Full Gospel Bible Fellowship Church

Full Gospel Bible Fellowship Church Mahali linapohubiriwa Neno la Mungu lisiloghoshiwa
(2 WAKORINTHO 2:17)

■ IBADA KUU, JUMAPILI 31.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanza...
31/05/2026

■ IBADA KUU, JUMAPILI 31.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Hii ni Ibada Kuu ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; Jumapili ya tarehe, 31.5.2026; ambapo maelfu ya watu, wamekusanyika ili kusikia Maneno yenye Uzima; ya BWANA wetu, Yesu Kristo (1 TIMOTHEO 6:3).

Maneno ya Uzima ya BWANA wetu Yesu Kristo, siku hii; yameletwa kwetu, kupitia kwa Mtumishi wa Mungu, Mchungaji Hellen Kakobe; aliyefundisha Somo lenye kichwa, "NALIKUWA MGENI, MSINIKARIBISHE". Heri (Amebarikiwa), yeye aliyelisikia Neno hili; na kulishika (LUKA 11:28).

Aidha, kutokana na Neno hili; watu kadha wa kadha, wenye dhambi; wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 26:20); na kumkaribisha Yesu Kristo, katika mioyo yao; aliyewasafisha dhambi zao kwa Damu yake iliyomwagika msalabani (MATHAYO 26:28; 1 YOHANA 1:7); na kuwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12; 1 YOHANA 3:8-10).

Baada ya Somo hili zuri, lenye ufunuo mkubwa; Mungu wetu, tunakusihi; umpe kila mmoja wetu, kukumbuka daima Neno lako, katika YAKOBO 1:22, "Lakini iweni watendaji wa Neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu"; ili siku zote, tudumu kufanya yale yakupendezayo (YOHANA 8:29). ●

■ IBADA KUU, JUMAPILI 24.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanza...
24/05/2026

■ IBADA KUU, JUMAPILI 24.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Mtu awaye yote, akitaka kuwa miongoni mwa washindao (UFUNUO WA YOHANA 2:7,11,17,26-29; 3:5,12); inampasa kuwa na shauku isiyoisha, ya kupata Maneno ya Maarifa (MITHALI 23:12); na Maneno ya Ufahamu (MITHALI 1:2). Ni kwa sababu hii, sasa; ndiyo maana, maelfu ya watu hawa, wamekusanyika tena, Jumapili, tarehe 24.5.2026; katika Ibada Kuu ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge.

Siku hii, Maneno ya Maarifa, na Maneno ya Ufahamu, yaliyotoka kwa BWANA; yamekuja kwa Kanisa, kupitia kwa Mtumishi wa Mungu, Mchungaji Hellen Kakobe; aliyefundisha Somo lenye kichwa, "K**A YESU ALIVYOSHINDA (UFUNUO WA YOHANA 3:21)". Heri (Amebarikiwa), yeye aliyelisikia Neno hili; na kulishika (LUKA 11:28).

Aidha, kutokana na Neno hili; watu kadha wa kadha, wenye dhambi; wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 26:20); na kumpokea Yesu Kristo, aliyewasafisha dhambi zao kwa Damu yake iliyomwagika msalabani (MATHAYO 26:28; 1 YOHANA 1:7); na kuwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12; 1 YOHANA 3:8-10).

Mungu wetu, na Ashukuriwe; atupaye kushinda, kwa Bwana wetu Yesu Kristo (1 WAKORINTHO 15:57). Utukufu una Yeye, milele na milele; Amina (WAGALATIA 1:5).

■ INJILI MITAANI, JUMAMOSI 23.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM ■ KUHUBIRI INJILI MITAANI, KATIKA MITAA NA VICHOCHOR...
24/05/2026

■ INJILI MITAANI, JUMAMOSI 23.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ KUHUBIRI INJILI MITAANI, KATIKA MITAA NA VICHOCHORO VYA JIJI LA DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

■ NI INJILI YA MTU KWA MTU, NYUMBA KWA NYUMBA, NA VICHOCHORO VYAKE; NA KWA KILA KUNDI LA WATU (MATENDO YA MITUME 20:20, 26-27)

■ JUMLA YA IDADI YA WATU WAZIMA WALIOOKOKA SIKU HIYO: 1385

■ NI KAZI YA MUNGU, ILIYOFANYWA NA WASHIRIKA WA KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM, JUMAMOSI YA UINJILISTI; 23.5.2026

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Hizi, ni picha zinazowaonyesha baadhi ya Washirika; ambao ni miongoni mwa mamia ya Washirika wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; waliokuwa wakihubiri Injili Mitaani; mtu kwa mtu, nyumba kwa nyumba, na vichochoro vyake; na kwa kila kundi la watu; katika pembe zote za Jiji la Dar-Es-Salaam, na viunga vyake; Siku ya Jumamosi, tarehe 23.5.2026. Wakati unapozitazama picha hizi, ZINGATIA PIA, UJUMBE UFUATAO, KUTOKA KWA ASKOFU MKUU ZACHARY KAKOBE:

