bhgministry

bhgministry Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from bhgministry, Pentecostal Church, Salasala, Dar es Salaam.

𝖑𝖧𝖦𝖬 under Prop. πŸ†Žβ“‚οΈ has the purpose of bringing people to God
"π–§π—ˆπ—Žπ—Œπ–Ύ π—ˆπ–Ώ π–¦π—ˆπ–½, π–¦π–Ίπ—π–Ύπ—Œ π—ˆπ–Ώ π–±π–Ύπ—π–Ύπ—…π–Ίπ—π—‚π—ˆπ—‡"
Mentorship programs, Spiritual Growth & Prayers MpSgP
Deliverance, Renewed & Salvation DRS
GOD HAS ZERO TOLERANCE FOR SIN.

NJIA YA KWELI- Yohana 14:6Yesu akamwambia (Tomaso), Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia...
27/05/2026

NJIA YA KWELI

- Yohana 14:6

Yesu akamwambia (Tomaso), Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

- [ ] Nani anakutazama katika wakati ulio nao? Umepoteza muelekeo, haha hujui hufanye nini?

Daudi anasema katika Zaburi 121, nitayainua macho yangu nitazame milima, msaada wangu utatoka wapi? *msaada wangu* u katika Bwana aliyezifanya mbingu na nchi.

Kuendelea kuteseka ni kutokutambua njia sahihi ambayo unaweza kusaidika, umekosa majibu ya mafumbo katika maisha yako.

Daudi alitambua njia sahihi ya kupata majibu ya shida yake mateso yakamkimbia, na aibu ikaondoka kwake.

Hata wewe na mimi, tukitambua njia sahihi ya kufumbua mafumbo ya maisha yetu, mateso yatatukimbia na amani itarejea, aibu itaondoka na utukufu utafunuliwa, dhiki itaondoka na neema itakuja.

- [ ] Tumaini lako liko wapi? Mbona mzigo umekulemea namna hii.

Tusimame na Yesu leo, maana hata pepo ni kazi ya mikono yake, zinamtii, kwa Yeye kila goti linapigwa, anayo mamlaka juu kila kilichopo katika nchi na mbingu.


Anaposema mimi ndimi njia ya kweli, maana yake salama ya maisha yetu iko katika njia Yake, na ili tuondoke katika mateso, ni lazima tuichague njia ya Yeye.

Kupitia njia Yake tuna uzima, na katika Yeye tunamfikia Baba, na katika Yeye kuna mwisho wa kila kitu.

Tufanya nini basi? Tumchague kuwa mwanzo wa kila kitu na kisha atakuwa mwisho wa kila kitu kwetu.

UTULIVU WAKO WA NDANI UMEBEBA USHINDI WAKO- Zaburi 46:10        Tulieni, mkajue ya kuwa mimi ni Mungu.    Ni hallelujah,...
25/05/2026

UTULIVU WAKO WA NDANI UMEBEBA USHINDI WAKO

- Zaburi 46:10

Tulieni, mkajue ya kuwa mimi ni Mungu.


Ni hallelujah, nguvu za shetani zimeshindwa, na neema ya Mungu imetukomboa.

Neema inapokuja, hakuna awezaye kuifikiria au kuielewa kwa akili ya kawaida. Ni vigumu kutambua ujio wake, hasa pale kelele zinapokuwa nyingi nje.

Lakini najifunza jambo moja: unapozungukwa na kelele nyingi kuhusu jambo fulani, mara nyingi hiyo ni ishara ya ujio wa neema ya Mungu kwako.

Tambua hata kabla ya Daudi kumkabili Goliathi, kelele zilikuwa nyingi sana. Mfalme alimwambia Daudi, β€œWewe ni nani hata uende kumpiga Goliathi?” Kulikuwa na watu wenye uzoefu mkubwa wa vita, lakini walishindwa kumshinda.

