bhgministry

bhgministry 𝖡𝖧𝖦Church under Prop. 🆎Ⓜ️ has the purpose of bringing people to God.

"𝖧𝗈𝗎𝗌𝖾 𝗈𝖿 𝖦𝗈𝖽, 𝖦𝖺𝗍𝖾𝗌 𝗈𝖿 𝖱𝖾𝗏𝖾𝗅𝖺𝗍𝗂𝗈𝗇"

Mentorship programs,

Spiritual Growth & Prayers,

Deliverance, Renewed & Salvation.

◄ UNA NEEMA ALIYONAYO YESU ►- Warumi 4:16 16        Kwa sababu hiyo, ahadi hiyo inatokana na imani ili iwe kwa njia ya n...
29/08/2026

◄ UNA NEEMA ALIYONAYO YESU ►

- Warumi 4:16 16

Kwa sababu hiyo, ahadi hiyo inatokana na imani ili iwe kwa njia ya neema, ili ahadi hiyo iwe na hakika kwa uzao wote; si kwa wale tu walio wa sheria, bali pia kwa wale walio na imani ya Ibrahimu, ambaye ni baba yetu sote...


Unayo thamani kubwa sana mbele za Mungu, fikiria Mungu kumtoa mwanaye pekee kufa kwa ajili ya mtu k**a wewe.

- HII NI THAMANI YA NAMNA GANI?
- JE! NI UPENDO MKUU NAMNA GANI?

Mungu ni pendo na anadhihirisha kwa vitendo. Na tunapoyajua haya, tunaona kuwa Neema ya Mungu ni kibali ambacho hatukustahili, hatukukitolea jasho, wala hatukukipata kwa sababu ya matendo yetu.

Na kwa kuwa hatukustahili wala kukitolea jasho, sote tunastahilishwa kukipokea kwa neema tu.

# Lakini tunaiishije neema hiyo?

K**a unavyoweza kutumia password _(nenosiri)_ likakupa ruhusa ya kutumia programu ya kompyuta, imani nayo ni password inayotuwezesha kuishi katika neema ya Mungu ambayo hatukustahili.

Imani haina uhusiano wowote na yale tunayofanya au tunayoweza kufanya, bali Imani ni kuamini tu na kutangaza yale ambayo Mungu amefanya na atakayofanya kwa ajili yetu.

Tunapoamini kuwa kibali cha Mungu kiko juu yetu kwa sababu ya kazi aliyoimaliza Kristo, ahadi Zake zote zinakuwa na hakika kwetu, maana sisi ni uzao wake Ibrahimu. Hivyo tunayo "imani ya Ibrahimu".

Muangalie Ruthu alikuwa mjane wa Mataifa ambaye aliweka imani yake katika neema ya Mungu. Aliamini kwamba kibali cha Mungu kingemwongoza kwenye shamba sahihi la kuokota masazo ya mavuno, ambapo angepata kibali machoni pa mwenye shamba. (Ruthu 2:2)

Kwa sababu Ruthu alimtegemea Mungu, hakumweka tu katika shamba la Boazi tajiri, bali pia alimuingiza katika ukoo wa Yesu! (Mathayo 1:5)

Imani ya Ruthu ilimfungulia ulimwengu mpya kabisa. Alitoka katika umaskini kwenda kwenye utajiri, kutoka katika ujane kwenda kwenye ndoa, na kutoka kutokuwa na watoto hadi kuwa na familia kamili. Pia alikuja kuwa mtu anayeheshimika katika jamii. (Ruthu 4:13-15)

Ikiwa Ruthu, mtu wa Mataifa aliyekuwa chini ya agano la kale, alimtegemea Mungu, na kwa imani akapokea kibali, je! Sisi tulio chini ya agano jipya la neema tutafurahia zaidi kiasi gani baraka zinazoletwa na neema ya Mungu ambayo hatukustahili!

Mungu anatuona ndani ya Yule Apendwaye (Yesu) leo, tunafurahia kibali kilekile ambacho Yesu anacho!

- Waefeso 1:5-6

> Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake. Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.>

Rafiki yangu, unapoamini kuwa una kibali kilekile alicho nacho Yesu, ulimwengu mpya utafunguka mbele yako, ulimwengu ambamo ahadi zote za Mungu ni " Ndiyo" na "Amina" ndani ya Kristo!

Unapoamini kuwa kibali cha Mungu kiko juu yako kwa sababu ya kazi aliyoikamilisha Kristo, ahadi Zake zote zinakuwa hakika kwako.

