Efatha Ushindi-Kinyerezi

Efatha Ushindi-Kinyerezi Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Efatha Ushindi-Kinyerezi, Religious organisation, Dar es Salaam.

Efatha Church is a Spiritual Organization officially Aimed:-
To heal humanity from diseases and infirmities.To deliver humanity from body, soul and Spiritual bounds of evils.To prepare the church for the end-times and rupture.

26/07/2026
2 Wafalme 6:15-17 "Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi ...
26/07/2026

2 Wafalme 6:15-17 "Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao. Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote."

Kuna tofauti kati ya kuangalia na kuona watu wengi wanaangalia hawaoni, macho ya rohoni huona sawasawa unahitaji macho ya rohoni. Mungu akifungua macho yako utaona mambo makubwa yanatokea, Mungu huwaona watu tofauti na sisi tunavyowaona.

1 Samweli 16:7 "Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii k**a binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo."

tusiwahukumu watu kwa tuwaonavyo leo kwa sababu macho yaliyofunguliwa huona maono. Hakuna chochote kinachoenda pasipo maono, pia ukikosa maono unachoka haraka, ukiwa na kiburi, dhambi, wivu wa kiroho, mazoea kukosa muda wa kukaa mbele za Mungu inakupasa uvunje mapenzi yako na ya Mungu yapate kujengwa.

©️ MTUME SUZAN MUNGI - KANISA LA EFATHA KINYEREZI.

TENZI 8989. KWA KALVARI1.Muda mwingi nilipotea,Sikufahamu msalaba,Wala aliyenifilia,Kwa Kalvari. Rehema bure na neema,Sa...
26/07/2026

TENZI 89
89. KWA KALVARI

1.Muda mwingi nilipotea,
Sikufahamu msalaba,
Wala aliyenifilia,
Kwa Kalvari.

Rehema bure na neema,
Samaha nalo nilipewa,
Ndipo aliponifungua
Kwa Kalvari.

2.Kwa neno lake Bwana Mungu,
Nilijiona mimi mwovu,
Nikageuka na kutubu,
Kwa Kalvari.

Akili yako ikibadilika kuna jambo hutokea, akili yako ikifunguka ufahamu wako unafunguka. Tatizo unaloliona kwako ni dogo sana kwa Mungu, wana wa Ibilisi wanajua hasa kuutumia ulimwengu wa roho, hivyo wana wa mungu inatupasa tuutumie kwa bidii ulimwengu wa roho ili tumshinde shetani unachohitaji leo ni uamuzi wako wewe mwenyewe.

Ukombozi unaanzia kwa mtu binafsi inakupasa uelewe, sheteni huwa haogopi una upako kiasi gani bali huogopa Neno maana Neno ni silaha, ukitambua nafasi yako ya kuwa umezaliwa kwa sura na mfano wa Mungu utaamrisha mambo yatatokea

Warumi 12:2 "Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu."

Kwanini Mungu anataka tufunguliwe? Huweza kufanya mapenzi ya Mungu k**a macho yako yamefungwa na masikio yako yamefungwa. Kufanya mapenzi ya Mungu sio wingi wa sadaka zako au kuhubili kwako bali ni kutimiza kusudi la Mungu.

Mafanikio ya mtu hayapimwi kwa ukubwa wa chochote bali Mungu anapima kwa mapenzi yake, usipojua lile kusudi ambalo Mungu aliweka ndani yako huwezi timiza Mapenzi ya Mungu. ukishafanya mapenzi ya mungu hakuna utakaloomba asifanye, unaweza ukawa na wito au karama lakini usitimize mapenzi ya Mungu. Yona aliitwa lakini alikimbia mapenzi ya mungu jua nafasi yako na ukae katika nafasi yako. Ukifanya upya kia zenu, vita kubwa haipo nje bali ipo ndani yako, akili yako ikipona yale unayoyaona mbali yanakuwa karibu.

Macho yako yakifunguliwa utaona kila kitu kinaenda kwa wakati. Kwanini hujainuliwa ni kwa sababu bado hujafanya mapenzi ya Mungu. Mungu hubariki pale anapoona una jukumu unafanya.

