TAG - Faith Revival Mission Church

TAG - Faith Revival Mission Church We are a church that lives by faith, known by love, and a voice of hope to the world.

Hakika sikukuu ya vijana ilifana sana. Tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha kusherehekea sikukuu hii katika kanisa letu la...
07/10/2024

Hakika sikukuu ya vijana ilifana sana. Tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha kusherehekea sikukuu hii katika kanisa letu la TAG - Faith Revival Mission Church . Hakika tulibarikiwa sana.πŸ™πŸΎπŸ˜Š

31/12/2023

Heri ya Mwaka Mpya 2024

Tumefurahia siku ya jana ya sikukuu ya Krismasi. Hapa mchungaji Daudi Enos akiwapa zawadi ya sikukuu watoto waliofika Ib...
26/12/2023

Tumefurahia siku ya jana ya sikukuu ya Krismasi. Hapa mchungaji Daudi Enos akiwapa zawadi ya sikukuu watoto waliofika Ibadani.
Heri ya Krismasi na Mwaka mpya 2024.πŸ™πŸΎπŸ˜Š

25/12/2023

β€œMaana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”
β€” Isaya 9:6 (Biblia Takatifu)

Heri ya Krismasi. Baraka za Mwokozi na ziendelee kuwa juu yako unaposherekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwake ulimwenguni. Amen.

Mwinjilisti Sakina Maduche akihubiri jioni ya leo.
22/12/2023

Mwinjilisti Sakina Maduche akihubiri jioni ya leo.

Kipindi cha sifa mbele za Mungu πŸŽŠπŸ˜ŠπŸ™πŸΎ
22/12/2023

Kipindi cha sifa mbele za Mungu πŸŽŠπŸ˜ŠπŸ™πŸΎ

26/11/2023

KARIBU SANA IBADANI SIKU YA LEO.
IBADA INAANZA SAA 3.00 ASUBUHI.

12/11/2023

Asante Bwana Yesu kwa neema yako.
{40 days are over with abundant grace from Jesus Christ.}
TAG - Faith Revival Mission Church

09/11/2023

Tunaendelea na maombi vema kabisa. Na leo tupo siku ya 37. Mungu awabariki sana tunapoelekea kuhitimisha kwa ushindi.

09/11/2023

β€œUisikie sauti ya kilio changu, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, Kwa maana Wewe ndiwe nikuombaye.”
β€” Zaburi 5:2 (Biblia Takatifu)

β€œWewe usikiaye kuomba, Wote wenye mwili watakujia.”  β€” Zaburi 65:2 (Biblia Takatifu)Tunaendelea na maombi na leo ni siku...
02/11/2023

β€œWewe usikiaye kuomba, Wote wenye mwili watakujia.”
β€” Zaburi 65:2 (Biblia Takatifu)

Tunaendelea na maombi na leo ni siku ya 30.
Hakika tunamwona Mungu.

Faida za Kufunga na Kuomba.Zipo faida nyingi sana za kufunga na kuomba. Bwana Yesu alisisitiza jambo hili kwenye Mathayo...
17/10/2023

Faida za Kufunga na Kuomba.

Zipo faida nyingi sana za kufunga na kuomba. Bwana Yesu alisisitiza jambo hili kwenye Mathayo 17:21 (SUV):
β€œ[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”

Alimaanisha kuna mambo ambayo kuyatatua ni mpaka uchukue hatua ya kufunga na kuomba. Sasa, zipo faida nyingi za kufunga na kuomba. Hapa nitaorodhesha chache tu:

1. Kunaleta ule ushirika wa karibu wa kiroho Kati yako na Mungu.
2. Kunafungua roho yako kuweza kuisikia sauti ya Mungu vizuri.
3. Unapata kufunuliwa waziwazi mambo ya sirini na unaongozwa na Mungu kikamilifu.
4. Kunavunja ngome za Shetani.
5. Kunaleta hekima ya Mungu juu yako.
6. Kunaleta uponyaji/afya njema.
7. Kunakupa kibali machoni pa Mungu na wanadamu.
8. Unapata nguvu nyingi za rohoni/Mungu ndani yako.

Hizi ni faida chache kati ya nyingi ambazo tunaweza kuzipata pale tunapofunga na kuomba. Hivyo basi endelea kufunga na kuomba bila kukoma kadiri upatapo nafasi ya kufanya hivyo nawe utamwona Mungu.

Rev. Daudi Enos.
(+255 769 659 466)

NB: Leo ni siku yetu ya 14 katika maombi yetu ya siku 40. Tunamwona Mungu sana. Karibuni sana.

Address

Mji Mpya, Mivumoni "A" Street Near Mashamba Ya Jeshi
Dar Es Salaam
14130

Opening Hours

Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 18:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 18:00
Sunday 07:00 - 18:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAG - Faith Revival Mission Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share