05/03/2018
MARANATHA RECONCILIATION CHURCH
Maombi 4 – 11 Machi, 2018
Ungana na maelfu ya waamini kumshukuru Mungu kwa uaminifu wake kwa kukulinda, kukulisha kiroho na kimwili, na kukutana na mahitaji yako, katika kipindi cha mwezi Februari.
Maana za tarakimu katika utamaduni wa Kiebrania, 18 ni tarakimu za hukumu na mwanzo mpya. Tumwombe Mungu ili hukumu yake iangukie mifumo yote inayolenga kuharibu jamii kiroho na kimwili, pia tuombe ili kianze kipindi kipya cha mafanikio, kwa watoto wa Mungu.
Unabii wa Chuck Pierce unaonyesha kuwa huu ni mwaka wa malango, milango, vita na malaika. Tuombe ili malango yanayozuia baraka za watoto wa Mungu yaachie mwaka huu, malaika wawafungulie watu wa Mungu milango ya kutenda mambo makuu na uwe mwisho wa vita zilizokuwa zikiwasumbua waamini kwa muda mrefu.
Neno linasema tukimpenda Mungu tutatii amri zake. Kutokana na maneno haya, ni wazi kutokutii maagizo yanayotolewa na wachungaji, ni ishara ya kuporomoka kwa kiwango cha upendo wa waamini, kwa wachungaji wao. Inua kizazi kipya, cha waamini wenye kiu ya kuwapenda na kuwaheshimu wachungaji wao.
Ombea ustawi wa kiroho na kimwili, kwa Waafrika wanaoishi nje ya bara hili, wanaotegemeza kazi ya Mungu barani Afrika.
Msalaba unatutenga na dhambi, ubatizo wa Roho Mtakatifu unatutenga na dini zilizokufa, na udhihirisho wa karama za rohoni unatuwezesha kuzifanya kazi zilizofanywa na Yesu Kristo. Tufungulie kiu ndani ya kanisa, ya kuona udhihirisho wa karama za rohoni.
Omba kuwe na mabadiliko ya kisiasa yatakayoruhusu uhuru wa kuabudu, katika mataifa kumi yanayoongoza kwa kutesa Wakristo. Mataifa haya ni Korea kaskazini, Afghanistan, Somalia, Sudan, Pakistan, Eritrea, Libya, Iraqi, Yemen na Iran.
Kulingana na takwimu za kiuchumi, nchi 9 kati ya 10 maskini kuliko zote duniani, ziko barani Afrika. Nchi hizi ni Afrika ya kati, DRC, Burundi, Liberia, Niger, Malawi, Msumbiji, Eritrea na Madagasca. Tuwaombee waamini wa mataifa haya, ustawi na mafanikio ya kiuchumi.
Wakati Wakristo wakilaumu magaidi kwa kufunza watoto wao kuua, nao wamekuwa wakifanya hivyo bila kujua, kwa kuwanunulia watoto wao ‘video games’ za vita, mauaji na uchawi. Tuwaombee waamini watambue hili kuzuia uchafu huu kwa watoto wao.
TuombeE kuachiliwa kwa waamini waliofungwa katika nchi zisizokubali Ukristo. Ni pamoja na Shafgat Emanuel na mkewe Shagfuta Kausar, waliokamatwa tarehe 20/7/ 2013 na kuhukumiwa kuuawa kwa madai ya kumkufuru mtume Muhammad.
Ingawa bado wako watumishi wa k**e wanaowika duniani, bado hawajapatikana wanawake wa kuvaa viatu vya Catheren Khulman na Maria Woodworth-Etter. Tumwombe Mungu ili ainue jeshi la wanawake wenye kiu ya kutumiwa na Mungu, kwa kiwango cha kustaajabisha.
Tufungulie kiu ya kutafuta uso wa Mungu, kwa waamini wote waliookoka katika juma la tarehe 25/2 – 4/3.
K**a unafurahishwa na huduma yetu ya kufikisha Injili vijijini, waweza kutoa sadaka yako katika akaunti ya: Maranatha Reconciliation church, CRDB Holland House Branch, no 1022645600