Siku zote, ukichagua kusikiliza kelele za nje, utapoteza mwelekeo wako. Lakini ukichagua kutulia mbele za Mungu, utapata ushindi usiotarajiwa.

Unajua, ukifanikiwa kuishi na watu na kuwaelewa vizuri, ndipo utaanza kupata jibu la kwa nini Mungu ni Mungu

SIRI YA NEEMA- Mithali 16:9        Moyo wa mtu huifikiri njia yake, bali Bwana huelekeza hatua zake.     Neema ya Mungu ...
20/05/2026

SIRI YA NEEMA

- Mithali 16:9

Moyo wa mtu huifikiri njia yake, bali Bwana huelekeza hatua zake.


Neema ya Mungu haiji wakati kila kitu kiko sawa, huja wakati kila kitu kinaonekana kimeharibika.

Wakati mwingine Mungu huruhusu mtu apitie majira ya kimya, yasiyo na majibu na yanayoonekana hayana maana, si kwa sababu amemuacha, bali kwa sababu kuna kazi ya ndani anafanya.

Imani hukua kwa kina zaidi katika ukimya kuliko katika nyakati za kustarehesha.

Sio kila swali lisilo na jibu linaashiria kuachwa na Mungu, mara nyingi ni darasa la kujifunza kumwamini hata pale ambapo macho hayaoni kwa uwazi.

Majaribu tunayopitia si mwisho wa safari, bali ni sehemu ya njia inayotupeleka kwenye neema iliyo mbele yetu.

Ukisoma Warumi 5:3-4, utaona Mtume Paulo anatufundisha kuwa dhiki huleta saburi, saburi huzaa uthabiti, na uthabiti huleta tumaini.

Neema ya Mungu haimkuti mtu katika mazingira mazuri, huja wakati mambo yamevurugika, matumaini yamepotea, na kila kitu kinaonekana kinyume.

Tunaposoma 2 Wakorintho 12:9, tunaona Paulo anaendelea kufundisha wazi kuwa uweza wa Mungu hutimilika katika udhaifu wa mwanadamu.

Na hata nikiangalia ushuhuda wa maisha yangu, neema ya Mungu haikunipata mahali pa raha, wala mahali pa kupendwa, ilinikuta katikati ya changamoto na hapo ndipo Mungu alijifunua kwangu.

Haijalishi maisha yako yamevurugika kwa kiwango gani, neno hili ni la uhakika, neema ya Mungu iko karibu.

Usikate tamaa, songa mbele, na weka tumaini lako kwake, endelea kuongeza imani yako na jifunze kuvumilia, kwa maana uvumilivu ni tunda la Roho k**a Paulo anavyosema na Wagalatia.


Kumbuka daima kwamba neema ya Mungu haiji wakati kila kitu kiko sawa, bali huja wakati kila kitu kinaonekana kimeharibika, na ili kudhihirisha kuwa Mungu bado yupo katikati ya kila hali.

Ongeza imani yako ule matunda ya tunda uvumilivu la roho.

SAFARI YA MAISHA- Mithali 24:3-4        Kwa hekima nyumba hujengwa, na kwa ufahamu huthibitishwa, na kwa maarifa vyumba ...
19/05/2026

SAFARI YA MAISHA

- Mithali 24:3-4

Kwa hekima nyumba hujengwa, na kwa ufahamu huthibitishwa, na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.

– Gari, Dereva na Fundi

Mwanamke utakaye muoa ni k**a gari la maisha, na mwanaume atakayekuoa ni k**a dereva wa maisha.

Ili safari iwe salama, vyote viwili vinapaswa kuwa katika ubora, angalau kufikia kiwango kinachokubalika.

Gari likiwa bovu, linakuwa chanzo cha huzuni kwa dereva, na gari likiwa salama, linampa dereva furaha na amani ya safari.

Hata gari liwe bora kiasi gani, k**a dereva hana maarifa ya kuendesha, safari haiwezi kufika salama.

