06/04/2026
SEMINA YA PASAKA 03/04/ 2026
KSMT- KIGAMBONI
SIKU YA 01.
SOMO: USHAHIDI KUWA YESU ALIKUFA KWA AJILI YETU.
Tunaposherehekea siku kuu ya pasaka ni muhimu kuzungumzia kifo cha Yesu Kristo. Kifo hiki cha Yesu ni halisi, siyo nadhalia kwasababu;
i. Ni kweli kwamba Yesu alikufa (kaburi lipo)
ii. Ni kweli kwamba Yesu alifufuka (Kaburi wazi lipo Yesrusalemu)
Marko 16:5 -6
Usibabaishwe na watu ambao wanasema kwamba Yesu hakufa na kwamba hakufufuka, Ushahidi upo na hao lengo lao ni kuiua Imani ya kweli iliyopo ndani yako.
Kifo cha Yesu hakikuwa kifo cha kawaida, bali kilikuwa kifo chenye faida.
MAMBO MATATU (3) KUTHIBITISHA KUWA YESU ALIKUFA KWA AJILI YETU.
i. Yesu hakuwa na kosa. Luka 23:4 -7
K**a kifo cha Yesu kingekuwa kifo cha kawaida, basi Yesu asingekufa.
Yesu aliposh*takiwa mbele ya pilato, pilato hakuona sababu ya kumhukumu kifo, akaamua kumpeleka kwa Herode, Herode naye akamrudisha kwa Pilato.
Yesu alikufa bila kosa ili sisi wanadamu tunaokosea, tukimwamini tuhesabiwe haki.
Warumi 3:23 -25
ii. Yesu alikufa badala ya mtu aliyekuwa amehukumiwa kifo. Luka 23: 24 – 25
- Yesu alihukumiwa badala ya Baraba.
- Baraba aliwakilisha watu wote wenye dhambi, badala ya wao kufa; sasa wanatakiwa kumwamini Yesu Kristo aliyekufa badala yao. Warumi 10:10
iii. Yesu alikufa ili kuleta upatanisho. Luka 23:12
Mfano mzuri wa jambo hili ni kile kilichotokea baina ya Pilato na Herode! Watu hawa walikuwa na uadui wa muda mrefu, lakini kutokana na kusurubiwa kwa Yesu na kifo chake walipatana kwa urafiki.
- Jambo hili lilikuwa limetabiliwa tangu wakati ule Yesu anazaliwa, yakwamba ameleta amani Duniani. Luka 2: 14
- Utaona pia kwamba baada ya Yesu kukata roho, waliokuwa hawaelewani, kwa maana ya kutokubaliana na ukweli kuhusu Yesu Kristo, waligeuka na kuwa kitu kimoja. Luka 23:47,
- Mtu mwenye dhambi aliye kuwa amesurubishwa msalabani, alipataniswa na Mungu akiwa msalabani, baada ya kumwamini Yesu. Lika 23:41:43
Huo ni muhtasari wa somo tulilojifunza katika semina ya pasaka. Siku ya kwanza tar 03/04/2026.
Nitashirikisha somo la siku ya pili.