" haupatikani kupitia mafundisho rasmi ya kidini ama desturi zilizo pangiliwa za kidini, bali wokovu hupatikana kwa Kuamka kiroho, kwamba kujitambua ndiyo Ufunguo wa kutambua Uhalisia wa Kimungu.

Mtazamo huo pia unapatikana katika kanuni za "The Kybalion" na katika falsafa za Kihemetiki pale walipo sema "k**a ilivyo ndani, ndivyo ilivyo nje".

Ufalme wa Mungu haupatikani kwa kusubiri tukio la nje, haupatikani kwa kumsubiri fulani aliyepanda farasi mweupe akitokea mawinguni, Bali Ufalme unapatikana kwa kujitambua na kugundua cheche ya kimungu ambayo tayari ipo ndani ya mwanadamu ... Ufalme wa mbinguni upo ndani yenu.

Kwahiyo, Injili ya Tomaso si kwaajili ya wafuasi wa imani na desturi wanao fuata tu bila kuhoji, bali ni maandiko ya watafutaji...wale walio tayari kuvuka pazia la mazoea na dhana za juu juu, ili kutafuta ukweli ndani yao wenyewe.

"Nuru ni ishara ya Ufahamu (consiousness). Giza sio nguvu kinzani, bali ni kukosekana kwa mwanga.Mwanadamu anapo kaa kat...
23/02/2026

"Nuru ni ishara ya Ufahamu (consiousness). Giza sio nguvu kinzani, bali ni kukosekana kwa mwanga.Mwanadamu anapo kaa katika ujinga hutembea gizani; na anapopata Ufahamu husimama katika mwanga. Wenye hekima wa kale walifundisha kwamba, Ulimwengu wenyewe ni udhihirisho wa nuru ya kimungu inayoshuka katika viwango tofauti vya msongamano hadi pale inapofikia kuwa mwili/ au mada kitu chenye kuonekana kimwili. Hivyo basi kuongezeka katika Hekima ni kurejea kwenye mwangaza, Ni kusafisha fikra zetu na mawazo yetu hadi yaakisi mng'aro wa milele".

~ Manly Palmer Hall "The Secret Teachings Of All Ages"

07/02/2026
"Unapotoa kile kilicho ndani yako, kile utakacho kitoa kitakuokoa"~Injili ya Thomaso 70Watu wengi husoma maneno haya k**...
07/02/2026

"Unapotoa kile kilicho ndani yako, kile utakacho kitoa kitakuokoa"

~Injili ya Thomaso 70

Watu wengi husoma maneno haya k**a mashairi tu, lakini ukweli ni kwamba maneno haya ni ramani ya ndani ya kiroho.

Tomaso anatujuza jambo lenye uzito mkubwa:

"Ufalme" hausubiriwi kutoka mbinguni". Ufalme hujifunua kutoka ndani yetu pale tunapo kuwa na Ufahamu wa nuru ambayo tayari imepandikizwa ndani yetu.

Yesu hakuja kutupa kitu ambacho hatuna. Alikuja kutuamsha kile tulicho kisahau.

Muujiza wa kweli sio tukio la kihistoria. Muujiza wa kweli ni pale ufahamu unapo inuka ndani ya mwanadamu. ...pale nuru ya ndani inapokuwa na nguvu kuliko hofu, pale nafsi iliyo gawanyika inapo kuwa kamili katika umoja, pale "jicho moja" linapofunguka na hatimaye kuweza kuona.

Huu ndiyo ujumbe ulio hifadhiwa katika Injili ya Tomaso

Kile unacho toa kutoka ndani yako ndicho nafsi yako ya kweli---ambacho ni nuru ya kristo iliyofichwa chini ya mazoea, hofu na kusahau.

Hakuna kitu cha nje kinacho weza kuchukua nafasi yake. Hakuna taasisi inayo weza kukitoa. Hakuna ibada inayo weza kukibadilisha.

Ufalme hujitokeza pale ulimwengu wa ndani unapo funguliwa.

Na pale unapotoa kile kilicho ndani yako. Haurokuwa k**a ulivyo kuwa awali.

Address

DAR ES SALAAM
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gospel Of Thomas Unveiled posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share