- [ ] Dereva asiyekuwa na elimu ya udereva, ataliharibu gari hata likiwa bora.

Pale kunapokosekana dereva mzuri na gari linalokidhi ubora, hapo ndipo safari ya maisha inakuwa ngumu, na yenye misukosuko isiyoisha.

- [ ] Kanuni ya Msingi

Mwanamke anahitaji dereva mzuri wa maisha, na mwanaume anahitaji gari zuri la maisha, lakini juu ya yote fundi wao ni Mungu.

Pale vitu hivi vitatu vinapokosekana, basi safari ya maisha inakuwa ngumu sana na yenye hatari.

1. Gari zuri
2. Dereva mzuri
3. Fundi bingwa (Mungu)

Mwanamke, anza kuwa bora wewe kwanza kabla hujampata dereva mzuri, na wewe mwanaume, anza kuwa dereva mzuri kabla hujapata gari zuri.

Usiingie kwenye ndoa ukiwa bado hujawa tayari kwa ndoa, epuka kufanya maamuzi kwa sababu wengine wamefanya.

Tenda kila jambo kwa sababu imekupasa kutenda, si kwa shinikizo la watu.

K**a bado hujamalizana na dunia, k**a bado hujajifunza kozi ya udereva, usitafute gari la kuendesha.

Watu wengi wameumia kwa sababu moja tu, waligundua kosa wakiwa tayari wako ndani ya kosa na walifanya maamuzi bila utayari.

- Mithali 20:7

Mwenye haki hutembea katika unyofu wake, heri watoto wake baada yake.

Muongozaji akikosa hekima nyumba inaporomoka, kwa tafasiri rahisi ni kuwa mwanaume asiye na hekima anaweza kuharibu familia yote au unaweza kusema tabia ya mwanaume inaweza kuinua au kuharibu kizazi kizima.

Hivyo tusifikiri mwanamke ndiye muharibu namba moja wa ndoa, la hasha! Bali tumtafute Mungu kwa pamoja ili tutengeneze nguzo imara ya familia.

NGUVU YA ROHO- Matendo 1:8        Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashah...
18/05/2026

NGUVU YA ROHO

- Matendo 1:8

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu

- [ ] Nataka tuelewe jambo hili:

Maisha ya Mkristo bila nguvu ya Roho Mtakatifu ni maisha ya kawaida sana.

Mungu hakutuita tuokoke tu, ametuita tuishi kwa nguvu, na nguvu hiyo inatoka kwa Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu si kwa ajili ya kukaa kimya ndani yako, ni kwa ajili ya kufanya kazi kupitia wewe.

- Maandiko yanasema kupitia Zekaria 4:6

Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali kwa Roho yangu, asema Bwana wa majeshi.

Hivyo, unapojazwa na Roho Mtakatifu, maisha yako yanapaswa kuonyesha matokeo, nguvu ya Mungu ndani yako inapaswa kuonekana katika maneno yako, matendo yako, na maisha yako kwa ujumla.

Watu wengi wana Roho Mtakatifu, lakini hawaonyeshi nguvu yake, unajua kwa nini? Kwa sababu hawajamruhusu afanye kazi kwa uhuru.

Roho Mtakatifu anahitaji mtu anayethubutu, mtu anayesimama kwa imani na kusema, Mungu, nitafanya kile ulichoniita kufanya.

Imani bila matendo haina nguvu, Roho Mtakatifu anapokaa ndani yako, anakupa ujasiri wa kutenda, si kuogopa.

Anakufanya usiwe mtu wa kawaida tena, bali mtu wa matokeo, mtu ambaye maisha yake yanaonyesha kuwa Mungu yuko hai.

- 2 Timotheo 1:7

Kwa maana Mungu hakutupa roho ya woga; bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.

Usikubali kuishi maisha ya woga na mashaka, simama katika nguvu ya Roho Mtakatifu, fanya kile Mungu ameweka moyoni mwako bila kuogopa.

