Pro-life Tanzania- Human Life International Tanzania

Pro-life Tanzania- Human Life International Tanzania UHAI:ZAWADI YA MUNGU,MALI YA MUNGU-tupokee,tutunze,tulinde na tudumishe

"Familia ni msingi wa utu; mlee mtoto katika upendo na heshima, kwani huo ndio utajiri namba moja unaojaza roho na kuach...
23/04/2026

"Familia ni msingi wa utu; mlee mtoto katika upendo na heshima, kwani huo ndio utajiri namba moja unaojaza roho na kuacha alama isiyofutika duniani."

✍️Padre Vedastus Machibula

21/04/2026
Jukumu namba moja la malezi ni la wazazi wenyewe na wengine ni wasaidizi tu; ni lazima mtoto ajifunze kupenda, kuheshimu...
21/04/2026

Jukumu namba moja la malezi ni la wazazi wenyewe na wengine ni wasaidizi tu; ni lazima mtoto ajifunze kupenda, kuheshimu utu wa kila mtu, kufanya kazi kwa bidii, na kuwa na msimamo wa kukataa kila ubaya ndani ya familia, hasa kutoka kwa wazazi.

✍️ Padre Vedastus Machibula

"Malezi bora si kumpa mtoto kila anachotaka, bali ni kumjengea uwezo wa kusimama imara hata pale anapokosa kila kitu, ak...
16/04/2026

"Malezi bora si kumpa mtoto kila anachotaka, bali ni kumjengea uwezo wa kusimama imara hata pale anapokosa kila kitu, akijua kuwa utu wake ndio hazina yake kuu. "


✍️Padre Vedastus Machibula

*TUJIFUNZE KUTAMBUA MPANGO WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU*Wana uhai kote nchini na watu wenye mapenzi mema wameaswa kujifun...
25/03/2026

*TUJIFUNZE KUTAMBUA MPANGO WA MUNGU KATIKA MAISHA YETU*

Wana uhai kote nchini na watu wenye mapenzi mema wameaswa kujifunza kutambua mpango sa Mungu katika maisha yetu

Wito huu umetolewa na Padre Gaspar Shekigenda Mkurugenzi wa Litrujia Jimbo katoliki la Tanga na Paroko wa Parokia ya Moyo Mtakatifu wa Yesu MKUZI katika adhimisho la Misa takatifu sherehe ya Kupashwa habari Bikira maria Machi 26,2026

Padre Gaspar Shekigenda amesema Mama Bikira Maria na Malaika Gabriel ni alama ya mfuasi mwaminifu wa Mungu anayepokea na kukubali mpango wa Mungu katika maisha yake
Kwa NDIO ya Bikira maria,tumempata mkombozi,aliyekuja kutukomboa baadhi ya dhambi Adamu wa Kwanza,Kristo Adamu WA pili mshindi anakuja kutukomboa katika utumwa wa dhambi

Ameongezea Kwa kuwaasa Tujifunze kutambua mpango wa Mungu katika maisha yetu, na zaidi sana katika kuutunza uhai. Wakina Mama waige mfano wa Maria aliyekubali mpango wa Mungu kupitia ujumbe wa malaika Gabriel sote tunaalikwa kuupokea mpango wa Mungu katika maisha yetu

Sherehe ya Bikira Maria kupashwa habari na Malaika kwamba, atakuwa ni Mama wa Mungu iwe ni fursa kwa waamini na watu wot...
25/03/2026

Sherehe ya Bikira Maria kupashwa habari na Malaika kwamba, atakuwa ni Mama wa Mungu iwe ni fursa kwa waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuiga mfano wa maisha na utume wa Bikira Maria kwa kujisadaka bila ya kujibakiza kwa ajili ya kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha
Tuwaombe wajawazito wote waweze kulinda zawadi hiyo waliyobarikiwa Amina 🙏

Nyuma ya kila utoaji mimba kuna sababu ambayo imejificha; maisha magumu, hofu au hata malengo binafsi. Ishinde hofu yako...
17/03/2026

Nyuma ya kila utoaji mimba kuna sababu ambayo imejificha; maisha magumu, hofu au hata malengo binafsi. Ishinde hofu yako, zikabili changamoto. Yawezekana huyo mtoto unayetaka kumuua ndiyo njia, ndio tumaini, na ndiye mbeba maono ya kesho yako Usiizike kesho yako mapema

✍️ Padre Vedastus Machibula

Vijana wametakiwa kujenga msingi imara, maadili huku wakisimama katika kutetea uhai kwa mustakabali mwema wa maisha yao ...
06/03/2026

Vijana wametakiwa kujenga msingi imara, maadili huku wakisimama katika kutetea uhai kwa mustakabali mwema wa maisha yao ya baadaye.