"Ndugu yangu mpendwa, jambo la kuzingatia, ni kwamba; picha hizi, siyo picha za tukio spesheli au mahususi, lililopangwa na kuandaliwa maalum, linalotokea kwa nadra; bali ni shughuli au hali ya utendaji wa kawaida, katika maisha ya Washirika wengi wa Kanisa la FGBF Dar-Es-Salaam. Kwa miaka mingi sasa, kuhubiri Injili mitaani, imekuwa ni sehemu ya maisha ya Washirika wengi wa Kanisa la FGBF Dar-Es-Salaam. Ukiacha Jumamosi kadhaa kila mwezi, zinazoitwa "JUMAMOSI ZA UINJILISTI"; ambapo Washirika wote huingia mitaani kushuhudia au kuhubiri Injili, katika maeneo mbalimbali ya Zoni zao; vilevile, Washirika katika Seksheni, na Makanisa ya Nyumbani, kadha wa kadha; hupanga mikakati yao wenyewe, na kuwa na siku tofauti tofauti, katika wiki, za kufanya kazi hii; achilia mbali makundi ya Washirika wachache wachache, ambao huhubiri Injili, takriban kila siku. Na zaidi sana, Washirika wengi binafsi hutumia kila fursa wanayoipata kila siku, kuhubiri Injili; iwe ni katika daladala, au mahali pengine popote. Kila Mshirika katika Kanisa hili, ni wajibu wake kuihubiri kila mahali; Habari Njema ya MWOKOZI WA ULIMWENGU, YESU KRISTO (1 YOHANA 4:14; YOHANA 4:42)."

"Kazi hii ya Kuhubiri Injili, siyo kazi ya Askofu au Mchungaji fulani, PEKE YAKE; wala siyo kazi ya Mwinjilisti au Mhubiri fulani "Mkubwa" wa Kimataifa, peke yake! NI KAZI INAYOPASWA KUFANYWA NA KILA MTU ALIYEOKOKA, awe ni mwanamume au mwanamke (MATENDO YA MITUME 2:18, 21); au ameokoka zamani, au ameokoka hivi karibuni (YOHANA 1:40-42; 4:5-30, 39-42). Hivi ndivyo ilivyokuwa Nyakati za Kanisa la Kwanza. Sauli aliposababisha adha kuu ya Kanisa la Kwanza, WASHIRIKA WOTE (wanaume pamoja na wanawake); walitawanyika na kwenda huko na huko, KULIHUBIRI NENO. Biblia inatupa simulizi hii, katika MATENDO YA MITUME 8:1, 3-4, "Siku ile kukatukia adha kuu ya Kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; WOTE WAKATAWANYIKA katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. Sauli akaliharibu Kanisa, akaingia kila nyumba, na kuwaburuta WANAUME NA WANAWAKE na kuwatupa gerezani. Lakini WALE WALIOTAWANYIKA (wangapi? Wote!) WAKAENDA HUKO NA HUKO WAKILIHUBIRI NENO." Unaweza kuona! Mitume, wao hawakwenda; bali WASHIRIKA WOTE, WANAUME KWA WANAWAKE walikwenda; kwa kuogopa kuburutwa na Sauli, na kupelekwa gerezani. Na kule walikokwenda, WOTE wakalihubiri Neno, wote wakaihubiri Injili."

"Hapo awali, Yesu Kristo alikuwa amewapa Washirika hao, Agizo Kuu, ambalo linatuhusu sisi pia; la kwenda kuhubiri Injili kwa kila kiumbe (MARKO 16:15); na baadaye Yesu akawaambia wakawe mashahidi wake Uyahudi wote na Samaria (MATENDO YA MITUME 1:8); lakini hawakutii maagizo hayo, bali waliendelea tu kujibariki na kujiburudisha wenyewe Kanisani, kwa mapambio; k**a wengi wetu tunavyofanya; mpaka pale Sauli alipoanza kuingia nyumba kwa nyumba, na kuwaburuta gerezani; NDIPO wakalazimika kwenda kuhubiri Injili Uyahudi na Samaria!! Je, na ninyi katika Kanisa lenu, au na wewe binafsi, unasubiri mpaka Mungu amwachie Sauli awaletee, au akuletee adha kuu, ndipo ulazimike kwenda kuhubiri huko na huko? SAA YA KUAMKA KATIKA USINGIZI IMEKWISHA KUWADIA! (WARUMI 13:11-12). Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, itahubiriwa katika Ulimwengu wote, KUWA USHUHUDA KWA MATAIFA YOTE; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja (MATHAYO 24:14)."

"Ndugu yangu, uliyeokoka; bila kujali kwamba, WEWE ni Mshirika wa Kanisa gani; kumbuka kwamba, NI OLE WAKO USIPOIHUBIRI INJILI (1 WAKORINTHO 9:16-17). Usingojee mpaka Mungu amlete Sauli kukushurutisha, kufanya hivyo! Wala usitoe udhuru kwamba, wewe bado mchanga kiroho; hujajua sana Neno la Mungu. KILA AMWAMINIYE YESU, MWANA WA MUNGU; ANAO HUO USHUHUDA NDANI YAKE (1 YOHANA 5:10). Ndani yako kuna ushuhuda, utumie ushuhuda huo, katika kuwashuhudia au kuwahubiria Injili, watu wengine. Ushuhuda wako ni upi? Ni Neno lile ulilolipokea, ambalo lilikufanya ukate shauri kuokoka. Nenda mitaani, ukalitumie Neno hilohilo kuwahubiria watu wengine. Anzia hapo!! (YOHANA 1:35-46)."