Unapochukua hatua kwa imani, Roho Mtakatifu ataidhihirisha nguvu ya Mungu kupitia wewe, na dunia itaona kuwa Mungu unayemtumikia ni wa kweli.

UHALISIA WA ROHO- 2 Wakorintho 3:17        Bwana ndiye Roho, na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo Pana uhuruRoho Mtakatifu...
18/05/2026

UHALISIA WA ROHO

- 2 Wakorintho 3:17

Bwana ndiye Roho, na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo Pana uhuru

Roho Mtakatifu si wazo la kidini, bali ni uwepo wa Mungu aliye hai ndani ya maisha ya mtu aliyeokoka.

Bila Roho Mtakatifu, Mkristo anaweza kuwa na jina la wokovu lakini kukosa nguvu ya kuishi maisha ya ushindi.

Roho Mtakatifu ni Mtu wa Kiungu anayekuja kujaza, kuponya, na kubadilisha maisha ya mtu kabisa.

Anapokuja kwa nguvu, haachi mtu k**a alivyo, anabadilisha mioyo, anaondoa mizigo inayotulemea, na kuleta uhuru wa ndani.

Tatizo kubwa ni kwamba watu wengi wanamjua Roho Mtakatifu kwa akili, lakini hawajawahi kumkaribisha kwa moyo wa wazi.

- [ ] Lakini ninakuambia leo:

Unapomkaribisha Roho Mtakatifu kwa unyenyekevu na imani, uwepo wake unaleta mabadiliko ya kweli, amani isiyoelezeka, uponyaji wa ndani, na nguvu mpya ya kuishi kwa ajili ya Mungu.

Roho Mtakatifu anapokuja, anafanya Yesu kuwa halisi ndani ya maisha yako, hufanyi tena kwa nguvu zako, bali kwa nguvu yake, na hapo ndipo maisha ya kiroho yanapokuwa hai, yenye moto, na yenye matokeo.

Ninakusihi leo, fungua moyo wako, umkaribishe Roho Mtakatifu kila siku, usimweke pembeni.

Kumbuka pale alipo Roho Mtakatifu, ndipo palipo na uhuru, uponyaji, na uhai wa Mungu halisi.

UFUNUO WA MAMLAKA KATIKA KRISTO- 2 Wakorintho 5:17        Kwa hiyo ikiwa mtu yu ndani ya Kristo, ni kiumbe kipya.    Ndu...
18/05/2026

UFUNUO WA MAMLAKA KATIKA KRISTO

- 2 Wakorintho 5:17

Kwa hiyo ikiwa mtu yu ndani ya Kristo, ni kiumbe kipya.

Ndugu zangu, nataka uelewe jambo hili kwa ufunuo wa kiroho, maisha ya Mkristo hayapaswi kuongozwa na hisia au mazingira, bali na Neno la Mungu na uongozi wa Roho Mtakatifu.

Mkristo amepewa uzima wa Mungu na mamlaka ya kiroho ya kuishi juu ya mazingira. Hii inamaanisha kuwa ndani yako kuna uwezo wa kushinda, kubadilisha hali, na kuleta matokeo ya mbinguni duniani.

Tatizo ni kwamba watu wengi hawaijui nafasi yao katika Kristo, wanajaribu kuishi k**a waombaji wa baraka badala ya kuishi k**a watoto wa Mungu waliopewa mamlaka.

Roho Mtakatifu aliyeko ndani yako si dhaifu, Yeye ni nguvu ya Mungu inayofanya kazi ndani yako.

Unapojua Neno la Mungu na kulitamka kwa imani, Roho Mtakatifu analifanya hilo Neno kuwa halisi katika maisha yako, na ndiyo maana imani yako lazima ijengwe juu ya ufunuo wa Neno, si hisia.

- [ ] Jifunze kuishi k**a Mungu alivyokusudia.

