29/07/2025
JE UNAJUA KUWA MUMGU ANAKUPENDA?
Biblia katika Injili ya Yohana inasema " Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milile"
+ Mungu ndiye aliyeumba ulimwengu huu ambamo wewe unakaa na kufanya shughuli za maisha yako.
+ Kusudi la Mungu la kukupatia zawadi hii yaani ulimwengu ni ili awe na ushirika na wewe, awe Mungu na Baba kwako nawe uwe mwana wake wa kiume au wa k**e.
Biblia katika Waraka kwa Warumi 5:12 inasema " Kwa hiyo k**a kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.
+ Mtu wa kwanza kuishi hapa ulimwenguni( Adamu) alimkosea Mungu kwa kuasi amri yake. Akavunja ushirika na Mungu.
+ Binadamu wote wamezaliwa kutokana na Adamu aliyemwasi Mungu kwa kutenda dhambi na kwa sababu hiyo wako dhambini, hawana ushirika na Mungu. Hata wewe uko dhambini.
+ Mungu ni Mtakatifu sana na mwenye haki anachukia dhambi, na hivyo atamhukumu mwanadamu mwenye dhambi kwa kumtupa katika ziwa la moto wa milele yaani Jehanamu.
+ Lakini Mumgu pia ni mwenye upendo na ni mwenye huruma. Kwa kumpenda na kumhurumia Mwanadamu alimtuma Yesu Kristo ili aje azichukue dhambi za Mwanadamu ili kurudisha ushirika na Mungu kwa kujitoa kufa msalabani badala ya mwanadamu.
Biblia katika waraka kwa Warumi 10:9 inasema " Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka
+ Kwa kumkiri Yesu kuwa Bwana na mwokozi wako( kuwa dhabihu ya dhambi zako); Utasamehewa dhambi zako zote, utasafishwa na udhalimu wako wote na kufanywa Mwana wa Mungu. Ushirika wako na Mungu muumba wako utarudishwa tena.Utaokoka na madhara ya dhambi.
K**a unapemda kuitikia upendo huu wa ajabu wa Mungu, omba ombi hili kwa kumaanisha: Baba Mungu nakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi. Napokea upendo wako. Namkiri Yesu kuwa Bwana wangu na Mwokozi wangu. Unisamehe dhambi zangu zote. Kwa Jina la Yesu unifanye kuwa mtoto wako, Amina.
Kwa msaada zaidi wasiliana nami kwa simu namba 0754290177 au Fika Kanisa la TAG Kibo Spiritual Centre.