"Aidha, wako watu wengine wanaosema kwamba wamejazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu, na wananena kwa lugha (MATENDO YA MITUME 1:8; 2:4). Ni vema, na ni vizuri sana! Hata hivyo, kinachoshangaza, ni kwamba; baadhi ya watu hawa, wanaosema wamejazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu; tangu "wajazwe Nguvu hiyo", siyo tu kwamba, hawajamleta hata mtu mmoja kwa Yesu; bali pia, hawana ujasiri wowote kabisa wa kumhubiria Injili, mtu hata mmoja! Wamejaa aibu na woga! K**a wewe ni mtu wa jinsi hii, niruhusu kukuuliza, "Wewe kweli umempokea Roho Mtakatifu, VILEVILE k**a Mitume wa Kanisa la Kwanza (MATENDO YA MITUME 10:44-47)? Kimsingi, Nguvu ya Roho Mtakatifu, au Uwezo utokao juu; ni Uwezo unaomwezesha mtu kuwahubiria watu juu ya makosa na dhambi zao; na toba na ondoleo la dhambi hizo; kwa ufanisi na tija kubwa (LUKA 24:47,49). Biblia inasema katika MIKA 3:8, "Bali mimi NIMEJAA NGUVU KWA ROHO YA BWANA; NIMEJAA hukumu na UWEZO; NIMHUBIRI YAKOBO KOSA LAKE; NA ISRAELI DHAMBI YAKE."

"Nguvu ya Roho Mtakatifu, inamfanya mtu, kulinena Neno la Mungu, kwa ujasiri wa kipekee (MATENDO 4:31). Wanafunzi wa Yesu waliokuwa waoga kuishindania Imani (MATHAYO 26:56; 69-75); baada ya kujaa Nguvu ya Roho Mtakatifu, walibadilishwa, na kuwa na ujasiri wa ajabu (MATENDO YA MITUME 4:13; 18-20). Walisema, "MAANA SISI HATUWEZI KUACHA KUYANENA MAMBO TULIYOYAONA NA KUYASIKIA (MATENDO YA MITUME 4:20). Ni kwa nini walikuwa hawawezi kuacha kumhubiri Yesu? Kujazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu, kunaitwa pia, kubatizwa kwa Roho Mtakatifu na KWA MOTO (MATHAYO 3:11). Mtu akibatizwa kwa moto huo wa Roho Mtakatifu, moto huo uwakao ndani yake; unamfanya mtu huyo kushindwa kujizuia kumhubiri Yesu! (YEREMIA 20:9)."

"Siyo hilo tu, bali pia, mtu aliyebatizwa kwa moto wa Roho Mtakatifu, anapohubiri, maneno yake yanakuwa moto! (YEREMIA 5:14; 23:29). Mtu huyu, anapomshuhudia mtu, au kumhubiri Injili; Roho Mtakatifu, ambaye ni Mungu, Aliye Moto Ulao (WAEBRANIA 12:29); Yeye naye, wakati huohuo; humshuhudia mtu huyo. Mhubiri huyo hushuhudia, na vilevile; Roho Mtakatifu, Naye; hushuhudia PAMOJA NA MHUBIRI HUYO (YOHANA 15:26-27). Roho Mtakatifu humwongoza mtu anayehubiriwa, na kumtia katika Kweli yote; kwa kumhakikishia kwamba, yeye ni mwenye dhambi, na kwamba, hukumu nzito ya milele itamkabili, asipoyatilia maanani, maneno ya haki; anayoambiwa na Mhubiri huyo (YOHANA 16:8, 13). Ni kwa ajili hii sasa, ndiyo maana; mahubiri ya mtu aliyejaa Nguvu ya Roho Mtakatifu, huwa na tija kubwa. Sasa nikuulize tena, Je, umempokea Roho Mtakatifu VILEVILE walivyompokea Mitume? K**a, Jibu lako ni Ndiyo; basi amka, Ewe Shujaa uliyelala usingizi (YONA 1:6); nenda mitaani, ukamhubiri Yesu Kristo; ya kwamba, Anakuja upesi, wala hatakawia!! (WAEBRANIA 10:37; UFUNUO WA YOHANA 22:12)."