◄ ENDELEA KUOMBA ►- 1 Petro 3:12       > "Kwa maana macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikia maombi...
19/08/2026

◄ ENDELEA KUOMBA ►

- 1 Petro 3:12

> "Kwa maana macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikia maombi yao..."
>

Dunia na watu wake wanaweza kukusaliti, marafiki wakakuacha, lakini wewe usiisaliti imani.

Kwa kuwa Mungu hawezi kukusaliti wala kukuacha wewe, Yeye atakuwa bega kwa bega na wewe, katika kila hali uliyonayo.

Haijalishi ni wakati wa furaha au huzuni, Mungu ni pendo anapenda watu wake, na wewe ni mtu wa Mungu hawezi kukuacha.

Usiangalie majeraha uliyo nayo, wala maumivu uliyonayo, wewe mtazama Yesu, alishanda vita ya mateso ya msalaba, akashinda vita mateso ya kaburi, fikiria ni maumivu ya namna gani.

K**a alishinda vita zote, ukiwa Naye, na ukimkaribia, wewe ni mshindi. Yeye anaweza kubadilisha hali yako ya leo, anaweza kubalisha hiyo roho ya mateso ndani yako.

- Unahitaji nini wewe?

> Chochote kilicho haja ya moyo wako, unaweza kukipata kwa Yesu, mtafute Yeye upate vyote bado hujachelewa.
>

- Moyo wako umekuwa mdhaifu kwenye nini?

> Anasema atawapa roho atakaye wasaidia katika madhaifu yenu. Kumbe Mungu alijua tunayo madhaifu, na bila roho wake hatuwezi kuushinda udhaifu tulionao.
>

- Maandika yanasema Warumi 8:26

> "Kadhalika Roho naye hutusaidia katika udhaifu wetu. Kwa maana hatujui jinsi inavyotupasa kuomba, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa."
>

Ni kweli hatuwezi kuomba ipasavyo, ndio maana roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kwa sababu ya madhaifu yetu. Tusikate tamaa tuzidi katika kuomba.

Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, baya halitakuua wewe, na meno ya simba wala makucha yake hayatagusa mwili wako.

- Ufanye nini basi ili uwe salama?

> Tafuta kuwa huyo mwenye haki, na endelea kuomba kuomba, maana masikio ya Mungu husikia maombi ya watu hao. Na bidii ya huyu mwenye haki katika kuomba, itamkinga na kadhia zote.
>

17/07/2026

LEO NI SIKU NJEMA

- Maombolezo 3:22-23

Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.


Usikate tamaa hata k**a moyo wako umechoka. Mungu bado yuko pamoja nawe, na nguvu zako hazitegemei hali uliyonayo sasa bali neema ya Mungu inayokufunika.

Kila changamoto unayopitia, si ishara kwamba umeachwa, bali ni nafasi ya kuona uaminifu wa Mungu ukiendelea kukushikilia.

Kumbuka kwamba siku mpya huja na rehema mpya, hata k**a jana ulikuwa na maumivu, huzuni, au mawazo mengi, leo bado kuna nafasi ya kuanza tena.

Mungu hafuti thamani yako kwa makosa uliyofanya, badala yake, anakupa tumaini, amani, na moyo wa kusimama tena kwa imani.

Usiogope hatua ndogo, maana hatua moja ya imani leo inaweza kuwa mwanzo wa ushindi mkubwa kesho.

Endelea kusali, endelea kuamini, na endelea kusonga mbele hata k**a ni kwa mwendo mdogo, kwa maana Mungu huwategemeza wote wanaomtegemea.

- [ ] Endelea kuamini kwa maana:

1. Mungu anaweza kukupa mwanzo mpya.
2. Usibebe makosa ya jana.
3. Omba, shukuru, na endelea mbele kwa imani.

◄ NGUVU ZA MUNGU HAZIZUILIKI ►- Zaburi 5:1-2        Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari kwangu. Ui...
14/07/2026

◄ NGUVU ZA MUNGU HAZIZUILIKI ►

- Zaburi 5:1-2

Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari kwangu. Uisikie sauti ya kilio changu, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, Kwa maana Wewe ndiwe nikuombaye.


Ukijua uzuri wa Mungu, hutoacha kusali zaburi ya Daudi ikujenge na kukurejesha, naam hutoweza kuacha kuimba tenzi roho yako irejeshwe kwa upya.

Huyu Mungu ni mzuri sana, k**a ukimpa nafasi atawale ndani ya moyo wako, anasema unavyozidi kujitakasa ndivyo ndivyo utakavyozidi kutakaswa.

Ninampenda sana kwa sababu ni wa haki, hamtoi roho wake kwa kipimo, ila kadiri tunavyozidi kujitakasa na kuomba, ndivyo tunavyozidi kujazwa na roho wake Mtakatifu.

