18/07/2020
Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth kila mwenye Roho, nafsi na mwili.
SOMO: KUTEMBEA NA ROHO MTAKATIFU
Unaweza kujiuliza nataka kutembea na Roho Mtakatifu ,nitafanyeje ili niweze kutembea na Roho Mtakatifu, hii ni misingi michache ya kutembea na Roho Mtakatifu.
(I) Ukweli na uhalisia kuhusu Roho Mtakatifu.
(ii) Kuelekeza na kuwekeza akili kwenye mambo ya Rohoni na si ya mwilini.
(iii)Kuusulubisha mwili.
Utofauti wa agano la kale na agano jipya ni kwamba kwenye agano la kale hawakupewa karama au zawadi ya Roho Mtakatifu ambayo inamsaidia mwamini kushinda dhambi.Roho Mtakatifu ni ahadi na zawadi ya Bwana Yesu Kristo mwenyewe kwamba imempasa yeye aende kwa Baba ili aje msaidizi hapa duniani.
(i) Ukweli na uhalisia kuhusu Roho Mtakatifu.
-Roho Mtakatifu ndiye anatufanya kuwa familia moja na Mungu, tunakuwa watoto wa Mungu Warumi 8:14 "kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu hao ndio wana wa Mungu" na ukisoma Wagalatia 4:4-7" Hata ulipowadia utimilifu wa wakati Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke ,amezaliwa chini ya sheria kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu aliaye aba yabi Baba" Katika andiko hili amtumwa Yesu Kristo na baada ya Yesu kuondoka akatumwa Roho Mtakatifu duniani ili amdhihirishe Yesu Kristo duniani.
-Kazi ya Roho Mtakatifu ni msaidizi ambaye anatembea na mwamini muda wote na anatuweka katika uhusiano wa moja kwa moja na Yesu kwa sababu ni Roho wa Mungu mwana na anatupa uhusiano na Mungu Baba kwa sababu ni Roho wa Mungu.
-Roho Mtakatifu anatufanya kuwa sehemu ya mwili wa Kristo kwa sababu ni Roho wa Roho wa mwana wa Mungu(Yesu).1Wakorintho 6:17" Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni Roho moja naye"
-Roho Mtakatifu anatupa nguvu ya kushinda dhambi.Hatuko chini ya sheria ila tuko chini ya neema Wagalatia 5:16" Basi nasema enendeni kwa Roho wala hamtazitimiza kwamwe tamaa za mwili" ili uweze kushinda maisha ya dhambi unahitaji msaada wa Roho Mtakatifu akuongoze katika mambo yote.
Wakristo wengi wa sasa tunaishi katika kiwango ambacho Mtume Paulo alisema katika kitabu cha Warumi 7:19 "Kwa maana lile jema nilipendalo,silitendi,Bali like baya nisilolipenda ndilo nilitendalo"
Mtume Paulo alikuwa anaelezea maisha bila Roho Mtakatifu yanavyokuwa yani Roho inashindana na mwili ata usijue ufanye nini lakini Roho Mtakatifu akiongoza hatuki chini ya sheria na unakuwa huru mbali na dhambi" 2Wakorintho3:17" Basi Bwana ndiye Roho walakini alipo Roho wa Bwana hapo ndipo penye Uhuru".
(ii) Kuelekeza na kuwekeza akili kwenye mambo ya Rohoni na sio ya mwilini.
-Kwanza inatakiwa mwamini ajazwe Roho Mtakatifu.Kusifu na kuabudu ni muhimu kuwa kuwa katika uwepo wa Roho Mtakatifu.
-Kuomba msaada na kushirikiana na watu waliokuwa kiroho kuliko wewe.Anza Siku
na maombi
(iii) Kuusulubisha mwili. Wagalatia 5:24" Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake" mwili wa mwamini umesulubiwa lakini bado haujafa.
Roho nia yake ni uzima na dhambi zote ni za mwili bila mwili mwanadamu hawezi kufanya dhambi kwa sababu ili afanye dhambi hap duniani anahitaji kitambulisho cha kuonekana kwa macho ya damu na nyama ambacho ndiyo mwili ,Wagalatia 5:19" Basi matendo ya mwili ni dhahiri ndiyo haya uasherati,uchafu,ufisadi,ibada ya sanamu,uchawi,uadui,ugomvi,wivu,hasira,fitina,husuda,uzushi,faraka,ulevi,ulafi na mambo yanayofananana hayo" andiko jingine linatupa athari za kuongozwa na Mwili ni Warumi 8:13" Kwa maana k**a tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili mwataka kufa Bali k**a mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho mtaishi".
Ashukuriwe Mungu atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Eng B.G Nyamega,
+255653664479,
Dar es salaam.