Efatha Church Chanika Ukombozi

Efatha Church Chanika Ukombozi EFATHA maana yake FUNGUKA.

SOMO:      UKOMBOZI WA FIKRAKNGZ :      MCH GEORGE MWANYIKAUkombozi ni mchakato ambao mtu lazima apitie ili kurudi kweny...
13/08/2025

SOMO: UKOMBOZI WA FIKRA
KNGZ : MCH GEORGE MWANYIKA

Ukombozi ni mchakato ambao mtu lazima apitie ili kurudi kwenye asili yake na kuwa mkamilifu.
Ukombozi ni hatua ya mtu kukamilishwa, kuna aina tatu kuu za ukombozi.
(1)Ukombozi wa nafsi
(2)Ukombozi wa mwili
(3)Ukombozi wa roho

UKOMBOZI WA NAFSI
Nafsi ni kiunganishi kati ya mwili na roho, hivyo kwenye nafsi ndipo palipo na asili yetu
( mwanzo 2:7)
Uwezo na asili ya mtu imebebwa kwenye nafsi, hii ndio maana falme zikitaka kukufanya usiwe chochote chini ya jua wanak**ata nafsi yako

HIVYO NAFSI NDIO INAYOKOMBOLEWA NA SIO ROHO WALA MWILI
(Isaya 42:22 )
Kwenye nafsi ndio mtu anafungwa minyororo, Kamba, nira na katika mwili unaona huyu mtu hakuna mahali anakwenda
Kwenye nafsi ndio kuna; fikra, maamuzi, uwezo, akili.

UKOMBOZI WA MWILI
Hapa ndio kuna kuponywa magonjwa, maradhi
Hapa ndipo unaona yote yanayoendelea katika nafsi na roho
Ndio maana yesu alitoa mwili wake kuwa sadaka takatifu kwaajili yetu, hivyo na wewe unapaswa kutoa mwili wako kuwa dhabihu kwa Bwana,
(WARUMI 12: 1-2)
Hivyo namna ulimwengu unavyoenenda ambavyo mwisho wake ni uharibifu,Paulo anatushauri tutoe miili yetu kuwa dhabihu kwa Bwana
(WARUMI 8:13)
Hivyo njia salama ya kuponya mwili wako na uharibifu ni kuufanya kuwa dhabihu,
Paulo kaanisha matendo ya mwili
(WAGALATIA 5:19-21)
UKOMBOZI WA MWILI UNAHUSISHWA NA MAAMUZI YAKO MWENYEWE

UKOMBOZI WA ROHO
Hapa ndipo mtu anazaliwa kwa mara ya pili
Hapa ndipo asili yetu ilipo (YOHANA 3:3-6)

SASA BAADA YA HAYA YOTE KUFANYIKA HAIMAANISHA SASA UPO SALAMA, LIPO JAMBO LA MSINGI SANA LA KUZINGATIA , ILI UFIKE KWENYE UKAMILIFU
(MATHAYO 12: 43-45)

03/08/2025
NAMNA YA KUSHINDA KWENYE NAFASI NA KUDUMU NDANI YAKE1. Tambua nafasi yako ni kwa Ajili ya MunguKila nafasi ni kwa ajili ...
03/08/2025

NAMNA YA KUSHINDA KWENYE NAFASI NA KUDUMU NDANI YAKE

1. Tambua nafasi yako ni kwa Ajili ya Mungu
Kila nafasi ni kwa ajili ya kazi ya Mungu, si kwa ajili ya sifa au malengo binafsi.

Mungu akikupa nafasi, kuna watu wanaopaswa kuponywa, kuinuliwa au kuongozwa kupitia wewe.

Kukwazika au kukataa kutimiza nafasi kwa sababu ya changamoto ni ishara ya kiburi kwamba unajiona wewe ni wa muhimu kuliko roho za watu walioko kwenye hatari.

2. Kuwa Macho wakati wote na kuwa na Umakini
Yesu alisema, “Kesheni na kuomba…” (Mathayo 26:41).

Ukimakinika rohoni, hata ukiwa kwenye shughuli zako za kila siku, roho yako inaweza kuwa katika hali ya maombi.

3. Tunza Neno na maelekezo yanayohusu Nafasi Yako

4. Boresha utendaji wako kila iitwapo leo, uwe na mtembeo wa kwenda mbele na sio kurudi nyuma.

5. Chunga Kinywa Chako
Mithali 18:21: “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi.."

Unaweza kuamini kwa moyo, lakini kinywa ndicho kinachokuletea wokovu au maangamizi.

Kila neno unalosema linaanza kukufanyia kazi wewe kwanza kabla ya kufikia mtu mwingine.

Mfano: Ukisema maneno ya laana, yanakuharibu wewe kwanza ndipo yaende kwa wengine.
Kinywa kinaweza kuwa daraja la baraka au la laana, hivyo chagua kwa hekima.

© Katibu Mkuu Kanisa la Efatha- Professor Emmanuel Chao

NENO LA LEO:Ufunuo wa Yohana 2:1-4 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo...
03/08/2025

NENO LA LEO:

Ufunuo wa Yohana 2:1-4 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azishikaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo; tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka. Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.”