"Ndugu yangu mpendwa; ninakuambia tena kwa msisitizo! Uwe na huruma kwa wenye dhambi, walioko mitaani, ambao wanaangamia; au siyo ni OLE WAKO; damu ya watu hao itatakwa mkononi mwako; hukumu itakukabili (EZEKIELI 3:18-19). HUKUMU HAINA HURUMA KWAKE YEYE ASIYEONA HURUMA (YAKOBO 2:13). Kila mtu anayekwenda kuwahubiria Injili, watu walioko huko mitaani; katika ulimwengu wa roho, huko mitaani; anakwenda kuwaokoa watu hao, kwa KUWANYAKUA KATIKA MOTO. Katika YUDA 1:22-23, tunasoma, "WAHURUMIENI .... WAOKOENI KWA KUWANYAKUA KATIKA MOTO ...." Ni kwa nini, wenye dhambi hao wanatajwa wako katika moto? Sababu ni kwamba, Neno la Yesu Kristo mwenyewe, linasema katika YOHANA 3:18, ".... ASIYEAMINI AMEKWISHA KUHUKUMIWA ..." Unaweza kuona! Kimsingi, wasioamini, wamekwisha kupewa hukumu ya kutupwa katika moto wa milele! (UFUNUO WA YOHANA 21:8; MATHAYO 25:41). Hivyo, ukiwapelekea Injili, Mwokozi Yesu Kristo anayefanya kazi pamoja na sisi wahubiri katika kuokoa (1 WAKORINTHO 3:9; WARUMI 10:13-14); anakutumia WEWE, kuwanyakua wenye dhambi hao, katika hukumu ya moto wa milele! Uwe na huruma! Yeye asiyewahurumia wenye dhambi hao, na kuchukua hatua ya kwenda kuwanyakua katika moto, kwa kwenda kuwahubiria Injili; tunaweza kumfananisha na dereva wa gari la zimamoto lenye vifaa vyote vya uokoaji; anayejistarehesha kwa kunywa soda, na kula nyama choma, mahali fulani; bila huruma wala kujali, huku akiwa ameliegesha gari hilo, hapo alipo; ambapo siyo mbali na nyumba inayoungua moto, ambamo ndani ya nyumba hiyo, kuna watu wa familia kadha, walioshindwa kutoka kwenye nyumba hiyo!! WEWE SASA, NDIYE DEREVA HUYO!! Mwenye masikio, na asikie (MATHAYO 11:15)."

"Nimalize kwa kusema kuwa, inakupasa kufahamu pia kwamba, ziko nchi kadha duniani, ambazo, kumhubiria Injili mtu yeyote aliyeko mahali popote; ni kosa la jinai, ambalo hukumu yake ni kutoweshwa duniani. Hata hivyo, wako watu wachache wanaothubutu kuwahubiria Injili watu kadhaa, katika nchi hizo, na kuwa tayari kwa lolote; baada ya kuk**atwa. Ikiwa tumezungukwa na mashahidi wa Yesu, wa viwango hivi (WAEBRANIA 12:1); sisi tulioko Tanzania, au katika nchi nyingine; zilizo na uhuru wa kuhubiri Injili hii, kwa mtu yeyote; tutapataje kupona? (WAEBRANIA 2:1-3). TAFAKARI!!! Ni maombi yangu, kwamba, wewe uliyeokoka unapoangalia picha hizi; wewe pia utaumbiwa mzigo wa kwenda mitaani kuhubiri Injili. Umepewa vingi, hivyo BWANA atavitaka vingi kwako! (LUKA 12:47-48). Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho yako (FILEMONI 1:25)."

■ KANISA LA FGBF MAFINGA■ UBATIZO WA MAJI TELE (YOHANA 3:23) ■ JUMAPILI, 17.5.2026■ Mahali lilipo Kanisa, katika Halmash...
20/05/2026

■ KANISA LA FGBF MAFINGA

■ UBATIZO WA MAJI TELE (YOHANA 3:23)

■ JUMAPILI, 17.5.2026

■ Mahali lilipo Kanisa, katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga; Tanzania:

KINYANAMBO "B", MTAA WA MSOLA; NYUMA YA SHELL YA CF MJINI MAFINGA

Jumapili, tarehe 17.5.2026; imekuwa ni Siku nyingine ya Ubatizo wa Maji Tele (YOHANA 3:23), katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), MAFINGA; lililoko Kinyanambo "B", Mtaa wa Msola; nyuma ya Shell ya CF, Mjini Mafinga. Ni katika Wilaya ya Mafinga Mjini, Mkoa wa Iringa.

Ubatizo huo, ulifanyika baada ya Ibada Kuu ya Siku hiyo. Wale wote waliohubiriwa Injili, na kuiamini; au kuamua kumpokea Yesu, na kupewa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12); wamebatizwa, sawasawa na Agizo la BWANA wetu, Yesu Kristo (MARKO 16:16).

Ubatizo huu, hufanyika katika Maji Tele; yanayotosha kumwezesha mtu aliyeamini, kuzikwa pamoja na Yesu katika Ubatizo huo; unaokuwa k**a, "Kaburi la Maji"; na kufufuka pamoja naye; k**a tunavyosoma katika WAKOLOSAI 2:12, "MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; NA KATIKA HUO MKAFUFULIWA PAMOJA NAYE, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu." Na pia, k**a Neno la Mungu, lisemavyo katika WARUMI 10:9; na WARUMI 6:4.

Aidha; Ubatizo wa Maji Tele, ni tendo (YAKOBO 2:17-26), au jibu; linaloonyesha kwamba, mtu huyo aliyemwamini Yesu; ana dhamiri safi mbele za Mungu (1 PETRO 3:21), au ana nia thabiti ya kuitimiza haki yote (MATHAYO 3:13-15), yaani, ana nia thabiti, ya kuyatimiza maagizo yote ya Mungu; kwani, maagizo yake yote ni ya haki (ZABURI 119:172); na pia, ana nia ya kufuata kielelezo au nyayo za Yesu Kristo; na kuwa tayari kuwa Mwanafunzi wa Yesu; na kujifunza KUYASHIKA YOTE aliyotuamuru Yesu Kristo (MATHAYO 28:19-20; 3:13-17; YOHANA 13:15; 1 PETRO 2:21). Kwa hakika, wamebarikiwa wote waliotubu dhambi zao, kwa kumaanisha kuziacha; na kubatizwa (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 2:38; YOHANA 13:17).