- Warumi 10:17

Imani huja kwa kusikia, na kusikia huja kwa Neno la Kristo.

Tambua wewe ni nani katika Kristo, kisha zungumza Neno, simama katika imani, na acha Roho Mtakatifu afanye kazi kupitia wewe.

Maisha yako hayakuwekwa kuendeshwa na dunia, yamewekwa kuonyesha utukufu wa Mungu.

AKILI CHOMBO CHENYE NGUVUMaisha ya mwanadamu yanaongozwa moja kwa moja na ubora wa mawazo yake. Akili ya binadamu ni k**...
10/05/2026

AKILI CHOMBO CHENYE NGUVU

Maisha ya mwanadamu yanaongozwa moja kwa moja na ubora wa mawazo yake.

Akili ya binadamu ni k**a bustani, ikiwa mtu hatachagua kwa makini mbegu (mawazo) anazopanda, basi magugu (fikra hasi) yataota yenyewe na kuharibu mavuno (matokeo ya maisha).

Watu wengi huishi bila kufahamu kwamba wanaruhusu mawazo ya hofu, shaka, hasira, na kukata tamaa yatawale akili zao, na hatimaye mawazo hayo hugeuka kuwa tabia na matokeo halisi katika maisha yao.

Hakuna tukio linalotokea kwa bahati mbaya kabisa, bali mengi ni matokeo ya mfululizo wa mawazo ya ndani ambayo mtu amekuwa akiyalea kwa muda mrefu.

Kuna uhusiano wa karibu kati ya mawazo, hisia, na matendo. Mawazo huzalisha hisia, na hisia huathiri maamuzi, ambayo hatimaye huamua mwelekeo wa maisha ya mtu.

Hivyo basi, mtu anayetaka kubadilisha maisha yake hawezi kuanza na matokeo ya nje, bali lazima aanze na kubadilisha mfumo wake wa kufikiri.

Nidhamu ya akili (mental discipline), inamsaidia mtu kujifunza na kutambua mawazo hasi yanapokuja.

Mafanikio si tukio la ghafla, bali ni zao la mawazo yanayorudiwa mara kwa mara kwa muda mrefu.

Jenga mazoea ya kufikiri kwa mtazamo wa ushindi, imani, na matumaini, hata pale hali halisi inapo-onekana kuwa ngumu.

Nguvu ya imani binafsi na taswira ya ndani (self-image), vile unavyojiona ndani ya nafsi yako huamua kiwango cha mafanikio utakachofikia.

Ikiwa mtu anajiona hana thamani au hawezi kufanikiwa, basi hatajituma ipasavyo, lakini anapojiona ana uwezo, ataweka juhudi zinazolingana na imani hiyo.

Una wajibu wa moja kwa moja juu ya maisha yako kupitia mawazo yako.

Hakuna mabadiliko ya kudumu yanayoweza kutokea bila mabadiliko ya ndani ya akili.

Hivyo basi, unaweza kubadilisha kabisa hatima yake na kuishi maisha yenye mafanikio, amani, na kusudi.

Tunapongalia maisha ya Daudi, tunaona alikuwa mchungaji mdogo asiyepewa nafasi kubwa hata na familia yake, lakini neema ...
07/05/2026

Tunapongalia maisha ya Daudi, tunaona alikuwa mchungaji mdogo asiyepewa nafasi kubwa hata na familia yake, lakini neema ilipomgusa, ilimuinua kutoka kuwa mchungaji wa kondoo na kuwa mfalme.

Ni neema ilimfanya Yusufu kutoka kifungoni hadi kuwa mtawala, hakufika hapo kwa nguvu zake, bali kwa sababu neema ilibadilisha hadithi ya maisha yake.

Neema ilibadilisha historia ya Ibrahim, akatoka kuwa mtu wa kawaida na kuwa baba wa mataifa baada ya kuitwa na Mungu.

