13/07/2025
JE UMEKUA MPWEKE, JE UMETENGWA NA ULIO WAAMINI SANA.?
Huwa inaumiza sana pale unapopita katika mazingira magumu na unapohitaji msaada unakuja kugundua hakuna mtu upande wako angalau wa kukupa bega wakati
Wakulia kwako, ingawa hapo awali unakuta ulikuwa na watu wengi sana ambao walikua pamoja nawe wakati neema imekutembelea!! Unakuta kipindi hicho kila alikua anakuambi yuko pamoja na wewe, lakini baada ya magumu kukufika wote wametawanyika, maumivu yako sio yao tena ingawa raha zako walitaka ziwe zao.
USIOGOPE mwanangu, waliokuacha acha waondoke
“WAKATI MWINGINE MUNGU HUKUONDOLEA MARAFIKI ILI UMTEGEMEE YEYE PEKEE, WAKATI MWINGINE UWEZO WA KUKABILIANA NA HALI YA KUTENGWA KWAKO UTAKUFUNDISHA KUUJUA MWELEKEO WAKO”
Sikia Mungu alipotaka kumbariki Ibrahimu alimtenganisha na watu wake wote waliomfanya awe kwenye comfort zone
MWANZO 12:1-2
BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;
Wakati mwingine ili uweze kufanikiwa katika maisha lazima baadhi ya watu waondoke katika maisha yako, so usiwalalamikie wanaokuacha.
Pastor Sitta Majani
+255 692 950 285