Ikiwa wewe nawe, unaishi katika Mji wa Mafinga, au katika viunga vyake; na unapenda kuwa Mwanafunzi wa Yesu, kwelikweli (YOHANA 8:31); na kujifunza Kweli ya Neno la Mungu, kwa kina, mapana na marefu; amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo (ISAYA 28:10); basi, mahali hapa; ndiyo penyewe haswa!!!

■ Ibada za Kanisa la FGBF MAFINGA, za kila Jumapili; huanza saa 4 kamili, asubuhi.

■ MAWASILIANO: 0762580050

■ IBADA KUU, JUMAPILI 17.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanza...
17/05/2026

■ IBADA KUU, JUMAPILI 17.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

".... Wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, WAKIFANYA IMARA ROHO ZA WANAFUNZI ...." (MATENDO YA MITUME 14:21-22). Jumapili, tarehe 17.5.2026; imekuwa ni Siku nyingine ya kuzidi kufanywa imara, kwa NENO LA KWELI (2 TIMOTHEO 2:15; WAEFESO 1:13; 2 WAKORINTHO 6:7; YAKOBO 1:18). Ni katika Ibada Kuu ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge.

Siku hii, Neno la Kweli; lililozifanya imara zaidi, roho za Wanafunzi; limeletwa na BWANA kwetu, kupitia kwa Kiongozi wa Zoni ya SAMARIA; Dada, Subilaga Kasyupa; aliyefundisha Somo lenye kichwa, "NAYE ATAKUKUFURU". Kwa hakika, kila aliyekuwepo katika Ibada hii; ametoka akiwa tofauti na jinsi alivyokuja!

Aidha, kutokana na Neno hilo; watu kadha wa kadha, wenye dhambi; wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 26:20); na kumpokea Yesu Kristo, aliyewasafisha dhambi zao kwa Damu yake iliyomwagika msalabani (MATHAYO 26:28; 1 YOHANA 1:7); na kuwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12; 1 YOHANA 3:8-10).

Asante Mungu Baba, kwa jinsi unavyozidi kutufinyanga kwa Neno la Kweli; k**a unavyoona vema (YEREMIA 18:1-4). Pokea wingi wa Shukurani, na Sifa zote!

■ IBADA KUU, JUMAPILI 10.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanza...
10/05/2026

■ IBADA KUU, JUMAPILI 10.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Hatuachi kukusanyika pamoja, bali tunazidi kufanya hivyo; kwa kadiri tuonavyo Siku ile ya kuja kwake Yesu, kuwanyakua watakatifu wake, inakaribia (WAEBRANIA 10:25); tukiwa na nia ya kupokea Maneno yenye Uzima, ya Bwana wetu Yesu Kristo (1 TIMOTHEO 6:3). Ni katika Ibada Kuu ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; Jumapili, tarehe 10.5.2026.

Siku hii, Maneno yenye Uzima ya Bwana wetu Yesu Kristo; yamekuja kwetu, kupitia kwa Mtumishi wa Mungu, na Mpakwa mafuta wa BWANA; Mchungaji Hellen Kakobe; aliyefundisha Somo lenye kichwa, "WAJIBU WETU K**A WATUMWA TUSIO NA FAIDA (LUKA 17:7-10)". Heri (Amebarikiwa), yeye aliyelisikia Neno hili; na kulishika (LUKA 11:28).

Aidha, kutokana na Neno hilo; watu kadha wa kadha, wenye dhambi; wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 26:20); na kumpokea Yesu Kristo, aliyewasafisha dhambi zao kwa Damu yake iliyomwagika msalabani (MATHAYO 26:28; 1 YOHANA 1:7); na kuwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12; 1 YOHANA 3:8-10).

Asante Bwana wetu Yesu Kristo, kwa Neno lako lisafishalo; ambalo kwa hilo, tumezidi kuwa safi (YOHANA 15:3). Pokea wingi wa Shukurani, na Sifa zote!

■ INJILI MITAANI, JUMAMOSI 9.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM ■ KUHUBIRI INJILI MITAANI, KATIKA MITAA NA VICHOCHORO...
09/05/2026

■ INJILI MITAANI, JUMAMOSI 9.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ KUHUBIRI INJILI MITAANI, KATIKA MITAA NA VICHOCHORO VYA JIJI LA DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

■ NI INJILI YA MTU KWA MTU, NYUMBA KWA NYUMBA, NA VICHOCHORO VYAKE; NA KWA KILA KUNDI LA WATU (MATENDO YA MITUME 20:20, 26-27)

■ JUMLA YA IDADI YA WATU WAZIMA WALIOOKOKA SIKU HIYO: 1041

■ NI KAZI YA MUNGU, ILIYOFANYWA NA WASHIRIKA WA KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM, JUMAMOSI YA UINJILISTI; 9.5.2026