Isaya 55:8-9 "Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.Kwa maana k**a vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu."

Ukifunguliwa akili utaona fursa ambazo hujawahi kuziona, ukifunguliwa akili utaona yaliyo magumu yanakuwa mepesi.

©️ MTUME SUZAN MUNGI - KANISA LA EFATHA KINYEREZI.

MATOLEO 1 Samweli 7:7-9 "Hata Wafilisti waliposikia ya kuwa wana wa Israeli wamekusanyika huko Mispa, mashehe wa Wafilis...
26/07/2026

MATOLEO
1 Samweli 7:7-9 "Hata Wafilisti waliposikia ya kuwa wana wa Israeli wamekusanyika huko Mispa, mashehe wa Wafilisti walipanda juu ili kupigana na Israeli. Nao wana wa Israeli waliposikia, wakawaogopa Wafilisti. Wana wa Israeli wakamwambia Samweli, Usiache kumlilia Bwana, Mungu wetu, kwa ajili yetu, kwamba atuokoe na mikono ya Wafilisti. Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa nzima; Samweli akamlilia Bwana kwa ajili ya Israeli; Bwana akamwitikia"

Wana wa Israeli walivyokusanyika , maadui waliwaona wamekusanyika kwa ajili ya Bwana, pasipo silaaa lakini walihisi ni rahisi kuwavamia,bali samweli alitoa sadaka nzima na kuiteketeza ndipo Bwana alituma ngurumo wakapigwa katikati ya vita toa sadaka muamini Mungu. Pia unapotoa sadaka yako Mungu anakutetea kwa kila changamoto unayopitia.

©️ MTUMISHI CAROLINE KIWONYI - KANISA LA EFATHA KINYEREZI.

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 26/07/2026 KANISA LA EFATHA MKOA Wa USHINDI, DAR ES SALAAM TANZANIA Tenzi No 241.Tangu siku ...
26/07/2026

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 26/07/2026 KANISA LA EFATHA MKOA Wa USHINDI, DAR ES SALAAM TANZANIA

Tenzi No 24

1.Tangu siku hiyo aliponijia,
Akae moyoni mwangu,
Sina giza tena, ila mwanga pia
Kwa Yesu mwokozi wangu.

Amani moyoni mwangu,
kwa Yesu, Mwokozi wangu;
Sina shaka kamwe,
Kwa sababu yeye,
Yu nami moyoni mwangu.

2.Sina haja tena, ya kutanga-tanga,
Ndiye kiongozi wangu.
Dhambi zangu zote zimeondolewa,
Na Yesu, Mwanawe Mungu.

3.Matumaini yangu ni ya hakika,
Katika Mwokozi wangu.
Hofu zangu na hamu zimeondoka,
kwa kuwa ninaye Yesu.

Zaburi 51:1-4 "Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu.Unioshe kabisa na uovu wangu, Unitakase dhambi zangu. Maana nimejua mimi makosa yangu Na dhambi yangu i mbele yangu daima. Nimekutenda dhambi Wewe peke yako, Na kufanya maovu mbele za macho yako. Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo, Na kuwa safi utoapo hukumu."

Tenzi No 157

1.Kijito cha utakaso
ni damu ya Yesu,
Bwana anao uwezo
kunipa wokovu

Kijito cha utakaso,
Nizame kuoshwa humo
Namsifu Bwana kwa hiyo
Nimepata utakaso

2.Viumbe vipya naona;
damu ina nguvu,
imeharibu uovu
ulionidhulumu

Zaburi 24:1-10 "Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mito ya maji aliithibitisha. Ni nani atakayepanda katika mlima wa Bwana? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila. Atapokea baraka kwa Bwana, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Inukeni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.Ni nani Mfalme wa utukufu? Bwana mwenye nguvu, hodari, Bwana hodari wa vita. Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Naam, viinueni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia. Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Bwana wa majeshi, Yeye ndiye Mfalme wa utukufu."