Natamani tuimbe tenzi za rohoni, natamani tusali Zaburi ya Daudi, labda pengine tutaona uzuri wa kuwa karibu naye.

Mpendwa narudia kusema kwako, *huyo Yesu ni mzuri sana,* anapendeza sana na anamfaa kila mtu atakaye mkaribia, maana anasema na Yakobo yeyote atakaye mkaribia Naye humkaribia.

*Nipo katika mlima wa maombi* ninazidi kuona uzuri wake, ambao ninatamani kila mmoja wenu afike hapo.

Ufungue moyo wako, umkiri Yesu popote ulipo, unapoona ujumbe huu, ipo nguvu ya Mungu inaweza kukugusa na kubadilisha kitu kwenye maisha yako.

Kila Mungu anachokifanya si kwa faida yake, ila ni ili sisi tupate faida, na amenituma kwako leo ili upate hiyo faida leo. *WEWE AMINI TU!*

Ee Bwana uyasikilize maneno yangu, ukuangalie kutafakari kwangu, maana katika kuwaza kwangu nalitenda makosa.

Sikuwahi kuwa mkamilifu katika mawazo yangu, siku zote nimekutenda makosa, ambayo hata sasa nimejutia.
Wanadamu wametengeneza makwazo ambayo nisingeweza kupona, nimekuwa na vidonda vya muda mrefu, vilivyo jificha ndani ya moyo wangu.

Tazama moyo wangu umetengeneza chuki ambayo sikuweza kujizuia, lakini leo ninafuraha kwa sababu nimetambua sio wenye chuki wala kiburi unaopendezwa nao.

Moyo wangu umekuwa mdanganyifu kila mara, maana umewaza ubaya, nami nimejutia, nimekuja k**a Daudi aliyetenda dhambi unisamehe, na nimekuja k**a mwana mpotevu aliyekosa maarifa unipokee.

Natamani uniumbie moyo safi kwa mara nyingine k**a Daudi, ufanye makazi yako ndani yangu, uwe na kuwaza kwangu sikuzote.

Ee Mungu wangu, kile kitu sitamani ni kukosea zaidi, njia yangu iangazwe na nuru yako, ili nisikanyage uchafu, uisikie sauti ya kilio changu Mungu wangu, kwa maana Wewe ndiwe nikuombaye.

Bwana nimetambua ya kuwa mtu muovu hatakaa kwako, maana hupendezwi na watendao mabaya. Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako, unawachukia wote watendao ubatili.

Bwana uniongoze kwa haki yako, kwa sababu yao wanaoniotea, uisawazishe njia yako mbele ya uso wangu.

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo, umenifanyizia nafasi wakati wa shida, unifadhili na kuisikia sala yangu.
Ee Bwana uwafanye adui zangu wakae chini ya miguu yangu.

Tubarikiwe sote!!

◄ USIWE VUGUVUGU ►- 2Timotheo 2:19        Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua wa...
14/07/2026

◄ USIWE VUGUVUGU ►

- 2Timotheo 2:19

Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.


Anayelitaja jina la Mungu na auche uovu, maana Yeye na uovu hawapatani, wala hawaketi katika meza moja.

Mwanadamu anaweza kujichelewesha kwa kushika mambo mawili, huku anamtaja Mungu, na kule anataka kuitumikia dunia.

Mungu ni mwenye haki na tena ni mwenye wivu, ili mchezaji wa mpira wa miguu aweze kufunga goli, lazima mpira uwe kuna mahali umetokea, inaweza kuwa ni kwa mchezaji mwenzake au mpinzaji wake.

Na ili ubarikiwe itategemea baraka yako inatoka wapi? Malaika anayetoa baraka ameshikilia waraka wako, lakini kila anapokuja anakukuta unatangatanga na mambo machafu ya dunia.

Huwezi kujisikia vizuri ukifanya kazi sifa zikaenda kwa mtu mwingine ambaye hakujishughulisha na kazi yenyewe.

Na k**a nilivyo tangulia kusema Mungu ni mwenye wivu, na sauti ya Yake imeweka wazi hilo kupitia Musa, Je! atapewa nani utukufu ikiwa utapona ugonjwa uliouguzwa na waaguzi wa wawili wa miungu tofauti?


- Ufunuo 3:15

Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri k**a ungekuwa baridi au moto.

- [ ] Nataka kusema nini?

Mungu anachukizwa na kashika mawili mawili, k**a umeamua kuzichagua mbingu kushughulika na maisha yako, wacha mbingu zishughulike.