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Hizi, ni picha zinazowaonyesha baadhi ya Washirika; ambao ni miongoni mwa mamia ya Washirika wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; waliokuwa wakihubiri Injili Mitaani; mtu kwa mtu, nyumba kwa nyumba, na vichochoro vyake; na kwa kila kundi la watu; katika pembe zote za Jiji la Dar-Es-Salaam, na viunga vyake; Siku ya Jumamosi, tarehe 9.5.2026. Wakati unapozitazama picha hizi, ZINGATIA PIA, UJUMBE UFUATAO, KUTOKA KWA ASKOFU MKUU ZACHARY KAKOBE:

"Ndugu yangu mpendwa, jambo la kuzingatia, ni kwamba; picha hizi, siyo picha za tukio spesheli au mahususi, lililopangwa na kuandaliwa maalum, linalotokea kwa nadra; bali ni shughuli au hali ya utendaji wa kawaida, katika maisha ya Washirika wengi wa Kanisa la FGBF Dar-Es-Salaam. Kwa miaka mingi sasa, kuhubiri Injili mitaani, imekuwa ni sehemu ya maisha ya Washirika wengi wa Kanisa la FGBF Dar-Es-Salaam. Ukiacha Jumamosi kadhaa kila mwezi, zinazoitwa "JUMAMOSI ZA UINJILISTI"; ambapo Washirika wote huingia mitaani kushuhudia au kuhubiri Injili, katika maeneo mbalimbali ya Zoni zao; vilevile, Washirika katika Seksheni, na Makanisa ya Nyumbani, kadha wa kadha; hupanga mikakati yao wenyewe, na kuwa na siku tofauti tofauti, katika wiki, za kufanya kazi hii; achilia mbali makundi ya Washirika wachache wachache, ambao huhubiri Injili, takriban kila siku. Na zaidi sana, Washirika wengi binafsi hutumia kila fursa wanayoipata kila siku, kuhubiri Injili; iwe ni katika daladala, au mahali pengine popote. Kila Mshirika katika Kanisa hili, ni wajibu wake kuihubiri kila mahali; Habari Njema ya MWOKOZI WA ULIMWENGU, YESU KRISTO (1 YOHANA 4:14; YOHANA 4:42)."

"Kazi hii ya Kuhubiri Injili, siyo kazi ya Askofu au Mchungaji fulani, PEKE YAKE; wala siyo kazi ya Mwinjilisti au Mhubiri fulani "Mkubwa" wa Kimataifa, peke yake! NI KAZI INAYOPASWA KUFANYWA NA KILA MTU ALIYEOKOKA, awe ni mwanamume au mwanamke (MATENDO YA MITUME 2:18, 21); au ameokoka zamani, au ameokoka hivi karibuni (YOHANA 1:40-42; 4:5-30, 39-42). Hivi ndivyo ilivyokuwa Nyakati za Kanisa la Kwanza. Sauli aliposababisha adha kuu ya Kanisa la Kwanza, WASHIRIKA WOTE (wanaume pamoja na wanawake); walitawanyika na kwenda huko na huko, KULIHUBIRI NENO. Biblia inatupa simulizi hii, katika MATENDO YA MITUME 8:1, 3-4, "Siku ile kukatukia adha kuu ya Kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; WOTE WAKATAWANYIKA katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. Sauli akaliharibu Kanisa, akaingia kila nyumba, na kuwaburuta WANAUME NA WANAWAKE na kuwatupa gerezani. Lakini WALE WALIOTAWANYIKA (wangapi? Wote!) WAKAENDA HUKO NA HUKO WAKILIHUBIRI NENO." Unaweza kuona! Mitume, wao hawakwenda; bali WASHIRIKA WOTE, WANAUME KWA WANAWAKE walikwenda; kwa kuogopa kuburutwa na Sauli, na kupelekwa gerezani. Na kule walikokwenda, WOTE wakalihubiri Neno, wote wakaihubiri Injili."

"Hapo awali, Yesu Kristo alikuwa amewapa Washirika hao, Agizo Kuu, ambalo linatuhusu sisi pia; la kwenda kuhubiri Injili kwa kila kiumbe (MARKO 16:15); na baadaye Yesu akawaambia wakawe mashahidi wake Uyahudi wote na Samaria (MATENDO YA MITUME 1:8); lakini hawakutii maagizo hayo, bali waliendelea tu kujibariki na kujiburudisha wenyewe Kanisani, kwa mapambio; k**a wengi wetu tunavyofanya; mpaka pale Sauli alipoanza kuingia nyumba kwa nyumba, na kuwaburuta gerezani; NDIPO wakalazimika kwenda kuhubiri Injili Uyahudi na Samaria!! Je, na ninyi katika Kanisa lenu, au na wewe binafsi, unasubiri mpaka Mungu amwachie Sauli awaletee, au akuletee adha kuu, ndipo ulazimike kwenda kuhubiri huko na huko? SAA YA KUAMKA KATIKA USINGIZI IMEKWISHA KUWADIA! (WARUMI 13:11-12). Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, itahubiriwa katika Ulimwengu wote, KUWA USHUHUDA KWA MATAIFA YOTE; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja (MATHAYO 24:14)."

