21/05/2026
ποΈβπ¨οΈ HAMUONI NINIποΈβπ¨οΈ
1.
Mbona inafahamika, mambo yalipofikia.
Mauaji na kuteka, kila siku hutokea.
Hukuti zikiandika, ripoti sosho midia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
2.
Mnaona kwa hakika, kwa hakika munajua.
Lakini mwatetemeka, tarifa hizi kutoa.
Ni woga umewashika, tunajua munajua.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
3.
Vyombo vyetu vya habari, ni vyombo vya kunawia.
Vyaficha ule ukweli, ama kuunyamazia.
Raia ndo wako mbali, japo kuzungumzia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
4.
Mekubali kukubali, watu kutukanyagia.
Nao wakanyaga kweli, bila kutuhurumia.
Kwa nyundo na misumari, gonga na kushindilia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
5.
Tumebakiwa na hofu, amani imekimbia.
Vioo na maarufu, meshindwa kutusemea.
Hata sisi madhaifu, tukisema watuua.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
6.
Nchi mejaa machafu, sote tunashuhudia.
Mashehe na masharifu, ni kimya wametulia.
Mapadri na maskofu, k**a mnavyosikia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
7.
Nasi umoja hatuna, tukiwa k**a raia.
Neno moja la HAPANA, twashindwa kulitetea.
Kimya cha kutokunena, twazidi kuangamia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
8.
Mekuwa na woga sana, haki kuipigania.
Hayo tunayoyaona, twabaki kuangalia.
Kunao wengi vijana, lakini bora bamia.
IKIWA SISI TWAONA, NINYI HAMUONI NINI..?
9.
(π₯΅π₯΅π₯΅π₯΅π₯΅)
(π¨π¨π¨π¨π¨)
(πββ¬πββ¬πββ¬πββ¬πββ¬)
(πππππ)
(π€π€π€π€π€)
10.
Mungu anipe hekima, kwenye kwangu kuongea.
Ila taifa lazama, na sisi tunazamia.
Naiombea salama nchi yangu Tanzania.
Naiombea salama, nchi yetu Tanzania.
π©π©π©π©
π©π©π©π©
π¨π¨π¨π¨
β¬β¬β¬β¬
β¬β¬β¬β¬
π¨π¨π¨π¨
π¦π¦π¦π¦
π¦π¦π¦π¦