Na k**a umeamua kuicha dunia ishughulike na maisha yako, wacha dunia ishughulike. Lakini kipi bora? Ni aheri mbingu kule kilipo kiti cha enzi kuliko dunia iliyo jaa uasi.

Mjengee Mungu nyumba nzuri ya moyo wako, yani mkubali umpe moyo wa ibada na utachanua k**a ule mti uliopandwa kando ya kijito cha maji mengi.

Kuna kitu kinaitwa IMANI ni ngumu lakini inaweza kubadilisha historia ya mtu, IMANI ya Ibrahim ilipimwa kwa njia ngumu s...
13/07/2026

Kuna kitu kinaitwa IMANI ni ngumu lakini inaweza kubadilisha historia ya mtu, IMANI ya Ibrahim ilipimwa kwa njia ngumu sana kabla ya Mungu kumbariki.

Nasi tusisahau ya kuwa hatuwezi kubadilishwa pasipo kuwa na IMANI, yani ili Yesu afunuliwe kwako lazima uwe na IMANI

NINI KIMEINGILIA MUELEKEO WAKO?- Wagalatia 3:1        Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yes...
13/07/2026

NINI KIMEINGILIA MUELEKEO WAKO?

- Wagalatia 3:1

Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

Si kila muelekeo alionao mtu unaeleweka, k**a bado hajajua ni nani anayefanya kazi ndani yake.

Ile roho inayomuongoza mtu ndiyo humuelekeza katika muelekeo alionao, ikiwa ni roho wa Mungu itakupa muelekeo mwema na ikiwa sio roho wa Mungu itakupa muelekeo wa uharibifu.

Ni wangapi wanaumia safarini, au kidhurika katika muelekeo walio nao? Inawezekana ni muelekeo wa kazi, pengine ni muelekeo wa biashara, au muelekeo wa ndoa.

Mungu ni wa haki, chagua kuanza naye, kutembea naye na usimame kwa uaminifu utavuna matunda ya muelekeo wako.

Mfanyabiasha anapoona kukosa faida katika biashara yake iliyoanza vizuri, anaanza kutazama muelekeo wa biashara yake, ni nini kimetokeo njiani?

Je! Katika safari yako unaona nini?, ni jambo gani linaonekana kukukosesha furaha katika muelekeo wako.

Kinachotokea kwenye uelekeo wako kinaweza kisimaanishe dhambi, k**a wengi wetu tunavyoweza kuwaza, sio kila mapigo yanaletwa na dhambi.

- [ ] Watu wengi wamekuwa wanauliza ni wapi nimekosea?

Wakati mwingine kuna vitu tunatakiwa tubadilishe tu, ili tutoke kwenye maumivu, CHANGE POSITION, position inaweza kukuletea maumivu.

Nimetaka kuondoa mkanganyiko kuwa sio kila mapigo yanaletwa na dhambi, turudi darasani!!!

- [ ] Lengo hasa la somo hili ni kutaka tuangalie ni wapi tumeisahau kweli ya Mungu?

Paulo anawauliza Wagalatia ni nani aliyewaloga, kwa sababu matendo yao hayaendani tena na utakatifu, anasema je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?

- [ ] Ni wapi umeisahau kweli ya Mungu?

Mwanzo ulikuwa na muda wa kuomba siku za hivi karibuni nafasi yako ya kuomba imeenda wapi?

Ulikuwa muombaji mzuri ambaye watu walibarikiwa ukisifu na kuabudu, huduma yako imeingiliwa na nini?

Mbona ulikuwa mtu mwenye afya njema tena ya kupendeza, ni mdudu gani ameingia katika muelekeo wako na kukuletea maradhi?

Ulikuwa mtu mwema na mwenye upendo, chuki imetoka wapi? Uko wapi upendo wako wa mwanzo?

Furaha na amani uliyo kuwa nayo tele, imeenda wapi? mbona uso wako umekunjamana hivi, mapindo ni ya nini kwenye usoni mwako?

Ulikuwa na mwanzo mzuri, lakini sasa kumegeuka kuwa majuto, ni nini kimetokea katika muelekeo wako?

Safisha uwanda wa moyo wako leo, kisha usafishe uwanda wa hatua zako, pale adui aliposimamisha mnara wake.

Mwambie Yesu afunuliwe kwako kwa upya, bado hujachoka kuona utukufu wake, na atakapofunuliwa atakupa muelekeo chanya, roho nyang'anyi zitakimbia katika uwanda wako nawe utakuwa na muelekeo chanya.

Haijalishi unaona nini? Nataka nikwambie kuwa kwa Yesu kila kilichokuwa mfu kinafufuliwa.

