Kanisa la sauti ya matumaini Tanzania

Kanisa la sauti ya matumaini Tanzania Kanisa la sauti ya matumaini Tanzania linajikita katika huduma ya kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi.

19/05/2026

Siri Moja wapo itakayomsaidia Kila mtu kuishi maisha yenye furaha ni kujua kwamba Kila kitu kimefungwa katika majira yake.

Yohana 10:39, ukisoma hapo unakuta badhi ya Wayahudi walimk**ata Yesu, lakini Kwa Sababu yalikuwa siyo majira ya Yesu kuk**atwa na Hilo alilijua, kwahiyo hakupoteza furaha yake, Bali alitoka mikononi mwao.

Nataka utiwe moyo Kwa ujumbe huu!

Kila Hali unayoipitia ambayo siyo majira yake, ikuachie Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazereti.

17/05/2026

Moja ya Siri zitakazo msaidia Kila mtu kuishi maisha ya furaha ni Maombi.

Yesu aliishi maisha ya ushindi Kwa sababu alipenda sana Maombi.

01/05/2026

Maombi ambayo Mungu hasikii,

Sina hakika k**a umewahi kujiuliza kuhusu aina hii ya Maombi! Ndiyo! Maombi ambayo Mungu hajibu.

Siyo Kila Maombi ambayo tunaomba kwamba Mungu anayajibu, mengine Mungu Huwa hajibu.

MATHAYO 6: 5-8.

Mstari wa 7 anasema "Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, k**a watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi".

Kutokea hapo tunaona aina ya kwanza ya Maombi ambayo Mungu hajibu.
===> Maombi ya kupayuka - payuka. Mungu huwa hajibu aina hii ya Maombi.
Sasa hapa Yesu hakukatazi kuomba Kwa sauti, maana hata yeye Aliomba Kwa saiti.
Hapa jambo la muhimu ni maana ya kupayuka - payuka. Kwa kawaida kupayuka - payuka ni kuongea Kwa sauti bila kuhusisha roho yako.

Maombi ya kupayuka - payuka ni kuomba Maombi ambayo hayatoki moyoni. Maneno yanatoka mdomoni ila siyo moyoni, hayo Mungu hajibu.

Yeremia 1:15.
Hapa tunaona aina ya pili ya Maombi ambayo Mungu hasikii.

===> Maombi ya Mwenye dhambi.
Mungu hasikikii maombi ya mtu mwenye dhambi, isipokuwa pale anapoomba toba.

Unapokuwa umetubu dhambi zako, na kuomba kutoka katika roho (Kwa kumaanisha) haijalishi ni Kwa sauti kwabwa au ndogo, Mungu anasikia na kujibu.

Lakini pale unapoomba ukiwa na dhambi zisizo tubiwa Mungu hajibu au unapoba Maombi ya juu juu bila kuingia rohoni Mungu hajibu.

Shalom shalom

Hii ndiyo Sababu kwanini ulimwengu unamuhitaji sana Yesu.K**a isingekuwa kosa ambalo shetani alilifanya la kushindwa kum...
29/04/2026

Hii ndiyo Sababu kwanini ulimwengu unamuhitaji sana Yesu.
K**a isingekuwa kosa ambalo shetani alilifanya la kushindwa kumtii Mungu kusingekuwa na dhambi kabisa.
Kwasababu shetani aliasi, na kutupwa chini ndiyo Sababu iliyopelekea amdanganye mwanadamu. Ule udanganyofu ulipelekea dhambi kuingia katika maisha ya mwanadamu.

Sasa Yesu anahitajika kwa Sababu katika nafasi yake k**a mwanadamu alikubali kutii hata kifo Cha msalaba. Kwahiyo kule kutokutii wa Shetani kunakuwa siyo kitu tena Kwa Sababu utii wa Bwana Yesu, ambaye tunapomwamini tunapatanishwa na Mungu.

Kukosa imani katika Kristo ni hasara. "Warumi 3:23-24
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;"

Shalom Shalom.