"Ndugu yangu, uliyeokoka; bila kujali kwamba, WEWE ni Mshirika wa Kanisa gani; kumbuka kwamba, NI OLE WAKO USIPOIHUBIRI INJILI (1 WAKORINTHO 9:16-17). Usingojee mpaka Mungu amlete Sauli kukushurutisha, kufanya hivyo! Wala usitoe udhuru kwamba, wewe bado mchanga kiroho; hujajua sana Neno la Mungu. KILA AMWAMINIYE YESU, MWANA WA MUNGU; ANAO HUO USHUHUDA NDANI YAKE (1 YOHANA 5:10). Ndani yako kuna ushuhuda, utumie ushuhuda huo, katika kuwashuhudia au kuwahubiria Injili, watu wengine. Ushuhuda wako ni upi? Ni Neno lile ulilolipokea, ambalo lilikufanya ukate shauri kuokoka. Nenda mitaani, ukalitumie Neno hilohilo kuwahubiria watu wengine. Anzia hapo!! (YOHANA 1:35-46)."

"Aidha, wako watu wengine wanaosema kwamba wamejazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu, na wananena kwa lugha (MATENDO YA MITUME 1:8; 2:4). Ni vema, na ni vizuri sana! Hata hivyo, kinachoshangaza, ni kwamba; baadhi ya watu hawa, wanaosema wamejazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu; tangu "wajazwe Nguvu hiyo", siyo tu kwamba, hawajamleta hata mtu mmoja kwa Yesu; bali pia, hawana ujasiri wowote kabisa wa kumhubiria Injili, mtu hata mmoja! Wamejaa aibu na woga! K**a wewe ni mtu wa jinsi hii, niruhusu kukuuliza, "Wewe kweli umempokea Roho Mtakatifu, VILEVILE k**a Mitume wa Kanisa la Kwanza (MATENDO YA MITUME 10:44-47)? Kimsingi, Nguvu ya Roho Mtakatifu, au Uwezo utokao juu; ni Uwezo unaomwezesha mtu kuwahubiria watu juu ya makosa na dhambi zao; na toba na ondoleo la dhambi hizo; kwa ufanisi na tija kubwa (LUKA 24:47,49). Biblia inasema katika MIKA 3:8, "Bali mimi NIMEJAA NGUVU KWA ROHO YA BWANA; NIMEJAA hukumu na UWEZO; NIMHUBIRI YAKOBO KOSA LAKE; NA ISRAELI DHAMBI YAKE."

"Nguvu ya Roho Mtakatifu, inamfanya mtu, kulinena Neno la Mungu, kwa ujasiri wa kipekee (MATENDO 4:31). Wanafunzi wa Yesu waliokuwa waoga kuishindania Imani (MATHAYO 26:56; 69-75); baada ya kujaa Nguvu ya Roho Mtakatifu, walibadilishwa, na kuwa na ujasiri wa ajabu (MATENDO YA MITUME 4:13; 18-20). Walisema, "MAANA SISI HATUWEZI KUACHA KUYANENA MAMBO TULIYOYAONA NA KUYASIKIA (MATENDO YA MITUME 4:20). Ni kwa nini walikuwa hawawezi kuacha kumhubiri Yesu? Kujazwa Nguvu ya Roho Mtakatifu, kunaitwa pia, kubatizwa kwa Roho Mtakatifu na KWA MOTO (MATHAYO 3:11). Mtu akibatizwa kwa moto huo wa Roho Mtakatifu, moto huo uwakao ndani yake; unamfanya mtu huyo kushindwa kujizuia kumhubiri Yesu! (YEREMIA 20:9)."

"Siyo hilo tu, bali pia, mtu aliyebatizwa kwa moto wa Roho Mtakatifu, anapohubiri, maneno yake yanakuwa moto! (YEREMIA 5:14; 23:29). Mtu huyu, anapomshuhudia mtu, au kumhubiri Injili; Roho Mtakatifu, ambaye ni Mungu, Aliye Moto Ulao (WAEBRANIA 12:29); Yeye naye, wakati huohuo; humshuhudia mtu huyo. Mhubiri huyo hushuhudia, na vilevile; Roho Mtakatifu, Naye; hushuhudia PAMOJA NA MHUBIRI HUYO (YOHANA 15:26-27). Roho Mtakatifu humwongoza mtu anayehubiriwa, na kumtia katika Kweli yote; kwa kumhakikishia kwamba, yeye ni mwenye dhambi, na kwamba, hukumu nzito ya milele itamkabili, asipoyatilia maanani, maneno ya haki; anayoambiwa na Mhubiri huyo (YOHANA 16:8, 13). Ni kwa ajili hii sasa, ndiyo maana; mahubiri ya mtu aliyejaa Nguvu ya Roho Mtakatifu, huwa na tija kubwa. Sasa nikuulize tena, Je, umempokea Roho Mtakatifu VILEVILE walivyompokea Mitume? K**a, Jibu lako ni Ndiyo; basi amka, Ewe Shujaa uliyelala usingizi (YONA 1:6); nenda mitaani, ukamhubiri Yesu Kristo; ya kwamba, Anakuja upesi, wala hatakawia!! (WAEBRANIA 10:37; UFUNUO WA YOHANA 22:12)."