With Arnwald Bryson – I just got recognised as one of their top fans! 🎉
07/07/2026

With Arnwald Bryson – I just got recognised as one of their top fans! 🎉

maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atasema atakayoyasikia na kuwajulisheni yatakayokuja. Yohana 16:13
07/07/2026

maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atasema atakayoyasikia na kuwajulisheni yatakayokuja.

Yohana 16:13

TUZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.- Luka 11:13        “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipa...
07/07/2026

TUZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

- Luka 11:13

“Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”.


Kufuatana na maandiko haya, ni wazi kuwa Biblia inatufundisha ujazo wa Roho Mtakatifu ni jambo endelevu siku zote za maisha ya mtu.

Kadiri tunavyodhidi kuomba au kutafuta uso wa Mungu ndivyo tunavyodhidi kujazwa na Roho Mtakatifu, kwani Yeye hamtoi Roho kwa kipimo k**a ilivyoandikwa na Yohana.

- Waefeso 5:18

“Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”.

- [ ] Sasa tunajazwaje Roho Mtakatifu? si kwa njia nyingine bali kwa kuomba.

---

Vifuatavyo ni vipengele muhimu katika maombi ya ujazo wa Roho Mtakatifu:

1. OMBA KUFUNDISHWA NA ROHO MTAKATIFU.

- Yohana 14:26

“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, ATAWAFUNDISHA YOTE…”


Unaposoma BIBLIA, Roho Mtakatifu akawe mwalimu wako katika kulielewa vizuri Neno, tenga muda wa kutosha kumwomba MUNGU akakujaze Roho wake wa ualimu.

Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli, wanajifunza Biblia na kuielewa vizuri kwasababu ndani yao Roho Mtakatifu anawafundisha.

Pia wanakuwa ni watu wenye maisha yaliyostaarabika kwasababu ndani yao wanaye mwalimu anayewafundisha kanuni za maisha.

---

2. OMBA KUKUMBUSHWA NA ROHO.

- Yohana 14:26

“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na KUWAKUMBUSHA YOTE niliyowaambia”.


Kuna mambo uliyowahi pengine kufunuliwa na MUNGU zamani, kwa njia ya Neno au ndoto, na umesahau, unapojaa Roho Mtakatifu, basi atakukumbusha yote aliyekuambia au kukuonesha.

Na sio tu kukumbusha maneno ya Mungu au maagizo yake bali hata mambo yako mengine ya kimaisha yaliyo ya muhimu, Roho Mtakatifu atakukumbusha na kukutahadharisha.

Hata katika elimu za Dunia, wanafunzi waliojaa Roho Mtakatifu, ni ngumu kusahau kabisa waliyojifunza, kwani yupo msaidizi ndani yao anayewakumbusha waliyojifunza.

Hali kadhalika watu wenye Roho Mtakatifu kweli kweli huwa hawasahau maelekezo au maneno ya Mungu kwani yupo Msaidizi, Roho Mtakatifu anayewakumbusha kila siku.

Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba ujazo wa Roho Mtakatifu ndani yako.

---

3. KUONGOZWA NA ROHO.

- Yohana 16:13

“Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, ATAWAONGOZA awatie kwenye kweli yote….”.


Pia Roho Mtakatifu kazi yake nyingine ni kumwongoza Mtu, nini cha kusema, nini cha kufanya, au ni wakati gani wa kusema na wakati gani wa kunyamaza, ni wakati gani wa kutenda na wakati gani wa kutulia.

Zaidi sana Roho Mtakatifu pia anamwongoza mtu nini cha kusikiliza na nini ambacho hakifai kusikiliza au kufanya..

Na katika maombi pia, Roho Mtakatifu anamwongoza mtu nini cha kuomba na jinsi ya kuomba.

- Warumi 8:26

Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo…..


Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba Ujazo wa Roho Mtakatifu, ili uweze kunufaika na tunda hili la kuongozwa na Roho.

---

4. OMBA KUFUNULIWA NA ROHO MAMBO YAJAYO.

- Yohana 16:13

Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, NA MAMBO YAJAYO ATAWAPASHA HABARI YAKE.


Ni muhimu sana kuyajua mambo yajayo yahusuyo maisha yako, kanisa, familia nk. kwasababu uishivyo sasa ni kutokana na kile unachokiona mbele yako, na Roho Mtakatifu pekee ndiye awezaye kufunua mambo yajayo ya mtu au watu kwa usahihi.

Kwa mambo haya manne, tutaimarisha ile safari yetu ya kuenenda kwa Roho.

- Wagalatia 5:16

“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.

Address

Salasala
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when bhgministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to bhgministry:

Shortcuts

Share