28/04/2026

Huku ndiko hekima na maarifa ziliko.
Kujihurumia ni Sababu kubwa sana ya kumzuia mtu kupiga hatua katika maisha

Yesu katika Mathayo 7:13-14  alifundisha kuhusu Njia. Akiwaambia watu kuingia kupitia mlango ulio mwembamba, ambao njia ...
27/04/2026

Yesu katika Mathayo 7:13-14 alifundisha kuhusu Njia.
Akiwaambia watu kuingia kupitia mlango ulio mwembamba, ambao njia yake ni imesonga, na anasema wengi watatamani kuingia lakini wasiweze na yakwamba wengi wataingia kupitia mlango mpana ambao na njia yake ni pana.

Kuna ufunuo niliupata wakati nasoma mistari hiyo: -
1. Njia hizi ni kuhusu matendo yetu ya Kila siku. Kwamba ni rahisi mtu kutenda mambo yasiyompendeza Mungu kuliko kutenda Yale ya kumpendeza Mungu.

Kwa maelezo zaidi juu ya hili ni kwamba, Yale yote yanayotusogeza karibu na Mungu hatuyafanyi kirahisi, inahitaji kujikana na kuwa na bidii, lakini Yale ambayo hayana umuhimu Kwa habari ya ufalme wa Mungu mtu anaweza kujikuta ameyatenda hayo hata bila kutumia nguvu yoyote. Ndiyo maana Yesu alisema wengi huingia kupitia mlango mpana.

2. Kwanini Yesu alitumia kielelezo Cha njia kufundisha habari za ufalme wa Mungu?
- Watu waliomwamini Mungu kupitia Yesu Kristo, waliitwa watu wa Njia Ile ( Ndo 22:4)
- Watu walianza kuitwa wakristo mwaka 47 baada ya Kristo kuzaliwa (Mdo 11:26)
Lakini pia Yesu alitumia kielelezo Cha njia Kwa Sababu Yeye mwenyewe alijitambulisha k**a Njia. Yoh 14:6

Kwahiyo Mtu anapomwamini Kristo anakuwa ameingia katika Njia ya uzima, kuwa mkristo ni kuwa mtu wa Njia Ile.

Ukristo ni njia,
Njia inalindwa,
Njia ukiifuata Kwa usahihi haupotei.
Kaa kwenye njia, safari bado inaendelea.

SHALOM SHALOM
MWL HELMAN JOHN
0765002856
27/04/2026

26/04/2026

Leo somo letu lilikuwa kuhusu Njia.
Imekuwa jumapili ya Baraka sana.

Maumivu yenye faida.Hakuna mtu ambaye hajawahi kupita kwenye maumivu Fulani, na Kila wakati mtu anapopitia kwenye maumiv...
11/04/2026

Maumivu yenye faida.
Hakuna mtu ambaye hajawahi kupita kwenye maumivu Fulani, na Kila wakati mtu anapopitia kwenye maumivu anakuwa na maswali ya kujiuliza. Mara nyingi maswali hayo ni kuhusu watu ambao huenda ndio ambao wamesababisha maumivu hayo.

Jambo ambalo nataka nikuonyeshe ni kwamba Kuna baadhi ya maumivu Huwa ya ebeba faida ndani yake.

Mfano.
Maumivu aliyoyapitia Daniel yalikuwa yamebeba faida ya kuwa waziri mkuu katika nchi ya Babeli.

Yale aliyoyapitia ayubu yalikuwa yamebeba faida ya kumtambulisha k**a mcha Mungu wa kweli, na kumthibitishia shetani kuwa siyo Kwa sababu ya Mali Wala afya Ayubu kumpenda Mungu.

Maumivu anayoyapata mama wakati wa kujifungua yanakuwa yamebeba faida ya kumleta mtoto katika familia.

Je, wewe unapitia katika maumivu Gani?
Jambo unalotakiwa kuwa na uhakika nalo ni Sababu ya maumivu unayoyapitia.
Ukipitia maumivu k**a Yale ambayo Yona aliyapitia ujue ni Kwa sababu umekataa kwenda ninawi!
Ukipitia maumivu k**a ya Samsoni baada ya kutobolewa macho, ujue ni kwasababu umejiachilia kwa Dalila.