"Ndugu yangu mpendwa; ninakuambia tena kwa msisitizo! Uwe na huruma kwa wenye dhambi, walioko mitaani, ambao wanaangamia; au siyo ni OLE WAKO; damu ya watu hao itatakwa mkononi mwako; hukumu itakukabili (EZEKIELI 3:18-19). HUKUMU HAINA HURUMA KWAKE YEYE ASIYEONA HURUMA (YAKOBO 2:13). Kila mtu anayekwenda kuwahubiria Injili, watu walioko huko mitaani; katika ulimwengu wa roho, huko mitaani; anakwenda kuwaokoa watu hao, kwa KUWANYAKUA KATIKA MOTO. Katika YUDA 1:22-23, tunasoma, "WAHURUMIENI .... WAOKOENI KWA KUWANYAKUA KATIKA MOTO ...." Ni kwa nini, wenye dhambi hao wanatajwa wako katika moto? Sababu ni kwamba, Neno la Yesu Kristo mwenyewe, linasema katika YOHANA 3:18, ".... ASIYEAMINI AMEKWISHA KUHUKUMIWA ..." Unaweza kuona! Kimsingi, wasioamini, wamekwisha kupewa hukumu ya kutupwa katika moto wa milele! (UFUNUO WA YOHANA 21:8; MATHAYO 25:41). Hivyo, ukiwapelekea Injili, Mwokozi Yesu Kristo anayefanya kazi pamoja na sisi wahubiri katika kuokoa (1 WAKORINTHO 3:9; WARUMI 10:13-14); anakutumia WEWE, kuwanyakua wenye dhambi hao, katika hukumu ya moto wa milele! Uwe na huruma! Yeye asiyewahurumia wenye dhambi hao, na kuchukua hatua ya kwenda kuwanyakua katika moto, kwa kwenda kuwahubiria Injili; tunaweza kumfananisha na dereva wa gari la zimamoto lenye vifaa vyote vya uokoaji; anayejistarehesha kwa kunywa soda, na kula nyama choma, mahali fulani; bila huruma wala kujali, huku akiwa ameliegesha gari hilo, hapo alipo; ambapo siyo mbali na nyumba inayoungua moto, ambamo ndani ya nyumba hiyo, kuna watu wa familia kadha, walioshindwa kutoka kwenye nyumba hiyo!! WEWE SASA, NDIYE DEREVA HUYO!! Mwenye masikio, na asikie (MATHAYO 11:15)."

"Nimalize kwa kusema kuwa, inakupasa kufahamu pia kwamba, ziko nchi kadha duniani, ambazo, kumhubiria Injili mtu yeyote aliyeko mahali popote; ni kosa la jinai, ambalo hukumu yake ni kutoweshwa duniani. Hata hivyo, wako watu wachache wanaothubutu kuwahubiria Injili watu kadhaa, katika nchi hizo, na kuwa tayari kwa lolote; baada ya kuk**atwa. Ikiwa tumezungukwa na mashahidi wa Yesu, wa viwango hivi (WAEBRANIA 12:1); sisi tulioko Tanzania, au katika nchi nyingine; zilizo na uhuru wa kuhubiri Injili hii, kwa mtu yeyote; tutapataje kupona? (WAEBRANIA 2:1-3). TAFAKARI!!! Ni maombi yangu, kwamba, wewe uliyeokoka unapoangalia picha hizi; wewe pia utaumbiwa mzigo wa kwenda mitaani kuhubiri Injili. Umepewa vingi, hivyo BWANA atavitaka vingi kwako! (LUKA 12:47-48). Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho yako (FILEMONI 1:25)."

■ IBADA KUU, JUMAPILI 3.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzan...
03/05/2026

■ IBADA KUU, JUMAPILI 3.5.2026 - KANISA LA FGBF DAR-ES-SALAAM

■ Mahali lilipo Kanisa katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Tanzania:

BARABARA YA SAM NUJOMA, MWENGE; MKABALA NA MLIMANI CITY

Ni Siku ya Bwana (UFUNUO WA YOHANA 1:10), Jumapili, tarehe 3.5.2026; ambapo wana wa Mungu (1 YOHANA 3:1), wamekusanyika pamoja katika Ibada Kuu ya Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; ili kupokea Habari Njema ya Ufalme wa Mungu (LUKA 4:43; 8:1).

Siku hii, Habari Njema ya Ufalme wa Mungu; tumeipokea kupitia kwa Kiongozi wa Zoni Msaidizi, wa Zoni ya MIZEITUNI; Dada, Sarah Mwilima; aliyefundisha Somo lenye kichwa, "SIRI ILIYOFICHULIWA NA SHETANI MWENYEWE". Heri (Amebarikiwa), yeye aliyelisikia Neno hili; na kulishika (LUKA 11:28).

Aidha, kutokana na Neno hilo; watu kadha wa kadha, wenye dhambi; wametubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha (MITHALI 28:13; MATENDO YA MITUME 26:20); na kumpokea Yesu Kristo, aliyewasafisha dhambi zao kwa Damu yake iliyomwagika msalabani (MATHAYO 26:28; 1 YOHANA 1:7); na kuwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu (YOHANA 1:12; 1 YOHANA 3:8-10).

Asante Roho Mtakatifu, kwa jinsi unavyotuongoza na kututia kwenye Kweli yote; ambayo kwa hiyo, tunazidi kuwekwa huru; kila iitwapo leo! (YOHANA 16:13; 8:32). Pokea wingi wa Shukurani, na Sifa zote!

Address

Sam Nujoma Road, Mwenge
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Full Gospel Bible Fellowship Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share