27/05/2026
NJIA YA KWELI
- Yohana 14:6
Yesu akamwambia (Tomaso), Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
- [ ] Nani anakutazama katika wakati ulio nao? Umepoteza muelekeo, haha hujui hufanye nini?
Daudi anasema katika Zaburi 121, nitayainua macho yangu nitazame milima, msaada wangu utatoka wapi? *msaada wangu* u katika Bwana aliyezifanya mbingu na nchi.
Kuendelea kuteseka ni kutokutambua njia sahihi ambayo unaweza kusaidika, umekosa majibu ya mafumbo katika maisha yako.
Daudi alitambua njia sahihi ya kupata majibu ya shida yake mateso yakamkimbia, na aibu ikaondoka kwake.
Hata wewe na mimi, tukitambua njia sahihi ya kufumbua mafumbo ya maisha yetu, mateso yatatukimbia na amani itarejea, aibu itaondoka na utukufu utafunuliwa, dhiki itaondoka na neema itakuja.
- [ ] Tumaini lako liko wapi? Mbona mzigo umekulemea namna hii.
Tusimame na Yesu leo, maana hata pepo ni kazi ya mikono yake, zinamtii, kwa Yeye kila goti linapigwa, anayo mamlaka juu kila kilichopo katika nchi na mbingu.
Anaposema mimi ndimi njia ya kweli, maana yake salama ya maisha yetu iko katika njia Yake, na ili tuondoke katika mateso, ni lazima tuichague njia ya Yeye.
Kupitia njia Yake tuna uzima, na katika Yeye tunamfikia Baba, na katika Yeye kuna mwisho wa kila kitu.
Tufanya nini basi? Tumchague kuwa mwanzo wa kila kitu na kisha atakuwa mwisho wa kila kitu kwetu.