Wito huo umetolewa wakati Shirika la Kutetea Uhai Tanzania (Pro-Life) lilipoendesha semina ya mafunzo kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Carmelite iliyopo Mbezi jijini Dar es Salaam.

Semina hiyo imelenga kuwajengea vijana uelewa juu ya thamani ya uhai na umuhimu wa usafi wa moyo katika maisha yao.

Katika semina hiyo mada mbalimbali zilitolewa k**a mwongozo kwa wanafunzi, zikiwemo Mwanzo wa Uhai, Vitisho Dhidi ya Uhai pamoja na Maadili na Mwana Uhai, kwa lengo la kuwasaidia vijana kuelewa wajibu wao katika kulinda na kuthamini uhai.

Akitoa mada ya “Mwana Uhai”, mkufunzi Antony Lihepa amewahimiza wanafunzi hao kujijengea msingi bora wa maisha yao ya sasa na ya baadaye.

Amesema vijana wanapaswa kusimamia yale mema ambayo Mwenyezi Mungu ameweka ndani yao, na kuwa watetezi wa uhai katika jamii wanamoishi.

Aidha amesisitiza kuwa Mwana Uhai wa kweli anapaswa kuwa na hofu ya Mungu na kuishi kwa kuzingatia maadili mema.

Lihepa pia amewakumbusha wanafunzi hao kuwa tabia wanazojijenga leo ndizo zitakazounda maisha yao ya kesho, hivyo ni muhimu kujenga tabia njema ili kuwa watu bora na wenye mchango chanya kwa jamii.

Kwa upande wake Grace Shayo ambaye alitoa mada ya Safari ya Mtoto tangu kutungwa mimba hadi kuzaliwa, amewataka Wanafunzi hao kujitunza na kamwe wasikubali kuharibu utu wao wa ndani.

✍️Frida Manga

MATUKIO KATIKA PICHA - PUGU DSM▪︎ Adhimisho la sadaka ya Misa Takatifu ya kumuombea Hayati Mwadhama Polycarp Kardinali P...
28/02/2026

MATUKIO KATIKA PICHA - PUGU DSM
▪︎ Adhimisho la sadaka ya Misa Takatifu ya kumuombea Hayati Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, katika Kituo cha Hija Pugu, Jimboni humo.

▪︎ Misa Takatifu ya maziko imeadhimishwa na Mhashamu Judde Thaddaeus Ruwa'ichi Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, katika Kituo cha Hija Pugu.
www.hlitanzania.org

HABARI PICHA MAANDAMANO MISA YA MAZISHI YA KARDINALI POLYCARP PENGOPicha ni  baadhi ya Maaskofu na Makardinali wakati wa...
28/02/2026

HABARI PICHA MAANDAMANO MISA YA MAZISHI YA KARDINALI POLYCARP PENGO

Picha ni baadhi ya Maaskofu na Makardinali wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Mazishi ya Marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo (1944_2026).

Misa Takatifu iliadhimishwa na Mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa’ichi OFMCap, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, katika kituo cha Hija Pugu-jimboni humo.
Www.hlitanzania.org

MAASKOFU WALIVYOTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO (1944 - 2026)- Picha mbali...
27/02/2026

MAASKOFU WALIVYOTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO (1944 - 2026)
- Picha mbalimbali ni wakati Maaskofu kutoka ndani na nje ya Tanzania kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo - Askofu Mkuu Mstaafu wa Dar es Salaam.
Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alifariki dunia Februari 19, 2026 alipokuwa akipata matibabu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na atazikwa Jumamosi Februari 28, 2026 katika kituo cha Hija Pugu, Jimbo Kuu la Dar es Salaam.
www.hlitanzania.org


Address

Mbagala Chamanzi
Dar Es Salaam

Telephone

+255621557160

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pro-life Tanzania- Human Life International Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Pro-life Tanzania- Human Life International Tanzania:

Share