03/12/2024
➖MISEMO YA SIRI YA YESU NA MAANA ZAKE KATIKA INJILI YA THOMASO.
Injili ya Tomaso :- Msemo '01
➖1.Haya ndiyo maneno ya siri aliyo sema Yesu aliye hai ambayo Didmos Yuda ambaye ni Thomaso aliyaandika.
"Naye akasema, yeyote atakaye pata tafairi ya maneno haya hataona mauti"'
➖MAANA YA MSEMO NO 1
➖Haya ndiyo maneno ya mafumbo aliyo sema Yesu, Aliye hai, na Didymos (yule pacha) Yuda, aitwaye Thomaso, aliandika.
"Akasema, yeyote asikiaye maneno haya (na) akagundua na kupata maana yake (Ya kweli na kisha kufanyia kazi na kupata uzima) hata onja mauti milele (kupotea kwa maana ya maneno haya).
➖MSEMO NAMBA 2
Yesu alisema, "Anaye tafuta na asiache kutafuta mpaka apate. Na atakapo pata atasumbuliwa, (na) atakapo sumbuliwa, atastaajabu na atatawala juu ya wote.
➖MAANA YA MSEMO NAMBA 2 (Unveilled).
Ysu alisema, Anayetafuta (maana ya maneno haya), asiache, (bali) aendelee kutafuta (kwa ajili yake) mpaka aipate (Siri). Atakapo pata (Maana, Siri) atafadhaika (atahangaika na kufanyia kazi kisha kupata uzima) (na) atastaajabu. Atakapo taabika (na) anapo staajabu, basi atashangaa, (maana) atatawala (juu ya dunia) (na) atatawala juu ya wote. Na atakapo tawala basi atapumzika (Pumziko la Sabato katika Millenia ya 7).
➖MSEMO NAMBA 3.
Yesu alisema, "Ikiwa viongozi wenu wakiwaambia, " Tazama, Ufalme uko mbinguni",!basi ndege wa angani watawatangulia. Ikiwa watakwambia, "Uko baharini; basi Samaki watafika hapo kabla yenu.
- " Bali Ufalme umo ndani yako na nje yako. Mtakapo jitambua wenyewe, ndipo mtakapo julikana, na kufahamu ya kuwa ninyi ni wana wa Baba aliye hai. Lakini ikiwa hamjitambui, basi mnaishi katika umasikini na ninyi ndiyo huo umasikini -Umasikini ulio fanyika mwili
➖MAANA YAMSEMO NAMBA 3.
Yesu alisema, wale wanao kuongoza wakikujaribu kwa dhihaka (na) kusema, "Tazama Ufalme upo angani/mbinguni (kwamba viongozi wa kidini pekee ndio wenye uwezo wa kuuelewa na kuufikia). Basi ndege wa angani (ambao ni viongozi wa kidini, walio kula mbegu au neno la mungu) wangekutangulia (wameficha funguo na kukukataza ninyi kuzifikia kwa kuwaambia mafunuo haya ya siri ni ushetani)
Na k**a pia wakikwambia upo chini ya ardhi, (kwamba unapatikana kwa kusoma sana elimu ya kidunia au kuwa mwanazuoni), (Au) upo baharini (Unapatikana chini ya mafundisho ya kanisa), (k**a ni hivyo) basi samaki wa baharini (viongozi wa kikristo) wangekupiga kwa hilo.
Badala yake ni kwamba Ufalme upo ndani yako na nje yako (Huitaji viongozi ili kuuona). Wale watakao jitambua wenyewe (uzima, nuru , mamlaka na ukweli) watajua kupitia (kujitaabisha na kufanyia kazI, na kutafuta uzima) kwamba hii ni kweli. Utakapo jitambua wewe ni nani, ndipo utakapo julikana. (katika mantiki ya kibiblia ni pale yesu atakapo kuwa wewe fungu la 108), na utatambua kuwa ninyi ndiyo wana wa Baba aliye hai (Fungu la 106).
Lakini k**a hamto jitambua, mtakuwa mnakaa katika umasikini wa (mwili) na ninyi wenyewe ni umasikini huo (mwili).