SOMO: MAMBO YA KUZINGATIA NA TAHADHARI YA KUHUSU NAFASI

Tahadhari 1: Usiache Upendo wako wa Kwanza

• K**a Kanisa la Efeso, unaweza kuwa umeanza vizuri, ukiwa na bidii, subira na uaminifu, lakini ukasahau upendo wa kwanza.
• Mungu anapima mwisho wa safari yako, si mwanzo tu. Ni lazima uzidi kuwa bora kila iitwapo leo.
• Tabia za wale wanaokaa na Mungu ni kuwa kila iitwapo leo wanakuwa bora kuliko jana, hatutegemei mtu anayetembea kwenye ufalme wa MUNGU , anaanza na mambo mazuri lakini kila iitwapo leo, watu wanamuewekea mashaka.
• Hakikisha namna ulivyoanza unakamilisha kwa bora zaidi

Tahadhari 2: Majaribu Yanayohusiana na Nafasi

• K**a Kanisa la Smirna, lililoonekana maskini lakini lilikuwa tajiri kiroho.
• Kuna majaribu mawili:
1. Jaribu la kukufikisha kwenye nafasi (k**a Yusufu au Ibrahimu).
2. Jaribu la kukutoa kwenye nafasi (k**a wana wa Israeli walioshindwa kuingia Kaanaani).
• Usipite jangwani bila kujifunza. Elimu ya jangwani ni kuhusu imani na utii.

Tahadhari 3: Kusikiliza Taarifa za Uongo
• K**a Kanisa la Pergamo, lililokaa “katika kiti cha enzi cha shetani.”
• Mafundisho ya uongo na maneno yasiyo ya dini huiba "amana" yako ya imani.
• Kuwa mwangalifu na kile unachosikiliza, maneno mabaya huharibu tabia njema.

Tahadhari 4: Kuridhika Katika Nafasi
• K**a Kanisa la Thiatira, lililokuwa na matendo mazuri lakini likaruhusu mafundisho ya uongo ya Yezebeli.
• Kuridhika na kutosheka kunaua bidii, kunaondoa njaa ya kiroho.
• Usikubali hali yako ya sasa kuwa mwisho wa maendeleo yako ya kiroho.

K**a MUNGU anakuinua, nyenyekea zaidi, maana hivyo ndiyo silaha ya vita yako.

© Katibu Mkuu Kanisa la Efatha- Professor Emmanuel Chao

Zaburi 100:1-5 "Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwa...
03/08/2025

Zaburi 100:1-5 "Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi."

17/07/2025

KANISA LA EFATHA CHANIKA BUYUNI _ DAR ES SALAAM Limekuandalia Semina kubwa ya neno la MUNGU itakayofanyika tarehe 31/7-2/8/2025 Katika kanisa la Efatha Chanika Buyuni.

Semina hii itaongozwa na Mchungaji Michael Kabalila na Mchungaji Bertha Masaki wa kanisa la Efatha Chanika Buyuni na itaanza 10:00 alasili hadi 12:00 Jioni.

Usipange kukosa mwana wa MUNGU, Walete wagonjwa na wenye shida mbali mbali wataombewa, nyote mnakaribishwa.

17/07/2025

SOMO: ONDOA HOFU NDANI YAKO

2 Timotheo 1:7 "Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. "

Rum 8:15 "Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba".

Hofu inaua haraka kuliko hata tatizo lenyewe. Hofu siyo tu inaondoa ujasiri, bali inaua ujasiri na nguvu chanya ndani yako ni chanzo cha wengi kutotimiza ndoto, maono na malengo yao. Ni silaha kubwa anayoitumia shetani na mawakala wake ili kuchinja, kuharibu na kuua hatima nzuri za watu.

Shetani huitumia hofu k**a silaha kubwa ya kutufanya tuogope kuthubutu katika kufanya mambo mazuri kwa ajili ya hatima zetu. Hofu ni silaha anayoitumia shetani ili tushindwe kuutumia uwezo wetu wote na kuua Imani yetu kwa Mungu. Pia ni pepo au mlango wa kuzimu wa kutuondolea amani, furaha na upenyo.

Usikubali hofu ikutawale, usikubali mtu au kitu kikupandikize hofu, usikubali kumezwa na hofu wala usiruhusu moyo na akili zako ziatamiwe na hofu.

Chochote kizuri unachowaza kufanya au unachokifanya Kifanye kwa ujasiri bila woga.

Novatus Robert - Efatha Kahama.

08/07/2025

Tarehe 4/7/2025
MKESHA WA IBADA YA SIFA

Yesu wetu mzuri sana. Uliwezaje kukosa?
Hakikisha wakati ujao haukosi kuhudhuria kwenye Mkesha wa Kusifu na Kumwabudu Bwana.

08/07/2025

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Mimi na Familia yangu TUMEBARIKIWA na BWANA; Furaha, Amani, Kicheko havitaondoka katika Nyumba yetu.

Haleluya, YESU ni Mzuri sana.

Tarehe 4/7/2024Wachungaji wa Kanda "D" wakiongozwa na Mch Bertha katika ibada ya Kusifu na Kuabudu iliyofanyika Chanika ...
08/07/2025

Tarehe 4/7/2024
Wachungaji wa Kanda "D" wakiongozwa na Mch Bertha katika ibada ya Kusifu na Kuabudu iliyofanyika Chanika Ukombozi.
Kusifu kwawapasa Wanyoofu wa Moyo

Tarehe 4/7/2025Efatha church Chanika ukombozi.Wachungaji na waumini mbalimbali katika mkesha wa kusifu na kuabudu.
08/07/2025

Tarehe 4/7/2025

Efatha church Chanika ukombozi.

Wachungaji na waumini mbalimbali katika mkesha wa kusifu na kuabudu.

Address

Zogoali
Dar Es Salaam

Telephone

+255784662055

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Chanika Ukombozi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Chanika Ukombozi:

Share