©️ MTUME MAGRETH ILOMO - KANISA LA EFATHA MKOA WA USHINDI.

BADA MAALUMU YA VIONGOZI MKOA WA USHINDI/DAR ES SALAAM, TANZANIA.UMUHIMU WA KULINDA KONDOOLuka 15:4  "Ni nani kwenu, mwe...
25/07/2026

BADA MAALUMU YA VIONGOZI MKOA WA USHINDI/DAR ES SALAAM, TANZANIA.

UMUHIMU WA KULINDA KONDOO

Luka 15:4 "Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?"

Unaweza ukaambiwa wewe ufike saa tatu lakini ukifika unaweza ukakuta shetani tayari ameshakalia kiti chako, huwezi ukaitwa kondoo k**a bado hujaingia kwenye mfumo wa kanisa.

Ezekieli 34:2-6 "Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo. Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala. Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika. Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta."

Kuangalia kondoo ni wito mkuu, pia ni kazi yetu mimi na wewe kuwaponya wenye maradhi, kuwarudisha waliorudi nyuma na kuwatafuta waliopotea. Mbinu na lugha yako unayotumia ndiyo inayoweza kusababisha watu wabaki au wapotee. Mungu anataka vingozi wawe na upendo, huruma na kuwajali wale wanao waongoza.

Marko 9:42 "Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini."

Siku zote mungu anakutumia wewe umrudishe mtu mmoja, uwe ni mkakati wetu kumrudisha mtu aliyerudi nyuma ili asikose mbingu, maana thawabu yako iko kwa Bwana. Tusiwahukumu wale waliorudi nyuma bali tuwafuate na kuwarudisha kanisani kwa upendo. Mungu anataka tubebane sisi kwa sisi.

©️ MTUME SUZAN MUNGI - KANISA LA EFATHA MKOA WA USHINDI.

25/07/2026
Mapokezi ya mitume wa kanda, ya mikoa ya Dar es salaam na Pwani Wakiwa wamewasili Kwa ajili ya ibada maaulumu Ya viongoz...
25/07/2026

Mapokezi ya mitume wa kanda, ya mikoa ya Dar es salaam na Pwani Wakiwa wamewasili Kwa ajili ya ibada maaulumu Ya viongozi wa Kanisa la Efatha Mkoa wa Ushindi

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 19/07/2026 KANISA LA EFATHA KINYEREZI MKOA WA USHINDI.Tenzi No 125: ATI TWONANE MTONI?1.Ati ...
19/07/2026

IBADA YA JUMAPILI YA TAREHE 19/07/2026 KANISA LA EFATHA KINYEREZI MKOA WA USHINDI.

Tenzi No 125: ATI TWONANE MTONI?
1.Ati twonane mtoni?
Maji mazuri ya Mbingu;
Yanatokea mwangani,
Penye kiti cha Mungu.

Naam, twonane mtoni!
Watakatifu, kwenu ni mtoni!
Tutakutanika mtoni
Penye kiti cha Mungu.

2.Tukitembea mtoni
Na Yesu mchunga wetu
Daima tu ibadani
Usoni pake kwetu.

3.Kwang’ara sana mtoni
Cha Mwokozi ni kioo,
Milele hatuachani,
Tumsifu kwa nyimbo.

Zaburi 42:1-4 "K**a ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu. Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu? Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako. Nayakumbuka hayo nikiweka wazi nafsi yangu ndani yangu, Jinsi nilivyokuwa nikienda na mkutano, Na kuwaongoza nyumbani kwa Mungu, Kwa sauti ya furaha na kusifu, mkutano wa sikukuu."

©️ Mchungaji Edwin Masamu Kanisa la Efatha Kinyerezi.

Address

Dar Es Salaam
5537+Q78,DARESSALAAM

Opening Hours

Monday 08:30 - 17:00
Tuesday 08:30 - 16:00
Wednesday 08:30 - 17:00
Thursday 08:30 - 17:00
Friday 08:30 - 17:00
Saturday 08:30 - 12:00
Sunday 08:00 - 16:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Ushindi-Kinyerezi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share