An Abdulrazzaq

An Abdulrazzaq FannaniGPT

πŸ“ Story & Poem Writer. (Composer)
πŸ“Έ Video Maker & Editor.
πŸ–ΌοΈ Logo Creator.
πŸ“Ί Video Director.

πŸ•‹BASED ON ISLAMIC LAWS.

29/05/2026
Mambo ya Mapenzi
25/05/2026

Mambo ya Mapenzi

πŸ’πŸ’πŸ’–πŸ’–πŸ’πŸ’πŸ’–πŸ’–
24/05/2026

πŸ’πŸ’πŸ’–πŸ’–πŸ’πŸ’πŸ’–πŸ’–

22/05/2026

MANENO YA WATU SUMU οΏ½οΏ½

22/05/2026

UMEOA... AU UNA MKE

πŸ‘οΈβ€πŸ—¨οΈ HAMUONI NINIπŸ‘οΈβ€πŸ—¨οΈ1.Mbona inafahamika, mambo yalipofikia. Mauaji na kuteka, kila siku hutokea. Hukuti zikiandika, r...
21/05/2026

πŸ‘οΈβ€πŸ—¨οΈ HAMUONI NINIπŸ‘οΈβ€πŸ—¨οΈ

1.
Mbona inafahamika, mambo yalipofikia.
Mauaji na kuteka, kila siku hutokea.
Hukuti zikiandika, ripoti sosho midia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

2.
Mnaona kwa hakika, kwa hakika munajua.
Lakini mwatetemeka, tarifa hizi kutoa.
Ni woga umewashika, tunajua munajua.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

3.
Vyombo vyetu vya habari, ni vyombo vya kunawia.
Vyaficha ule ukweli, ama kuunyamazia.
Raia ndo wako mbali, japo kuzungumzia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

4.
Mekubali kukubali, watu kutukanyagia.
Nao wakanyaga kweli, bila kutuhurumia.
Kwa nyundo na misumari, gonga na kushindilia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

5.
Tumebakiwa na hofu, amani imekimbia.
Vioo na maarufu, meshindwa kutusemea.
Hata sisi madhaifu, tukisema watuua.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

6.
Nchi mejaa machafu, sote tunashuhudia.
Mashehe na masharifu, ni kimya wametulia.
Mapadri na maskofu, k**a mnavyosikia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

7.
Nasi umoja hatuna, tukiwa k**a raia.
Neno moja la HAPANA, twashindwa kulitetea.
Kimya cha kutokunena, twazidi kuangamia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

8.
Mekuwa na woga sana, haki kuipigania.
Hayo tunayoyaona, twabaki kuangalia.
Kunao wengi vijana, lakini bora bamia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?

9.
(πŸ₯΅πŸ₯΅πŸ₯΅πŸ₯΅πŸ₯΅)
(😨😨😨😨😨)
(πŸˆβ€β¬›πŸˆβ€β¬›πŸˆβ€β¬›πŸˆβ€β¬›πŸˆβ€β¬›)
(😭😭😭😭😭)
(🀐🀐🀐🀐🀐)

10.
Mungu anipe hekima, kwenye kwangu kuongea.
Ila taifa lazama, na sisi tunazamia.
Naiombea salama nchi yangu Tanzania.
Naiombea salama, nchi yetu Tanzania.

🟩🟩🟩🟩
🟩🟩🟩🟩
🟨🟨🟨🟨
⬛⬛⬛⬛
⬛⬛⬛⬛
🟨🟨🟨🟨
🟦🟦🟦🟦
🟦🟦🟦🟦

NAAAM
08/05/2026

NAAAM

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
11101

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when An Abdulrazzaq posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to An Abdulrazzaq:

Share