Neema ilibadilisha historia ya Yakobo, akapewa jina jipya Israeli, maisha yake yakabadilika.

Neema ilibadilisha historia ya Musa, kutoka mchungaji wa kondoo akawa mkombozi wa taifa baada ya kukutana na Mungu kwenye kichaka kilichowaka moto.

Neema ilimfanya Isaya kuona utukufu wa Mungu na alisema β€œOle wangu!”, lakini akatakaswa na kutumwa.

Neema ilibadilisha historia ya Petro, akatoka kuwa mvuvi wa kawaida na kuwa mtume mwenye nguvu baada ya kukutana na Yesu.

Neema ilibadilisha historia ya Paulo, kutoka kuwa mtesaji wa kanisa akawa mhubiri mkuu baada ya kukutana na Kristo njiani kwenda Dameski.

Neema ilibadilisha historia ya Yohana, akapata ufunuo mkubwa kisiwani Patmo, na kuandika kitabu cha Ufunuo.

Ita neema ya Mungu kwako na hadithi ya maisha yako itabadilika.

NEEMA YA MUNGU1 PETRO 5:10Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiish...
07/05/2026

NEEMA YA MUNGU

1 PETRO 5:10
Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

Neema ni kustahilishwa pale usipo stahili, au kupokea kitu ambacho hukukifanyia kazi.
Neema ni nguvu ya Mungu isiyopimwa kwa juhudi za mwanadamu, wala haifungwi na historia ya mtu.

Neema inapokuja haikagui vyeti vyako, haipimi uwezo wako, wala haisikilizi maneno ya watu, huja kimya kimya, lakini matokeo yake huonekana wazi na hubadilisha kabisa hadithi ya maisha ya mtu.

Katika maisha ya kawaida, dunia hutufundisha kuwa mafanikio yanatokana na elimu, uzoefu, au sifa fulani, lakini neema ya Mungu hufanya kazi tofauti.

Inamchukua mtu aliyedharauliwa na kumweka juu, inamchukua aliyekataliwa na kumpa heshima, inamchukua aliyepoteza matumaini na kumrudishia kusudi.

Hapo ndipo tunaona kuwa si kila kitu kinategemea juhudi zetu binafsi, Bali kuna mkono wa Mungu unaoweza kubadilisha mambo ndani ya mfupi.

Neema inapokuja juu yako, ghafla mambo huanza kubadilika, ndio pale watu huanza kusema inawezekanaje? lakini jibu lake ni moja tu NI NEEMA

Neema inafungua milango iliyofungwa, inakuinua pale ulipoanguka, na inakuweka mahali ambapo usingefika kwa nguvu zako mwenyewe.

Jambo la muhimu na kuzingatia ni kuwa neema ya Mungu inahitaji moyo wa unyenyekevu na imani, huwezi kuipokea ukiwa umejaa kiburi au kukata tamaa.

Lazima uwe tayari kuamini kuwa Mungu anaweza kukufanyia jambo jipya, hata k**a hali yako ya sasa inaonekana tofauti.

Haijalishi watu wanasema nini juu yako, haijalishi una vyeti vingapi au hujasoma, neema ya Mungu inaweza kubadilisha maisha yako leo.

Hadithi yako haijaisha, inaweza kuandikwa upya na Mungu kwa njia ambayo hata wewe mwenyewe itakushangaza.

Neema haiji kwa sababu unastahili, huja kwa sababu Mungu ameamua kukutazama kwa upendo wake na inapokupata, haitaki ruhusa ya mtu yeyote.

Tunaposoma maandiko tunaona jinsi neema ya Mungu ilivyobadilisha historia za watu k**a Daudi, Yusuf, Petro, Yohana, Ibrahim, Yakobo, Musa na wengine wengi.

Ita neema ya Mungu kwako na hadithi ya maisha yako itabadilika.

Address

Salasala
Dar Es Salaam

Telephone

+255754586607

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when bhgministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to bhgministry:

Share