15/01/2026
🌍KATIKA KUSHEREKEA NA KUMSHANGILIA MUNGU KWAAJILI YA FAMILIA YA MAWAKILI WA INJILI(GOSPEL STEWARDS FAMILY - GSF) KUTIMIZA MIAKA MITANO
✍️ Mawakili wa injili (GSF) Hii ni familia ya watu walioamua kuwa watunza injili, inayounganishwa kwa kupitia WhatsApp group. Isiyojali madhehebu bali watu waliotayari kujifunza pamoja neno la Mungu na walioamua kumpa Yesu maisha yao kuwa Bwana na kiongozi wa maisha yao binafsi. Katika familia hii pamekuwa mahali salama pa kujifunza na kukua kiroho.
Tamtukuza Mungu kwaajili ya neema na rehema zake ametupa kutimiza mwaka wa tano tangu Familia hii kubwa ya Mawakili wa injili (GSF) ianze nitakuletea mambo kumi(10) yahusuyo familia hii usiyoyajua:
1. Familia hii ilianzishwa 15/1/2021 na EV. Japhet Katana. Ili kujifunza zaidi neno la Mungu na kulea watumishi mbalimbali wa Mungu, walio na kiu na shauku ya kujifunza neno la Mungu na wenye dhamira ya kumtumikia Mungu kwa ushuhuda mwema na viwango vikubwa kuufikia ulimwengu.
2. Familia hii ilianza ikiwa na idadi ya watu watano ukijumlisha na admin. Lakini ndani ya miaka hii mitano pamoja na kufuata ratiba zetu tumefikia watu 1000+ lengo letu kuwa na group zaidi za WhatsApp na kuwafikia watu wengi zaidi kwa injili ya upendo wa Yesu Kristo.
3. Familia hii inajiendesha kwa ratiba maalumu kila siku, ambayo inahusisha semina za watumishi wa ndani ya familia, kusoma neno la Mungu, maswali mbalimbali yanayotatiza watu kukua kiroho, maombi na maombezi, kufunga , kusoma vitabu, kuwasilisha tuliyojifunza makanisani kwetu n.k
4. Familia hii inaamini katika ubora na karama ambazo Mungu ameweka ndani ya watu hivyo huwa tunaandaa semina na kualika watumishi kutoa nje ya familia hii kufundisha mada mbalimbali k**a vile, uchumi wa Kiungu, ndoa, mahusiano, utakatifu, Roho mtakatifu, Imani, maombi, hekima, n.k
5. Familia hii inamchanganyiko wa watu wa rika zote na madhehebu mbalimbali ya watu wanaomuamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao binafsi na wameokoka, tunajifunza pamoja kwa upendo na kuheshimiana.
6. Familia hii inamuundo wa uongozi ambao kwa Sasa unaundwa na mwenyekiti, katibu mkuu, Mhazina, viongozi wa idara, Ndiyo viongozi wa familia hii.
7. Mwaka huu tunayo malengo ya kutanua huduma zetu kuendelea kuwaona yatima na walio katika Hali ngumu, kwenda hospitali kuhubiri na kuombea wagonjwa pia kuwapelekea matunda. Na malengo mengine mengi kuinua huduma zetu, na tunatazamia kukua hata kuwafikia magerezani wafungwa, na baadae kuanza kuwafikia hata wasiofikiwa na injili.
1/1/2025 tuliweza kwa msaada wa Mungu kufanya Charity 3 au matendo ya huruma. Katika mkoa wa Dar es salaam kituo BABU NA BIBI WATOTO (BABIWA) Huko madale
Geita kituo cha MOYO WA HURUMA
KIGOMA KASULU KATIKA GEREZA LA KASULU MJI.
1/1/2026 tuliweza kufanya tena charity katika maeneo matatu, Buloma foundation (Kibaha) Kituo cha kulea watoto Yatima Igogwe (Kiwira-Mbeya) naTulitembelea wagonjwa hospitali ya Wilaya Tunduru (Ruvuma)
Sehemu hizi tuliweza kufanya charity tukishirikiana na wadau wetu wanaopenda injili.
8. Tunayo channel yetu YouTube GOSPEL STEWARDS TV ambayo imeanza mwezi desemba 2021, tunatarajia kuwa na subscribers 10k kufikia mwisho wa mwaka huu. K**a hujasubscribe kwenye Television yetu tafadhali fanya hivyo kupitia link hapa chini ili kuendelea kujifunza zaidi na kutuwezesha kutimiza malengo yetu ya mwaka kwa utukufu wa Mungu. Hata Sasa tunao subscribers 1.05k
https://youtube.com/channel/UCCsdQYg1TSs1Z3Jlm6VEKvQ
9. Katika familia hii kweli ya Kristo yaani Neno la Mungu na maarifa kutoka kwa watumishi mbalimbali wanaoandika vitabu hata wanaotoa mafundisho kwa njia mbalimbali ili kuujenga mwili wa Kristo, tunahimizana kufuatilia na hata kuwaalika kufundisha semina katika familia yetu.
10. Tumeiita familia kwasababu malengo yetu ya kuwa pamoja na kuishi kwa upendo kujaliana, kuinua vipawa na kuwasaidia watu kujua na kutumikia kusudi la kuumbwa kwao, kuheshimiana pia kujaliana. Hii imefanya kuwa sehemu nzuri ya kukua na kustawi kiroho. Zaidi tumefanikiwa Kwa neema ya Mungu kufikia nchi zaidi ya 11 ambazo zinawanafamilia.
✍️Kipekee kabisa napenda kumshukuru Sana Mchungaji Imani Oscar Katana, mchungaji kiongozi wa kanisa la Moto Ulao Baptist Church lililopo Dege kigamboni na Moto Ulao online church, ndiye alikuwa mshauri wa kwanza kuona tunaweza kuwa na familia hii. Moja ya shuhuda mbalimbali zinapotajwa basi hakika siwezi kumsahau katika kudumu kwa familia hii.
🌺Ukiwiwa kutoa sadaka yako kwa haya tuyafanyayo au kujitolea bundle na zawadi kwa mtumishi wa Mungu basi unakaribishwa kuwasilisha kwa namba hizi;
+255745746691 M-pesa na +255693177947 Eartel money, jina Japhet Katana.
Endapo unaye mtu unatamani kuwa mmoja wa familia hii kwa moyo mkunjufu tunamkaribisha sana, mtumie malengo yetu na akiwa tayari tutaungana pamoja nawe. Ajitambulishe ni nani na anapatikana wapi ili kutunza kumbukumbu zetu.
Unaweza kubofya link hii kuja moja kwa moja WhatsApp. Https://wa.me/+255745746691/
HERI YA MIAKA MITANO KWETU SOTE MAWAKILI WA INJILI (GOSPEL STEWARDS FAMILY) TUNAWAPENDA WOTE.
🇹🇿🇲🇿🇲🇼🇿🇲🇰🇪🇨🇩🇧🇮🇳🇦🇺🇬🇷🇼❤️