Maana yake ni kwamba maumivu yanayotokana na makosa ambayo tumeyafanya Huwa hayana faida kamwe Bali Huwa yamebeba maumivu ndani yake.

_________________________KESHO____________________________
NITAFUNDISHA SOMO HILI NA KUOMBEA WATU AMBAO WAPO KWENYE MAUMIVU.

KSMT - KIGAMBONI
Saa 9:00 - 11:30 asubuhi.
0765002856

SEMINA YA PASAKA 03/04/ 2026KSMT- KIGAMBONISIKU YA 01. SOMO: USHAHIDI KUWA YESU ALIKUFA KWA AJILI YETU.Tunaposherehekea ...
06/04/2026

SEMINA YA PASAKA 03/04/ 2026
KSMT- KIGAMBONI
SIKU YA 01.
SOMO: USHAHIDI KUWA YESU ALIKUFA KWA AJILI YETU.
Tunaposherehekea siku kuu ya pasaka ni muhimu kuzungumzia kifo cha Yesu Kristo. Kifo hiki cha Yesu ni halisi, siyo nadhalia kwasababu;
i. Ni kweli kwamba Yesu alikufa (kaburi lipo)
ii. Ni kweli kwamba Yesu alifufuka (Kaburi wazi lipo Yesrusalemu)
Marko 16:5 -6
 Usibabaishwe na watu ambao wanasema kwamba Yesu hakufa na kwamba hakufufuka, Ushahidi upo na hao lengo lao ni kuiua Imani ya kweli iliyopo ndani yako.
 Kifo cha Yesu hakikuwa kifo cha kawaida, bali kilikuwa kifo chenye faida.

MAMBO MATATU (3) KUTHIBITISHA KUWA YESU ALIKUFA KWA AJILI YETU.
i. Yesu hakuwa na kosa. Luka 23:4 -7
K**a kifo cha Yesu kingekuwa kifo cha kawaida, basi Yesu asingekufa.
 Yesu aliposh*takiwa mbele ya pilato, pilato hakuona sababu ya kumhukumu kifo, akaamua kumpeleka kwa Herode, Herode naye akamrudisha kwa Pilato.
 Yesu alikufa bila kosa ili sisi wanadamu tunaokosea, tukimwamini tuhesabiwe haki.
Warumi 3:23 -25

ii. Yesu alikufa badala ya mtu aliyekuwa amehukumiwa kifo. Luka 23: 24 – 25
- Yesu alihukumiwa badala ya Baraba.
- Baraba aliwakilisha watu wote wenye dhambi, badala ya wao kufa; sasa wanatakiwa kumwamini Yesu Kristo aliyekufa badala yao. Warumi 10:10

iii. Yesu alikufa ili kuleta upatanisho. Luka 23:12
Mfano mzuri wa jambo hili ni kile kilichotokea baina ya Pilato na Herode! Watu hawa walikuwa na uadui wa muda mrefu, lakini kutokana na kusurubiwa kwa Yesu na kifo chake walipatana kwa urafiki.
- Jambo hili lilikuwa limetabiliwa tangu wakati ule Yesu anazaliwa, yakwamba ameleta amani Duniani. Luka 2: 14
- Utaona pia kwamba baada ya Yesu kukata roho, waliokuwa hawaelewani, kwa maana ya kutokubaliana na ukweli kuhusu Yesu Kristo, waligeuka na kuwa kitu kimoja. Luka 23:47,
- Mtu mwenye dhambi aliye kuwa amesurubishwa msalabani, alipataniswa na Mungu akiwa msalabani, baada ya kumwamini Yesu. Lika 23:41:43

Huo ni muhtasari wa somo tulilojifunza katika semina ya pasaka. Siku ya kwanza tar 03/04/2026.

Nitashirikisha somo la siku ya pili.

Nakutakia heri ya pasaka ya Leo 2026 Kutokea  KSMT - KIGAMBONI
05/04/2026

Nakutakia heri ya pasaka ya Leo 2026 Kutokea KSMT - KIGAMBONI

Address

P. O. BOX 14868 DSM
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kanisa la sauti ya matumaini Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kanisa la sauti ya matumaini Tanzania:

Share